Nchi hii inapoteza uelekeo, wasomi mko wapi?

Tatizo ni moja tu mkuu watu waliosoma kukubali kutumika kisiasa tena chini wa wasiosoma!!!!

Ok wote hatuwezi kuwa viongozi lakini hata wanapokosea kuwaambia pia hao waliosoma hawataki!!!! Yaani wamekuwa watumwa wa wanasiasa!!!!!

Mengine ni kukosa uzalendo na kuendekeza sifa na njaa,unakuta msomi mzuri tu eti anashika mkoba wa mtu ambaye hana tija kwa Taifa ili tu awe karibu na kiongozi na hatumii usomi wake kumshauri huyo muhusika!!!!

Ukiniuliza tuanzie wapi mimi ntasema mawaziri wasiwe wabunge kwanza ili nafasi nyeti za nchi zishikwe kwa minajili ya utaalamu na uzoefu wa lile mtu alilosomea na kufanyia kazi!!!! Hii itaamsha ari na hadhi ya elimu na utaalamu na pia itajenga mipaka ya kazi na heshima kati ya wanasiasa na professionals!!!!
Hivi niulize usomi ni sifa au Cheo? Huko kwenye wizara wapo mawaziri ambao pia ni ma-professor na wengine ni PhD.sitawataja kwakuwa mnawafahamu. Kwa kudokeza tu wapo prof. Maghembe, Msolwa n.k. wamefanya nini? kama hawajafanya kitu basi tukubaliane kuwa uongozi ni karama zaid ya elimu.
 
Maneno yako tu yanaonesha wewe ni bongo flavor. Utaongeleaje miaka ya 60, miaka ambayo ndo kwanza tulikuwa tumetoka kwenye mikono ya wakoloni? jipambanue tu kuwa wewe ni bongoflaver kuliko kuzunguka mbuyu.
Miaka ya 60 hata uhuru ulikuwa bado!
 
Nimesikia na kusoma kwenye vyombo vya habari mbalimbali kuwa kuna wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dar-es- salaam wameelani vikali kauli ya mwenyekiti wa CHADEMA, shida yangu haipo kwenye wao kulaani hiyo kauli maana mimi sio mshabiki wa vyama vya siasa ila shida yangu iko kwa wasomi hawa wasioweza kutafuta 'solution' ya matatizo yanayoikumba nchi yao na wakiwa wamenyamaza kimya kwenye mambo ya msingi yahusuyo nchi, utawasikia tu 'boom' likiwa limechelewa au kujibu/kulaani kauli za wanasiasa!

Kuna fedha za 'account' ya escrow inayohusiana na tanesco wao hiyo kwao sio muhimu, hizi fedha zinazotafunwa bungeni bila kupata katiba woa hawatafuti 'solution' ya kuepusha fedha hizo zisitafunwe bali wanakaa kudandia hoja za wanasiasa, hii nchi kama inatengeneza wahitimu wa vyuo vikuu wa staili hii basi tujiandae kutawaliwa na 'vichaa' wasioweza kubuni na kutatua vitu vya msingi bali kudandia hoja na na kwenda na matukio!

wanafunzi jipangeni, hamuutendei haki ubongo wenu, elimu yenu, nchi yenu bali mnataka umaarufu wa kipumbavu!
 
Tanzania ukitaka kuonekana mzalendo fanya haya
-piga makofi na vigelegele kwa kila asemacho kiongozi wa nchi
-kubali kila anachofanya kiongozi
-kubali kuwa rushwa ni mtu kupewa zawadi na si dhambi
-kubali yote ya CCM
-kubali kuwa kuiba hela ya Serikali si dhambi.

Hapo wewe utakuwa mzalendo safi unayependa nchi yako Tanzania.
Inatia aibu kwa hao wanaojiita wasomi kuona kuwa wanachofanya katika Hilo bunge la katiba ni SAWA.
 
mkuu unaambiwa tanzania kati ya watu 100 watu 49 ni wadumavu wa akili na mwili....

maisha duni, elimu duni, lishe duni, mazingira duni, ndio maana uwezi kumu tofautisha mwanafunzi wa chuo kikuu wa tanzania na mtoto wa darasa la pili wa UK.
 
Hakuna mtu aliyelaani kauli ya mbowe bali ni watu wanaofanywa kwa hila ili ionekane hivyo,ni ujinga,tutawafruta
 
Mkuu hao wanaojiita wanafunzi wa sasa ni shidaa sijui wamerogwa na nani, kwasababu hawajiamini wanaishi kwa hofu kana kwamba wanategemea matuta kwa kila kitu, jitu lina chukua degree yake but limejaa hofu ya ajira shame on them, yanafundishwa ujasilia mali ili wajiamini kuwa bado wananafasi ya kujiajiri lakini wapo full mashaka. Nawashauri zingatieni mstakabali wa nchi yetu.
 
Kwanza hawajajua siku vyuo vyao vitakapofunguliwa. kwa sababu Bodi ya Mikopo haina pesa, pesa yote ieenda kwa Bunge la katiba. Chadema wanawapigania ili hospitali zipate madawa, shule ziwe na madawati na wasome wasome kwa raha, hawa washenzi wa uvccm wanakula matapishi yao. Kweli? Ninaamini kuwa kati ya watu 100 watu 49 wanaupungufu wa akili ikiwa ni pamoja na hao wanaojiita wasomi
 
mh! kama 49 wana upungufu wa akili basi tumekwisha! mana tutakua na 'waropokaji' wengi kwenye hii nchi kushinda wajenga hoja! Nani ameturoga kwenye hii nchi! yani kila kitu siasa hakuna vitu 'real' hata!
 
hawa ni wachumia tumbo mkuu sio wanafunzi wanafunzi wamefunga vyuo hawa wametoka wapi kuwasemea wenzao kwanza wakifungua vyuo utasikia boom alitoshi sasa sijui wataanzaje kuandamana
 
Msomi mwenye njaa ni sawa na Mjinga mwenye njaa; HAKUNA TOFAUTI HAPA TZ, unasoma ujikombe sio uboreshe mazingira unayoyakabiri
 
Hivi wakuu, hawa wanafunzi wa sasa wa vyuo vikuu wana hadhi ya kuitwa eti "Wasomi wa Nchi hii"???
 
WAPO 51 KATI YA 100 wenye mbongo ya kweli, na hao CCM inawatesa popote walipo iwe makazini au vyuoni, nyumbani au mitaan
 
CCM ingekuwa mche tayari mizizi yake imeshaliwa na mchwa. Tusiuchimbue au tusiukate bado CCM utakufa tu! ALUTA....
 
Sisi tuliotoka vyuo vikuu imefika mahali hata kusema kuwa umesoma ni aibu kubwa ,kwani fikra zetu hazina tofauti na wale tuliowaacha mtaani tukaenda kusoma elimu ya juu.Nataka kusema leo ukitaka kuleta mabadiliko katika nchi hii kwa kuwategemea wasomi wa kizazi hiki utachelewa sana .Wengi wao hawajitambui, waoga ,wenye fikra za utegemezi.MUNGU isaidie Tanzania
 
Ukipiga kelele hizo na hela za escrow zitarudishwa?? Hela ya EPA imerudi??
 
mtaala wa chuo kikuu ulishabadilika kitambo... Kama unabisha ni aina ya wanafunzi wanaotoka kutoka katika vyuo , vyuo vyote , kutokana na mfumo uliopo ni assemby line au mass production au voda fasta tu.

Usitegemee watatoa msimamo na ukisikia wametoa msimamo fulani, chunguza kuna rupia imepenyezwa mahali fulani:flame:
 
Back
Top Bottom