Original komedy kwishiney

Status
Not open for further replies.
hawa jamaa acha tu.walishawai kuniaibisha mbele ya mama mkwe hivihivi kwa kumpaka mama mkwe live,"tunakushukuru wewe m'mkwe kwani tokea umetoka kijijini kuja kwenye harusi ya mwanao hutaki kurudi kwako umeng'ang'ania tu kwenye sofa"kiukweli nilijisikia vibaya kama mimi ndo nimewatuma siku ya pili mama aliaga.!!
 
Hao ni wajinga!wameishiwa ubunifu!Tangu wahame ETV hawana jipya,wanawachekesha mamaza wa kiswazi na watoto tu!Nadhani CCM imefanikiwa kuwamaliza,kwani baada ya kuonekana mwiba kwa serikali kwa kuiumbua na kuwaigiza viongozi wa serikali wanapofanya uhayawani,CCM ikaamua kuwapeleka TBC ili show zao ziwe edited before being broadcasted ili kupunguza makali!Kwishney karega!
 
Wangeendelea kuwepo na Mengi hizo Harrier na majumba waliojenga wangeyatolea wapi?Yule Mchaga anaijua hela kuliko unavyodhani ndiyo maana hata wafanyakazi wake anawalipa kiduchu sana!!Nilimsikia juzi akiendesha kipindi Clouds Mpoki alisema ana pub kigamboni.Jamaa wameshakaa vizuri kiuchumi sidhani kama kunyimwa mkataba mpya TBC (kama ni kweli) kutawayumbisha sana kiuchumi!!
 
Kosa kubwa walilolifnya ni kukubali kutumika kisiasa, na kwa kuwa sasa wameshakuwa kama 'used condom' nani ahangaike nao tena? Imeshakula kwao, tutakutana nao tu mitaani. Ngoja mie niandae mshiko ninunue lile gari la .................., niondokane na kero ya jirani!

nani aendelee kuwajali tena ili hali kila mtu anahangaikia kutuliza manyoka nyoka yao yanayowasumbua kila uchao machoni mwa jamii?
 
Wangeendelea kuwepo na Mengi hizo Harrier na majumba waliojenga wangeyatolea wapi?Yule Mchaga anaijua hela kuliko unavyodhani ndiyo maana hata wafanyakazi wake anawalipa kiduchu sana!!Nilimsikia juzi akiendesha kipindi Clouds Mpoki alisema ana pub kigamboni.Jamaa wameshakaa vizuri kiuchumi sidhani kama kunyimwa mkataba mpya TBC (kama ni kweli) kutawayumbisha sana kiuchumi!!

Mpoki ana 'pub', pub, pub, aisee umeongea 'point' kweli aisee, duuuuuuuu! pub, pub!
 
Nakumbuka walivyomsimanga Abiola, kwa ajili ya kutunisha matumbo yao, kimbunga kinawajia, na hivi walivyo watupu 'upstairs' kazi wanayo.

Shigongo alisahwahi kutoa makala ndefu tu, tena akimuasa SEKI juu ya dharau zake kwa Mzee Mengi aliyemtoa mbali maishani mwake, atajua kwamba walosema 'usinyee kambi' walikwa wanamaanisha nini haswa!
 
bora waishie zao mbali! wanaboa sana na ukosefu wao wa creativity!

Huwezi kuwa creative wakati unatakiwa uipambe pambe chama tawala kwa namna yoyote ile katika vichekesho vyako wakati watazamaji wana hasira na "tawala". Labda wakaongeze nguvu FUTUHI!
 
Hata kama wangebaki EATV kwa miaka 50 wasingeweza kumiliki hata 1/10 ya assets walizonazo kwa sasa. Mru yeyote makini pale ITV ni pakupita tu, siyo mahali ambapo imaweza create wealth. Wanachopaswa kufanya ni kuangalia "next move" na siyo kwa nini TBC hawa renew mkataba wao. Lakini the dudes bado wana mvuto kuliko vikundi hasara vingine vyote
 
Kwa utaratibu wa tbc1,nazani wanatakiwa wajiandae kuaga hapo,maana hata kwa tido mhando ilitokea kama hivi then mwisho wa siku wakaja mbwaga,
so wajiandae na maisha ya mengine,
najua ni wapiganaji tangu zamani,hawawezi kufa njaa
 
Mpoki namsikia sana clouds FM anachonga sana mademu fulani ka mipasho vile! Kweli dunia mduara!
 
katika mambo waliyolaniwa hawa jamaa ni kitendo cha kumtukana mzee mengi hadharani. Kwa kweli walifanya vibaya sana hata kama kulikua n amatatizo bado walikuwa hawana haki ya kufanya hivyo.
 
Usiache,mbachao kwa msala upitao,na usimtukane mamba kabla hujavuka mto!
By the way mzee mengi anachofanya ni biashara,wakitaka kurudi hatokataa kuwapokea,under the contract,ambayo itakuwa inampa maslahi yake binafsi!
 
Hivi wakuu ilikuwaje hawa jamaa kumwingiza mzee mengi kwenye mambo yao?kwa sababu najua mengi ni member wa ccm,labda walikuwa wanapigana vita wasiyo ijua??kweli dunia hadaa!DUNIANI TEMBEA KWA UANGALIFU USIJE TUMBUKIA SHIMONI!
 
kama ni hivyo wajipange kweli, maana nimeshasikia wengi wao wakisema miradi wanayoimiliki lakini ukija kuiona unabaki kushangaa na mwishoni utasikia mradi ushakufa, kuendesha biashara kwa mafanikio si kazi ndogo ingawa kuianzisha inaweza isiwe tabu sana!
Wangeendelea kuwepo na Mengi hizo Harrier na majumba waliojenga wangeyatolea wapi?Yule Mchaga anaijua hela kuliko unavyodhani ndiyo maana hata wafanyakazi wake anawalipa kiduchu sana!!Nilimsikia juzi akiendesha kipindi Clouds Mpoki alisema ana pub kigamboni.Jamaa wameshakaa vizuri kiuchumi sidhani kama kunyimwa mkataba mpya TBC (kama ni kweli) kutawayumbisha sana kiuchumi!!
 
Mabosi wa TBC wamekuwa wakipigana vikumbo kukwepa ku renew contract ya hawa vijana machachari wanaokosa umaarufu kila kukicha,taarifa zinasema wao wenyewe wameanza kushtukia hiyo baada ya kipigwa kalenda kila siku huku ma technicians wa TBC wakirudia rudia show zao zilizopita miaka mingi,,kwa nini TBC wasiwe wazi na kukataa ku sign au ku sign ili hawa wandugu wajue moja??Tbc wakikataa ku sign hawa jamaa itakuwa ndio mwisho wao au wataenda ITV?watathubu kwenda ITV na walishamtukana mzee Mengi live kila mtu aliona??waswahili wanasema usinyee kambi,,kazi ipo!

Litakuwa ni jambo zuri sana kwani kipindi walivyojizolea umaarufu kupitia EATV walilewa na kumwona kama dodoki aliyewafikisha pale, Na walisahau malipo ya ubaya niya hapa hapa duniani na wenzake wenye tabia kama hii wajifunze kupitia kwa hawa.
 
mimi naona walishindwa kutumia nafasi yao kufika mbali

Hii naweza kuifananisha na ule usemi unaosema mke wa kwanza ni mke wa kwanza tu hata ukioa hata zaidi ya 10 hawatomfikia yule wa kwanza
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom