Ole wenu CHADEMA!

Mlalahoi,
kwanza labda nianze kwa kamsemo "mambo ya tibwilitibwili tumuachie tibwili mwenyewe"
lakini mzee umeongea mambo mazito sana, unajua mimi ni mkereketwa sana wa siasa za tanzania na kweli wakati nasoma reply zako damu ilikuwa inachemka.

Sijaweza kupata muda wa kusoma reply zote katika hii subject lakini nimeona mmegusia mambo mbalimbali ambayo kwa mtazamo wangu ni "very hot or burning issues of our time"
mfano hili la freeman mbowe na chedema kwa ujumla,

Influence of media katika siasa za bongo na influence za politicians na dola kwa media,
issue ya independent candidates,

Na suala zima la jinsi gani ya kupambana na umaskini katika taifa hili ambalo kila siku inapopita raia wake wanasema "afadhali ya jana"

nikianza na suala la freeman mbowe, nafikiri huyu bwana mpaka sasa amejitahidi kwa kiasi fulani katika kukuza demokrasia hii ya vyama vingi hasa ukimlinganisha na viongozi wengine wa vyama vya upinzani kama ibrahim lipumba,augustion mrema, james mbatia na wengine...

Lakini ni wazi kuwa kura alizopata freeman kwenye uchaguzi hazilingani kabisa na nguvu na gaharama alizotumia katika kampeni,na hata kwa upande wa ubunge chadema imefanya vibaya sana kuliko tulivyotarajia,

Kwa mtazamo wangu nafikiri chadema hawakufanya analysis vizuri na hawakua na longterm stratergy ya kufanya vizuri katika uchaguzi,

Hii unaweza kuangalia kwa mfano kwenye sera ambazo mbowe alikuwa akizinadi kama hii ya "majimbo" ni wazi kuwa alikuwa akinadi sera ambayo ilikuwa ikimmaliza mwenyewe na hata kama kuna watu au watalaam walimshauri auze sera hii kwa kweli hawakufanya research yao vizuri,

Sera ya majimbo (iwe ni nzuri au mbaya) ni vigumu sana kuiuza kwa watanzania kwasababu watanzania wanaamini zaidi katika sera zinazo waunganisha zaidi kuliko kuwatenga na ni wazi kuwa CCM waliitumia sera hii kama msumari kwa chadema kwa kusema kuwa chadema wanataka kuigawa nchi mfano eti mlima wa kilimanjaro uwe ni wa "wachaga" na ziwa la tanganyika ni la "waha", wakati watanzania wanataka kujivunia kwa pamoja rasilimali zilizopo.

Hivyo kwa mtazamo wangu "atleast" kwa miaka kumi ijayo sera kama hii waisitishe kwanza na inahitaji mda kuwaelewesha watanzania mpaka waelewe.

Kwa sasa nafikiri chadema itumie "tactics" kama zile za ccm za kunadi sera za UMOJA WA WATANZANIA, KUPIGA VITA UKABILA NA UDINI na muhimu kuja na sera makini ambazo zinaweka wazi ni jinsi gani chadema inaweza kuwa chama mbadala kwa ccm hasa katika kuondoa umaskini katika taifa hili.

Kwa kweli watanzania wameichoka ccm lakini wanajaribu kuangalia ni chama gani mbadala kwa ccm wanajikuta hawana jibu zaidi ya kuendelea kuiweka ccm,

mfano

wakati mrema alivyokuwa "mrema hasa" na alipo ingia NCCR mageuzi alikuwa ni tishio sana, na infact aliungwa mkono na watanzania wengi sana including a lot af academicians pale mlimani,
baada ya mrema "kubore" na kuanza kuyumba na kuwayumbisha watanzania alidissapoint watu wengi saana na hivyo kufanya upinzani uzaraulike kwa watanzania,

kwahiyo dhana ya kuwalaum watanzania katika failure za upinzania tanzania haina mantiki bali tatizo linatoka kwa viongozi,upinzani upo tu kama meli iliyo baharini bila nahodha wa kuilekeza iende wapi,

watanzania bado hatujapata chama cha kukiamini kukipa dola kwa sasa na kama hali hii ya sasa ya kusubiri mpaka wakati wa uchaguzi ndio watu wanaamka kuanza kunadi sera zao nafikiri hatutapata madiriko yeyote ya uongozi katika taifa hili.

na zaidi vyama hivi vijenge utaratibu wa kubadilisha hata wagombea, mfano tungependa kuona watu walioshindwa uchaguzi mwaka jana wakae pembeni walete watu wapya,

tumechoka kusikia mtu kama ibrahimu lipumba,augustion mrema, mtikila, kwakweli kuliko kuja na hao watu ni bora hata wasisimamishe wagombea maana uchaguzi wa mwakajana umeonyesha kuwa wengine hawakupigiwa kura hata na ndugu zao.

kwahili suala la "influence" ya media katika politics za tanzania nalo kwakweli ni very "serious" kwasabababu hatari iliyopo ni hii ya vyombo vya habari kuegemea upande fulani kutokana na either vile vyombo kuwa na uhusiano au kuwa na hofu ya "existence" yake baada ya uchaguzi,
tunatakiwa tuwe na "independent body" ambayo itakuwa ina "scrutinize" hivi vyombo vya habari, ili tuwe na free, independent na fair media,

its ok kama chombo cha habari kama uhuru kikisema kabisa kabla ya uchaguzi kuwa kitakuwa kinacampagne kwa ccm ,

lakini kitendo cha vyombo kama vya ippmedia kusema kuwa viko neutral wakati vinatoa asilimia 90 "coverage" kwa mgombea wa ccm na pia "kuinflunce opinion" ya watanzania "it is totally unfair" and "unacceptable" na kwa hili ippmedia walitakiwa wawajibishwe na vyombo maalum.

kwa hili la independent candidate hilo tunaweza kuwa na maoni tofauti tofauti lakini zaidi hili ni "threat" kwa ccm kwasababu zote zile, wagombea wale watakao kuwa wananyimwa nafasi kule kwenye kura za maoni itakuwa ni rahisi kwa wao ku run kama "independent candidate".

lakini kwa upande mngine kama taifa sidhani kama ni suala zuri sana, kwasababu mtu anapo run kama independent inamaana hana sera yeyote ya chama bali yeye ni kama mtu na wakati mwingine inakuwa ngumu kwa serikali inayokuwa madarakani kusikiliza sera za mtu mmoja maana hakuna uhakika kama anaongea yeye kuwawakilisha watu wale waliomchagua au anaongea yeye kama yeye,

kama taifa hii siyo isu ya kuisimamia sana ingawa inaweza kuwepo hapo kama kuwapa watu nafasi ya kupumua pale wanapokuwa wanadhulumiwa katika vyama vya siasa.
naomba niwakilishe.
 
Wazee!

Kwa mtizamo opposition wanatakiwa kujijenga kwaza katika grassroot level. Kama sikosei Mwalimu (RIP) alimshauri Mzee wa Kiraracha kugombea ubunge ule uchaguzi wa mwanzo wa multiparty. Opposition can learn a lot from Hamas and Hezbolah (not their armed wings) how the nanaged to win hearts and minds of of voters through their social services. Matokeo yake ikawa ni windfal win kwenye elections (Hamas in particular). Vyama vya upinzani viache kupoteza muda na urais waanzie na udiwani + ubunge as well as investing in winning hearts and minds through provision of social services in one way or another. Tanzania needs a strong oppoition to keep CCM on their heels!
 
Wangeruhusu private candidates ruzuku ingepoteza umuhimu wake wa kudaiwa na kuchimbuka vyama kemkem. Ukweli ni kuwa upinzani bado hauna nguvu na mchawi wa upinzani ni vyama vya upinzani vyenyewe. Kila mmoja wa wakuu wa vyama vingi yeye anachoona ni njia ya ikulu, hawakubali kuwachia kama wafanyavyo wenzao wa Chadema. Elewa Mrema leo hii akiahidiwa kungombea uraisi kwa tiketi ya CCM atarudi huko kwa spidi ya chui. Kwanini kwa sababu anajuwa uraisi kwa sasa unapatikana kwa tiketi ya CCM tu.
 
