Mwanaume aliyelelewa na mama peke yake, ni mtu wa aina gani?

Pitia comment nying hapa utaona,wengi wanaunga mkono malezi mazuri ambayo wanaume wamepata toka kwa mama tu.NI KWELI NAMI NAKUBALI (nami nimelelewa malezi hayo). LAKIN kumbuka malezi tuliyo pata sisi (wanaume wa leo) toka kwa mama zetu ni TOFAUTI SANA ma malezi wanayopata watoto wa kiume wa miaka hii toka kwa single mothers.wala haiitaji mtabiri kuwatabiria namna watakavyo kuwa kwan malezi wanayo pata sasa toka kwa kina mama (hawana sifa na mamazetu) utajua namna watakavyo kuwa wanaume legelege,tegemezi kifikra,kimaamuzi,wavivu,kukosa ujasiri na zaidi kuiga tabia za kikekike

Kama ulikuwepo mkuu wa kiume wa cku hz majanga matupu
 
Rais wa Dunia Barack Obama alilelewa na mama yake baada ya baba kwenda AWOL.
 
Antolee ujinga wake hapa.. na akijaribu tu ntamtembezea mapanga ..sioni mapungufu yoyote..though askwambie mtu singe parental si mchezo unaweza ukawa na shida labda ya hela na huna option ya kumuomba mtu mwingine zaidi ya mama na akisema sina ujue imekula kwako..binafsi nimekula good time sana..shule nzuri..maisha mazuri..pocket monie ya kutosha..usafiri safii sasa huyo baba wa nini? sioni hata faida yake maana hakija haribika kitu..!
We bogasss kabisa. Still wewe bado ni shahawa zake tu.....
 
Namshukuru Mungu, Pia namshukuru mama yangu kwa kunizaa na kunilea yeye mwenyewe! hadi leo hii nimekuwa kijana wa kiume NILIYEKAMILIKA.Sijawahi kuiona sura ya baba yangu tangia nizaliwe hata kwa picha,Na taarifa nilizonazo tayari katangulia mbele za haki! "MWENYEZI MUNGU AMLAZE MAHARA PEMA PEPONI".Nampenda mamaangu na kila siku namuombea maisha marefu yenye afya na furaha tele.

you touched my heart.. Kissez to ur beautful n wonderful mama
 
Kwakawaida huyu upande wa ndoa ni mume mzuri sana. Huwa karibu na mkewe. Humpenda mkewe kwa dhati. Hayuko tayari kuona ananyanyasika. Huwa karibu na wanae. Humsaidia mkewe kila awapo na nafasi. Ila pia huwa na wivu sana kwa mkewe na binti zake. Kumbuka ameishi na Mama zaidi. Hivyo anakuwa anafeal zaidi wanawake. Actually,wanawake wanaoolewa na wanaume hawa,huenjoy sana hasa kama ni wanawake watulivu. Kama hawajatulia huona kero maaana wanaona wanaume wanakuwa kama wanawachunga vile.I like them!

U said it all!!!
Wana upendo sana!!
Ni husband material!!
Ila kwenye kazi mhhh!!!
Ambao hawaja pata elimu ni majanga!!
Wavivu huwa mara nyingi!!
 
Kulelewa na mama na baba kama wote wapo hai ni jambo zuri sana then ukute wazazi wanaishi kama marafiki ndani ya nyumba ni jambo la kufurahisha sana uhu ndio mfano niliochukua kwa wazazi wangu wananipa shauku nami nije kumpenda mke wangu na watoto wangu.wakati nipo mdogo nakumbuka baba alikuwa anamsahidia mama kupika kama mama ni mdhaifu hadi sasa hiv kuna wakati baba anaweza andaa meza wakati wa msosi upand wa vinywani na matunda.mwanzo mwisho nilpofurahia maisha ya kulelewa na wazaz wote ni SIKU YA JUMAPILI tunaenda wote church nyumba nzima hadi dada wa kazi watoto wote nyuma ya pick up hilux .duh wacha kabisa ilikuwa rhaaaaa , kama mtoto atalelewa na baba na mama wenye mapenz ya kweli anayomeng ya kujifunza katika kuja kuijenga familia yake.
Hapa umeongea kweli ila inauma kwa ss single parented
 
Baba atabaki kuwa baba tu ata kama alukutenda nini kuna waliofanyiwa ukatili mkubwa na baba zao na wakasamehe sembuse wewe sio kosa lako,inua mdomo wako umtukane unavyoweza umlaani unavyoweza hatapata madhara lakini siku atakapo inua mdomo wake na kukulaani iyo laana itakutafuna mpaka unaingia kaburini haijalishi alikutunza au hajakutunza,ni hayo tu.
cna neno ujue
 
Antolee ujinga wake hapa.. na akijaribu tu ntamtembezea mapanga ..sioni mapungufu yoyote..though askwambie mtu singe parental si mchezo unaweza ukawa na shida labda ya hela na huna option ya kumuomba mtu mwingine zaidi ya mama na akisema sina ujue imekula kwako..binafsi nimekula good time sana..shule nzuri..maisha mazuri..pocket monie ya kutosha..usafiri safii sasa huyo baba wa nini? sioni hata faida yake maana hakija haribika kitu..!
Hilo ndiyo tatizo la mtoto kulelewa na mzazi mmoja, hasa mama humjengea chuki mtoto juu ya baba, kitu ambacho kama mtoto ni wakike haji kuishi na mume vizuri. Ila nakuambia toa chuki uliyo nayo kishwani umepandikizwa,. mtafute baba utajinfunza mengi .Wengi waliolelewa na mzazi mmoja wamepandikizwa chuki juu ya mzazi mwingine ndiyo kosa kubwa wazazi wanalofanya.
 
Ukiacha mzazi aliyefiwa na mwenza, wengine huwajengea chuki watoto wao juu ya mzazi mwingine kitu hiki kwa bahati mbaya huwathiri watoto kike zaidi kuliko wa kiume. watoto wa kike wanakuwa hawaoni umuhimu wa mume katika maisha yao ni lahisi sana kuvunja mahusiano au ndoa. Kosa sio la watoto kulelewa na mzazi mmoja kosa ni mzazi anawaambia nini watoto wake juju ya mzazi mwingine ambaye hawakonaye.
 
Sijui tunaelekea wapi ndugu zangu,maana naona zimeanza thread za kujadili watoto wanaolelewa na mzazi mmoja naona mwishoe watakuja kunyanyapaliwa. Mwingine aseme sitaoa mtoto alielelewa na mama peke yake kwa kuwa wanafundishwa vibaya. Hao watoto hawajapenda ni sisi wazazi ndio tuliosababisha yote hayo,sasa kwanini waadhibike kwa makosa yetu???!!!! Mtoto anaweza kulelewa na both parents and still akawa kitu cha ajabu. Hebu tumuweke Mungu mbele kwenye malezi ya watoto na si kuanza kushupalia mambo ya ajabu.
We have a long way to go my people!
Umenena vyema ndugu yangu
 
Back
Top Bottom