Kuboresha mafao ya viongozi wa kitaifa kwa sheria za kawaida ni ukiukwaji wa katiba ya nchi hii

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Kuna sheria iko jikoni yenye kulenga kuboresha mafao ya viongozi wa kitaifa na kuhakikisha wenza wa viongozi hao kulipwa 25% kama mafao ya kustaafu. Pia familia zao kuvuna 60% ya mshahara mara baada ya viongozi wa kitaifa kufariki dunia.

La ajabu, huu muswada pamoja na kuchochewa na mapendekezo ya mbunge na mke wa Rais mstaafu mama Salma Kikwete aliyoyatoa bungeni tarehe ya April 22, 2022 katika Bajeti ya Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (2022/23) lakini pia yamo kwenye Rasimu ya marekebisho ya katiba iliyopendekezwa na bunge maalumu la katiba.

Yapo matatizo mengi kama hili bunge litapitisha muswada huo. Tatizo kuu mafao ya viongozi wa kitaifa wastaafu ni ya kikatiba na bunge halina mamlaka ya kuyaboresha bila ya kurekebisha katiba!

Tatizo kubwa ni kupanua nyufa ambazo zinatokana na viongozi wa kitaifa kuyatumia madaraka yao vibaya ya kujipendelea wao wenyewe kila kukicha.

Sheria tajwa inalenga kuimarisha matabaka ya wanaotawala na watawaliwa kwa sababu inapokuja watumishi wa umma wasiyo wa kitaifa utaona bunge hilo hilo hukaza buti kudhoofisha haki za wafanyakazi wa ngazi za chini na kuwaongezea ufukara mara wanapostaafu.

Aidha bunge limeweka ukomo wa umri wa kulipwa haki za kustaafu kwa watumishi wa kawaida na kuwa miaka 60 wakati kabla ya hapo ulikuwa miaka 50-55. Bunge halijali mtumishi akistaafu hana kipato na kumnyima mafao ya kustaafu hadi afikishe miaka 60 ni kumwongezea umasikini.

Pili, bunge hilo hilo limejenga matabaka wako watumishi wa umma wa kitaifa na wasiyo wa kitaifa huku wa kitaifa wanacho kikotoo tofauti na wale wasiyo wa kitaifa. Kikotoo cha viongozi wa kitaifa ni asilimia ya mshahara wa sasa wa cheo kilekile alichoondokea wakati wale wasiyo wa kitaifa msingi wake kwanza haijulikani na pia hujikita kwenye majumlisho ya mtumishi husika aliyolipwa wakati wa utumishi wake na wala siyo asilimia ya cheo alichoondoka nacho.

Tatizo ni kuwa Kikotoo cha viongozi wa kitaifa kigezo chake kikuu ni kumlinda mstaafu dhidi ya mfumuko wa bei na mapato. Wakati cha watumishi wasiyo viongozi wa kitaifa kikotoo chao kinalenga kudidimiza mafao ya kustaafu kwa kuhakikisha hakuna uhusiano wowote ule na mfumuko wa bei na mapato!

Hili ni tatizo kubwa la kwanini hakuna kikotoo kimoja kwa watumishi wote wa umma? Lengo la kujitawala lilikuwa kuamini dhana ya kuwa kwa kuwa viongozi wanatoka miongoni mwetu basi watafanya maamuzi yanaboresha masilahi ya wote lakini hali halisi ni kinyume chake.

La kusikitisha sasa hata wenza na familia za wastaafu sasa kulipwa mafao endapo viongozi wa kitaifa watakuwa wamefariki dunia. Tuna maswali mengi ya kujiuliza. Mwajiriwa wa umma ni nani haswa? Tunapomwajiri kiongozi wa kitaifa huwa tunaajiri na familia yake pia? Ni wapi kwenye katiba inasema hivyo?

Katiba yetu haitambui wenza na familia za viongozi wa kitaifa kama ni waajiriwa wa umma na kutunga sheria ya mafao ya wenza wa marehemu waliokuwa viongozi wa kitaifa ambao haki zao ni za kikatiba ni ukiukwaji wa katiba. Inabidi kwanza katiba iwatambue wenza wa viongozi wa kitaifa na familia zao ni watumishi wa umma ndipo hapo haki za kustaafu zitawahusu. Bunge haliwezi kuajiri familia ya wastaafu wa viongozi wa kitaifa na kuwalipa mafao ya kustaafu wakati katiba haiwatambui. Na maelezo yanahitajika kwanini watumishi wengine wasio wa kitaifa familia zao nazo siyo sehemu ya ajira wa umma? Zoezi zima lina mwelekeo wa kuondoa misingi ya usawa.

Kama bunge linataka kuongeza nyufa za matabaka miongoni mwa watumishi wa umma basi warekebishe katiba kama rasimu ya marekebisho ya katiba iliyopitishwa na bunge haramu la katiba.

Bunge likifanya hivyo litakuwa halijakiuka katiba bali litakuwa limewabagua watumishi wengine wa umma ambao siyo viongozi wa kitaifa ambao wenza wao na familia zao hawatalipwa baada ya wao kuaga dunia.

USHAURI

Hili bunge ni kinara sana wa kupitisha maazimio na sheria zinazokinzana na katiba ni vyema sasa mkaanza kurudi kwenye mstari na kuikataa hii sheria ya mafao ya wenza na familia za viongozi wa kitaifa waliofariki dunia.

Sababu kuu ya kuikataa hii sheria ni kuwa bunge halina mamlaka ya kubuni ofisi zaidi ya zile zilizoainishwa kwenye katiba. Ili mwenza wa Rais alipwe hiyo 25% ya mshahara wa mstaafu inabidi awe alikuwa akilipwa yeye mwenyewe huo mshahara kama mtumishi wa umma. Kama hakuwa halipwi sasa hoja ya malipo tajwa inatoka wapi?
 
Nani wa kuheshimu hako Kakitabu?
Kanyaga kabisa kakitabu
20230908_040257.jpg
 
Asilimia 90 ya wabunge Mkuu wa chama chao ndio Rais wa nchi, ukiona jambo limepita hapo jua lina baraka kabisa za mwenyekiti wao, hawajakurupuka, tutawaone bure wabunge, kansa inajulikana ilipojificha.
 
Kuna sheria iko jikoni yenye kulenga kuboresha mafao ya viongozi wa kitaifa na kuhakikisha wenza wa viongozi hao kulipwa 25% kama mafao ya kustaafu. Pia familia zao kuvuna 60% ya mshahara mara baada ya viongozi wa kitaifa kufariki dunia.

La ajabu, huu muswada pamoja na kuchochewa na mapendekezo ya mbunge na mke wa Rais mstaafu mama Salma Kikwete aliyoyatoa bungeni tarehe ya April 22, 2022 katika Bajeti ya Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (2022/23) lakini pia yamo kwenye Rasimu ya marekebisho ya katiba iliyopendekezwa na bunge maalumu la katiba.

Yapo matatizo mengi kama hili bunge litapitisha muswada huo. Tatizo kuu mafao ya viongozi wa kitaifa wastaafu ni ya kikatiba na bunge halina mamlaka ya kuyaboresha bila ya kurekebisha katiba!

Tatizo kubwa ni kupanua nyufa ambazo zinatokana na viongozi wa kitaifa kuyatumia madaraka yao vibaya ya kujipendelea wao wenyewe kila kukicha.

Sheria tajwa inalenga kuimarisha matabaka ya wanaotawala na watawaliwa kwa sababu inapokuja watumishi wa umma wasiyo wa kitaifa utaona bunge hilo hilo hukaza buti kudhoofisha haki za wafanyakazi wa ngazi za chini na kuwaongezea ufukara mara wanapostaafu.

Aidha bunge limeweka ukomo wa umri wa kulipwa haki za kustaafu kwa watumishi wa kawaida na kuwa miaka 60 wakati kabla ya hapo ulikuwa miaka 50-55. Bunge halijali mtumishi akistaafu hana kipato na kumnyima mafao ya kustaafu hadi afikishe miaka 60 ni kumwongezea umasikini.

Pili, bunge hilo hilo limejenga matabaka wako watumishi wa umma wa kitaifa na wasiyo wa kitaifa huku wa kitaifa wanacho kikotoo tofauti na wale wasiyo wa kitaifa. Kikotoo cha viongozi wa kitaifa ni asilimia ya mshahara wa sasa wa cheo kilekile alichoondokea wakati wale wasiyo wa kitaifa msingi wake kwanza haijulikani na pia hujikita kwenye majumlisho ya mtumishi husika aliyolipwa wakati wa utumishi wake na wala siyo asilimia ya cheo alichoondoka nacho.

Tatizo ni kuwa Kikotoo cha viongozi wa kitaifa kigezo chake kikuu ni kumlinda mstaafu dhidi ya mfumuko wa bei na mapato. Wakati cha watumishi wasiyo viongozi wa kitaifa kikotoo chao kinalenga kudidimiza mafao ya kustaafu kwa kuhakikisha hakuna uhusiano wowote ule na mfumuko wa bei na mapato!

Hili ni tatizo kubwa la kwanini hakuna kikotoo kimoja kwa watumishi wote wa umma? Lengo la kujitawala lilikuwa kuamini dhana ya kuwa kwa kuwa viongozi wanatoka miongoni mwetu basi watafanya maamuzi yanaboresha masilahi ya wote lakini hali halisi ni kinyume chake.

La kusikitisha sasa hata wenza na familia za wastaafu sasa kulipwa mafao endapo viongozi wa kitaifa watakuwa wamefariki dunia. Tuna maswali mengi ya kujiuliza. Mwajiriwa wa umma ni nani haswa? Tunapomwajiri kiongozi wa kitaifa huwa tunaajiri na familia yake pia? Ni wapi kwenye katiba inasema hivyo?

Katiba yetu haitambui wenza na familia za viongozi wa kitaifa kama ni waajiriwa wa umma na kutunga sheria ya mafao ya wenza wa marehemu waliokuwa viongozi wa kitaifa ambao haki zao ni za kikatiba ni ukiukwaji wa katiba. Inabidi kwanza katiba iwatambue wenza wa viongozi wa kitaifa na familia zao ni watumishi wa umma ndipo hapo haki za kustaafu zitawahusu. Bunge haliwezi kuajiri familia ya wastaafu wa viongozi wa kitaifa na kuwalipa mafao ya kustaafu wakati katiba haiwatambui. Na maelezo yanahitajika kwanini watumishi wengine wasio wa kitaifa familia zao nazo siyo sehemu ya ajira wa umma? Zoezi zima lina mwelekeo wa kuondoa misingi ya usawa.

Kama bunge linataka kuongeza nyufa za matabaka miongoni mwa watumishi wa umma basi warekebishe katiba kama rasimu ya marekebisho ya katiba iliyopitishwa na bunge haramu la katiba.

Bunge likifanya hivyo litakuwa halijakiuka katiba bali litakuwa limewabagua watumishi wengine wa umma ambao siyo viongozi wa kitaifa ambao wenza wao na familia zao hawatalipwa baada ya wao kuaga dunia.

USHAURI

Hili bunge ni kinara sana wa kupitisha maazimio na sheria zinazokinzana na katiba ni vyema sasa mkaanza kurudi kwenye mstari na kuikataa hii sheria ya mafao ya wenza na familia za viongozi wa kitaifa waliofariki dunia.

Sababu kuu ya kuikataa hii sheria ni kuwa bunge halina mamlaka ya kubuni ofisi zaidi ya zile zilizoainishwa kwenye katiba. Ili mwenza wa Rais alipwe hiyo 25% ya mshahara wa mstaafu inabidi awe alikuwa akilipwa yeye mwenyewe huo mshahara kama mtumishi wa umma. Kama hakuwa halipwi sasa hoja ya malipo tajwa inatoka wapi?
Siku wakianza kufuata Katiba naomba NI-Tag.
 
Imeandikwa wafalme wenu watajikuza na kujiona ni miungu kila kukicha wakitunga sheria za kujineemesha wao na vitambi vyao.

Lakini sasa asema BWANA wa Majeshi watakula lakini hawatashiba, watalala vitandani mwao lakini hawatapata usingizi kwa sababu wameabudu matumbo yao badala ya Muumba wao.

Khofu ya kisichokuwepo itawatesa siku za uhai wao na wataona taharuki popote walipo kwa sababu hawakuwajali watu wangu.

Na jina la Bwana lihidimiwe.
 

Attachments

  • PSX_20231102_225147.jpg
    PSX_20231102_225147.jpg
    243.5 KB · Views: 4
SHERIA YA MAFAO YA WENZA NI WIZI WA MALI YA UMMA ULIOHALALISHWA NA BUNGE!


View: https://youtu.be/fYGKoLzTWRg?si=s79zKsc5ji1ieBSX


View: https://youtu.be/-WQuc0faRio?si=vRNwF4bpOY48bg0f


Laana ya kutegemea fadhila ili uvute siku ni kuwa unaukana ubunifu aliokupa Mwenyezi Mungu na unabakia kuwa mdoezi wa jasho la walalahoi.

Hebu tujiulize hawa wastaafu wanalolote la maana waliwahi kutufanyia zaidi ya kulambalamba kodi zetu.

Nchi ambazo hazimjui Mwenyezi Mungu viongozi wake hukaza buti kujirundikia mapochopocho ambayo wala hata hawayahitaji.

Mwasisi wa hii sheria tunamwona anajikokota na kuchechemea kwa magongo lakini bado analitumikia tumbo lake.

Badala ya kuwapigania wapigakura wake yeye kashinikiza alipwe pensheni na hawa vibogoyo wetu wamesalimu amri wakijua hastahili lakini wako kifungoni "state capture" kwa kubebwa na mbeleko za wastaafu.

Ikija masilahi ya raia huwalisha maneno ya matumaini: kunyweni mtori kwani minofu mtaikuta chini wakati wao wanatafuna minofu ambayo haina baraka ya Mwenyezi Mungu.

Zaidi ya miaka 20 iliyopita kuna profesa mmoja alisema huyu Nyerere Tanzania mtamkumbuka baada ya kuona ulafi wa watakaomfuata watajirundikia kila kitu ila khofu yao ya kuogopa kifo chao ndiyo itakuwa shubiri yao maana hawana mbingu nyingine ila hapa wamewasili.

Wasichojua wanaacha mbachao kwa msala upitao.

Hivi tofauti ya viongozi wa kitaifa na watumishi wengine wa umma ni nini haswa?

Hawa kwenye majukwaa kwa unafiki usiyo na kifani hujiita na kujibatiza watumishi na hata hutupigia magoti na kujigalagaza kwenye mavumbi kama vile unafiki unalipa lakini wakitoka hapo wanapakia hadi wanavimbiwa. Baadaye hukimbilia Ulaya kusaka tabibu wa ulafi wao! We repeat shame on you, all!

Hii sasa ni aibu yenu mmejivua nguo mchana kweupe kila mmoja sasa anaukodolea macho utupu wenu lakini ulafi wenu umewapofua macho hamwoni mko uchi.

Akina Adam na Hawa walipomkana Mwenyezi Mungu waliona haya wakajificha lakini ninyi kwisha habari yenu.

Sisi kazi yetu ni kusubiri ratiba ya mazishi yenu mmoja baada ya mwingine na tutakapokuwa tunahudhuria mazishi yenu hatuji kuwalilia bali kuona mali mlizojilimbikizia zitakuwa za nani? Jisomee Luka 12:15-21 & Zaburi 91: 8

Huu ubaguzi ndiyo utamaduni wetu maana utamaduni usiojulikana hutumika kuhimiza maadili



Kweli mwamba ngoma huvutia kwake. Huku wanahimiza tujibane huku walafi hawa wanaendelea kujilimbikizia kila kitu sijui mnajidanganya hamtakufa na kuacha kila kitu.

Na hata hao wenza na watoto mnaowarundikia mali za umma kuna siku kapu...umeme utakatika tu sasa ubinafsi wa kupitiliza unathibitisha ututusa wenu wa kutomtafuta Mwenyezi Mungu kabla hajawapa hizo nafasi ambazo sasa mnajikuza na kujiona ni bora kuliko wengine.

Kuleni lakini mjue na msisahau mna laana ya ulafi na baada ya miezi michache atazuka juha mwingine atasema wazazi wanapostaafu watoto wa viongozi wa kitaifa mnawaachaje na hawa wafungwa wa fadhila za kitaifa watakimbia na kuja na marekebisho ya kuboresha matumbo ya familia za viongozi wa kitaifa ambao utumishi wao hauna kichwa wala miguu.

Yaani ni mzigo kwa wananchi yaani ubunifu wao ni michoro ya kujilimbikizia mali hawana jipya.

Tunahitaji sababu viongozi wa kitaifa huu umungu wenu hamwoni ni mtego wa panya utakaowaongezea maumivu humu duniani kwa sababu badala ya kuwa wanyenyekevu na kutambua nchi hii haiwezi kuwagharimia wenza kwa sababu ni nchi ya masikini wa kutupwa ninyi mnajidanganya tutunge sheria za kuhalalisha na kuulinda ufisadi wetu!

Shame on you!

Huku mnatembeza bakuli huku ni viwavi jeshi kama hamjitambui basi imekula kwenu.

Wenza wa watumishi wengine mnawaachaje? Msichojua athari kubwa ya ubaguzi ni kuchochea wizi, ubadhirifu na rushwa ambayo sasa inahalalishwa na ufisadi uliohalalishwa na sheria za wanadamu.


Watu wanawaona kila siku ni ninyi tu mishahara iko juu, posho juu, mafao ya kustaafu juu, matibabu ulaya lakini huku mnasema mmeboresha huduma za afya ambazo ninyi wenyewe hamzitumii.

Kama huduma za afya ni bora kiguu kwa njia St. THOMAS uingereza unaenda kuangua?

Mjipime au kuna siku panya road watawapima na hao askari wenu watajificha yasiwakute maovu ambayo Mwenyezi Mungu kawaandalia.

Kwa hii kasi ya kutumia sheria kuiba mali ya umma maana huu ni ujambazi serikali inaufanya hakuna ubishi.
 

Attachments

  • PSX_20231102_231556.jpg
    PSX_20231102_231556.jpg
    271.7 KB · Views: 4
Hiv huko kaburini watakwenda na hizo pesa au???

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni laana ya ulafi. Tuna nchi tajiri duniani kama marekani na nyingi za ulaya hatujawahi kuona ubinafsi, majigambo na m'mom'monyoko wa maadili kama hawa viwavi jeshi.


Yaani kufikiri mambo ya maana hutawaona lakini kwenye maovu na kuibua hasira za Mwenyezi Mungu wako mstari wa mbele.

Kuna mambo hatukutegemea tutayaona kwenye maisha yetu lakini sasa tunaelewa kuishi kwingi ni kuona mengi.


Mwenza wa viongozi wa taifa naye ni mtumishi wa umma kweli hii laana ni nzito
 
Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumwekea mwanadamu kifo maana hawa viwavi jeshi wangekuwa hawafi nadhani tungeteseka sana humu duniani.


Jina la bwana lihidimiwe.
 
Back
Top Bottom