Chama cha CHADEMA na NPP cha Ghana ni vyama marafiki. Miongoni mwa mambo waiyoshirikiana ni pamoja na NPP kuwakaribisha CHADEMA kwenda Ghana kujifunza jinsi ya kuendesha siasa.
Somo linalopaswa kusomwa na watanzania ni jinsi Ghana inavyoendeshwa na NPP ili waweze kutabiri jinsi Tanzania itakavyoendeshwa iwapo wataipa CHADEMA dhamana ya kuongoza nchi.
Mfano mmojawapo ni huu hapa.


Ghana spends $1.4m on gold medals

By Will Ross
BBC News, Accra

John Kufuor has been compared to medallion-wearing rap star, 50 Cent
The Ghanaian government spent more than $1.4m (£704,000) buying 515 gold medals from a company based in the Channel Islands, officials have confirmed.

Almost half the medals were given out last week to prominent citizens at a colourful national awards ceremony.

The government says the rest will be presented over the next four years.

The medals are intended to reward outstanding contributions to Ghana. But critics say the money would have been better spent alleviating poverty.

Eighteen-carat gold

Recipients included politicians, chiefs, business leaders and even the country's President, John Kufuor, who will step down at the end of the year.

We are suffering. As of now, some of us cannot even pay our school fees

Accra businessman

He was given the highest award, the Grand Order of the Star and Eagles of Ghana.

Set in 18-carat gold, it was also the most expensive.

At $65,000 (£32,700), President Kufuor's award cost many times more than an Olympic gold medal.

This prompted one journalist to make a joke comparing Mr Kufuor to the medallion-wearing American rapper, 50 Cent.

Medals 'not extravagant'

As people woke up in Ghana to learn the cost of the medals from newspapers and radios, many were shocked and disappointed.

"We are suffering," one Accra businessman told the BBC. "As of now, some of us cannot even pay our school fees," he said.

How can the president decorate himself with such expensive jewellery when people are in dire need of basic amenities?

Dr Tony Aidoo
National Democratic Congress (NDC)

"The medals will not bring anything to the country," said another.

"They are just for individuals so the money has just gone to waste," he added.

The Deputy Information Minister, Frank Agyekum, disagreed.

"You can't put a price tag on an award which is meant to encourage, motivate and congratulate people for making a great contribution to the country," he said. "This was not extravagant."

"The remaining medals will be used for the next three to four years," he added, before noting that even beauty pageant winners are given a whole house these days.

Parliamentary enquiry

In recent years, the awarding of national honours has been a low key affair, but this year the government said it was keen to help unite the politically divided country.


Ghana is Africa's second biggest producer of gold

Politicians from rival parties were offered medals, but the opposition National Democratic Congress (NDC), boycotted the event.

Not surprisingly, the NDC is now making a noise about the cost of the awards

"This was a severe misplacement of priority and an insult to the intelligence of Ghanaians," said Tony Aidoo, a senior member of the party.

"How can the president decorate himself with such expensive jewellery when people are in dire need of basic amenities?" he asked, calling for a parliamentary enquiry, and for evidence that the remaining medals really exist.

Stability 'priceless'

The fact that the head of the Ashanti Kingdom, Asantehene Otumfuo Osei Tutu II, could not collect his award because he was mediating a chieftaincy dispute, shows the need for nation building in Ghana.

Peace and stability are priceless on the African continent

Bright Simons, Imani Centre for Policy and Education

"Peace and stability are priceless on the African continent," said Bright Simons, of the Ghanaian think tank, the Imani Centre for Policy and Education.

"If the process had succeeded in building a lot of reconciliation across the political spectrum, it would have been worth it," he added.

Mr Simons said the intention was honourable, but suggested the governing New Patriotic Party (NPP), could have managed the event better - by including members from across the political divide in an independent awards committee.

Ghanaians are also waiting to learn how the proceeds are spent from recently discovered oil in the country, estimated to total 2 billion barrels.

Those worried that Ghana may follow the lead of Angola and Nigeria will seek little comfort from news of how $1.4m has been spent on the medals. Some Ghanaians are also asking why the medals could not have been produced locally - especially as their country is Africa's second largest producer of gold.
 
Chama cha CHADEMA na NPP cha Ghana ni vyama marafiki. Miongoni mwa mambo waiyoshirikiana ni pamoja na NPP kuwakaribisha CHADEMA kwenda Ghana kujifunza jinsi ya kuendesha siasa.
Somo linalopaswa kusomwa na watanzania ni jinsi Ghana inavyoendeshwa na NPP ili waweze kutabiri jinsi Tanzania itakavyoendeshwa iwapo wataipa CHADEMA dhamana ya kuongoza nchi.
Mfano mmojawapo ni huu hapa.


Ghana spends $1.4m on gold medals
By Will Ross
BBC News, Accra



John Kufuor has been compared to medallion-wearing rap star, 50 Cent
The Ghanaian government spent more than $1.4m (£704,000) buying 515 gold medals from a company based in the Channel Islands, officials have confirmed.

Almost half the medals were given out last week to prominent citizens at a colourful national awards ceremony.

The government says the rest will be presented over the next four years.

The medals are intended to reward outstanding contributions to Ghana. But critics say the money would have been better spent alleviating poverty.

Eighteen-carat gold

Recipients included politicians, chiefs, business leaders and even the country's President, John Kufuor, who will step down at the end of the year.

We are suffering. As of now, some of us cannot even pay our school fees

Accra businessman

He was given the highest award, the Grand Order of the Star and Eagles of Ghana.

Set in 18-carat gold, it was also the most expensive.

At $65,000 (£32,700), President Kufuor's award cost many times more than an Olympic gold medal.

This prompted one journalist to make a joke comparing Mr Kufuor to the medallion-wearing American rapper, 50 Cent.

Medals 'not extravagant'

As people woke up in Ghana to learn the cost of the medals from newspapers and radios, many were shocked and disappointed.

"We are suffering," one Accra businessman told the BBC. "As of now, some of us cannot even pay our school fees," he said.

How can the president decorate himself with such expensive jewellery when people are in dire need of basic amenities?

Dr Tony Aidoo
National Democratic Congress (NDC)

"The medals will not bring anything to the country," said another.

"They are just for individuals so the money has just gone to waste," he added.

The Deputy Information Minister, Frank Agyekum, disagreed.

"You can't put a price tag on an award which is meant to encourage, motivate and congratulate people for making a great contribution to the country," he said. "This was not extravagant."

"The remaining medals will be used for the next three to four years," he added, before noting that even beauty pageant winners are given a whole house these days.

Parliamentary enquiry

In recent years, the awarding of national honours has been a low key affair, but this year the government said it was keen to help unite the politically divided country.


Ghana is Africa's second biggest producer of gold

Politicians from rival parties were offered medals, but the opposition National Democratic Congress (NDC), boycotted the event.

Not surprisingly, the NDC is now making a noise about the cost of the awards

"This was a severe misplacement of priority and an insult to the intelligence of Ghanaians," said Tony Aidoo, a senior member of the party.

"How can the president decorate himself with such expensive jewellery when people are in dire need of basic amenities?" he asked, calling for a parliamentary enquiry, and for evidence that the remaining medals really exist.

Stability 'priceless'

The fact that the head of the Ashanti Kingdom, Asantehene Otumfuo Osei Tutu II, could not collect his award because he was mediating a chieftaincy dispute, shows the need for nation building in Ghana.

Peace and stability are priceless on the African continent

Bright Simons, Imani Centre for Policy and Education

"Peace and stability are priceless on the African continent," said Bright Simons, of the Ghanaian think tank, the Imani Centre for Policy and Education.

"If the process had succeeded in building a lot of reconciliation across the political spectrum, it would have been worth it," he added.

Mr Simons said the intention was honourable, but suggested the governing New Patriotic Party (NPP), could have managed the event better - by including members from across the political divide in an independent awards committee.

Ghanaians are also waiting to learn how the proceeds are spent from recently discovered oil in the country, estimated to total 2 billion barrels.

Those worried that Ghana may follow the lead of Angola and Nigeria will seek little comfort from news of how $1.4m has been spent on the medals. Some Ghanaians are also asking why the medals could not have been produced locally - especially as their country is Africa's second largest producer of gold.


Unaona sasa kumbe CHADEMA ikiwa madarakani nchi itakuwa na matumaini.

Ona sisi chini ya CCM tunajadili uwizi wa EPA, Richmond, Kiwira na ununuzi wa Ndege ya Rais. Wenzetu wanajadili juu ya kununua medali za kutunuku watu waliofanya vizuri, sio kununua mitambo ya Richmond au ndege mbovu za ATCL.


Hii ni ishara kuwa Ghana wako mbele chini ya NPP.

Sasa umefungua mjadala- Tujadili miongo kadhaa ya utawala wa chama cha NDC ambacho kilihemea ikulu kama CCM ya Tanzania ambayo ni chama rafiki ya CCM ya Tanzania kilichokuwa chini ya Jerry Rawlings.

Halafu jadili miaka chini ya kumi ya utawala wa chama kidogo kilichokuwa cha upinzani cha NPP ambacho kiliiondoa serikali ya Rawlings madarakani kikiwa kidogo kuliko CHADEMA, John Koffour akaingia madarakani na kufanya makubwa ambayo chama cha NDC hakikuweza kufanya kama CCM ilivyoshindwa zaidi ya miaka 40 baada ya uhuru wa Tanzania.

Huyu ndiye Kufour aliyekataa anasa na kuuza ndege ya Rais alipoingia madarakani.

Hawa ndio marafiki wa karibu wa CHADEMA hapa Afrika, Chama cha NPP cha Ghana.

Asha
 
Unaona sasa kumbe CHADEMA ikiwa madarakani nchi itakuwa na matumaini.

Ona sisi chini ya CCM tunajadili uwizi wa EPA, Richmond, Kiwira na ununuzi wa Ndege ya Rais. Wenzetu wanajadili juu ya kununua medali za kutunuku watu waliofanya vizuri, sio kununua mitambo ya Richmond au ndege mbovu za ATCL.


Hii ni ishara kuwa Ghana wako mbele chini ya NPP.

Sasa umefungua mjadala- Tujadili miongo kadhaa ya utawala wa chama cha NDC ambacho kilihemea ikulu kama CCM ya Tanzania ambayo ni chama rafiki ya CCM ya Tanzania kilichokuwa chini ya Jerry Rawlings.

Halafu jadili miaka chini ya kumi ya utawala wa chama kidogo kilichokuwa cha upinzani cha NPP ambacho kiliiondoa serikali ya Rawlings madarakani kikiwa kidogo kuliko CHADEMA, John Koffour akaingia madarakani na kufanya makubwa ambayo chama cha NDC hakikuweza kufanya kama CCM ilivyoshindwa zaidi ya miaka 40 baada ya uhuru wa Tanzania.

Huyu ndiye Kufour aliyekataa anasa na kuuza ndege ya Rais alipoingia madarakani.

Hawa ndio marafiki wa karibu wa CHADEMA hapa Afrika, Chama cha NPP cha Ghana.

Asha

Asha sidhani kama umesoma vizuri habari yote ukaielewa, otherwise usingeweza kuunga mkono ufujaji wa serikali ya Ghana. Kumbuka pia extravagancy kumbwa zaidi ilifanyika kwenye sherehe ya miaka 50 ya uhuru. Hizi ni njia zinazotumiwa na NPP kudig deep into Ghanian reserves kwa ajili ya uchaguzi unaokuja later this year. Haya ndio waliyojifunza CHADEMA! na haya ndio mnayoyaunga mkono kina Asha!!!
 
Unaona sasa kumbe CHADEMA ikiwa madarakani nchi itakuwa na matumaini.

Ona sisi chini ya CCM tunajadili uwizi wa EPA, Richmond, Kiwira na ununuzi wa Ndege ya Rais. Wenzetu wanajadili juu ya kununua medali za kutunuku watu waliofanya vizuri, sio kununua mitambo ya Richmond au ndege mbovu za ATCL.


Hii ni ishara kuwa Ghana wako mbele chini ya NPP.

Sasa umefungua mjadala- Tujadili miongo kadhaa ya utawala wa chama cha NDC ambacho kilihemea ikulu kama CCM ya Tanzania ambayo ni chama rafiki ya CCM ya Tanzania kilichokuwa chini ya Jerry Rawlings.

Halafu jadili miaka chini ya kumi ya utawala wa chama kidogo kilichokuwa cha upinzani cha NPP ambacho kiliiondoa serikali ya Rawlings madarakani kikiwa kidogo kuliko CHADEMA, John Koffour akaingia madarakani na kufanya makubwa ambayo chama cha NDC hakikuweza kufanya kama CCM ilivyoshindwa zaidi ya miaka 40 baada ya uhuru wa Tanzania.

Huyu ndiye Kufour aliyekataa anasa na kuuza ndege ya Rais alipoingia madarakani.

Hawa ndio marafiki wa karibu wa CHADEMA hapa Afrika, Chama cha NPP cha Ghana.

Asha
Hamjaingia ikulu mnakula ruzuku za majimbo kwa ajili ya helikopta ya mtu mmoja. mkiingia IKULU mtaanza kununua AIRFORCE ONE.
 
sasa linakuja hili gazeti na hadithi ambayo ni pure uongo! Freeman ni CCM anyway, na anashinda kila siku na kina Kingunge, JM, Chenge, Kinana, Msekwa, Sitta, Rostam, na wengineo wote,

Mkuu FMES nimekua nikikuaminia sana linapokuja suala la Dataz, Lakini kwa hili nachelea kukubali moja kwa moja.Nadhani unapokua mwana siasa haina maana kuwa wewe na wale wanaotofautiana na misimamo yako ni maadui.Kukaa pamoja hakumaanishi yuko upande wao.
 
Hili gazeti lililoandika hii article lina utata kidogo, kwani linamilikiwa na baadhi ya viongozi wa CCM wasiokuwa Mtandao, kama uko bongo ukalifuatilia hili gazeti utagundua kuwa siku zote lina habari za ujanja ujanja,



Anyway my point ni kuwa hili gazeti na yale yote ya Mengi wakati umefika yanahitaji kufungwa!


Hii ni mwaka 2006 Jamani!

Eti FMES

Tanzania Daima inamilikiwa na wanamtandao haimilikiwi na Mbowe?

Halafu kwanini unadhani ni bora Tanzania Daima na Magazeti yote ya Mengi yafungiwe?

Yamefanya kosa gani?

Asha
 
Je, mambo yote yametokea kwa nasibu au ni mpango?

Hii habari ni ya mwaka 2006.

Mwishoni mwa mwaka huo 2006 ukasambaa waraka kwenye mtandao na baadaye ukaja hapa JF dhidi ya Mwenyekiti Mbowe. Mjadala ukawa mzito, hatimaye ukafa kifo cha mende. Wakati huo ukiwa ni tuhuma kwamba Mbowe amewahi kuvunja na kuiba benki kuu na pia amewahi kufanya biashara ya madawa ya kulevya.

Halafu 2007 ukafuata mjadala wa madeni ya Mbowe ambao 2008 ukajitokeza kurasa za mbele za magazeti ya Rai na Mtanzania chini ya maelekezo ya Rostam Aziz kwa Ballile. Kabla ya hapo ulitanguliwa na ule mjadala wa kwenye mtandao wa kumchafua Zitto Kabwe. Mara baada ya Orodha ya Mafisadi ukafuatia ule wa Kumchafua Dr Slaa kwamba ni muuji na kwamba ameshindwa upadre nk. Baada ya mjadala yote haya yakafa kifo cha mende.

Hii ni 2008 katika, mashambulizi dhidi ya Mbowe yamepanda kwa kiwango cha ziada, ujumbe mkuu ukiwa ni kuwa Mbowe ni kiongozi dhaifu, mbaguzi, mkabila na mbadhirifu wa matumizi ya ruzuku. Hata maamuzi yaliyofanywa na Kamati Kuu ya chama kwa uamuzi wa wajumbe wenyewe juu ya Chacha Wangwe yote yanaitwa kuwa ni ya Mbowe, yanaitwa ni shinikizo lake. Ndani ya tuhuma hizo kwa Mbowe, Dr Slaa naye anaingizwa kwa namna fulani fulani kuwa naye ni kiongozi mwenye kufanya maamuzi kwa ukanda na ni mbadhirifu wa ruzuku.

Je, matukio haya ni ishara ya udhaifu na uchafu wa Mbowe na Dr Slaa au kuna mpango na nguvu ya ziada ya kuwachafua?

Ndio maana nimeomba huu mjadala urudi hasa wakati huu ambapo CHADEMA inaelekea kwenda kujipanga vizuri zaidi.

I rest my case!

Asha
 
Dada Asha,

Unaweza kubomoa nyuma ambayo haijajengwa? (ze marcopolo)

Swali dogo tu.

Why not? Unaweza kubomoa mipango ya kuijenga, au unaweza kubomoa vifaa vya kujengea au unaweza kubomoa nyumba ambayo haijakamilika kujengwa au unaweza kuibomoa nyumba iliyojengwa kabisa. Yote ni kubomoa! Heheeeeeeeee.

Taking the anology of a house: Mbowe ni nyumba kwa sababu tayari ni Mwenyekiti wa chama na tayari alikuwa mgombea Urais tayari. Wewe umeshawahi kuwa hata katibu kata? CHADEMA ni nyumba, ni chama cha siasa chenye usajili wa kudumu, chenye wabunge na matawi sehemu mbalimbali nchini.

Satisfied?

Asha
 
Weak argument to make. Just because the two parties have an MoU doesn't mean that they have an identical modus operandi. Incidentally the ruling party and the Chinese communist party have had a more or less similar relationship for decades, does this mean that CCM will turn Tanzania into a communist/market socialist state?

In this present climate one has the all reasons to be cautiously aware of the nation's interest but there's no need to sensationalize things.
 
Weak argument to make. Just because the two parties have an MoU doesn't mean that they have an identical modus operandi. Incidentally the ruling party and the Chinese communist party have had a more or less similar relationship for decades, does this mean that CCM will turn Tanzania into a communist/market socialist state?

In this present climate one has the all reasons to be cautiously aware of the nation's interest but there's no need to sensationalize things.


oooohhhhhh Patpending

Rock them hard, they call themselves comrades of Mugambe and sister party to Zanu PF of Zimbambwe.

Asha
 
kama kuna mtu anastahili kulaumiwa sana kwa kuvurunda upinzani ni Mbowe. Alikuwa na nafasi kubwa sana mwaka jana kuweza kunyakua viti vingi zaidi lakini akapoteza nafasi hiyo kwa kujaribu kugombea Urais ambao alikuwa ana uhakika asingeupata. Sifikiri kama CCM ina sababu yoyote ya kumbomoa.. nadhani ameishajibomoa mwenyewe!!!!

Hasira ulikuwa nayo nadhani ulitamani kumpiga ..
 
Why not? Unaweza kubomoa mipango ya kuijenga, au unaweza kubomoa vifaa vya kujengea au unaweza kubomoa nyumba ambayo haijakamilika kujengwa au unaweza kuibomoa nyumba iliyojengwa kabisa. Yote ni kubomoa! Heheeeeeeeee.

Taking the anology of a house: Mbowe ni nyumba kwa sababu tayari ni Mwenyekiti wa chama na tayari alikuwa mgombea Urais tayari. Wewe umeshawahi kuwa hata katibu kata? CHADEMA ni nyumba, ni chama cha siasa chenye usajili wa kudumu, chenye wabunge na matawi sehemu mbalimbali nchini.

Satisfied?

Asha

Asha unatisha bibie, laiti wanachadema wengi wangekuwa na moyo na mwamko kama wewe, mbona kazi ya kuing'oa CCM ingekuwa "smuuzi".

Kwenu viongozi wa Chadema:
kuweni na umoja kuliko wakati wowote ule, hivi sasa hili tufani lililokikumba chama chenu si la kupuuzia na kuact "individually", wakishammaliza Mbowe msidhani imekwisha hiyo Watakumalizeni na nyinyi, huu ni wakati wa kumsaidia Mbowe na kuwa naye bega kwa bega.
 
MGOGORO wa uongozi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umenikumbusha enzi za Augustine Mrema na NCCR-Mageuzi. Kwa sababu hiyo, hatuwezi kuujadili mgogoro wa sasa wa CHADEMA bila kurejea yaliyotokea kwa NCCR-Mageuzi.

Na tukichunguza vema, tunagundua mambo kadhaa yanayotofautiana na kufanana katika migogoro hii miwili. Yote ni migogoro ya uongozi. Haya masuala ya ukabila, ruzuku, udini, ushushushu na mengine yaliyotamkwa na yanayotamkwa na baadhi ya washindani, ni baadhi ya kete tu za kisiasa, za kuwasaidia kuchochea hoja zao, kuamsha hisia za wafuasi wao na kukoleza mapambano.

Vumbi litakapokuwa limetua, chama kimepona au kimekufa, ndipo tutagundua kwamba suala halisi lilikuwa vyeo na madaraka. Hali halisi katika NCCR-Mageuzi imethibitisha hivyo. Bado tunakumbuka kuwa katika mgogoro wa NCCR-Mageuzi, Mrema na wafuasi wake, wakiwamo vinara na washauri wake wakuu, kina Prince Bagenda, Harold Jaffu, Thomas Ngawaiya na wengine; walisisitiza kuwa kisa cha ugomvi ni ruzuku ambayo walisema ilikuwa inatafunwa na viongozi wao wa Kamati Kuu chini ya Katibu Mkuu Mabere Marando.

Kauli hii imewakaa sana wananchi waliokuwa na imani isiyotetereka na Mrema, waliomwamini kama masiha ambaye neno lake lilikuwa msahafu kwao. Akitumia vizuri uzoefu wake wa propaganda alizozoea akiwa CCM, aliwanasa wengi. Alichosema kiliaminiwa kilivyo. Na wengine wameendelea kuamini maneno yake hata leo, kwamba alikuwa sahihi.

Lakini waliochunguza kiini cha mgogoro ule, wakazama katika historia ya chama chenyewe na jinsi Mrema alivyojiunga na kupewa madaraka papo hapo; wakatazama mwenendo wake wa kiuongozi (kiimla) na kuupima kwa ule alioukuta (mjadala na ushindani wa hoja na maamuzi ya pamoja vikaoni); wakachanganya na hasira za ‘kudharauliwa’ na wasomi sambamba na kushindwa urais (na wengine ubunge), huku wenzao wakiwa na nyadhifa mbili au tatu kwenye chama, ukiwamo ubunge (kabla yeye hajapata wa Temeke); wakimfuatilia mwenendo wake hata huko alikohamia baada ya kushindwa kuwafukuza wenzake kwenye chama, hawawezi kukubali propaganda za mgogoro wa ruzuku.

Ruzuku kilikuwa chambo. Ilikuwa kete. Leo, tuwaulize kina Bagenda, Jaffu na Ngawaiya kilichowasibu wakiwa na Mrema TLP. Ni matatizo yale yale ya uongozi. Tumuulize Leo Lwekamwa, mwasisi wa TLP aliyemkaribisha Mrema katika TLP na kumpa uongozi pale pale, halafu baadaye Mrema akamtimua hata kwenye nyumba yake iliyokuwa inatumika kama ofisi. Ni matatizo yale yale ya uongozi.

