Ndiyo, Lowassa ni fisadi na hilo halina ubishi lakini ndani ya CCM yupi ni afadhali Urais 2015!

Siwapingi na Chaguo lenu, lakini tafadhali msitake kuupoteza Umma kama nyie mnamchagua Lowassa mchagueni kwa matakwa yenu lakini kumpigia chapuo hapa JF kama vile sisi mijinga iliyolala hapo wakuu zangu mnatupeleka kusiko....
Mkandara kwa nini umengia kwenye mtego wa kukumbatia falsafa ya George Bush ya "either you are with us or against us"? Mimi simuungi mkono Lowassa lakini pia siwaungi mkono watu wanaopenda kufanya ukasuku. siipendi tabia ya watu wanaoua mtu mwingine kwa sababu tu wamesikia sauti ya watu wengine wakimwita huyo mtu mwizi. Imeshawahi mara nyingi tu watu wameuawa kwa kuitwa mwizi na wagoni wao.

Mimi nasema hizi "allegations" zisipojengwa katika misingi ya kisayansi yaani kuegemea katika uthibitisho, mwisho wa siku tutakuja kuombana radhi na wale ambao leo tunawaona ni mafisadi wa kutupa. kati ya watu wanaomini kwamba Lowassa ana mapungufu makubwa ya uadilifu mimi ni mmojawapo, lakini siipuuzii nguvu ya Lowassa katika jamii na jamii ya wanasiasa hapa Tanzania.

Siku Lowassa alipofanikiwa kuwa Mwenyekiti ya kamati ya Ulinzi na mambo ya nje niliwaambia wenzangu kwamba pamoja na ufisadi wake bado ana nguvu sana kwenye siasa za Tanzania. Kama ukitaka kupambana na Barcelona na ukaichukulia nguvu yake ni sawa na Mtibwa Sugar ya Morogoro, utakuwa unajidanganya.

Kamati anayoiongoza Lowassa ndiyo inayosimamia majenerali wetu, Idara ya Usalama wa Taifa, Wizara ya mambo ya Nje ya Nchi, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. pamoja na ufisadi wote tunaoujua wa Lowassa bado jamaa ilishindikana kumzuia kupewa kamati nyeti namna hii. Mkandara hata mimi sina ndoto ya kuwa na Rais anayeitwa Edward Ngoyai Lowassa, lakini pia najua kwamba sitapiga kura peke yangu na hao wenzangu sijui mitizamo yao kuhusu Lowassa.

Hoja yangu ni lazima wale "wanaojua" madhambi ya Lowassa watupe ushahidi usiotia shaka "Beyond resoanable doubt" ili na sis tuweze kuwaeleza wengine kinagaubaga ubaya wa huyu jamaa bila ya kubuni buni mambo au kushabikia yale yanayosemwa na wengine. Ndiyo maana sipendi watu wachache tu ndiyo wayajue madhambi ya Lowassa.
 
Mkandara kwa nini umengia kwenye mtego wa kukumbatia falsafa ya George Bush ya "either you are with us or against us"? Mimi simuungi mkono Lowassa lakini pia siwaungi mkono watu wanaopenda kufanya ukasuku. siipendi tabia ya watu wanaoua mtu mwingine kwa sababu tu wamesikia sauti ya watu wengine wakimwita huyo mtu mwizi. Imeshawahi mara nyingi tu watu wameuawa kwa kuitwa mwizi na wagoni wao.

Mimi nasema hizi "allegations" zisipojengwa katika misingi ya kisayansi yaani kuegemea katika uthibitisho, mwisho wa siku tutakuja kuombana radhi na wale ambao leo tunawaona ni mafisadi wa kutupa. kati ya watu wanaomini kwamba Lowassa ana mapungufu makubwa ya uadilifu mimi ni mmojawapo, lakini siipuuzii nguvu ya Lowassa katika jamii na jamii ya wanasiasa hapa Tanzania.

Siku Lowassa alipofanikiwa kuwa Mwenyekiti ya kamati ya Ulinzi na mambo ya nje niliwaambia wenzangu kwamba pamoja na ufisadi wake bado ana nguvu sana kwenye siasa za Tanzania. Kama ukitaka kupambana na Barcelona na ukaichukulia nguvu yake ni sawa na Mtibwa Sugar ya Morogoro, utakuwa unajidanganya.

