JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 626
- 938
Wadau mbalimbali wa elimu wamekuwa wakilalamikia mfumo wa sasa wa Elimu ya Tanzania.
Jamiiforums kama mdau mmoja wapo wa elimu na mabadiliko inatoa fursa kwa Wanachama wake na umma kwa ujumla kutoa maoni yao juu ya nini hasa kibadilike katika mfumo wa elimu uliopo.
Ili kupata nafasi hii tafadhali jiunge nasi katika Mjadala wa TwitterSpace ya JamiiForums utakaofanyika tarehe 16 Februari, 2023 kuanzia saa 12:00 jioni mpaka saa 02:00 Usiku.
Pia, unaweza kuandika maoni yako kwenye uzi huu ambayo yatasomwa siku ya mjadala.
Karibuni.
UPDATE
- Karibu kujiunga nasi katika Mjadala unaoendelea hivi sasa kupitia TwitterSpace ya JamiiForums kujiunga tafadhali gusa link hii Unapendekeza nini kibadilike katika Mfumo wa Elimu ya Tanzania?
BAADHI YA MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU
MDAU JFSPACES: Muda wa kukaa Darasani upungue. Shule ya awali iwe Miaka 2, ya msingi iwe Miaka 5, Elimu va upili iwe Miaka 4 vilevile hakuna haja ya A- level Mitaala ifumuliwe yote, Watoto wafundishwe kulingana na mahitaji ya sasa. Specialization (ubobezi) uanze ngazi ya msingi.MDAU JFSPACES: Kuwe na Mtaala wa kuwajengea Watoto 'Career choice development' kuanzia Shule ya msingi yaani kuanzia primary Mtoto ajue anataka kuwa nani Masomo ya lazima yawepo mfano Hesabu na uraia ila Historia iwe option Watoto waisome tu.
MDAU JFSPACES: Mfumo wa #Elimu ufanyiwe marebisho makubwa hususani ktk kumjengea uwezo Mtoto wa kutenda Katika shule kuwepo na Miundombinu yenye kumwezesha Mtoto kujifunza vitu vingi kuboresha ufahamu. Mfano ufundi wa Ushonaji, Umeme, Ufugaji, Kilimo na Miradi ya Uzalishaji.
MDAU JFSPACES: Miradi au shughuli zingizwe kwenye vipindi kabisa ili Mwanafunzi aweze kuhudhuria na itawasaidia Wanafunzi wengi kupata Maarifa na kupanua wigo wa Soko la Ajira tofauti na sasa ambapo Wanafunzi wengi wamehitimu Shule ila katika Study za Kazi hawana ujuzi wowote.
MDAU JFSPACES: Nionavyo Mimi, Elimu yetu ijikite zaidi kujiajiri, ipunguze kukaririsha Vijana wetu. Mafunzo kwa vitendo yapewe kipaumbele. Elimu ya kujitegemea irudishwe. Elimu iwe complete. Kijana wa form four awe na ujuzi wa kumuwezesha kuishi na kutengeneza kipato.
MDAU JFSPACES: Unasoma Miaka saba unafanya Mtihani siku moja, unasoma Miaka minne unafanya mitihani siku moja halafu wanakuja kukwambia umefeli? Masomo yenyewe meeeeeengi kweli Ufundi stadi uwekwe kwenye Mitaala kuanzia shule ya msingi. Usitumike kama mbadala baada ya kufeli.
MDAU JFSPACES: Unasoma Miaka saba unafanya Mtihani siku moja, unasoma Miaka minne unafanya mitihani siku moja halafu wanakuja kukwambia umefeli? Masomo yenyewe meeeeeengi kweli Ufundi stadi uwekwe kwenye Mitaala kuanzia shule ya msingi. Usitumike kama mbadala baada ya kufeli.
MDAU JFSPACES: Masomo ya Kilimo primary na secondary yapewe kipaombele. Pia, Masomo yapunguzwe. Walimu wapewe Pikipiki mikopo kwa malipo nafuu maana wengi wanaishi mbali na vituo kwasababu Nyumba za Watumishi hazipo.
MDAU JFSPACES: Elimu ilenge kuwafundisha Wanafunzi mbinu za moja kwa moja za kukabiliana na matatizo yaliyopo. Mtu amalize form four akiwa ameandaliwa kusoma Chuo kikuu moja kwa moja. Masomo ya five na six yagawanywe mengine yaende varsity na Sekondari.
MDAU JFSPACES: Mfumo wa Elimu ubadilishwe ili Watu wasome mambo ambayo yatamsaidia ktk Maisha halisi Kwa mfano Mtoto anasomea Physics na Chemistry hadi kidato cha Sita, akifika chuo anabadili mwelekeo anasoma Political Science au BBA baada ya hapo anaingia mtaani, anakosa ajira.
MDAU JFSPACES: Mfumo wa Elimu ubadilishwe ili Watu wasome mambo ambayo yatamsaidia ktk Maisha halisi Kwa mfano Mtoto anasomea Physics na Chemistry hadi kidato cha Sita, akifika chuo anabadili mwelekeo anasoma Political Science au BBA baada ya hapo anaingia mtaani, anakosa ajira.
MDAU JFSPACES: Kwanza viboko viharamishwe mashuleni, pili mitaala inayowaandaa watoto kimtihani ibadilishwe badala yake iwe ni mitaala inayowajenga/ inayowapa wanafunzi uwezo/ maarifa (capacity building curriculum).
MDAU JFSPACES: Moja ya jambo muhimu la kubadili katika Mitaala ya Elimu ni kuachana na Elimu ya kikoloni, tufocus na Elimu ya mabadiliko ya Kisayansi na Teknolojia kwa kuwa na Elimu ambayo ni 'practical based not more theoretically' Elimu kuhusu Taifa letu iwe kipaumbele.
MDAU JFSPACES: Matumizi ya Teknolojia katika Elimu, kuwezesha Wanafunzi kupata ujuzi wa Wlimu pamoja na Teknolojia baada ya kumaliza kusoma na kupunguza idadi kubwa ya wasubiri Ajira za Serikali bali kujiajiri kupitia ujuzi wa Kompyuta.
MDAU JFSPACES: Kwanza kabisa muda wa kukaa Shuleni upunguzwe, itawezekana kwa kupunguza vitu visivyo na tija kwa wakati huu Pia, Elimu iwe kwa vitendo zaidi hasa kwa Masomo ya Sayansi. Kingine, tuangalie hii fani ya Ualimu, wengi wanaonekana kutokumudu Masomo husika.
MDAU JFSPACES: Wapunguze Masomo yasiyo na lazima na Watu wasome kwa Combination kuanzia form one. Lugha ya kufundishia iwe kiswahili Kungekuwa na Masomo 5 tu ya Kimkakati kwa ajili ya Maendeleo sio hii 'how Europe under developed Africa' Miaka yote.
MDAU JFSPACES: Kuanza kufundisha Masomo ya Biashara na Uchumi katika ngazi za Sekondari, kuondoa somo la GS ama DS kuweka Somo la Uchumi kuwa la lazima Tuachane na Ujasiriamali wa kuambiwa tupambane na Soko la Dunia Kitaalamu.
MDAU JFSPACES: Elimu inatakiwa kujikita na mambo ya msingi zaidi kuliko kuwejenga na hadithi za chopeko na mnofu Tuache kupeana Moyo kwenye kupambana na Simba kama hawafu mwenye nguvu badala yake Masomo ya Ujasiriamali yapewe nafasi kubwa huku Mtaani thamani ya X haipo.
MDAU JFSPACES: Kiukweli nafikiri ingefunguliwa Shule ya Watundu. Tuwachunguze Vijana wote ambao ni Wezi na Vibaka tuwapeleke huko, tuwachunguze vijana wote wenye uwezo wa kuiba kupitia Kompyuta tuwaweke huko, wanaoweza kuhack wote, wanaoweza kutengeneza Ndege. hao ni rasilimali
MDAU JFSPACES: Shule za Advance ziwe vyuo vya ufundi stadi (VETA). Vifundishe Ufundi wa Kilimo, na ujuzi mwingine itasaidia Watu kuishi Kuanzia chekechea hadi chuo lugha ya kufundishia iwe Kingereza, Kiswahili tunadanganyana watasoma tu Watoto wa Masikini kwenye huo Mfumo.
MDAU JFSPACES: Civics, History, Regional study liwe Somo moja lenye mwendelezo kihatua. Agriculture, Commerce na BooKeeping yawe lazima kwa asiyesoma Physics, Chemistry na Biology Masomo ya lugha za Kigeni angalau kuwe na Kujua kwa lazima lugha mbili za Kimataifa.
Kila wilaya iwepo shule ya kukuza vipaji mbalimbali, Ikianzia primary to secondary tutapata matured talents tofauti na sasa hakuna uniformity.
MDAU JFSPACES: Tuchague moja katika Lugha ya kufundishia Kiswahili au Kiingereza, hii itaepusha kupoteza muda kujifunza jambo moja Mfano kifo cha Mkwawa wasoma standard four, ukiwa kidato cha kwanza ama pili kuna Death of mkwawa tofauti ni nini? Hii tunapoteza muda kisa Lugha.
MDAU JFSPACES: Nje ya Shule, Serikali itenge Wanafunzi wawe na Kazi maalumu ya vile vitu wanavyosemea ili kukuza ujuzi wao kuwa bora zaidi Hapo Serikali ni lazima washirikiane na sekta binafsi ktk kuwapa Ajira hizo kwa ajili ya Wanafunzi. Tutapata Watu wenye uwezo mkubwa.
MDAU JFSPACES: Nje ya Shule, Serikali itenge Wanafunzi wawe na Kazi maalumu ya vile vitu wanavyosemea ili kukuza ujuzi wao kuwa bora zaidi Hapo Serikali ni lazima washirikiane na sekta binafsi ktk kuwapa Ajira hizo kwa ajili ya Wanafunzi. Tutapata Watu wenye uwezo mkubwa.
MDAU JFSPACES: Shule chakavu na Vyuo ziondolewe uchakavu kwa kukarabatiwa Mwalimu mmoja kwa Somo moja na kwa darasa moja. Mfano Mwalimu mmoja afundishe Darasa la 4 somo moja tu na asifundishe Darasa lingine. Hisabati na Kiingereza wapewe Walimu mahiri wanaoyaweza masomo hayo.
MDAU JFSPACES: Elimu ijiondoe kwenye Nadharia na kwenda kwenye Vitendo Mitaala mibovu, Tanzania tunasoma Elimu isiyoendana na Dunia ya leo. Tafiti zifanyike tujue wenzetu wanafanya nini, mazuri tukicopy sio mbaya.
MDAU JFSPACES: Elimu yetu kwa sasa ina mambo mengi mno, ukiangalia ni Mifumo ambayo tulichukua kwa Wakoloni lakini Wakoloni wameshabadilisha vingi kwenye Mifumo yao Sisi bado tumebaki palepale na hata vikibadilika ni kwa uchache na sio kwa namna ambayo Watu wanashauri.
MDAU JFSPACES: Elimu yetu itambue vipaji, ni kawaida kuona Mtoto anakuwa bize sana na Masomo lakini hana nafasi ya kuboresha au kukuza kipaji chake Mfano Mwanafunzi akiwa na kipaji cha kucheza Mpira, anapata muda mfupi sana wa kuonesha kipaji chake, tuingize kwenye Mitaala yetu.
MDAU JFSPACES: Elimu yetu itambue vipaji, ni kawaida kuona Mtoto anakuwa bize sana na Masomo lakini hana nafasi ya kuboresha au kukuza kipaji chake Mfano Mwanafunzi akiwa na kipaji cha kucheza Mpira, anapata muda mfupi sana wa kuonesha kipaji chake, tuingize kwenye Mitaala yetu
MDAU JFSPACES: Mitaala ndiyo inayotakiwa kutuongoza siyo Lugha, #Kiswahili tumezaliwa nacho Kingereza hatuwezi kukikwepa, hivyo shida yetu ni kwenye vitabu vinavyotumika, kuna mazingira tofauti ya vitabu vinavyotumika.
Mfano Shule binafsi wanafundisha Kingereza kuanzia mwanzo, wale wa Shule za Serikali wanakutana nacho Sekondari tena katika vitabu ambavyo vinatofautiana, hiyo ni ngumu.
MDAU JFSPACES: Nchi yetu tulishindwa kujua tunataka nini kwenye Elimu. Mimi nilisoma History 2 but so what, inanisaidia nini Tunatakiwa kujua kuweka mkazo katika Vitendo.
MDAU JFSPACES: Elimu yetu kwa sasa ina mambo mengi mno, ukiangalia ni Mifumo ambayo tulichukua kwa Wakoloni lakini Wakoloni wameshabadilisha vingi kwenye Mifumo yao Sisi bado tumebaki palepale na hata vikibadilika ni kwa uchache na sio kwa namna ambayo Watu wanashauri.
MDAU JFSPACES: Elimu ya msingi iwe Miaka 10. Elimu ya sekondari iwe miaka 4, tusiwe na a level, chuo iendelee ilivyo. Mtoto amalize Elimu ya Msingi akiwa angalau na Miaka 16 ili asipofaulu aende veta. Waliofaulu wasome Miaka minne yaani kwenda University angalau Mtoto awe na Miaka 20.
Maudhui yabadilishwe kuwepo na Somo la uzalishaji la lazima kwa kila Mtoto na lifanywe kwa vitendo. Ufundi, kilimo, biashara na ufugaji. Yaani watoto wanaofanya Biashara wawe wanaenda stand kuuza vitu. Kilimo wawe na mashamba. Ufugaji wawe na Mifugo. Ufundi waende workshop.
MDAU JFSPACES: Naona Mtaala wetu hakutakuwa na tatizo kama tutaenda kwenye Lugha ya Kiingereza. Wanaotumia Lugha zao huko ni kwasababu wanaweza kujitegemea Sisi hatuwezi bado kujitegemea kwenye Teknolojia.
MDAU JFSPACES: Natamani kwenye Mabadiliko ya Sera Serikali ichague Shule za Mfano wafanyike Sample na wao watakuja kuwa-train hao wengine Sioni shida ya Kiswahili na tunaweza kwenda na Lugha yetu halafu Mtu akihitaji Lugha nyingine hiyo inaweza kuwa ni Fursa kwa Wakalimani.
MDAU JFSPACES: Darasa la 7 & Kidato cha 6 hayamsaidii Mwanafunzi kwa kuwa asilimia kubwa mambo yanayofundishwa ni yaleyale. Kuna Watu ambao walipohitimu kidato cha 4 wakapita ngazi nyingine za Elimu kama cheti, wakifika Chuo wanakuwa bora kuliko yule aliyehitimu kidato cha 6.
MDAU JFSPACES: Kwa Mtaala tulionao bado kuna vitu vingi hatujafanya, tunatakiwa tuweke msingi kwenye 'Competence Based Learning' Mfumo wetu unatakiwa umpime Mtoto kwenye uelewa wake sio kwenye alichokisoma. Watoto wa darasa la 3 wanatakiwa kuingia kwenye Teknolojia.
MDAU JFSPACES: Tukiangalia takwimu za ongezeko la Watu tunatakiwa kujua pia Miaka 10 ijayo bado tutakuwa tunatumia Teknolojia ya sasa? Tujiulize kwa Mitaala yetu je, hawa Wanafunzi wa sasa wanaandaliwa kukabiliana na trend ya Mabadiliko inayokuja?
MDAU JFSPACES: Mabadiliko ya Elimu yanatakiwa kwenda na Mpango wa Kitaifa, Ningeshauri masomo yabadilike na kuachana na kuzalisha wanasiasa au maafisa tuanze kuzalisha watu wenye skills, watu wengi waliojaa kwenye soko la ajira ni wenye makaratasi zaidi.
MDAU JFSPACES: Nadhani kama Taifa tunatakiwa kuchagua aina ya Lugha ya kufundishia Shuleni Inashangaza kuona Mtoto anatoka kufundishwa kwa Kiswahili Miaka 7, akimaliza hapo anaingia kusoma kwa Kingereza, tuchague Lugha moja inayoweza kutumika kuanzia chini hadi juu