Tuwaulize wote waliowahi kufanya kazi kama makatibu wakuu chini ya Mrema wakiwa TLP - Bagenda, Jaffu na Hamad Tao. Kama watakuwa waungwana, watakiri makosa waliyotenda kwa kumsaidia Mrema kuivuruga na hatimaye ‘kuiua’ NCCR-Mageuzi; na watakubali kuwa kilichowakuta wao ndicho Marando na wenzake walipambana nacho kisiwatokee - kufukuzwa.

Lakini hatima ya yote, NCCR-Mageuzi ilipomsimamisha Mrema uenyekiti mnamo Februari 1999 katika kikao cha Halmashauri Kuu kilichofanyika Zanzibar, baadaye naye akahama chama kabla hajatimuliwa, madhara yaliyokuwa yamefanyika yalikuwa makubwa mno. Mrema alihama na wanachama wengi kwenda TLP. Wengine walikataa kumfuata, wakajiunga CUF. Wengine walirejea CCM. Wengine waliachana kabisa na siasa na upinzani hadi leo.

Ingawa wapo wanaosema CCM ndiyo iliwatumia waliogombana ili kukivuruga chama hicho, nadhani chimbuko la mgogoro halikutoka nje ya NCCR-Mageuzi. Kama CCM ilishiriki, ni katika kusukuma waliochuchumaa - wakaangukia pua! Ingawa Mrema alimshutumu sana Marando (na mashabiki wa Mrema wakaendelea kuamini hivyo hadi leo) kwamba alikuwa ametumwa na serikali kukivuruga chama hicho; ukweli ni kwamba Marando ndiye aliyekiasisi na wenzake kadhaa, wakati Mrema akiwa waziri wa serikali ya CCM, akiwatuma askari kuwapiga mabomu hata walipoandamana kupongeza ushindi wa Frederick Chiluba wa Zambia dhidi ya Rais Kenneth Kaunda.

Marando mwenyewe, ingawa alijua kuwa hata Mrema ni shushushu, hakumtuhumu Mrema kwa kutumwa na CCM wala serikali kuiua NCCR-Mageuzi, bali alidhani Mrema anatumia hulka yake, na papo hapo anatumiwa bila kujua. Lakini kwa kuwa Mrema alikuwa maarufu kuliko hata chama chake, umma wa wanachama uliamini kila kauli yake, maana ulimuona ni mkombozi, anayetaka kusafisha chama.

Naamini kwamba kama NCCR-Mageuzi isingesambaratika, mwisho wa CCM kutawala Tanzania ungekuwa mwaka 2000. Na inawezekana kama Mrema angekuwa na uvumilivu wa kufanya kazi na wasomi aliokuwa anawaogopa, akakubali maamuzi ya vikao, na akafanya kazi akiwa na timu ile aliyokuwa anataka kuiengua, angepata kura za kutosha mwaka 2000. Na haya masuala ya ufisadi wa EPA, Kiwira, Richmond na mengine tunayojadili leo, ama yasingekuwapo au yangekuwa ya viwango tofauti kabisa.

Lakini jeuri ya umaarufu ilimpa wafuasi ambao walimfikisha asikotaka. Tazama kilichotokea. Katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 1995, Mrema alipata asilimia 27.77 ya kura zote, akiwa wa pili nyuma ya Benjamin Mkapa. Alipogombea mwaka 2000 kwa tiketi ya TLP, aliambulia asilimia 7.80 akiwa wa tatu nyuma ya Rais Mkapa na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF. Mwaka juzi 2005, alipata asilimia 0.75, akiwa wa nne nyuma ya Jakaya Kikwete, Ibrahim Lipumba na Freeman Mbowe.

Haya ni matokeo ya mgogoro wa uongozi ndani ya NCCR-Mageuzi (1996-1999). Hadi sasa, miaka 10 ya ukombozi imepotea bure kwa sababu ya ugomvi wa madaraka yaliyoongozwa na Mrema, na kujibiwa na wenzake. Chama alichotaka kukikomboa ‘kimekufa’ na waliokigombania ‘wamekufa kisiasa’. Na ruzuku aliyotaka kuilinda haipo tena! Harakati zimedorora. Wanachama na Watanzania kwa jumla wamefaidika na nini katika ugomvi huu?

Jeuri ya CCM na uzezeta wa wananchi vimetawala nyanja za kisiasa kwa muda wote huo, kwa sababu wapambanaji walivutwa mashati, yakachanika na wengine wanachubuka vibaya. Ni bahati tu, kwamba katika miaka mitatu hii tangu mwaka 2005, kumetokea msisimko mpya wa kisiasa nchini mwetu ukiongozwa na CHADEMA kwa upande wa Tanzania Bara na CUF kwa upande wa Tanzania Visiwani. Mageuzi na mapinduzi ya kisiasa sasa yanategemea uhai wa vyama hivi.

Vita dhidi ya ufisadi nchini inategemea uhai wa vyama hivi na wote wanaoviunga mkono, hata wasio wanachama. Ukiwaondoa wale wanaofaidika na ufisadi wa serikali ya sasa na iliyopita, hakuna Mtanzania mwenye akili timamu angependa kuchochea mazingira ya kuharibu vyama hivi viwili.

Uwajibikaji wa serikali yetu unategemea uimara wa safu ya wapinzani bungeni na nje ya Bunge, wakishirikiana na wanaharakati mbalimbali katika asasi za kiraia na vyombo vingine vyenye wajibu wa kuimulika na kuisimamia serikali.

Lakini tunajua kuwa wakubwa hawataki kuona nguvu ya CUF wala ya CHADEMA. Hawataki kuona wananchi wanafumbuka macho kupambana na mafisadi walio madarakani. Gazeti hili lilishaandika kuhusu mbinu zilizoasisiwa Desemba 2005 dhidi ya CHADEMA, katika vikao vya siri vilivyofanyika Songea Mjini, Mkoa wa Ruvuma. Walishaanza kujiweka sawa kushambulia kutoka ndani na nje ya serikali na chama chenyewe wanachokilenga, wakakwama kwa muda, kwa sababu ufisadi uliwazunguka pande zote, na CHADEMA ikawa mstari wa mbele kuongoza vita ya ufisadi.

Wakati tunaanza kudhani kwamba labda Watanzania wamepata jukwaa jipya, upenyo wa kuingilia, kukuza harakati na kujenga uwanja mpana wa mapambano, kunajitokeza hiki kijimgogoro kinachomhusisha Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe na Kamati Kuu ya chama chake. Watanzania wenye nia njema na taifa hili hawawezi kudharau kijimgogoro hiki, na lazima wawaonye wanaokichochea kwenye chama na magazetini.

Ni kijimgogoro kinachotaka kutupeleka kule kule ilikoelekea NCCR-Mageuzi; kwenye kifo cha harakati za mageuzi. Ni kijimgogoro kinacholenga kusaidia ushindi wa mafisadi dhidi ya wananchi. Na katika mgogoro huu, sitaki kukituhumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) moja kwa moja. Lakini wana CHADEMA wasipokuwa makini, CCM itautumia mgogoro huu kuwagawa na kuwaua kisiasa.

Katika mazingira ya sasa, kwa mtazamo wangu, Wangwe anataka kurudia kosa la Mrema - kutanguliza ubabe binafsi, akisindikizwa na wapambe wenye maslahi na kifo cha harakati au baadhi ya viongozi wa harakati, na akitumia vibwagizo na vikolezo vya ‘kuokoa ruzuku’ na ‘kuondoa ukabila’ kama alivyofanya Mrema.

Hata kama chama kina matatizo kadhaa anayosema Wangwe, njia anzotumia ni za kukiua. Anapandikiza sumu ambayo anatakiwa kuwanywesha washindani wake, lakini haitawaacha pia wafuasi wake. Nina hakika Wangwe ana watu wanaoamini kauli zake, wanaomwongezea hamasa ya kuwavuruga viongozi wenzake, kwa sababu hataki kuonekana amekosea au ameshindwa. Lakini sidhani kama amepima vizuri nguvu zake, kwamba zinakaribia walau hata robo ya zile alizokuwa nazo Mrema, na kama zinatosha kuokoa anachokitetea. Mrema alikuwa na nguvu ya kitaifa, lakini alishindwa.

