Revolutionary
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 456
- 86
Mimi ni mtanzania niliyeichoka CCM, na siamini kama kwelli watanzania tunataka maendeleo kuichekea CCM iendelee kushika hatamu ya nchi.
Kwa kuwa suala la CCM kuondoka madarakani ni lazima, sasa mbadala wake ni Chadema, chama ambacho kinaonesha matumaini makubwa kwa watanzania, chama kinachofumua mengi ambayo watanzania tulikuwa tumefumbwa macho na kutawaliwa kama mazezeta huku tukiambiwa nchi yetu ni maskini.
Bila shaka nina imani kubwa na Chadema katika kuikomboa nchi hii, na sina shaka kama si 2015 basi very soon Chadema kitachukua uongozi wa juu kabisa wa nchi , yaani uraisi na kuongoza nchi.
Tunapozungumzia haya ni Chadema kitatoa watendaji wote wakuu na muhimu pindi kitakaposhika madaraka ya nchi.
Yaani kuanzia
- mawaziri
- makatibu,
- wizara,
- Mabalozi
- wakuu wa idara mbalimbali,
- mahakimu,
- wakuu wa mikoa na wilaya.
na wengineo wengi kwa ukubwa wa serikali yetu, tokea wizara, kanda mikoa hadi wilaya.
Suala ambalo hula linanijia kichwani mara kwa mara ni KUPWAYA kwa Chadema katika kusimamisha serikari hiyo. Na kwa kuwa mimi hufikiria mbele zaidi na napenda sana kuwa realistic huwa naichukua Chadema namna hii na naitapanya katika serikali kwa ukubwa wake, kwa kweli naona inapwaya, Haswa ukuzingatia kwamba chama hakijajikita katika katika kurecruit wanachama katika ngazi zote za ukubwa wa nchi.
Chadema kinapwaya si kwa sababu hakina viongozi na wanachama makini na wachapakazi la hasha, Chama kina watu makini, (Kuanzia, Dr Slaa, Mbowe, Tundu Lisu, Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika, Godbless Lema na wengineo wengi) la hasha bali viongozi hawa makini na wenye uwezo mkubwa hawatoshi kufit katika nyadhifa na idara zote na kutengeneza serikali yenye ufanisi na kasi moja. kimsingi kwa idadi yao wanapwaya.
Ukichukulia mfano tu ile kambi ya upinzani bungeni, inayoongozwa na Mbowe, mgawanyo wamawaziri kivuli katika wizara kivuli hizo ambao ndio unatoa picha ya nani atashika nafasi gani kama Chadema itashika madaraka, waliochaguliwa utagundua kabisa kuwa Chadema hakuna NGUVU KAZI YA KUTOSHA. Kuna wengi ambao ni makini lakini sio 'the best' we can get kwa ajili ya kusimamia maendeleo ya taifa kwa ukubwa wake.
Wako wanaoweza kuwa mawaziri na viongozi makini sehemu mbali mbali serikalini, kama Zitto Kabwe, Tundu Lissu, Mnyika kiasi, Mbowe, Mdee kiasi........kimsingi hata ninavyoitaja hii list unaona kabisa kwamba tunarun out of options.....nguvu kazi inayohitajika haitoshi. Iitakapokuja katika suala la kuteua Nguvu Kazi kwa ajili ya nyadhifa zote kwa ukubwa wake, naona Chadema inapwaya. Labda waje kutumia kujuana, kitu ambacho hakitaleta tija katika maendeleo (najua Chadema haitafanya hivyo).
Nadhani, Suala la kurecruit wanachama wapya linahitajika kufanyika, tena kila sehemu hadi vijijini, Chama kirecruit wachapakazi, wanachama makini, kitoe mafunzo na warsha mbalimbali ili kuinspire vijana wengi zaidi na kupata nguvu ya kutosha kuendesha nchi wakati utakapofikia. Bila hivyo kwa kweli naona Chadema kinapwaya jamani, hebu nyie wenyewe semeni.
Kwa kuwa suala la CCM kuondoka madarakani ni lazima, sasa mbadala wake ni Chadema, chama ambacho kinaonesha matumaini makubwa kwa watanzania, chama kinachofumua mengi ambayo watanzania tulikuwa tumefumbwa macho na kutawaliwa kama mazezeta huku tukiambiwa nchi yetu ni maskini.
Bila shaka nina imani kubwa na Chadema katika kuikomboa nchi hii, na sina shaka kama si 2015 basi very soon Chadema kitachukua uongozi wa juu kabisa wa nchi , yaani uraisi na kuongoza nchi.
Tunapozungumzia haya ni Chadema kitatoa watendaji wote wakuu na muhimu pindi kitakaposhika madaraka ya nchi.
Yaani kuanzia
- mawaziri
- makatibu,
- wizara,
- Mabalozi
- wakuu wa idara mbalimbali,
- mahakimu,
- wakuu wa mikoa na wilaya.
na wengineo wengi kwa ukubwa wa serikali yetu, tokea wizara, kanda mikoa hadi wilaya.
Suala ambalo hula linanijia kichwani mara kwa mara ni KUPWAYA kwa Chadema katika kusimamisha serikari hiyo. Na kwa kuwa mimi hufikiria mbele zaidi na napenda sana kuwa realistic huwa naichukua Chadema namna hii na naitapanya katika serikali kwa ukubwa wake, kwa kweli naona inapwaya, Haswa ukuzingatia kwamba chama hakijajikita katika katika kurecruit wanachama katika ngazi zote za ukubwa wa nchi.
Chadema kinapwaya si kwa sababu hakina viongozi na wanachama makini na wachapakazi la hasha, Chama kina watu makini, (Kuanzia, Dr Slaa, Mbowe, Tundu Lisu, Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika, Godbless Lema na wengineo wengi) la hasha bali viongozi hawa makini na wenye uwezo mkubwa hawatoshi kufit katika nyadhifa na idara zote na kutengeneza serikali yenye ufanisi na kasi moja. kimsingi kwa idadi yao wanapwaya.
Ukichukulia mfano tu ile kambi ya upinzani bungeni, inayoongozwa na Mbowe, mgawanyo wamawaziri kivuli katika wizara kivuli hizo ambao ndio unatoa picha ya nani atashika nafasi gani kama Chadema itashika madaraka, waliochaguliwa utagundua kabisa kuwa Chadema hakuna NGUVU KAZI YA KUTOSHA. Kuna wengi ambao ni makini lakini sio 'the best' we can get kwa ajili ya kusimamia maendeleo ya taifa kwa ukubwa wake.
Wako wanaoweza kuwa mawaziri na viongozi makini sehemu mbali mbali serikalini, kama Zitto Kabwe, Tundu Lissu, Mnyika kiasi, Mbowe, Mdee kiasi........kimsingi hata ninavyoitaja hii list unaona kabisa kwamba tunarun out of options.....nguvu kazi inayohitajika haitoshi. Iitakapokuja katika suala la kuteua Nguvu Kazi kwa ajili ya nyadhifa zote kwa ukubwa wake, naona Chadema inapwaya. Labda waje kutumia kujuana, kitu ambacho hakitaleta tija katika maendeleo (najua Chadema haitafanya hivyo).
Nadhani, Suala la kurecruit wanachama wapya linahitajika kufanyika, tena kila sehemu hadi vijijini, Chama kirecruit wachapakazi, wanachama makini, kitoe mafunzo na warsha mbalimbali ili kuinspire vijana wengi zaidi na kupata nguvu ya kutosha kuendesha nchi wakati utakapofikia. Bila hivyo kwa kweli naona Chadema kinapwaya jamani, hebu nyie wenyewe semeni.