Ndalichako ashauri Maboss kuwawekekea Gym wafanyakazi makazini

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako amewagiza waajiri kuweka mifumo kwa wafanyakazi wao ya kuwewezesha kufanya mazoezi ikiwemo ‘gym’ ili kuwa na wafanyakazi wenye afya njema.

Waziri huyo amesema moja ya sababu ya kutaka gym ziwepo maeneo hayo ya kazi ni kutokana na waajiri kuhitaji watu wenye afya njema ili kuwa na uzalishaji wenye tija hivyo suala la kuweka mfumo wa kufanya mazoezi litakuwa jambo jema.

Jingine amesema ni kupunguza magonjwa yasiyoambukiza yanayochangiwa kwa kiasi kikubwa na mfumo wa maisha ikiwemo kutofanya mazoezi.

“Magonjwa hayo yasiyo ya kuambukiza kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), yamekuwa yakichangia asilimia 33 ya vifo vyote duniani.

“Lakini ukiacha vifo, pia yamekuwa na gharama katika kuwatibu wagonjwa wake na hivyo kuiongezea serikali mzigo, fedha ambazo zingeweza kufanyia shughuli nyingine za kuwaletea wananchi maendeleo, hivyo tufanye mazoezi kuyapunguza,” amesema.
 
Daah wanapewa chai sasa wanataka Gym baadae wakiona Gym haiwasaidii watasema wawekewe hospital makazini kinachotakiwa ni wafanyakazi watambue umuhimu wa mazoezi kwa pamoja au wakitenga muda wenyewe hiyo itawasaidia kupunguza baadhi ya magonjwa yasio ya kuambukiza..
 
Mazoezi ni
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako amewagiza waajiri kuweka mifumo kwa wafanyakazi wao ya kuwewezesha kufanya mazoezi ikiwemo ‘gym’ ili kuwa na wafanyakazi wenye afya njema.

Waziri huyo amesema moja ya sababu ya kutaka gym ziwepo maeneo hayo ya kazi ni kutokana na waajiri kuhitaji watu wenye afya njema ili kuwa na uzalishaji wenye tija hivyo suala la kuweka mfumo wa kufanya mazoezi litakuwa jambo jema.

Jingine amesema ni kupunguza magonjwa yasiyoambukiza yanayochangiwa kwa kiasi kikubwa na mfumo wa maisha ikiwemo kutofanya mazoezi.

“Magonjwa hayo yasiyo ya kuambukiza kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), yamekuwa yakichangia asilimia 33 ya vifo vyote duniani.

“Lakini ukiacha vifo, pia yamekuwa na gharama katika kuwatibu wagonjwa wake na hivyo kuiongezea serikali mzigo, fedha ambazo zingeweza kufanyia shughuli nyingine za kuwaletea wananchi maendeleo, hivyo tufanye mazoezi kuyapunguza,” amesema.
Namkumbusha waziri kuwa afya njema kwa maana ya kuepuka non communicable diseases hasa kuwa na proper BMI zetu ni lazima tuzingatie;
20% ni mazoezi
80% nama ya ulaji
Serikali ipunguze vifuatavyo maofisi;
1. Chai, refleshments kama artificial Juices,

2. Misosi kwenye vikao ilenge misosi ya diet mbogamboga etc...wanga na jamii yake viwe discouraged.
3. Iwe ni lazima kufanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki kwa kuanza tuanze kwa kutembea tukisubiri budget za Gym next FY.

Lakini namkumbusha pia waziri kuwa Mazoezi ni ari, commitment na nia ya dhati, u can install a high cost mashines lkn km hakuna utayar wa wao kufanya mazoezi is nothing.
 
Mazoezi ni

Namkumbusha waziri kuwa afya njema kwa maana ya kuepuka non communicable diseases hasa kuwa na proper BMI zetu ni lazima tuzingatie;
20% ni mazoezi
80% nama ya ulaji
Serikali ipunguze vifuatavyo maofisi;
1. Chai, refleshments kama artificial Juices,

2. Misosi kwenye vikao ilenge misosi ya diet mbogamboga etc...wanga na jamii yake viwe discouraged.
3. Iwe ni lazima kufanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki kwa kuanza tuanze kwa kutembea tukisubiri budget za Gym next FY.

Lakini namkumbusha pia waziri kuwa Mazoezi ni ari, commitment na nia ya dhati, u can install a high cost mashines lkn km hakuna utayar wa wao kufanya mazoezi is nothing.
Hii 20/80 rule wengi hawaijui. Fanya mazoezi utakavyo lakini kama diet ni mbovu hamna cha kupungua kwa minyama uzembe
 
Waache wajifie humo kazini watu wapate Ajira , vipaumbele vya kipumbavu sana khs gym kuwekwa maofisini na huku tuna changamoto kibao hakuna maji mijini ,vijijini ,umeme nao ..... eti gym
Real I miss CORONA tafadhali njoo utusafishie huko juu wamejisahau sana...
 
Back
Top Bottom