Namjua Wangwe. Ni rafiki yangu. Ni mpambanaji mwenzangu. Kwa hulka yake, hapendi na hakubali kushindwa. Wapo wanaomtuhumu, lakini kwa sasa siamini kama anatumika kuivuruga CHADEMA. Nionavyo mimi, Wangwe anajitumia - kama vile Mrema. Akifika viwango fulani vya kujitumia, wanaotaka kumtumia nao watajiingiza kwenye mgogoro, na watamtumia vizuri - hata kama hataki - maana sasa wanajiandaa, na wameshapima mwelekeo wa chama, na wanajua kwamba yeye hakubali kushindwa.

Naamini baadhi yao watakuwa ni wale wale waliokuwa wanamvizia katika viwanja ya Bunge Dodoma akiwa mbunge mpya mwaka 2006, wakitaka kumfunda jinsi ya kuwasilisha hoja zake bungeni. Wengine walifikia mahali pa kumshawishi ajiunge na CCM, kwa sababu hata wao waliwahi kuwa wapinzani wakaacha. Na mmoja aliyefanya hivyo, wakati huo, alikuwa serikalini!

Wakati ule, inasemekana Wangwe alitaka ‘kuwapiga’. Lakini sasa wanaweza kuwa jasiri, wasiogope kupigwa ngumi; wakaja kusaidia kuongeza nguvu. Mambo yatakapokuwa magumu, huku akifurahia sauti za wanaomuunga mkono, watamtumia kwa sababu wanajua anachokula, anachokunywa na kuvuta. Nikizichunguza kauli na mbinu za Wangwe, namuona Mrema wa NCCR-Mageuzi! Anagawa wanachama na kudhoofisha umoja wao. Nimesoma katika vyombo vya habari.

Wakati yeye anasema tatizo kubwa ni ruzuku (kuna mengine anayosema pia) ambayo anadai inaishia makao makuu, haipelekwi mikoani, katibu wake wa mkoani Mara, anakotoka yeye, anasema chama kinapokea ruzuku ya sh 400,000 kila mwezi. Sijui undani wa matumizi yao ya ruzuku, lakini naamini ni yale yale ya NCCR-Mageuzi.

Na wakiona la ruzuku halina nguvu za kutosha watasema ukabila (kwa maana wanayoijua wao). Wakiona hilo bado halijasaidia sana, watajadili utajiri na umaskini wa baadhi ya viongozi au wanachama, nani anachangia sana, nani ananyonya wenzake; ilimradi wapate kete ya kutumia kwenye mapambano ya kupata madaraka katika chama.

Lakini madaraka hayatawasaidia wananchi kama yatakuwa sawa na yale aliyopata Mrema TLP baada ya kusambaratisha NCCR-Mageuzi. Katika mgogoro wa NCCR-Mageuzi, wapambanaji wa pande zote mbili walikuwa wanajitapa kwamba wanafanya hivyo kukinusuru chama. Wengine walidai wanatetea demokrasia ndani ya chama. Wengine wakasema wanataka kuondoa magugu. Wengine walidai wanataka kulinda ruzuku ya chama. Wengine wakasema wanataka kukirejesha chama kwa wanachama, kukipa nguvu ya kupambana na CCM.

Mwisho wa yote, hakuna aliyekijenga chama. Walionyesha umahiri wa kurusha vijembe na kukusanya makundi ya wafuasi nyuma yao. Demokrasia haikurejea. Ruzuku ilibaki midomoni mwao; haikupatikana tena, maana chama kilikosa vigezo vya kupata ruzuku. Chama hakikurejea kwa wanachama, maana wengi walihama TLP na CUF; wengine wakarejea CCM, na wengine wakaacha siasa kabisa.

Hivi ninavyoandika, wengine wako CHADEMA. Na baadhi yao wamekuwa vinara wa kuanzisha migogoro mipya kwa visingizio vile vile vya zamani. Baada ya mgogoro, NCCR-Mageuzi haikupata tena nguvu ya kuikabili CCM, na taratibu kilipoteza wabunge wake wote, maana umma haukuiunga mkono tena.

Je, hawa wanaoanzisha makundi ndani ya CHADEMA wanataka kurudia historia ya NCCR-Mageuzi? Wanadhani kunguru huyu anayeitwa CCM amelala usingizi kiasi cha kushindwa kuona kwamba pembeni mwake kuna panzi wanono wanapigana vita ya wenyewe kwa wenyewe? Wataruhusiwa kumpa fursa kunguru huyu avune asichopanda? Kwa mtazamo wangu, CHADEMA ni mimba. Haijazaliwa. Ni mimba ya mwanamke aliyekuwa anadhaniwa tasa. Ni mimba ya uzeeni. Ole wake anayetaka kuiangamiza ikiwa tumboni mwa mama. Ole wake anayetaka kuua mama na mimba yake!
CHADEMA imejifunza nini katika migogoro ya waliotangulia? Ole wake kama haikujifunza, na kama itajiachia iuawe na wale wale walioshiriki kuijenga.

Inawezekana Watanzania walishamsamehe Mrema na wenzake kwa kilichotokea NCCR-Mageuzi na kwingine. Lakini sidhani kama wako tayari kumsamehe yeyote atakayejitokeza leo kuiua CHADEMA na kuzorotesha harakati za sasa dhidi ya ufisadi, na chachu ya harakati za kifikra kuelekea mageuzi makubwa ya kimfumo katika taifa.

Wangwe, akiwa nguzo ya CHADEMA jimboni mwake Tarime, angefanya kazi moja ya msingi. Kuieneza CHADEMA mkoani Mara, na kuiondoa katika eneo moja (Tarime), hasa kwa kuwa ana nafasi ya uenyekiti wa mkoa huo. Awaunganishe wana Mara katika mapambano, kile kilichotokea Tarime kisambae mkoa mzima. Lakini anaonekana kupenda siasa za makao makuu ambazo asipochunga vizuri, zinaweza kumgharimu hata ubunge wake hapo baadaye.

Ajifunze. Viongozi wa NCCR-Mageuzi walikalia mgogoro makao makuu wakasahau majimbo yao. Hawakurudi bungeni katika kipindi kilichofuata. Walishiba ushabiki wa wafuasi na vichwa vya habari magazetini. Lakini walipoteza hata ngome chache walizokuwa wamepata mwaka 1995.

Wangwe alikuwa NCCR-Mageuzi. Anayajua hayo, lakini hataki kusikiliza ushauri wala maamuzi ya vikao vya chama. Hata kama anadhani hakupewa fursa ya kusikilizwa vizuri vikaoni, ana fursa ya vikao vingine kujitetea. Lakini hii tangatanga yake ninayoiona katika vyombo vya habari, tena vyombo vyenyewe anavyotumia ni vile vinavyotetea CCM na watu wake, naamini anajiingiza katika kosa la kifundi, na kujiweka katika mazingira ya kutumiwa.

Kama vyombo vya habari havikumsaidia Mrema wala NCCR-Mageuzi, havitamsaidia Wangwe wala CHADEMA. Ushauri wangu nauelekeza kwa Wangwe kwa sababu ndiye anayepambana na Kamati Kuu ya chama chake! Itamshinda. Na itamdhuru kisiasa.

Anapaswa kujua hilo na kuwa tayari kukubali hukumu ya kamati kuukosa umakamu mwenyekiti. Akubali kufa kama Socrates, mwanafalsafa wa Kigriki aliyekubali kunywa sumu, si kwa sababu aliipenda au alitendewa haki, bali kwa sababu alisema amehukumiwa (vibaya) na demokrasia ile ile aliyokuwa anaitetea. Kama imekosea, si tatizo, bali kwamba hukumu yake imefanyika kidemokrasia! Akanywa sumu kwa heshima ya demokrasia.

Ningetarajia Wangwe aonyeshe ukomavu wa kisiasa na haiba ya uongozi kwa kupokea maamuzi ya Kamati Kuu ya chama chake, hata kwa shingo upande. Huu si wakati wa nyota yake kisiasa kuzimika kama ilivyokuwa ya Mrema. Huu si wakati wa yeye na wenzake kugawanyika na kutawanyika, bali kuwa wamoja.

Mhandisi mjasiriamali mahiri wa karne ya 20 nchini Marekani, Henry Ford, aliwahi kusema: “Kujumuika ni mwanzo, kuendelea kukaa pamoja ni hatua, na kufanya kazi pamoja ni mafanikio.”

Ford hakuwa anawaambia CHADEMA kwa sababu hawakuwapo wakati huo. Hata kama wangekuwapo, labda asingewajua. Lakini ukweli wa kauli yake unawahusu leo katika mazingira waliyomo. Ole wao CHADEMA wakikubali kushindwa, wakaanguka, na kusambaratika.

Wanaweza kuamua kuendelea kulumbana kupitia vyombo vya habari. Kama hawajui vizuri namna ya kufanya hivyo, wawaulize NCCR-Mageuzi walifanyaje. Au wakubali kuchukua hatua za msingi na kumaliza mgogoro kabisa. Uongozi wa CHADEMA lazima uchukue hatua na uzisimamie. Bila shaka wanao wataalamu wa uongozi na utatuzi wa migogoro. Kama hawana, watafute washauri wa kitaaluma katika migogoro wawasaidie kumalizana na ujinga huu unaojitokeza sasa. Na kama wanao, wawatumie sasa.

Zipo mbinu nyingi za kukabiliana na migogoro, lakini dhana moja muhimu inayotumika ni ile ya Thomas-Kilman, inayopendekeza njia tano za kutatua migogoro kwa kutegemea aina ya mgogoro wenyewe. Kwa Kiswahili rahisi, tunaweza kuziita kuwa ni njia kumbativu, shirikishi, shindani, nipe nikupe, na kupuuza.

Kama mgogoro ni mdogo, yapo mambo mengine ya muhimu zaidi ya kushughulikia, na kama kiongozi anahitaji muda kukusanya vielelezo vya kutosha, na kama ana nia ya kuwapa fursa watu washushe munkari ili jambo lijadiliwe bila jazba hapo baadaye, na hasa kama kiongozi hataki lawama; njia mwafaka ni ile ya kupuuza mgogoro kwa muda, au hata ikibidi kuwaachia wengine wautatue, ambao anadhani wanaweza kuliko yeye. Lakini hii ni mbinu ya viongozi dhaifu. Je, njia hii iliwafaa CHADEMA?

Iwapo nia ni kumpa mshindani fursa ya kushinda, iwapo azma ya kuleta amani na mwafaka ni muhimu kuliko ushindi, iwapo kiongozi anataka baadaye naye kupata hisani kutoka kwa mshindani wake, na iwapo ushindi wa upande mwingine ni muhimu zaidi, na iwapo uongozi uko tayari kupoteza ili upande shindani upate; njia mwafaka ya kutatua mgogoro ni kumbativu; kukubali mwingine ashinde. Je, njia hii iliwafaa CHADEMA?

Kama pande zinazohusika zinavutana mno kwa hoja kali na za msingi, na hakuna aliye tayari kukubali kupoteza, na kama hoja za pande zote lazima ziingizwe katika kutafuta ufumbuzi wa mgogoro, na hasa kama kuna haja ya kupoza hisia binafsi zinazotokana na washiriki wakuu wa mgogoro katika pande zote; njia mwafaka ya kutumia ni shirikishi ili kupata ufumbuzi bora. Je, njia hii iliwafaa CHADEMA?

Iwapo gharama ya kushindwa ni ndogo kuliko ya kukuza mgogoro, na iwapo washindani wana nguvu sawa, na lazima ufumbuzi upatikane haraka kwa sababu muda unawatupa mkono, na kama hata njia shirikishi haikufaulu; njia mwafaka inayohitajika hapa ni ile ya nipe nikupe. Kila mtu anakubali kupoteza kitu - kama walivyofanya Raila Odinga na Mwai Kibaki wa Kenya. Na labda ndiyo iliwafaa CCM na CUF katika mazungumzo ya mwafaka. Je, njia hii iliwafaa CHADEMA?

Na iwapo lazima ufumbuzi unahitaji haraka ili kuyapa nafasi masuala mengine yaliyo muhimu zaidi kwa jamii au taasisi, iwapo uongozi unahitaji kuweka msimamo wazi na imara, iwapo uamuzi unapaswa kuzima mtu au watu wanaotumia fursa kuvuruga na kuyumbisha msimamo; na kama nia ya uamuzi ni kurejesha nidhamu na kusisitiza kanuni, sheria na sera zifuatwe; njia mwafaka ya kutumia ni ile shindani, ambayo kawaida hutumiwa na walio na madaraka, vyeo au ujuzi unaohitajika kabla mambo hayajaharibika.

Nadhani hii ndiyo ilitumika dhidi ya Rais wa Zanzibar, Aboud Jumbe na Waziri Kiongozi, Seif Shariff Hamad (ndani ya CCM). Je, hii ndiyo iliwafaa CHADEMA?

CHADEMA ichukue hatua sasa. Iwadhibiti mamluki wa ndani na nje. Hata ikibidi, wafukuzane. Heri kelele ziendelee nje ya chama, lakini uwanja wa wananchi kupambana na mafisadi ubaki. Wasipoyafanya haya; wakaoneana aibu na kuwafaidisha mafisadi, hakuna atakayewasamehe kwa kosa la kutotenda.

Ni kweli chama kinakua, na migogoro itaongezeka. Uwezo wa kutatua migogoro hiyo ndiyo mtihani ambao jamii inasubiri kuona katika vichwa na mikono ya viongozi wa sasa wa CHADEMA. Chama ambacho kimeongoza mapambano na kimekuwa kinamlaumu Rais Kikwete kwa kushindwa kuchukua hatua kali dhidi ya viongozi wanaovurunda, lazima kionyeshe kwamba kinaweza kuchukua hatua bila kujali kelele za waombolezaji na waviziaji.

+447853850425
ansbertn@yahoo.com
www.ngurumo.blogspot.com
 
BILA ya shaka, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapita katika wakati mgumu hivi sasa katika historia yake kisiasa. Mgogoro ulioibuliwa na aliyekuwa Makamu mwenyekiti wake, Chacha Wangwe, unaonyesha dhahiri jinsi chama hicho kinavyopita katika tanuru la moto la kisiasa.

Na mimi nimeamua kuwashangaa na nina sababu kadhaa za kuwashangaa CHADEMA; kubwa ni kuwa nionavyo mimi, matatizo haya wamejitakiwa wenyewe. Hawana mtu wa kumlaumu zaidi yao wenyewe kwa sababu Wangwe hakujipachika hayo madaraka.

Sababu nyingine inayonifanya niwashange ni jinsi wanavyolishughulikia suala la Wangwe. Wamemsimamisha kwa sababu amekosa sifa za kuwa makamu mwenyekiti. Sawa. Lakini hii ni nafasi ya uongozi ambayo sifa za msingi za mtu atakayeishika, ni sifa za msingi za kiongozi anayeshika nafasi yoyote ile.

Mantiki inanifanya niamini kuwa iwapo mtu ataonekana hana sifa za kushika nafasi hiyo ya uongozi, mtu huyo hawezi kuaminiwa kushika nafasi nyingine ya uongozi. CHADEMA wametaka kutuaminisha kuwa Wangwe amepoteza sifa za kuwa makamu mwenyekiti wa taifa wa chama hicho. Lakini wakati huo huo, CHADEMA hao hao wanataka kutuaminisha kuwa Wangwe ana sifa za kuwa Mwenyekiti wa chama hicho katika ngazi ya mkoa, nafasi ambayo bado inamfanya awe mjumbe wa vikao vya juu vya chama hicho.

Kamati Kuu ya CHADEMA ilifikia uamuzi wa kumwondoa Wangwe kwenye nafasi hiyo, kutokana na tuhuma nne nzito.

