mito napenda sana mtu anayetoa mifano halisi manake hii ndiyo inayojenga ma dearest. real nimependa sana ulichokisema. sasa hapo nikuulize swali suppose umekutana na mtu wa aina hiyo waweza kumsifia yeye binafsi kwa kumwambia umzuri bi mkubwa?
Hiyo ndiyo point. Kuna kuvutiwa kwa kukubali kazi ya muumba; na kuvutiwa kuwa na serious relationship na mtu.
Wenye maumbo namba nane mara nyingi wanaume hawawachukilii serious; wanapenda ku past nao time tu si kuwaoa. Unless wawe wagumu kweli na wajitahidi ku prove kwa jamii kwamba wao si chombo cha kufurahisha wanaume.
Ila Wema si mfano wa umbo la kumtisha mtu kumfanya mke. Kinachimfanya Wema atishe ni kujulikana kwake (star) na tabia yake. Angekuwa nobody mbona umbo lake linafaa kuwa private wife (Lol)
Exactly
sasa kaka yangu wa moyoni platozoom tunakwenda sambamba ila hebu nijibu swali hili hapa, hivi mvuto ama uzuri wa huyu mwanamke at first eye utaangalia nini? je ni zile features unazozipenda ama zile wenzio wanazosema ni nzuri ama hauna sababu nyuma yake?
hivi BAK hujawah kuona mtu mwanamke mzuri sana wa sura na umbo lakin hapati mwanaume wa hata kumsalimia tu? je huyu kwake synonymous inakuwa wapi?
Huyu wa design hii utakuta ana nyodo kwani wanaue wengi watambua kwamba mwanamke anatakiwa kuringa lakini akizidisha sana pamoja na mashauzi kinachotokea ndio kama hicho ulichosema na mwisho wa siku wanawake wa design hii utakuta aechukuliwa na mwanaume ambae ingekuwa enzi zake ni hawaendani kwani wale wote makini waliokuwa wanajitutumua kumtokea walishaweka akilini kwamba ana nyodo hivyo hata strategy za kutokea wakazifuta mwisho wa siku anaibuka msela anachukua zigo kwani huwa inafika wakati mtu anahitaji mwenzake kwa kuwa inakuwa too late anaishia kwenye ule msemo wa NDEGE MJANJA HUNASA.................
linakatika na shoka tu Kisu au panga vyote havioni ndani
Inategemea na mtu mwenyewe, mazingira yenyewe na hasa mahusiano yake na mimi. Hivyo kuna watu huwa nawaambia na kuna wengine huwa siwaambii, namezea tu. Sisifii mara nyingi kwa sababu kubwa 3:
1) nimegundua kuna baadhi ya wanawake ukiwasifia anaona kama vile umeishamdondokea, hivyo hiyo ni gia tu ya kuingilia
2) nimegunda jamii kwa ujumla haichukulii hili kama jambo la kawaida. Yaani kuna watu wakikusikia unasifia mwanamke hadharani wanakuchukulia kama mhuni fulani hivi, so wanakushusha hadhi kutegemea na wewe mwenyewe ulivyo.
3) mke wangu mwenyewe hapendi kusikia nasifia mwanamke mwingine, so sitaki kuzoea kufanya hivyo kwani kuna siku naweza jisahau nikasifia mbele ya mke wangu. Nasema hivi kwasababu mwaka 2006 wakati wema anashinda umiss TZ nilikutana naye ghafla (but nikiwa na mke wangu) wizara ya mambo ya ndani, ilikuwa ni kama siku 3-5 hivi tangu aliposhinda. Alienda kushughulikia criminal clearance certificate. Bahati nzuri na mimi nilikuwa natafuta hiyo hiyo. So kumuona tu ghafla (kumbuka nilikuwa bado na zile memories za tukia zima la ushindi wake kwenye tv) nikachachawa na kumsalimia na kumsifia, of course na yeye alikuwa ana-respond vizuri tu. Lakini thereafter maiwaifu wangu hakujisikia vizuri, so i learnt something new!
Mmmh unasifiwa nini dada yangu gfsonwin, mbona unanichokonoa hivi?
Arvin sloane hivi kuna mwanamke mbaya? au nimesoma vibaya? ubaya kwako wewe ukoje?Mvuto kwa mwanamke unatokana na vigezo vya mwanaume mfano mimi nina mvuto na wanawake wabaya kwa hyo nikimuona mwanamke mbaya natamani ni do naye.
the first thing i look on a girl is her finger nails na kucha za miguu,then vitu vngine ila hvyo nilivyotaja ndio huvipa uzito.
gfsonwin, kweli tunatafautiana. Wakati mie nikiwa na mwenzangu huwa namuonyesha kabisa wenye miguu mizuri, makalio ya kukata na shoka (source BAK), wenye skin texture nzuri na pua za kishihiri. I understand I'm not the most beautiful woman he has ever seen, but I'm the woman he fell in love with. Ukiwa comfortable in your own skin utaonyesha hata walio vaa nusu uchi ili mshangae pamoja. Kisangani cha kumvalisha mawani ya mbao motto wa mwanamke mwenzio?yaani mito ukitaka nife siku hiyo aisee msifie mwanamke mwenzangu kama wewe ni mume wangu. lolest! yaani hata kama atapita mbele yako mdada mzuri kama malaika aisee usije ukamsifia nikikuskia na nashukuru sana mungu sinajawah pata hii experience.
hapo kwenye red mmmh!.....................siri ya mtungi aijuaye kata.
gfsonwin, kweli tunatafautiana. Wakati mie nikiwa na mwenzangu huwa namuonyesha kabisa wenye miguu mizuri, makalio ya kukata na shook (source BAK), wenye skin texture nzuri na pia za kishihiri. I understand I'm not the most beautiful woman he has ever seen, but I'm the woman he fell in love with. Ukiwa comfortable in your own skin utaonyesha hata walio vaa nusu uchi ili mshangae pamoja. Kisangani cha kumvalisha mawani ya mbao motto wa mwanamke mwenzio?
Dkweli bi dada charminglady tusubiri watudadavulie. lakini je swali la kizushi hujawah kuvutiwa na mkaka?
D
ah nshawahi kuvutiwa, tena me huvutiwa sana na wakaka warefu wenye mwili wa kimazoezi!