Nina mashaka na uwezo wa CHADEMA kuongoza SERIKALI 2015

Inabidi urekebishe heading yako maana wengine tunashindwa kuelewa kama unauliza swali toka kwa wana JF au unawakilisha mashaka yako kuhusu CHADEMA kukamata dola 2015.
 
Mimi ni mtanzania niliyeichoka CCM, na siamini kama kwelli watanzania tunataka maendeleo kuichekea CCM iendelee kushika hatamu ya nchi.

Kwa kuwa suala la CCM kuondoka madarakani ni lazima, sasa mbadala wake ni Chadema, chama ambacho kinaonesha matumaini makubwa kwa watanzania, chama kinachofumua mengi ambayo watanzania tulikuwa tumefumbwa macho na kutawaliwa kama mazezeta huku tukiambiwa nchi yetu ni maskini.

Bila shaka nina imani kubwa na Chadema katika kuikomboa nchi hii, na sina shaka kama si 2015 basi very soon Chadema kitachukua uongozi wa juu kabisa wa nchi , yaani uraisi na kuongoza nchi.

Tunapozungumzia haya ni Chadema kitatoa watendaji wote wakuu na muhimu pindi kitakaposhika madaraka ya nchi.
Yaani kuanzia
- mawaziri
- makatibu,
- wizara,
- Mabalozi
- wakuu wa idara mbalimbali,
- mahakimu,
- wakuu wa mikoa na wilaya.
na wengineo wengi kwa ukubwa wa serikali yetu, tokea wizara, kanda mikoa hadi wilaya.

Suala ambalo hula linanijia kichwani mara kwa mara ni KUPWAYA kwa Chadema katika kusimamisha serikari hiyo. Na kwa kuwa mimi hufikiria mbele zaidi na napenda sana kuwa realistic huwa naichukua Chadema namna hii na naitapanya katika serikali kwa ukubwa wake, kwa kweli naona inapwaya, Haswa ukuzingatia kwamba chama hakijajikita katika katika kurecruit wanachama katika ngazi zote za ukubwa wa nchi.

Chadema kinapwaya si kwa sababu hakina viongozi na wanachama makini na wachapakazi la hasha, Chama kina watu makini, (Kuanzia, Dr Slaa, Mbowe, Tundu Lisu, Zitto Kabwe, Halima Mdee, John Mnyika, Godbless Lema na wengineo wengi) la hasha bali viongozi hawa makini na wenye uwezo mkubwa hawatoshi kufit katika nyadhifa na idara zote na kutengeneza serikali yenye ufanisi na kasi moja. kimsingi kwa idadi yao wanapwaya.

Ukichukulia mfano tu ile kambi ya upinzani bungeni, inayoongozwa na Mbowe, mgawanyo wamawaziri kivuli katika wizara kivuli hizo ambao ndio unatoa picha ya nani atashika nafasi gani kama Chadema itashika madaraka, waliochaguliwa utagundua kabisa kuwa Chadema hakuna NGUVU KAZI YA KUTOSHA. Kuna wengi ambao ni makini lakini sio 'the best' we can get kwa ajili ya kusimamia maendeleo ya taifa kwa ukubwa wake.

Wako wanaoweza kuwa mawaziri na viongozi makini sehemu mbali mbali serikalini, kama Zitto Kabwe, Tundu Lissu, Mnyika kiasi, Mbowe, Mdee kiasi........kimsingi hata ninavyoitaja hii list unaona kabisa kwamba tunarun out of options.....nguvu kazi inayohitajika haitoshi. Iitakapokuja katika suala la kuteua Nguvu Kazi kwa ajili ya nyadhifa zote kwa ukubwa wake, naona Chadema inapwaya. Labda waje kutumia kujuana, kitu ambacho hakitaleta tija katika maendeleo (najua Chadema haitafanya hivyo).

Nadhani, Suala la kurecruit wanachama wapya linahitajika kufanyika, tena kila sehemu hadi vijijini, Chama kirecruit wachapakazi, wanachama makini, kitoe mafunzo na warsha mbalimbali ili kuinspire vijana wengi zaidi na kupata nguvu ya kutosha kuendesha nchi wakati utakapofikia. Bila hivyo kwa kweli naona Chadema kinapwaya jamani, hebu nyie wenyewe semeni.

Matatizo yako ni madogo sana. Una tatizo la kuabudu baadhi ya binadamu wenzako. Hata mimi naweza kuwa waziri, sijui wewe.
 
Tunapozungumzia haya ni Chadema kitatoa watendaji wote wakuu na muhimu pindi kitakaposhika madaraka ya nchi.
Yaani kuanzia
- mawaziri
- makatibu,
- wizara,
- Mabalozi
- wakuu wa idara mbalimbali,
- mahakimu,
- wakuu wa mikoa na wilaya.
na wengineo wengi kwa ukubwa wa serikali yetu, tokea wizara, kanda mikoa hadi wilaya.

