kwani tatizo nini? ni kwasababu kule pemba ndo kuna mafuta sasa wapemba ndo wamiliki mafuta yale peke yao? mbona hata bara kuna mafuta kule pwani ya kusini wamegundua na jana tu wameona dalili kubwa sana ya mafuta kwenye bonde la ziwa Rukwa? kama vipi, waacheni wapemba walale mbele na mafuta yao, na sisi wabara tutalala mbele na vyetu tulivyopewa na Mungu. tatizo kubwa ambalo ni moja ya hata kimegeo kinachomega muungano ni mafuta ya pemba. Je, kama mafuta yasingekuwapo pemba na yakawepo bara tu, kungekuwa na misukosuko yote hiyo?, basi muungano wetu ni wa siku za faida tu, siku zisizo na faida ni ugomvi. tunachowang'ang'ania sana wazanzibar ni nini? kwani sisi wabara hatuna nini? tunakosa nini, tunafaidika nini na wao kama sio wao kufaidika na sisi zaidi? you think we need them more than they need us? No, I don't think so. let them take their way and go. watuache watanganyika vyovyote watakavyo tuita, na sisi tutachimba mafuta vilevile. period.
 
Zanzibar inaonyesha ni Nchi maana walivyochachamaa utazani wanataka kupigana Jihadi,katika kikao walichoandaa Pinda aliingia mitini wakati Kikwete alisema ana uzuru flani flani ,na wahafidhina wanasema kuwa eti kuna chuki zilizojengwa na CCM bara baada ya kikao cha Butiama.........ndio niliwahi kusema kama hizi chokonoa zinatokana na hasira za Kikwete na akina kaka kazi wamepewa mitihani ya kuwafazaisha wahafizina kubwa lijalo.
 
Serikali yasisitiza madini si mali ya Muungano
JIBU LA SWALI LA MBUNGE JIMBO LA MKANYAGENI
blank.gif
blank.gif
Mnyaa-%20mkanyageni.jpg
blank.gif
Mhe. Mohamed Mnyaa (CUF)​
h.sep4.gif

na Irene Mark na Rahel Chizoza, Dodoma



KWA mara nyingine, serikali imesisitiza kwamba maliasili madini si mali ya Muungano, ingawa mapato yake yanaingia kwenye mfuko mkuu wa mapato ya serikali unaogharamia uendeshaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Akitoa msisitizo huo bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema kigezo kilichofanya maliasili madini isiwe ya Muungano, lakini mafuta na gesi kuwa vya Muungano, ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inayotoa mwongozo wa sheria zote za nchi zinazofuata katiba.
Alisema maliasili ya mafuta na gesi imekuwa ya Muungao tangu Katiba ya Jamhuri ya Muungani wa Tanzania ilipotungwa na kubainisha mambo yapi ni ya Muungano na yapi si ya Muungano.
Aidha, waziri alibainisha kwamba shughuli za utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi, hutekelezwa chini ya Sheria ya Utafutaji na Uzalishaji Mafuta ya mwaka 1980. Waziri Ngeleja alilazimika kutoa maelezo hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mkanyageni, Mohamed Mnyaa (CUF), aliyetaka kujua pamoja na mambo mengine vigezo vinavyofanya maliasili madini isiwe ya Muungano na kuanzia lini mafuta na gesi vimekuwa mali ya Muungano. Hata hivyo, katika majibu yake, Ngeleja alisema wakati wa mkutano wa nane, kikao cha 46 cha Bunge, aliwahi kujibu swali namba 427 lililotoa ufafanuzi wa kwa nini madini si mali ya Muungano kama lilivyoulizwa na mmoja wa wabunge.
 
duh mbona wazee mnalalama saaaaaaana, hebu toeni alternatives basi ya nini kifanyike na kwa namna gani huku tukiwasidia wenzetu kimawazo na kwa kuwatia nmoyo pale inapobidi!, i'm really sick and tired of this kushutumushutumu tuuu all the time,
tena kushutumu kwenyewe siyo constructive "crticism".

hili Taifa gani la ulalamishi lalamishi tuu tunakusudia kulijengal,mara Jk vile, mara Jk hivi,mara Sitta hivi, mara Sitta vile,alichokifanya Sitta kipo ndani ya uwezo wake kama Spika sasa badala ya kumlaumu tu semeni mlitaka afanyeje, na kwa namna gani, na kwa nini hivyo mnavyotaka afanye ni bora kuliko alivyofanya.
Watu wa kushutumushutumu tuu ni wanafiki na ni hatari pia kwa maendeleo yawe ya Taifa au ya kwao wao binafsi.
lets get real people, stop whinning and do the right thing

GN

Please matatizo ndio yanaimarisha mfumo, kwa hio SPIKA amearisha matatizo tu. Ujadiliwe upatikane ufafanuzi
 
What aspects of your background permit you to define yourself as a Zanzibari?
• Zanzibar being the country of my by birth and a land where my umbilical cord is lying
• Zanzibar being the country where my parents were born and grew up. The country where in some ways they have contributed towards its development
• Zanzibar being the country where there are numerous tombs of members of my extended family.
• Zanzibar being the country where I grew up and received my basic religious and secular education.
• Zanzibar being the country that I could identify with, in many ways, and that I could easily articulate on its various aspects.
• Zanzibar being the country that consciously and/or unconsciously, objectively and/or subjectively attached with and could dream about and even become nostalgic of.
• Zanzibar being the country that I could be proud of, that I could be sentimental with and going even as far as sacrificing my time, energy and even the best part of my life for its development and social welfare of its people.
• Zanzibar being the country where I could be discriminated against and considered alien by those who are more alien than anybody else, but where I could naturally have the courage to resist without any hesitation against the racist bunch.
• Zanzibar being the country where I could really and genuinely feel at home and at ease.
• Zanzibar being the country where I could find and recall various aspects of my childhood and find my playmates, school mates, etc.

2 In what ways does your upbringing, language, culture, class, religion (or sect), physical environment, legacy, confirms this identification:
• Upbringing: It is one of the fundamental factors confirming my Zanzibari identity. My upbringing in a coastal cosmopolitan Zanzibari society had a major impact in the formulation and development of my system of representation. Despite living abroad for many years, integrating in the process many other non Zanzibari socio-cultural elements, the basis of my system of representation remains essentially Zanzibari. It continues to date to influence in some ways my socio-cultural orientation and world outlook. Through my Zanzibari upbringing I was made to understand life in all its complexities, and to cherish honor and pride. These are some of the ideals that are highly valued by the society that one might find elsewhere, but for me, they reflect my Zanzibari identity.
• Language: I consider this to be an important element of my Zanzibari identity allowing me to differentiate with other Swahili speaking communities in many ways, including accents and colloquial. This is also true to the language used in Zanzibari literature, which I could identify with and feel part and parcel of it, allowing my assertion to the Zanzibari identity.
• Culture: Being part and parcel of the plural coastal societies of East Africa, with a number of socio-cultural similarities, my Zanzibari identity remains relevant by the existence and the performance of a number of customary rites, traditional and moral teachings giving room to some kind of differentiation with other non Zanzibaris. The inculcation of the following norms and values - principal moral foundation of Zanzibari, Swahili identity and culture further confirms my Zanzibari identification: respect (heshima), good behavior (adabu), honesty (uaminifu), ethics (uadilifu) and honour (ari).

Class: This factor does not seem to have any particular importance and to play any role in my identification to Zanzibar, hence to my Zanzibari identity

Religion: It forms an important part of social and moral background of my Zanzibari identity. Although, I am un-practicing Muslim but Islamic elements acquired through my Zanzibari upbringing still have a major impact in my world outlook and my daily life. However, I always make a difference between the Islamic religious practice that I grew up with in Zanzibar and those of elsewhere or the radical Islam. While talking about Islam in terms of Zanzibari identity, I put particular emphasis on tolerance. As a religion that came by dhow, and not imposed by sword, through trade, social and cultural interaction Zanzibar has been for many years characterized by religious tolerance. Zanzibari Islam has been all along open, tolerant and respectful of minority rights, including homosexuals. These elements contribute in my determining of my Zanzibari identity and in my differentiation with other Non Zanzibari Muslims or present Radical Zanzibari Muslims.

Physical Environment (architecture, urbanity, countryside, etc): These factors play a particular role in my taste and appreciation of physical environment of the foreign countries that I am visiting or choose to visit. The Zanzibari architectural background, aspects of Zanzibari urbanity and even countryside consciously or unconsciously remain as my major reference points of appreciation or comparison. In this sense while appreciating and comparing the above elements through the Zanzibari lenses I am affirming my Zanzibari background and by rebound my Zanzibari identity.

Legacy: Although identity is not static and is constantly being negotiated, most of the above mentioned elements remain to date valid and will take time to disappear. They remain the fundamental elements of what I could consider as part of my Zanzibari cultural legacy and identity. They are the elements that I could hardly replace but which I could very well, consciously or unconsciously, enrich with other socio-cultural elements of the foreign society that I am living in.
• Other
3 In what ways these aspects hinder your identification (if any?)
None of these aspects hinder my identification. On the contrary, they are the fundaments providing the intellectual basis for the struggle against cultural hegemony and the efforts of those who are creating confusion among the people in terms of their Zanzibari, Swahili identity and language.
4 Please add any other issues you think would be of interest:
Grew up in a Zanzibari cosmopolitan background facilitated a great deal and made me feel very much at ease mingling with people from other countries with similar plural background or not. For me identifying with Zanzibar goes even further to include a larger Swahili cosmopolitan coastal identity. For Zanzibar belongs to a larger Swahili plural identity of which I am attached and identify with.
Ah Hongera Ngekewa. Keep it up. I LIKE U.Be always a Zanzibari
 
Siku zote muonewa ndie anaye lalamika. Kwa nini malalamiko ya wa Zanzibari hayeshi au haya tatuliwi kwa namna yeyeto ile. Kwa nini wa Tanganyika wanganganie ule usemi wa changu -changu chako chetu. Wana sababu gani ya kukubali hivyo. Kuna sera ya kujificha hapa.
 
KWA mara nyingine, serikali imesisitiza kwamba maliasili madini si mali ya Muungano, ingawa mapato yake yanaingia kwenye mfuko mkuu wa mapato ya serikali unaogharamia uendeshaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Kituko kingine hiki.

Ndio ubaya wa kuimba "zidumu fikra za Mwenyekiti" bila kujua hasa anafikiria nini huyo mwenye hicho kiti.

Madini sio ya wote halafu yanaende kwenye mfuko wa wote ndio nini jamani!
 
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesisitiza kuwa ilitoa hisa wakati kuanzisha Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kinyume na ilivyoelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari.

SMZ imetoa tamko hilo baada ya Sumari kulieleza Bunge la Muungano hivi karibuni kuwa Zanzibar haina hisa BoT, wakati akijibu maswali ya wabunge, Hafidh Ali Tahir (Dimani) na Hamad Rashid Mohammed (Wawi).

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali iliyotolewa na Afisa wa Mawasiliano wa Wizara ya Fedha na Uchumi Zanzibar, baada ya kuvunjwa Bodi ya Sarafu za Afrika ya Mashariki (EACB), nchi zote zilizokuwa wanachama wa Afrika Mashariki ikiwemo Kenya, Uganda, Tanganyika na Zanzibar ziliamua kuanzisha Benki Kuu Alifahamisha kwamba, kwa vile Zanzibar na Tanganyika zilikuwa tayari zimeungana zilianzisha BoT na sehemu ya faida na malipo mengineyo yaliokuwa yapelekwe Zanzibar kutoka EACB yalipelekwa kwenye Serikali ya Muungano badala ya SMZ.


Mtazamo wa Zanzibar ni kuwa ina hisa za moja kwa moja katika mtaji wa kuanzishwa Benki Kuu mbali ya hisa zilizotolewa na muungano, msingi wa msimamo huo wa Zanzibar ni ukweli kuwa suala hili halipaswi kuamuliwa kwa kuzingatia vipengele vya sheria pekee bila ya kuzingatia historia ya BoT na asili ya mtaji wake,

imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Afisa Mawasiliano, Osmand Duwe.

Taarifa hiyo imesema baada ya kuvunjwa kwa EACB faida na malipo hayakuingizwa katika hazina ya Zanzibar bali yalipitishwa moja kwa moja katika hazina ya serikali ya Muungano na baadae kuanzishwa kwa BoT.

Inawezekana kuwa ni sawa kuwa fedha za mtaji kuanzisha benki kuu zilitoka hazina ya SMT kama ilivyo kwa matumizi mengine yoyote, lakini kwa kuwa hazina hiyo ilipewa fedha kutoka EACB kwa ajili ya kuanzisha BoT na kwa kuwa kati ya fedha hizo kuna sehemu ya Zanzibar, basi SMZ ina hisa iliyotokana na mtaji wa kuanzisha benki hiyo,

alisema Tamko hilo la SMZ limesema maelezo hayo yanapewa nguvu na kifungu cha 67 cha sheria iliyoanzisha Benki Kuu ambacho kinatambua hisa za Serikali ya Zanzibar katika iliyokuwa Bodi ya Sarafu za Fedha ya Afrika Mashariki kama mtaji wa kuanzisha benki hiyo.

Taarifa hiyo ya serikali imesema SMZ imeamua kueleza hayo ili wananchi wafahamu ukweli wake kwa vile taarifa zilizotolewa awali na Sumari hazikuwa sahihi. Katika hatua nyengine, SMZ imesema haijawahi kupokea msaada wa kibajeti kutoka serikali ya Muungano zaidi ya gawio linalotolewa kupitia misaada ya wahisani kwa ajili ua kusaidia bajeti na kwamba Zanzibar hunufaika kwa utaratibu wa mgao wa 4.5.

Mytake
Mie nimeanza kuogopa,Nani anayaongoza maneno haya..?Kuna kitu lazima ambacho kiko nyuma.Nimeanza kukumbuka maneno ya mwalimu,Rejea katika kitabu cha carlucci 'The Influence of Nyerere' © 1995 katika mahojiano hayo, Carlucci alisema: "Nyerere alilazimika kufanya jambo fulani kuhusiana na Zanzibar. Sijui kwa hakika kama wazo (la Muungano) lilikuwa lake mwenyewe, au kama ni sisi (Wamarekani) tulimpa maagizo.
 
sasa hivi mtasikia naye sumari anadai alipotoshwa juu ya taarifa alizozitoa,Tatizo nchi ipo reheni na kila mtu analopoka tu
 
Hayo ni mapambano kati ya timu ya Kikwete Butiama na timu ya Wahafizina Kisiwandui inayoongozwa na Karume , hapa pana ngumi tu au mmoja itabidi akubali kuinama .
 
Taifa ambalo haijulikani ipi ni nchi; taifa ambalo haijulikani nani mwenye akaunti ya mabilioni licha ya maafisa wake kutia sahihi; taifa ambalo hawajui mtaji wa Benki Kuu umetoka wapi ni ushahidi wa wazi kuwa tuna tatizo kubwa zaidi kuliko ufisadi.
 
Taifa ambalo haijulikani ipi ni nchi; taifa ambalo haijulikani nani mwenye akaunti ya mabilioni licha ya maafisa wake kutia sahihi; taifa ambalo hawajui mtaji wa Benki Kuu umetoka wapi ni ushahidi wa wazi kuwa tuna tatizo kubwa zaidi kuliko ufisadi.

Kama ni ugonjwa basi zote hizo ni dalili tu, gonjwa lenyewe ni genge la wachache wanaodhani wana haki na Taifa hili na kutojali hatima yake isipokuwa ya kwao.
 
Taifa ambalo haijulikani ipi ni nchi; taifa ambalo haijulikani nani mwenye akaunti ya mabilioni licha ya maafisa wake kutia sahihi; taifa ambalo hawajui mtaji wa Benki Kuu umetoka wapi ni ushahidi wa wazi kuwa tuna tatizo kubwa zaidi kuliko ufisadi.

Wameshindwa kutwambia mmiliki wa Meremeta na Tangold ambayo yameundwa hivi karibuni kama ni sirikali, fisadi au kundi la mafisadi wataweza kutwambia ni nani alitoa hisa kuanzisha BoT miaka 30 na ushee iliyopita? Siyo siri kwamba tuna SERIKALI ambayo haistahili kabisa kuwa madarakani maana haina uwezo wa kuendesha hata mtaa wachilia mbali kuendesha nchi.
 
kweli serikali ya tanzania sasa hivi inalega lega vibaya kutokana na kuwa haina rekodi zozote za maana inazoweka.

lakini hii hali ya zanzibar kwa upande wangu nahisi kuna kitu hapa kinaibuliwa. katika siku mbili hizi masuala ya zanzibar yamekuwa meng mno....
 
Taratiiibuuuu naanza kuoana MPASUKO WA MUUNGANO wetu na Zanzibar.........

Soon mabadiliko makubwa yatakuwa muhimu kama tunataka Muungano UDUMU.
 
Je Sumari alitoa tamko hilo kwa makusudi ili kuchochea mpasuko? au
Sumari hajui historia ya Benki Kuu ya Tanzania?

Benki Kuu ya Tanzania ilianzishwa mwaka 1966. Kabla ya hapo, Tanganyika, Zanzibar, Kenya na Uganda zilikua na Benki Kuu moja.

Nachojiuliza ni ile tabia ya Viongozi, wanasiasa na watendaji ambao hupenda kukurupuka na kutoa majibu kiholela.

Je Sumari ameshawahi kusoma historia ya BOT na kujua uundwaji wake na mtaji ulitoka wapi? Je kajiuliza ni kwa nini miaka ya karibuni, makamu wa Gavana anatoka Zanzibar?

I am sick and tired of educated fools that Tanzania has and especially on leadership circles!!
 
Ugonjwa wetu ni mkubwa sana. Hautibiki, bora tuwakinge watoto wetu wasiupate. Sisi basi tena. Hakuna aliepona.
Manake 60% ya watu ukiwauliza wanatamani kazi nzuri au uongozi fulani kwa ajili tu ya uwezekano wa kupata fursa ya kupokea rushwa, kupata fursa ya kutega kazi, kupata fursa ya kufuja mali za mwajiri nk.
Watoto wetu wanarithi nini. manake ndio school feez zao!
 
serikali lege lege ndo faida zake hiziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.TUJADILI HUU MUUNGANO WETU ILI UTOKANE NA WATU SIO WAASISI.
 
Hapa tuna tatizo kubwa, nadhani viongozi waliopo madarakani Zanzibar wana nia ya kuuvunja Muungano.Katika siku za hivi karibuni kauli zinazotolewa na kuhusu Muungano zinaleta sura kwamba kuna mpasuko ndani ya CCM juu ya Muungano na kwa bahati mbaya hakuna aliye tayari kukemea tabia hii. Mwl Nyerere alisema ubaguzi na sawa na kula nyama ya mtu leo sisi wanzanzibari, kesho sisi wapemba, kesho kutwa sis wazinzibara !!
 
as long as htutaki kuweka masuala ya muungano wazi, wala hatutaki kuujadili, basi matatizo kama haya tayaibuka kila siku.

viongozi wakati wa kujibu masuala wanakurupuka tu, kisha unasikia wansema i was missinformed!....

muungano umetawaliwa na ukungu, na inaonyesha watu wamechoka sasa.....
 
Back
Top Bottom