Moja, Wangwe alituhumiwa au anatuhumiwa kujihusisha na au kushiriki katika vikundi na au vitendo vya uchonganishi na au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa chama na au wanachama wake.

Pili, anatuhumiwa kutoa tuhuma nzito lakini zisizokuwa na msingi dhidi ya viongozi wenzake wa kitaifa na watendaji wa chama pasipo kupitia vikao halali na wala kuzingatia taratibu za chama.

Tatu, Wangwe ana tuhuma za kukikashifu chama chake, viongozi na watendaji wake, bila kutofautisha kashfa na ukosoaji wa kisiasa na au wa kiutendaji.

Na mwisho, Wangwe ameingia matatizoni kutokana na tuhuma za kuvujisha siri za vikao halali vya chama kwa watu wanaotaka kuhujumu chama.

Mlolongo wa tuhuma hizi ulisomwa kwa waandishi wa habari mjini Dodoma Jumapili, Juni 29, mwaka huu, na Mkurugenzi wa Sheria na haki za Binadamu wa chama hicho, Tundu Lissu, ambaye ni mmoja wa marafiki wa karibu wa Wangwe.

Lakini kama wanavyosema wahenga, si vema kumtuhumu mtu na kutompa nafasi yaa kujielezea au kujirekebisha, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema katyika mkutano huo wa waandishi wa habari kuwa jitihada zilikuwa zimefanywa kumrudisha Wangwe kwenye mstari, lakini ikashindikana.

Moja kati ya mambo yaliyofanyika ni kuendeshwa kwa vikao mbali mbali na vya muda kati ya Wangwe, Mwenyekiti Taifa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, kujadili tofauti na migongano kati yao ndani ya chama.

Pia ilifikia hatua ya pande zinazokinzana na Wangwe ndani ya chama hicho kusuluhishwa na kamati ya wazee wa chama ambapo Wangwe alitakiwa kuandika maandishi kwamba ataacha vitendo vyake dhidi ya chama, viongozi wa kitaifa na watendaji wa chama.

Kana kwamba hiyo haitoshi, Kamati Kuu ya chama ilimuonya na kumtaka kuacha vitendo vyake hivyo dhidi ya chama. Lakini baada ya jitihada zote hizi kushindikana, Kamati Kuu ilimsihi kujiuzulu kwa hiari yake yeye mwenyewe na hivyo kujiepusha na adha ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na kusimamishwa na Kamati Kuu.

Lakini ukitazama kwa makini, hata kwa haraka haraka utabaini mambo mawili makubwa. Kwanza, tuhuma zinazoshushwa kwa Wangwe ni nzito sana na pili, kwa mujibu wa tuhuma hizo, tabia hii ya Wangwe haikuzuka tu ghafla. Tuhuma zinaonyesha kuwa ni tabia yake ambayo anaishi nayo.

Kama ndivyo hivyo, hapa ndipo nilipoanza kuwashangaa CHADEMA na sikuficha mshangao wangu, wakati wa mkutano huo wa waandishi wa habari na kumhoji Mbowe, kwa nini watu makini waliopo CHADEMA walishindwa kuzitambua tabia hizi za Wangwe na wao wenyewe, kwa kutumia utaratibu mahsusi, walipitisha Wangwe awe makamu mwenyekiti wao?

Ninaushangaa umakini wa viongozi wa CHADEMA kwa sababu Wangwe hakuibuka ghafla na matatizo yake. Ni mtu anayefahamika kwa historia yake na hivyo, CHADEMA walipaswa kuwa makini sana walipomuona akiingia chamani, au walipoamua kumfuata aingie kundini.

Tabia hizi za Wangwe zilipaswa kuwapa viongozi wa CHADEMA mkakati wa kudumu wa kufanya kazi pamoja na mtu wa aina ya Wangwe.

Walipomchagua kuwa makamu mwenyekiti, mimi niliamini kuwa wanao mkakati huo na sikudhani hata mara moja kuwa wanaweza kugeukana baada ya muda mfupi namna hii.

Njia walizotumia kumrudisha Wangwe kwenye mstari zinafaa zaidi kama njia za ndani ya chama. Lakini sasa mgogoro huu umetoka nje ya chanma na Wangwe, ili kujihakikishia uhalali wa anayoyasema na kuyasimamia, ametoa tuhuma nzito dhidi ya chama hicho.

Hivi sasa, wakati CHADEMA walizungumzia madhambi ya Wangwe, watu wengine wanazungumzia tuhuma zilizotolewa na Wangwe dhidi ya chama hicho. Kuna masuala ya matumizi ya ruzuku na tuhuma za ukabila.

Haya yote yameshatolewa maelezo ya kina na viongozi wa CHADEMA lakini inaonekana kuwa tuhuma hizi hazitaki kuondoka. Wangwe anahusisha pia kampeni za uchaguzi ndani ya chama hicho na mambo yanayotokea hivi sasa. Anasema kuwa amefukuzwa kama sehemu ya kumchafua baada ya kubainika kuwa ana nia ya kuopambana na Mbowe kuwania uwenyekiti wa CHADEMA.

Kuna mambo mawili ambayo viongozi wa CHADEMA wanaweza kuyafanya ili kukabiliana na hali hii. Kwanza ni kujitahidi kutoa ufafanuzi wa kina zaidi kuhusiana na tuhuma zinazoelekezwa kwake na Wangwe.

Katika kufanya hili, Wangwe alionekane kama mtuhumiwa aliyekwishahukumiwa. Maelezo yatakayotolewa ndiyo yalenge kumfanya Wangwe aonekane kuwa ni mtuhumiwa ambaye ameshahukumiwa.

Lengo kuu lisiwe kupambana na Wangwe moja kwa moja. Lengo liwe ni kukabili makombora ya Wangwe. Iwapo itathibitika kuwa makombora hayo yalikuwa ni tuhuma zisizo na msingi, ni rahisi sana kumdharau aliyeyatoa. Hapo Wangwe atakuwa amejimaliza kwa silaha zake mwenyewe.

Lakini iwapo ushauri huu utaonekana haufai, ni vema wakafuata ushauri wangu mwngine ambao unatokana katika maandiko matakatifu. Na utekelezaji wa ushauri huu utanifanya niache kuwashangaa kwa kumwacha Wangwe aendelee kushika uongozi ndani ya chama hicho wakati akikabiliwa na tuhuma zilizompotezea sifa za kuwa kiongozi.

Ushauri huo unatoka katika Biblia Takatifu, katika kitabu cha Mtakatifu Mathayo, sura ya tano kuanzia mstari wa 30 ambako Yesu aliwafundisha wanafunzi wake akiwaambia; ‘Na mkono wako wa kuume ukikukosesha ukate uutupe mbali, kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee, wala mwili wako mzima usitupwe jehanamu.
 
Asha
Kweli inatusikitisha sana kwa haya yanayotokea ktk chama hiki chenye mtizamo chanya,Wangwe naona amejisahau, unajua uvumilivu ni jambo la heri sana kuliko kupayuka bila mtizamo wa siku za usoni, sisi hapa tarime tulimuamini tukamtuma aende bungeni akatuwakilishe na kutatua kero zetu kule bungeni ila yeye amesahau, naona kama matatizo yetu ameyapeleka chamani badala ya bungeni,

Tulitegemea chacha apeperushe bendera ya wana Mara vema kama vile watangulizi wake walivyofanya ila yeye ametusaliti sisi na mkoa wake, ajue CHADEMA ndiyo chama mbadala na yale mapungufu aliyoyakuta wangeyalekebisha pole pole,
Hakika tunashangazwa na huyu ndugu yetu.

Bado Chacha hajachelewa hata kidogo tunamuomba afunge mdomo wake kisha akiombe chama msamaha kisha asonge mbele.

Ama yawezekana ana ndoto za kuwa President? asisahau ana miaka 5 tu hapo mbele na kama ataendelea kujadili kuhusu chama na kutusahau sisi wananchi kero na matatrizo yetu , tutamsubili 2010.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom