Naombeni msaada wapendwa!!!!!

najisikia kuandika mchango kwa kirefu lakin basi tu, ngoja nipate glasi ya maji (Teamo amesema atalipia)
 
Asante Michelle, sasa unaiona hio red hapo, kwa jinsi nilivyoona mimi ndicho kinachochangia huyu baba anakuwa karibu zaidi na huyo bi mdogo. Kuhusu kusoma na ujasiriamali wa huyu mother house nimejikuta namtupia lawama huyu baba, kwa sababu, hakumpa ushirikiano katika hilo nafikiri. Manake baba ni mkali, ni ile staili ya Shikamoo baba kumbe mume wako!!

Wewe ulitaka aende kwa mpango wa kando asiye hata na akili aje kuchukua hata kidogo walichonacho hapo ndani na washindwe kuishi vizuri na familia?unajua hata kama kitu hakikubaliki,we should learn to see the good side of it....usiangalie ubaya tu wa huo mpango wa kando.....
Haiwezekani baba amfungulie mwanamke biashara ashindwe kumpa training ya kuchangamsha akili yake?huo mtaji wa biashara ni zaidi ya hiyo elimu......mwanamme mkali nini bwana,hajui tu kumpunguza makali huyo mama....mumeo mfanye rafiki,lakin unapompa status ya baba na yeye atakuwa baba......huyo mama angetaka shule angekuwa ashasoma kitambo......
 
Mwisho: Unamshauri nini huyu mama mwenye nyumba, ili aweze kuishi kwa furaha na amani katika ndoa yake?

Kama kila mwanaume aliyeoa au mwanamke aliyeolewa wangepewa nafasi ya kuamua kama wanapenda kuendelea na ndoa zao za sasa na wenza wao waliokula nao viapo kanisani/misikitini/kwa DC - asilimia 95 wangekataa!

Mpango wa nje ndiyo mpango sahihi, but sadly the society has failed to legalize it!
 
LD kabla sijamalizia hii insha ya msimamo wangu naomba kukuuliza:

Mama Mwenye nyumba anajua mzee ana mpango wa nje?
mama mwenye nyumba anajua kama mpango wa nje una mtoto?

Kama majibu ni ndio na mama ameridhia.....
Baba hajakosea kuwa na mpango wa nje........Thread Klozd!

Kama majibu ni hapana....
Baba anakaribia kukosea kuwa na mpango wa nje, japokuwa atakuwa bado hajakosea.
 
Je huyu baba alikosea kumuoa mke ambaye hana kiwango cha elimu zaidi ya elimu ya msingi?? (The Power of Love is always so strong. It existed and so they got married...... ila naamini watoto waliozaa, dini ndio kikwazo etc, otherwise wangekuwa wameachana.....)

Kumwendeleza kielimu kama mama hayuko tayari? Au ni kilaza? Au family commitments? Remember she is in her 50's? Kumbuka kusoma sio kuwa na vibrant mind.......

Mpango wa nje uko karibu sana katika huo uhusiano kwa sababu ya mtoto walie nae. Sioni ubaya kumtumia kwa ushauri mwisho wa siku cuz of the kid, huo mama she has her stake kwenye hilo chimbo. Angeweza kumtumia yeyote kwa ajili ya ushauri, sasa kwa sababu huyo mama yuko karibu, hakuna mbaya....

Mwisho: Unamshauri nini huyu mama mwenye nyumba, ili aweze kuishi kwa furaha na amani katika ndoa yake? Sipendagi hili swali, ni kama lile tangazo la Bwana nani sijui - ni Afisa Utumishi kazini yuko safi anapiga mzigo na ni role model wa staff wengine.... akifika home yeye na mkewe hawaongei..... ZUNGUMZA na MWENZIO... Halafu mbaya zaidi lile tangazo eti limefadhiliwa na watu wa Marekani.... Ufadhili hadi ktk ndoa zetu.... Kwamba kukaa na mwenzio hadi wamarekani wakukumbushe? Huyo mama akae na mumewe..... period....
 
Yaani kabla hata hujaufunga mlango wa kutokea kwenda huko unakokwenda SIKUBALIANI KABISA NA HILI Eti BABA AMEKOSEA!!

Hakukosea hata kidogo na nadhani alimpenda kwa dhati na kama alivyosema LD ni watu wazima na ndoa nyingi za wazee wetu ziko hivyo Baba ni msomi kuliko Mama. Kosa alilolifanya Mbaba huyu ni kutegemea maisha yake na maendeleo yake yaongozwe na nyumba ndogo badala ya kumwendeleza mkewe na kumpa ujuzi wa kuendesha maisha kwa pamoja ye anaendagawa ugali nje??

Hata mimi nimejikuta namlaumu huyu baba zaidi MJ1, halafu fikuiria na uzee huu,
mtu anajikatia tamaa, mpaka house girl anamdharau.
Anaishia kuona bora akae peke yake tu bila house girl.
Na mikazi ya nyumbani inavyochosha.
 
Je huyu baba alikosea kumuoa mke ambaye hana kiwango cha elimu zaidi ya elimu ya msingi?? (The Power of Love is always so strong. It existed and so they got married...... ila naamini watoto waliozaa, dini ndio kikwazo etc, otherwise wangekuwa wameachana.....)

Kumwendeleza kielimu kama mama hayuko tayari? Au ni kilaza? Au family commitments? Remember she is in her 50's? Kumbuka kusoma sio kuwa na vibrant mind.......

Mpango wa nje uko karibu sana katika huo uhusiano kwa sababu ya mtoto walie nae. Sioni ubaya kumtumia kwa ushauri mwisho wa siku cuz of the kid, huo mama she has her stake kwenye hilo chimbo. Angeweza kumtumia yeyote kwa ajili ya ushauri, sasa kwa sababu huyo mama yuko karibu, hakuna mbaya....

Mwisho: Unamshauri nini huyu mama mwenye nyumba, ili aweze kuishi kwa furaha na amani katika ndoa yake? Sipendagi hili swali, ni kama lile tangazo la Bwana nani sijui - ni Afisa Utumishi kazini yuko safi anapiga mzigo na ni role model wa staff wengine.... akifika home yeye na mkewe hawaongei..... ZUNGUMZA na MWENZIO... Halafu mbaya zaidi lile tangazo eti limefadhiliwa na watu wa Marekani.... Ufadhili hadi ktk ndoa zetu.... Kwamba kukaa na mwenzio hadi wamarekani wakukumbushe? Huyo mama akae na mumewe..... period....
 
Huyo nyumba ndogo ana umri gani? yuko rika sawa na mke wa mzee?
 
Kabla sijatoa sababu
Natoa msimamo wa babu,
Lakini isiwe bawabu,
La kuficha majawabu;

Msimamo wa babu:
Mzee hakukosea kuoa huyo anayeitwa mama mwenye nyumba
Na hakukosea pia kuwa na huyo anayeitwa mpango wa nje.

Ntarudi kufafanua kama hamjanielewa.

Sina budi tabaruku, ushauri wako Babu
Mkewe alimtunuku, kumfanya mahabubu
Na mpango kachunuku, nyumbani uwe bawabu
Kosa lilofanya Baba, Mkewe kumdharau

Wajua Babu ni kweli baba huyu hakufanya makosa kumwoa mkewe na (kama unavyosema kwa mtazamo wako) hakufanya makosa kuwa na mpango wa kando kwani umemletea manufaa (I hope hii ingekuwa tofauti iwapo Mpango huu ungekuwa ni ule wa hasara zaidi). Hagombwi kwa kuwa na mpango huo na pengine tumpongeze kwa kuweza kuwa makini na kuchagua mpango wa kando ulio bora (I guess na wetu wangekuwa na uwezo huo wala sie tusingepiga kelele loh). Angewezafanya moja kati ya yafuatayo
1. Kuamua kumtumia mpango wa nje (kwa akili kwa ajili ya maendeleo yake na familia kwa ujumla) Bila kumnyanyasa m,kewe na kumfanya akajua kuwa kuna small dogodogo anamsaidia au
2. Angechukua maujuzi ya mpango wa kando akaminduce mkewe ili hata baadae ikitokea la kutokea basi familia isitetereke.

Lakini pia tujiulize walikotokea na mpango wa nje huo..... isijekuwa umeegemea kwenye mhimili wa TRUE LOVE kiasi kwamba mpango wa kando uko genuine loh.
 
Kwa mazingira uliyoyaeleza mi nashauri huyo baba atafute kuwakutanisha na kuwapatanisha hao wamama wawili. Kisha wapange zamu ya kuwa na mzee, halafu mzee awe transparent kuhusu mapato kwa wote wawili na kila mmoja apate mapenzi na huduma sawa. Kama inawezekana

Huyo mama wa nyumbani wa darasa la saba utamuonea ukitaka aanze kusoma sasa hivi. Ukitaka mzee amwache bimdogo nayo nahisi itakuwa ngumu. Bimdogo kumuacha mzee nayo inaweza kuwa ngumu.

Ni mawazo yangu tu
 
i hereby rest my case.....!

upinzani ni mkali zaidi by the look
 
Hata mimi nimejikuta namlaumu huyu baba zaidi MJ1, halafu fikuiria na uzee huu,
mtu anajikatia tamaa, mpaka house girl anamdharau.
Anaishia kuona bora akae peke yake tu bila house girl.
Na mikazi ya nyumbani inavyochosha.
Pole but asikate tamaa si wanasema elimu haina mwisho?? kama bado ana nguvu ajienroll hata kwenye vikozi vya biashara na kisha ajichanganye. Kudispair hakutatui tatizo kunaongeza matatizo .....madepression, mapresha na mwishowe stroke.
 
Wewe ulitaka aende kwa mpango wa kando asiye hata na akili aje kuchukua hata kidogo walichonacho hapo ndani na washindwe kuishi vizuri na familia?unajua hata kama kitu hakikubaliki,we should learn to see the good side of it....usiangalie ubaya tu wa huo mpango wa kando.....
Haiwezekani baba amfungulie mwanamke biashara ashindwe kumpa training ya kuchangamsha akili yake?huo mtaji wa biashara ni zaidi ya hiyo elimu......mwanamme mkali nini bwana,hajui tu kumpunguza makali huyo mama....mumeo mfanye rafiki,lakin unapompa status ya baba na yeye atakuwa baba......huyo mama angetaka shule angekuwa ashasoma kitambo......

Yani Michelle tuko pamoja kabisa, ndo maana nimesema hili jambo limenipa utata,
Kwa sababu ukiangalia huyu mpango wa kando ana kila sababu ya kuendelea kubaki na huyu baba, yani ana efect kubwa sana kwenye maendeleo ya uchumi wake. Lakini sasa?? Hiyo ndoa hiyo, ilikuwa au ni wrong ndoa??
Ok, unajua kuna akili nyingine ipo vile ilivyo, hata ukiipa majibu ya mitihani inaweza ikafeli vile vile?
Hawa wanandoa walikosea wapi hasa?
 
i hereby rest my case.....!

upinzani ni mkali zaidi by the look
Teamo c'mon baana hebu tugaie busara zako .......you always have the talent of seeing what most of us fail to see in the first glance of the thread.
 
hii ipo sana kwenye jamii yetu.
kweli kinachotakiwa mwanamke kujiendeleza na kujipanga.ikifikia kuolewa uwe na jambo unafanya kama ni kazi au biashara,i hate kuwa tegemezi.
 
Sina budi tabaruku, ushauri wako Babu
Mkewe alimtunuku, kumfanya mahabubu
Na mpango kachunuku, nyumbani uwe bawabu
Kosa lilofanya Baba, Mkewe kumdharau

Wajua Babu ni kweli baba huyu hakufanya makosa kumwoa mkewe na (kama unavyosema kwa mtazamo wako) hakufanya makosa kuwa na mpango wa kando kwani umemletea manufaa (I hope hii ingekuwa tofauti iwapo Mpango huu ungekuwa ni ule wa hasara zaidi). Hagombwi kwa kuwa na mpango huo na pengine tumpongeze kwa kuweza kuwa makini na kuchagua mpango wa kando ulio bora (I guess na wetu wangekuwa na uwezo huo wala sie tusingepiga kelele loh). Angewezafanya moja kati ya yafuatayo
1. Kuamua kumtumia mpango wa nje (kwa akili kwa ajili ya maendeleo yake na familia kwa ujumla) Bila kumnyanyasa m,kewe na kumfanya akajua kuwa kuna small dogodogo anamsaidia au
2. Angechukua maujuzi ya mpango wa kando akaminduce mkewe ili hata baadae ikitokea la kutokea basi familia isitetereke.

Lakini pia tujiulize walikotokea na mpango wa nje huo..... isijekuwa umeegemea kwenye mhimili wa TRUE LOVE kiasi kwamba mpango wa kando uko genuine loh.

Napenda sana MJ1 waga unafikiri kwa mapana na marefu.....i admire that....

Unajua mimi nina amini kuna watu hawakupaswa kuoana,yaani pengine circumstances ziliwaweka pamoja,hasa hizo ndoa za zamani....sasa huyu baba kakutana na soulmate wake haswaaa na mambo ndo yamekuwa hivyo......maisha haya.....
 
LD kabla sijamalizia hii insha ya msimamo wangu naomba kukuuliza:

Mama Mwenye nyumba anajua mzee ana mpango wa nje?
mama mwenye nyumba anajua kama mpango wa nje una mtoto?

Kama majibu ni ndio na mama ameridhia.....
Baba hajakosea kuwa na mpango wa nje........Thread Klozd!

Kama majibu ni hapana....
Baba anakaribia kukosea kuwa na mpango wa nje, japokuwa atakuwa bado hajakosea.

Anajua lakini halipi furaha Babu,
Na hawajawahi kukubaliana, kwamba baba akataute mpango wa kando!!
Lakini alikuja kushangaa tu, kuna kitu kama hicho, na nyumba yake inaongozwa remotely na mpango wa kando.
 
LD naomba majibu ya haya maswali yangu tafazali:

LD kabla sijamalizia hii insha ya msimamo wangu naomba kukuuliza:

Mama Mwenye nyumba anajua mzee ana mpango wa nje?
mama mwenye nyumba anajua kama mpango wa nje una mtoto?

Kama majibu ni ndio na mama ameridhia.....
Baba hajakosea kuwa na mpango wa nje........Thread Klozd!

Kama majibu ni hapana....
Baba anakaribia kukosea kuwa na mpango wa nje, japokuwa atakuwa bado hajakosea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom