Ni kitu gani kimebadilika katika elimu Tanzania? Tukiendelea kuwaacha wajinga watuongoze watu wenye akili ni hatari

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,608
93,379
Labda niulize sisi tuliosoma miaka ya nyuma na sasa kuna kitu gani kimebadirika?

Tulisoma bila kuwa na vitabu, hatukujuwa sylubus yoyote, Primary tuliwahi namba SAA 12 asubuhi na SAA 8 mchana ni mwisho wa masomo na kurudi nyumbani na wengi hatukusoma masomo ya ziada tuition lakini kulikuwa na vipanga balaa.

Sasa uvumilivu umenishinda, nina kitoto ni one of dependant wangu anaamka Saa 10 usiku saa 12 asubuhi anaanza tuition ya lazima shuleni anaendelea na masomo mpaka Saa 12 jioni kisa eti ni darasa la saba.

Sasa nimepitia repoti yake leo asubuhi hii ya annual examination sijafurahishwa nayo lakini remarks za class teacher ameandika Good.

Nimejiuliza sana darasa la Watoto 60 mtoto anakuwa wa 50 hii good inatoka wapi? OK average B lakini kutesa kote huku Watoto haya ndio matokeo yake? Na ieleweke wazi hii ni private school.

Sasa labda Mimi nimepitwa na wakati naomba mnielimishe huku ndio tulikofikia?

Ifike sasa Wazazi hasa kina mama tuache ushamba, ni bora kutafuta shule ya umma nzuri mtoto asome huko umuwekee usimamizi mzuri tu kuliko huu Utapeli tunaofanyiwa na hizi private school.

Anyway nisiwachoshe lakini sijafurahishwa kwakweli.
 
Lakini kumbuka kuna walioshika nafasi za juu kutokana na hayo mateso. So, hitimisho ni kuwa mtoto wako uwezo wake ni huo ukimtesa na wenzake yeye anaishia hapo.

Siungi mkono watoto wanavyohangaishwa siku hizi hata mimi nina kibinti kinapata shida ilibidi hadi nikiamishie shule ya karibu maana alikuwa wa kwanza kufuatwa wa mwisho kurudishwa plus ma weekend kwenda shule nikaona nimtafutie shule ya karibu ambapo anafuatwa saa moja na robo saa tisa na robo yuko home.
 
Labda niulize sisi tuliosoma miaka ya nyuma na sasa kuna kitu gani kimebadirika?

Tulisoma bila kuwa na vitabu, hatukujuwa sylubus yoyote, Primary tuliwahi namba SAA 12 asubuhi na SAA 8 mchana ni mwisho wa masomo na kurudi nyumbani na wengi hatukusoma masomo...
Hizo tuition za asubuhi ni business as usual wa Mkuu wa Shule na walimu wake, kataa na mtoto kuamka saa 10 usiku kila siku za shule ni dhambi mbaya sana, kwani unamuharibu ubongo wake kwa kukosa usingizi mzuri, hata shuleni hataweza kusoma sbb ubongo wake utajaa usingizi mtupu.
 
Lakini kumbuka kuna walioshika nafasi za juu kutokana na hayo mateso. So, hitimisho ni kuwa mtoto wako uwezo wake ni huo ukimtesa na wenzake yeye anaishia hapo.
Siungi mkono watoto wanavyohangaishwa siku hizi hata mimi nina kibinti kinapata shida ilibidi hadi nikiamishie shule ya karibu maana alikuwa wa kwanza kufuatwa wa mwisho kurudishwa plus ma weekend kwenda shule nikaona nimtafutie shule ya karibu ambapo anafuatwa saa moja na robo saa tisa na robo yuko home.
Nakubaliana na hoja yako, maana malezi ya awali aliyopata kutoka kwa mzazi nayajuwa vizuri, ni aina ya malezi ambayo nayapinga sana kuwapenda Watoto kupita kiasi, halafu imagine Mungu amemchukuwa.

Kuna wakati nashindwa kumnyoosha kwa principal zangu asije kuona anafanyiwa hivyo kwa sababu mzazi wake amefariki dunia, inahitaji busara sana kuishi na Watoto walipatwa na mazingira haya.
 
Nakubaliana na hoja yako, maana malezi ya awali aliyopata kutoka kwa mzazi nayajuwa vizuri, ni aina ya malezi ambayo nayapinga sana kuwapenda Watoto kupita kiasi, halafu imagine Mungu amemchukuwa.

Kuna wakati nashindwa kumnyoosha kwa principal zangu asije kuona anafanyiwa hivyo kwa sababu mzazi wake amefariki dunia, inahitaji busara sana kuishi na Watoto walipatwa na mazingira haya.
Kweli hiyo ni changamoto. Hapo mpeleke taratibu mkuu maana ikiwa ghafla kweli anaweza kuhisi unamtesa.
 
Back
Top Bottom