Kamati anayoiongoza Lowassa ndiyo inayosimamia majenerali wetu, Idara ya Usalama wa Taifa, Wizara ya mambo ya Nje ya Nchi, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. pamoja na ufisadi wote tunaoujua wa Lowassa bado jamaa ilishindikana kumzuia kupewa kamati nyeti namna hii. Mkandara hata mimi sina ndoto ya kuwa na Rais anayeitwa Edward Ngoyai Lowassa, lakini pia najua kwamba sitapiga kura peke yangu na hao wenzangu sijui mitizamo yao kuhusu Lowassa.

Hoja yangu ni lazima wale "wanaojua" madhambi ya Lowassa watupe ushahidi usiotia shaka "Beyond resoanable doubt" ili na sis tuweze kuwaeleza wengine kinagaubaga ubaya wa huyu jamaa bila ya kubuni buni mambo au kushabikia yale yanayosemwa na wengine. Ndiyo maana sipendi watu wachache tu ndiyo wayajue madhambi ya Lowassa.
Ukitaka wale "wanaojua" madhambi ya Lowasa wawape ushahidi usiotia shaka "Beyond reasonable doubt" tutakesha hapa. Ni bahati mbaya tu kwamba ile sheria iliyounda TAKUKURU ya enzi za Mwalimu ilichakachuliwa, ikapoozwa kama uji wa mgonjwa. Sheria ile ya enzi hizo ingerudi sasa rushwa ingekwisha kabisa. Sheria ile ilikuwa inaruhusu kumpeleka mtu kama Lowasa mahakamani akatuthibitishie mali alizonazo sasa kazipataje. Sasa hivi hilo halipo ndio maana ushahidi wa kumpeleka Mh Chenge mahakamani na "vijisenti" vyake imeshindikana. Enzi za Mwalimu Chenge angesimama mahakamani aileze vijisenti vile alivipataje huku maisha yake yote amekuwa mtumishi wa serikali.
Hapa ndipo tulipofikishana hata kuvuana magamba kumekuwa shughuli pevu. Unatafutwa ushahidi kama huo unaoutaka wewe!
 
Sheria ile ya enzi hizo ingerudi sasa rushwa ingekwisha kabisa. Sheria ile ilikuwa inaruhusu kumpeleka mtu kama Lowasa mahakamani akatuthibitishie mali alizonazo sasa kazipataje.
Hapa ndipo kwenye hoja yangu na mimi. Nilipotaka nithibitishiwe pasipo shaka wizi wa Lowassa si kama siamini kwamba naye amewahi kukwapua mali za umma, la hasha! Hoja yangu ni kama ile aliyowahi kuitoa Mwanakijiji humu ndani kwamba tumbane Mwendesha Mashtaka wa serikali mashitaka atumie sheria ya uhujumu uchumi kuwashitaki mafisadi sheria ambayo bado imo kwenye vitabu vyetu vya sheria.

Kusemea "mitaani" kwamba Lowassa ni fisadi hakuwezi kumzuia Lowassa kuwa Rais kama akigombea na kushinda hata kama kwa magumashi. Italia walihangaika Silvio Berlusconi kwa miaka mingi sana kwa sababu badala ya kutumia njia sahihi la kumuondoa wao waliganda kwenye fikra sahihi za kumuondoa ambazo inawezekana si njia sahihi. Lowassa hatumpendi lakini njia tunazotumia za kulalama hazitusaidii.

Nimejifunza kwamba Lowassa anawatisha baadhi yetu humu ndani ndiyo maana ni rahisi kuanzisha Thread ya Lowassa na watu wakaiparamia kama vile wanagombania mana jangwani. Wengine hawamtaki kwa sababu wanaamini 2015 ni "zamu' yao kutoa rais huku wengine tukiamini hafai kuwa rais kwa sababu hana sifa za kuwa Rais.
 
inaonesha na ww fisadi sio? hainingii akilini jinsi ww, pasco, waberoya mnanvyomtetea lowassa, au na nyie ndio akina beno malisa kapewa v8 na lowasa kakimbia side ya jk na mbilikimo wake

tanzania bira lowassa inawezekana

Sasa wewe ndugu yangu, uliesema unanifahamu vizuri kiasi cha kutaja mpaka degree yangu ya kwanza kuwa nilifaulu vizuri n.k unashindwa kujua kama mimi ni fisadi au la?

Nina uhakika utakua unajua wazi mie ni mtu wa aina gani, sio mtu wa kuiba wala kuhongwa wala sitegemei kazi serikalini kama ulivyosema nipo Private sector na naendelea kujikita kwenye private sector.
Haya bana.

Ila Lowassa ndo chaguo langu
 
Hapa ndipo kwenye hoja yangu na mimi. Nilipotaka nithibitishiwe pasipo shaka wizi wa Lowassa si kama siamini kwamba naye amewahi kukwapua mali za umma, la hasha! Hoja yangu ni kama ile aliyowahi kuitoa Mwanakijiji humu ndani kwamba tumbane Mwendesha Mashtaka wa serikali mashitaka atumie sheria ya uhujumu uchumi kuwashitaki mafisadi sheria ambayo bado imo kwenye vitabu vyetu vya sheria.

Kusemea "mitaani" kwamba Lowassa ni fisadi hakuwezi kumzuia Lowassa kuwa Rais kama akigombea na kushinda hata kama kwa magumashi. Italia walihangaika Silvio Berlusconi kwa miaka mingi sana kwa sababu badala ya kutumia njia sahihi la kumuondoa wao waliganda kwenye fikra sahihi za kumuondoa ambazo inawezekana si njia sahihi. Lowassa hatumpendi lakini njia tunazotumia za kulalama hazitusaidii.

Nimejifunza kwamba Lowassa anawatisha baadhi yetu humu ndani ndiyo maana ni rahisi kuanzisha Thread ya Lowassa na watu wakaiparamia kama vile wanagombania mana jangwani. Wengine hawamtaki kwa sababu wanaamini 2015 ni "zamu' yao kutoa rais huku wengine tukiamini hafai kuwa rais kwa sababu hana sifa za kuwa Rais.
Atabaki nani Kigarama sheria hii ikitumika kwa Lowasa? Hilo hata Lowasa alilisema siku ile anaachia ngazi na ndio kinga yake kuu na mafisadi wengine ndani ya CCM na serikali yake! Hata "heading" ya thread hii anatafutwa aliye afadhali kuliko Lowasa! Tumekwisha.
 
Atabaki nani Kigarama sheria hii ikitumika kwa Lowasa?
Wildcard kama tunahofu ya kuitumia sheria ya uhujumu uchumi basi tujaribu njia nyingine iliyotumiwa na Nelson Mandela ya Tume ya Ukweli na Maridhiano (Truth and Reconciliation Commission) ili watu watapike wanayoyajua na kisha KUSAMEHEANA. Waliopora majumba ya serikali, waliojigawia vitega uchumi vya umma kifisadi na hata wale waliojipatia madaraka kwa rushwa waachie ngazi kwa hiyari ili tuanze upya.

Lakini kwa nini tunashindwa kutumia sheria ya uhujumu Uchumi, mimi nadhani sheria ile haikutungwa kinafiki wala haina makengenza katika kushughulikia mafisadi na kwa kweli kama tutaweza kumshinikiza Mwendesha Mashitaka wa Serikali kuwashitaki Mafisadi kwa kutumia sheria hii basi tutakuwa tumepiga hatua sana katika mapambano yetu dhidi ya ufisadi. Mimi si muumini kabisa wa KULALAMA wala KUSINGIZIA wengine kwa kushindwa kuchukua hatua.
 
Wildcard kama tunahofu ya kuitumia sheria ya uhujumu uchumi basi tujaribu njia nyingine iliyotumiwa na Nelson Mandela ya Tume ya Ukweli na Maridhiano (Truth and Reconciliation Commission) ili watu watapike wanayoyajua na kisha KUSAMEHEANA. Waliopora majumba ya serikali, waliojigawia vitega uchumi vya umma kifisadi na hata wale waliojipatia madaraka kwa rushwa waachie ngazi kwa hiyari ili tuanze upya.

Lakini kwa nini tunashindwa kutumia sheria ya uhujumu Uchumi, mimi nadhani sheria ile haikutungwa kinafiki wala haina makengenza katika kushughulikia mafisadi na kwa kweli kama tutaweza kumshinikiza Mwendesha Mashitaka wa Serikali kuwashitaki Mafisadi kwa kutumia sheria hii basi tutakuwa tumepiga hatua sana katika mapambano yetu dhidi ya ufisadi. Mimi si muumini kabisa wa KULALAMA wala KUSINGIZIA wengine kwa kushindwa kuchukua hatua.
Kigarama,
Angalia haiba na hadhi ya viongozi waliohakikisha sheria ile ya uhujumu uchumi inatungwa. Mwalimu na Sokoine. Viongozi wa aina hiyo ndio hawapo kwa sasa. Hakuna dalili kwamba tutawapata kwa miaka ya hivi karibuni. Na ndio maana akina Pasco, FP, Waberoya, Mag3 wanaona Lowasa ni afadhali!
Tume kama ile ya Mandela itawaumbua karibu wote. Hawawezi kuisimamia iundwe. Si umeona walivyounda ile Tume ya Katiba mpya kimachalemachale? Mageuzi ya kweli yatawezeshwa na vyombo vyetu vya DOLA vikiamua na uzalendo ukawa chachu kwao.
 
Bwana Wildcard,

Afadhali sisi tunakubali UDHAIFU ila tunaamini tutasonga mbele maana NIA, Mikakati na UWEZO tunao.

Lowassa all they way.

Na nyie nani all the way?
 
Kigarama,
Angalia haiba na hadhi ya viongozi waliohakikisha sheria ile ya uhujumu uchumi inatungwa. Mwalimu na Sokoine. Viongozi wa aina hiyo ndio hawapo kwa sasa. Hakuna dalili kwamba tutawapata kwa miaka ya hivi karibuni. Na ndio maana akina Pasco, FP, Waberoya, Mag3 wanaona Lowasa ni afadhali!
Tume kama ile ya Mandela itawaumbua karibu wote. Hawawezi kuisimamia iundwe. Si umeona walivyounda ile Tume ya Katiba mpya kimachalemachale? Mageuzi ya kweli yatawezeshwa na vyombo vyetu vya DOLA vikiamua na uzalendo ukawa chachu kwao.
Wildcard kama unachomaanisha kwenye nyekundu ni "Nigeria Style" mimi si muumini wa hiyo style. Najaribu kujenga kwa kuzunguka hoja kwamba, wanasiasa wetu wengi Hawaaminiki kiasi kwamba tukiwakabidhi kazi ya kusafisha uozo kwenye nyanja ya siasa hawataweza.

Wanasiasa wetu wengi kilichowapeleka kwenye siasa si utashi wao wa kuhusu siasa bali ni matarajio yao ya kukidhi tamaa zao za kilafi hatimaye kufikia malengo ya matakwa yao kwa njia rahisi ya kuhujumu uchumi huku wakilindwa na mfumo uliopo kupitia siasa. wananchi wako tayari kwa mabadiliko lakini na wao wanaishi kwa kufuata mfumo huu dhalimu kuendesha maisha yao.

Jana nilikuwa kwenye kambi ya waathirika wa mafuriko pale Hananasifu. Mmoja wa waratibu wa ile kambi ambaye ni mkereketwa mkubwa wa kuiondoa CCM madarakani akaniambia "hadi hii kambi ifungwe watu watakuwa wamejenga nyumba" yeye anafanya nini kuzuia watu wasijenga nyumba kupitia janga lililowapata wakazi wa mabondeni Dar? Huyu naye ni Kamanda mpinga ufisadi!!
 
Wildcard kama tunahofu ya kuitumia sheria ya uhujumu uchumi basi tujaribu njia nyingine iliyotumiwa na Nelson Mandela ya Tume ya Ukweli na Maridhiano (Truth and Reconciliation Commission) ili watu watapike wanayoyajua na kisha KUSAMEHEANA. Waliopora majumba ya serikali, waliojigawia vitega uchumi vya umma kifisadi na hata wale waliojipatia madaraka kwa rushwa waachie ngazi kwa hiyari ili tuanze upya.

Lakini kwa nini tunashindwa kutumia sheria ya uhujumu Uchumi, mimi nadhani sheria ile haikutungwa kinafiki wala haina makengenza katika kushughulikia mafisadi na kwa kweli kama tutaweza kumshinikiza Mwendesha Mashitaka wa Serikali kuwashitaki Mafisadi kwa kutumia sheria hii basi tutakuwa tumepiga hatua sana katika mapambano yetu dhidi ya ufisadi. Mimi si muumini kabisa wa KULALAMA wala KUSINGIZIA wengine kwa kushindwa kuchukua hatua.

hiyo sheria inabaki kukimbizana na wezi wa karanga, mfano mtu yaani mteja kaibia benk na benki ni binafsi alafu anafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi lol ahggah............ inatia kichefu chefu, kesi inafika mahakamani hakimu anaitupilia mbali kuwa uhujumu lazima uwe umepora mali ya nchi na si mtu binafsi kwa hiyo wanakwenda tena kubadilisha mastaka yanakuwa jinai. hivi hawasomi hizo sheria before kumshitaki mtu au upeo ndio mdogo wa kufikiri?

lowasa hafai kuwa rais hata awe chaguo lako FP!! ni mwizi na naendelea kusema unanipa mashaka sana pale unapokuwa una chaguo la mtu fisadi come back to your sense ww ni mtu msafi kama ulivyosema na upo private sector basi endelea kumsaport mtu safi nitakuelewa!
 
Mkandara kwa nini umengia kwenye mtego wa kukumbatia falsafa ya George Bush ya "either you are with us or against us"? Mimi simuungi mkono Lowassa lakini pia siwaungi mkono watu wanaopenda kufanya ukasuku. siipendi tabia ya watu wanaoua mtu mwingine kwa sababu tu wamesikia sauti ya watu wengine wakimwita huyo mtu mwizi. Imeshawahi mara nyingi tu watu wameuawa kwa kuitwa mwizi na wagoni wao.

Mimi nasema hizi "allegations" zisipojengwa katika misingi ya kisayansi yaani kuegemea katika uthibitisho, mwisho wa siku tutakuja kuombana radhi na wale ambao leo tunawaona ni mafisadi wa kutupa. kati ya watu wanaomini kwamba Lowassa ana mapungufu makubwa ya uadilifu mimi ni mmojawapo, lakini siipuuzii nguvu ya Lowassa katika jamii na jamii ya wanasiasa hapa Tanzania.

Siku Lowassa alipofanikiwa kuwa Mwenyekiti ya kamati ya Ulinzi na mambo ya nje niliwaambia wenzangu kwamba pamoja na ufisadi wake bado ana nguvu sana kwenye siasa za Tanzania. Kama ukitaka kupambana na Barcelona na ukaichukulia nguvu yake ni sawa na Mtibwa Sugar ya Morogoro, utakuwa unajidanganya.

Kamati anayoiongoza Lowassa ndiyo inayosimamia majenerali wetu, Idara ya Usalama wa Taifa, Wizara ya mambo ya Nje ya Nchi, Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. pamoja na ufisadi wote tunaoujua wa Lowassa bado jamaa ilishindikana kumzuia kupewa kamati nyeti namna hii. Mkandara hata mimi sina ndoto ya kuwa na Rais anayeitwa Edward Ngoyai Lowassa, lakini pia najua kwamba sitapiga kura peke yangu na hao wenzangu sijui mitizamo yao kuhusu Lowassa.

Hoja yangu ni lazima wale "wanaojua" madhambi ya Lowassa watupe ushahidi usiotia shaka "Beyond resoanable doubt" ili na sis tuweze kuwaeleza wengine kinagaubaga ubaya wa huyu jamaa bila ya kubuni buni mambo au kushabikia yale yanayosemwa na wengine. Ndiyo maana sipendi watu wachache tu ndiyo wayajue madhambi ya Lowassa.

mwe watanzania!! watanganyika!! nyie ndio mna hearsay oh lowassa oh lowassa!!! kwenye red riport ya richmond sio ushahidi tosha kwako? mwe watanganyika!!!
 
Samaki mtamu mkaange kwa mafuta yake yaani mafuta ya samaki, Uraisi mtamu unapatikana kwa mbinu ya kutumia fedha kuhonga wapiga kura na hii ndiyo maana yake tena fedha dhalimu zilizopatikana ndani ya nchi kwa kuwanyonya wananchi a.k.a ufisadi,waje waje tu watulipe na sisi ila watajuta kuzaliwa TZ.
 
Duh!! Masabuda!!! Sasa ndo nakushangaa rasmi! Duh!
Upo Iceland au? Lowassa kasema nini juzi kwenye NEC ya CCM?

Natural justice inayojadiliwa humu JF wewe husomi?
 
mwe watanzania!! watanganyika!! nyie ndio mna hearsay oh lowassa oh lowassa!!! kwenye red riport ya richmond sio ushahidi tosha kwako? mwe watanganyika!!!
Kwa mwendelezo wa jambo lenyewe la Richmond inaonyesha kwamba anayehusika ni JK na Lowassa alikuwa ni mjumbe tu. Dont kill a messenger!! Msimamo wangu siku zote huwa siungi mkono jambo kiushabiki, Lowassa hafai lakini si kwa sababu wengine wamesema hafai!!
 
Duh!! Masabuda!!! Sasa ndo nakushangaa rasmi! Duh!
Upo Iceland au? Lowassa kasema nini juzi kwenye NEC ya CCM?

Natural justice inayojadiliwa humu JF wewe husomi?

ndio kaka huku kunabalidi sana. back to the point ww unataka kunirudisha nyuma kwenye naturla justice na nimemeandika sana cheki my coments. hayo maneno unayaamini? obvious ni ndio na kwa nini hakuyasema bungeni? na kwa nini arudi bungeni badala yake anaishia kwenye tv tena ya uma tbc na makanisani mpaka kwa wakatoliki sasa!

hainingii akilini kwa mtu msafi kama ww ukawa na changuo la mtu MCHAFU
 
Hiyo sheria inabaki kukimbizana na wezi wa karanga,
Na mimi najua hii sheria haitumiwi ipasavyo, lakini kosa si la wale wasiyoitumia bali la sisi ambao tunajua kwamba kama sheria ya Uhujumu Uchumi ikitumiwa dhidi ya mafisadi itatufaidia. Tatizo la mijadala mingi humu ndani mategemeo yetu yooote huwa tunayaweka kwa wanasiasa. Bahati mbaya hata huko Ulaya wanasiasa wako vile walivyo kwa sababu wananchi wao walipigana kufa na kupona kutengeneza jamii ambayo haiendeshwi na wanasiasa balli wanasiasa wanashika dhamana kwa niaba ya wananchi.

Hapa kwetu tunataja majina ya watu badala ya kuweka mikakati ya kuhakikisha yeyote ajaye hawezi kutuendesha kinyume cha matakwa yetu. Watu wanaoonekana leo "wasafi" wanaweza kubadilika mbele ya safari na kama hatujajenga tabia ya kupambana mpaka mwisho basi tujue kwamba hakuna kitachobalika zaidi ya majina ya vyama na viongozi wake.
 
mara nyingi wabongo hatuko logic, ili rais asimame nani anamsimamisha? bila shaka chama chake...km JK hafai maana yke ccm haifaii. hao unaofikiria ni safi ndani chama kwa nini hawakusimama kupinga JK kupita? kama taifa tuna mambo muhimu ya kujadili mf. uzalendo ni nini? uzalendo unajitokezaje kwa mtu moja moja? kwa chama? kwa taasisi?...je tunahitaji kiongozi mzalendo au watu wazalendo?... hatupaswi kufikiri juu ya majina.
 
Bwana Masabuda Umesema hivi:

"hainingii akilini kwa mtu msafi kama ww ukawa na changuo la mtu MCHAFU"

Sasa ndo ujiulize, kwanini mie mtu msafi unayejua wazi kuwa rushwa kwangu mwiko, kwanini nimsapoti unayemuona ni mchafu.
Jibu ni simplo: Lowassa sio mchafu kama ulivyofanywa uamini. Na ndani ya CCM hakuna aliye msafi kuliko Lowassa miongoni mwa wagombea urais mpaka sasa wanne:

Lowassa, Bernard, Sumaye na Six.

Ukipima utendaji, uchafu na mengineo. Lowassa anaibuka kidedea wa kugombea urais 2015.

Mbona umekwepa aliyoongea Lowassa kwenye NEC ya CCM majuzi? Kama Lowassa ni mchafu kwanini hawamfukuzi CCM?
 
mara nyingi wabongo hatuko logic, ili rais asimame nani anamsimamisha? bila shaka chama chake...km JK hafai maana yke ccm haifaii. hao unaofikiria ni safi ndani chama kwa nini hawakusimama kupinga JK kupita? kama taifa tuna mambo muhimu ya kujadili mf. uzalendo ni nini? uzalendo unajitokezaje kwa mtu moja moja? kwa chama? kwa taasisi?...je tunahitaji kiongozi mzalendo au watu wazalendo?... hatupaswi kufikiri juu ya majina.
 
Hivi kwanini recently wameibuka watu wengi kumuongelea Lowassa?
Ina maana huyu jamaa ana uwezo sana na anaogopwa na wapinzani wake?
 
Back
Top Bottom