Ndugu yangu hadi mahakimu wanatoka CDM! unajua kweli unachoongea? Mbona ni sawa na kusema CDM ikiingia madarakani itabadili mipaka ya nchi. Hadi leo hujui kuwa mahakimu hawafuati maelekezo ya chama chochote katika majukumu yao?
 
Umeongea kiushabiki ila katika wachangiaji wotewewe ndio umenielewa sana
Licha ya kutokuwa na watu wa kuongoza , CHADEMA a.k.a. MAGWANDA watakuwa wanaiona nchi hii kama uchi wa mtoto. Kwani mtoto akiwa uchi utakuwa wamtizama tu na huna la kufanya
 
Haaa haaaa hapana mkuu, sina maana hiyo naeleewa sana unachokiongea. Refer to majibu niliyowajibu wenzako mmwanzoni tu mwa wachangiaji. Ninachomaanisha ni kwamba Workforce ya Chadema ya sasa haitoshi kurun serikali, think and respond to that perspective.kwa faida yako narudia tena ni kwamba Chama kinaposhika hatamu ni lazima kichague watu (ambao wana mlengo sawa na chama, na imani ya chama ambao si lazima wawe ni wanachama, ili serikari ifanye kazi kama kitu kimoja. Nia ya Chadema ni nzuri so most definetly itahitaji watu safi pia, so hao watu inawatoa wapi? Au itateua wale wale wa serikali ya CCM, kina Makame?
Ndugu yangu hadi mahakimu wanatoka CDM! unajua kweli unachoongea? Mbona ni sawa na kusema CDM ikiingia madarakani itabadili mipaka ya nchi. Hadi leo hujui kuwa mahakimu hawafuati maelekezo ya chama chochote katika majukumu yao?
 
Haya mkuu, nafurahi umechanganya na ya kwako ukanielewa!
Inabidi urekebishe heading yako maana wengine tunashindwa kuelewa kama unauliza swali toka kwa wana JF au unawakilisha mashaka yako kuhusu CHADEMA kukamata dola 2015.
 
Umejibu vizuri mkuu, pia nakubaliana sana na TK
Umenena vyema mkuu, ukiwa na Rais makini, Makamu wake makini, Waziri mkuu makini, Mawaziri makini na wachapakazi, kinachofuata ni kuweka utawala bora katika mikoa, wilaya na hata vijiji.Wanaosikika Chadema ni wachache lakini ndani ya Chadema kuna hazina kubwa sana ya viongozi bora, pia kuna wanachama na nje ya chama lakini kuna watu wenye mapenzi mema na nchi hii.Mfumo uliopo ndio unaoharibu nchi kukumbatia kwamba kila kiongozi lazima atoke ccm, hata kama kuna kiongozi mzuri kwa nafasi ya uwaziri laki hatoki ccm basi hapewi, who knows bwana kama Chadema ikikamata nchi inawezekana akina magufuli wakarudishwa kwenye uwaziri na wakajirekebisha walipo jikwaa na kuwatumikia watanzania, so hofu ondoa ndugu.
 
Kwahiyo unaridhika na kina Hawa Ghasia, Sophia Simba, Shukuru Kawambwa na mashudu mengine ya Ccm?
 
chadema ni a big mystery than a reality...

nguvu ya chadema inatokana na udhaifu wa ccm,

yaani bila ccm dhaifu na ya kifisadi,chadema haina nguvu

hawana nguvu ya kwamba wana better organisation
au a better vision......

waulize sera zao za viwanda kwa mfano,
utasikia tu, 'tutaimarisha viwanda'

kama vile ccm tu,siasa zaidi kuliko visionaries

na sasa wana tatizo kubwa zaidi kuliko ccm

ni tatizo la kutokukubali kukosolewa na kupingwa..

kuna thread nilianzisha hapa,inaitwa' Chadema wananidissapoint kwa kweli'

ukiona hata majibu ya dr slaa kwenye hiyo thread utashangaa,ni aibu kwa kweli...

juzi tu hapa jenerali ulimwengu kawashauri kile kile nilichoshauri mimi

kwamba watulie na wajipange,majukumu wanayoyaomba ni makubwa mno

but still hawaelewi kabisa
 
Ndugu mtoa mada samahani kama nitakukwaza, ila ukweli ni kwamba upeo wako ni mdogo sana katika mifumo ya uongozi, Nilichomuelewa mimi Dr Slaa aliahidi kuunda serikali ndogo isiyozidi mawaziri 20, na ukumbuke huko tuendako mawaziri hawatotokana na wabunge ilo ni moja ya madai makuu ndani ya katiba mpya.
Pale UDSM 90% ya malecture wote ni Chadema, usione watu wako kimya ukadhani CHADEMA ina uhaba wa wasomi, na ukumbuke serikali ijayo haitohitaji uwe mbunge au mwanasiasa kuweza kuitumikia nchi yako.
Nakupa changamoto unijibu Bingu wa Mutharika ameundaje serikali yake? au nieleze mgombea binafsi akiruhusiwa na akishinda ataundaje serikali yake? ndio maana hata Nduka amebeza huu utafiti wako butu.

Serikali makini siku zote itawaacha wanasiasa wapige porojo za kisiasa na wataalam ndio watakabidhiwa jukumu la kujenga nchi. usiwahesabu akina SUGU kwamba ndio serikali ijayo ya CHADEMA, hapana hapo utakuwa unajidanganya mwenyewe,, asilimia kubwa ya wabunge wa CHADEMA kazi yao kuu itakuwa ni kuisimamia serikali yao na kuiwajibisha pale itakapokwenda kinyume na matarajio ya Watanzania.
 
Atakayeikomboa Tanzania ni mtu, na wala sio chama chochote cha siasa kwa kuwa vyama vyote vya siasa vina sera nzuri tu, tatizo ni viongozi, na hasa kiongozi mkuu mwenye mamlaka ya kuamua iwe na ikawa.
 
Revolutionary,

Una hoja ya Msingi,watu kama ninyi mnasaidia sana katika kuimarisha upinzani hasa mnapo-expose doubt zenu ili kama kuna ukweli zifanyiwe kazi.
Chadema ni ni chama makini ni lazima kitumie jitihada zote kuhakikisha kwamba watanzania hawatakuwa na wasiwasi kama wakitupa ridhaa ya kuongoza.

Ila hapo kwenye suala la kupata watu wa kuongoza ni kwamba si lazima tufuate mfumo kama huu uliopo,inawezekana kiongozi mzuri aliye CCM akawa ndani yua serikali ya Chadema,CUF,NCCR n.k.Ni lazima tukomae katika hili.Kitakachowaongoza watu hawa kutoka vyama tofauti but the best brains ni sera na leadership values zitakazowekwa na Chadema.Uliona kule United States,Obama(Democrats) alimwacha Robert Gates waziri wa Ulinzi wa serikali ya Bush(Republican Party) katika portfolio yake kwa maslahi ya taifa.Kinachohitajika ni leadership values and commitment to the laid principles and values na uwezo wa chama na uongozi wa juu kufanya coordination and monitoring of Government machinery.

Hata hivyo,ukweli ni kwamba Chadema tunahitaji kujipanga zaidi ya hapa.Tuendelee kushirikiana,chaguzi zetu za ndani tutakazofanya kuanzia sasa tutakuwa tunafanya chaguzi zitakazotoa Taswira ya outcome ya general election 2015.Ni jukumu na wajibu wa Chadema kuhakikisha viongozi wote watakaochaguliwa wataongeza kasi ,na kurahisisha harakati za kuchukua dola.Uchaguzi wa ndani wa 2013 utakuwa ni uchaguzi pacha,yaani ni sawa na kupiga kura kwa ajili ya matokeo ya 2013 na kwa ajili ya matokeo ya uchaguzi mkuu 2015 yatakayoamua position yetu na Tumaini la watanzania kupata mabadiliko kupitia chama makini cha Upinzani

So,Watanzania waendelee kukiunga mkono Chadema kwa nguvu zote,tusaidiane kulikomboa Taifa Letu.Mjadala unaondelea sasa kuhusu kulazimishana posho na kutumia vitisho ni dhahiri kwamba sasa Watanzania wamejua ni chama gani na ni akina nani hasa wenye dhamira ya dhati katika kuwapigania,kuwajali na hasa wanyonge walio wengi

By the time they see us, they will know that something is happening in Tanzania and that people are ready for change. Let us never doubt what we can achieve if we work together. The time has come for change in Tanzania and we are the apostles of that change.We are asking Tanzanians to give us the opportunity to lead the country. If one party (Chama Cha Maapinduzi) has failed the nation, there are other Serious parties
 
Nadhani kwa sasa tusiwe sana na pressure,maana sidhani kwamba chadema akiingia madarakani ndio ataingia na watu wake wote,no bali kuna baadhi ya waliokuwa sasa madarakani ni wazuri ila sema chama cha magamba so nadhani wengine watatumiwa hao hao au kufanya changes kwenye system nzima......,wa huku kumpeleka kule na kule kuja huku,ila wale wote wa magamba waanguswe tu na mafisadi papa..........
 
Umetukika sana, I like mitazamo kama yako! You are a visionary!

Kumbuka hivyo vichwa vichache vya chadema ulivyovitaja ni sawa na Baraza zima la jk. Ndo maana jk anahitaji mawaziri 60 kuunda serikali wakati chadema wanahitaji wasiozidi 20. Kukuondoa wasiwasi, mwaka 2015 tutakapounda serikali, wabunge wa Chama Tawala (CDM) watakua zaidi ya theluthi mbili ya wabunge wote. Maandalizi yameshaanza. Kumbuka, kabla ya uchakachuaji wa mwaka jana kulikua na wabunge 112 wa cdm walioshinda. Hali hiyo hatutairuhusu tena kaka.
 
Wewe ni mtu makini sana, a visionary like me, you think outside the box too. I complement you for that.

Umeweza kuelewa na kuona ambacho wengine wanaignore either kwa kuwa naive ama tu kwa ushabiki. Running a country is not an easy thing, it requires massive efficiency na inahitaji to think beyond the ordinary,beyond your normal capacity.

2015 sio mbali ni muhimu Chadema kikaendelea kufanya vizuri kuendelea kuwapa imani watanzania na bila shaka watanzania wameshajua Chadema is a serious party.

Ni muhimu pia kuendelea kurecruit members ngazi zote ili kufanya chama kijitosheleze kuanzaia kata hadi taifa, fursa hiyo ipo, ni kubwa na itumike.

Last but not least, ni muhimu kuanza kufikiria uhlisia wa namna Chadema itakavyo endesha serikali mara itakapoingia madarakani, ku-foresee challenges na vikwazo halisi vitakavyowepo (cause tunasema tunataka nchi isitawalike, Tutakapoingia madarakani CCM hawatapenda, na wao wana nguvu zaidi ya kufanya nchi isitawalike kwa Chadema, haswa kimfumo, na ushahidi ninao) this is real and we have to think about it realistically.....

Revolutionary,

Una hoja ya Msingi,watu kama ninyi mnasaidia sana katika kuimarisha upinzani hasa mnapo-expose doubt zenu ili kama kuna ukweli zifanyiwe kazi.
Chadema ni ni chama makini ni lazima kitumie jitihada zote kuhakikisha kwamba watanzania hawatakuwa na wasiwasi kama wakitupa ridhaa ya kuongoza.

Ila hapo kwenye suala la kupata watu wa kuongoza ni kwamba si lazima tufuate mfumo kama huu uliopo,inawezekana kiongozi mzuri aliye CCM akawa ndani yua serikali ya Chadema,CUF,NCCR n.k.Ni lazima tukomae katika hili.Kitakachowaongoza watu hawa kutoka vyama tofauti but the best brains ni sera na leadership values zitakazowekwa na Chadema.Uliona kule United States,Obama(Democrats) alimwacha Robert Gates waziri wa Ulinzi wa serikali ya Bush(Republican Party) katika portfolio yake kwa maslahi ya taifa.Kinachohitajika ni leadership values and commitment to the laid principles and values na uwezo wa chama na uongozi wa juu kufanya coordination and monitoring of Government machinery.

Hata hivyo,ukweli ni kwamba Chadema tunahitaji kujipanga zaidi ya hapa.Tuendelee kushirikiana,chaguzi zetu za ndani tutakazofanya kuanzia sasa tutakuwa tunafanya chaguzi zitakazotoa Taswira ya outcome ya general election 2015.Ni jukumu na wajibu wa Chadema kuhakikisha viongozi wote watakaochaguliwa wataongeza kasi ,na kurahisisha harakati za kuchukua dola.Uchaguzi wa ndani wa 2013 utakuwa ni uchaguzi pacha,yaani ni sawa na kupiga kura kwa ajili ya matokeo ya 2013 na kwa ajili ya matokeo ya uchaguzi mkuu 2015 yatakayoamua position yetu na Tumaini la watanzania kupata mabadiliko kupitia chama makini cha Upinzani

So,Watanzania waendelee kukiunga mkono Chadema kwa nguvu zote,tusaidiane kulikomboa Taifa Letu.Mjadala unaondelea sasa kuhusu kulazimishana posho na kutumia vitisho ni dhahiri kwamba sasa Watanzania wamejua ni chama gani na ni akina nani hasa wenye dhamira ya dhati katika kuwapigania,kuwajali na hasa wanyonge walio wengi

By the time they see us, they will know that something is happening in Tanzania and that people are ready for change. Let us never doubt what we can achieve if we work together. The time has come for change in Tanzania and we are the apostles of that change.We are asking Tanzanians to give us the opportunity to lead the country. If one party (Chama Cha Maapinduzi) has failed the nation, there are other Serious parties
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom