Mkuu wa Wilaya aliyecharaza Walimu huyu Hapa

Mwendapole I beg to differ with you very seriously. Ile issue ya Tabata undani wake ni kuwa yule Mkurugenzi hakuwa na kosa ila alisukumiwa mzigo na Meya. Tafuta facts then ufikie mahali pa kumwaga sera zako. Mkurugenzi alikuwa wa kwanza kupinga zoezi lile ila Meya kwa kuwa anajuana na wakubwa akaamuru wafanyiwe unyama ule. Its a pity ukweli haukuwekwa wazi hata ile Tume haikuweka hadharani matokeo yao. hii ndio sababu wamempeleka mikoani asiwazibie riziki.
 
Ok DC anawezakuwa na dhamira ya kweli ya maendeleo wilayani kwake, hata hivyo viboko si suruhisho kwa walimu kufundisha vizuri na wanafunzi kufaulu.....

Next Level, hata kama ingekuwa viboko ndio suluhisho (walimu wakiogopa viboko wataongeza bidii), hiyo sio issue. The issue ni kwamba viboko ni adhabu inayotolewa mahakamani!

Mkuu wa wilaya hajafukuzwa kazi kwa kuwa na opinion kwamba viboko ni suluhisho. Wame mfire Mkuu wa Wilaya kwa sababu amechukua sheria mikononi.

Yale yale yalomfanya Pinda aende kujiliza bungeni alipopata backlash baada ya kutangaza uchochezi kwa wananchi kupeana adhabu wenyewe kwa wenyewe.
 
Hata kama wale walimu walikuwa na makosa kiasi gani......VIBOKO? Hapana kabisa.......nyie mnao msupport yule DC, ivi assume wangekuwa ni mama zenu wazazi mnaowapenda, eti unarudi nyumbani unaambiwa eti DC kaja kawachapa viboko kwasabau ya uzembe kazini.......No jamani isiwe mkuki kwa KTM kwa binadamu uchungu...[/QUOTE]

Nadhani kwa mtu anayempenda mama yake mzazi pia asinge mwachia awe mlevi kupiliza hadi asahau majukumu yake ya msingi, kama kweli unampenda usiacha hali ifikie hapo labda ungemshauri aache kufundisha afungue kilabu cha pombe. Na kwa mtu muadilifu hata kama aliyekosea ni mama yako mzazi basi hiyo haitoshi kuhalalisha makosa yake..awe baba yangu au nani uzembe kazini hasa utakao sababisha kuharibu maisha ya watoto wasio na hatia ni kosa.
Kwani adhabu ya viboko kwako ni kubwa sana? tuulize sisi tuliosoma msondo ngoma hiyo ilikuwa ni kama soseji zetu kila asubuhi,na u know what hao hao walimu ndio waliokuwa wana administer hiyo dose.(sijutii imenisaidia sana tu)
 
laiti matokeo ya darasa la nne na la saba yangekuwa (ya shule zote za tz) yanawekwa kwenye magazeti kama yawekwavyo ya form four na six, watu wengi zaidi wangeunga mkono viboko vya DC! Watoto wa shule za mikoani, hasa vijijini, wana uezo sawa sawa na wale wa shule za miji mikubwa, wakati mwingine hata kuwazidi. Lakini wao hawapati nafasi za ku-shine kwa sababu ya huo uzembe wa watu walio na dhamana ya kuhakikisha watoto hao wanasonga mbele! Halafu sijui mamlaka husika zina-react vipi kuona maendeleo duni ya wanafunzi kutoka shule hizo! Hayo maonyo yanayopelekea kufutwa kazi nasikia mpaka yafike sita! Hivi kweli mpaka yafike sita, wewe ni mkosaji wa kiasi gani?
sasa kwa hesabu ya haraka haraka uwafanye nini watendaji hawa?
 
Kama kuna jina ambalo ungestahili kwa kigeugeu hiki cha hoja basi ni MALAYA ni kipi haswa unachosimamia ndugu yetu? mara kuchapwa sio sawa mara iwe sawa? au analysis yako isiyo poor haina principles inazo zisimamia? im out here, my grade three daughter will respond to your next st*p*d post.[/QUOTE]

haaaaah ahaaaaah!:confused:.......! is the following post done by Burn's grade 3 daughter?

Hata kama wale walimu walikuwa na makosa kiasi gani......VIBOKO? Hapana kabisa.......nyie mnao msupport yule DC, ivi assume wangekuwa ni mama zenu wazazi mnaowapenda, eti unarudi nyumbani unaambiwa eti DC kaja kawachapa viboko kwasabau ya uzembe kazini.......No jamani isiwe mkuki kwa KTM kwa binadamu uchungu...[/QUOTE]

Nadhani kwa mtu anayempenda mama yake mzazi pia asinge mwachia awe mlevi kupiliza hadi asahau majukumu yake ya msingi, kama kweli unampenda usiacha hali ifikie hapo labda ungemshauri aache kufundisha afungue kilabu cha pombe. Na kwa mtu muadilifu hata kama aliyekosea ni mama yako mzazi basi hiyo haitoshi kuhalalisha makosa yake..awe baba yangu au nani uzembe kazini hasa utakao sababisha kuharibu maisha ya watoto wasio na hatia ni kosa.Kwani adhabu ya viboko kwako ni kubwa sana? tuulize sisi tuliosoma msondo ngoma hiyo ilikuwa ni kama soseji zetu kila asubuhi,na u know what hao hao walimu ndio waliokuwa wana administer hiyo dose.(sijutii imenisaidia sana tu)

Burn! burn! burn......!so hapa leo upo mwenyewe au binti?

Ok let's forget yaliyopita mkuu Burn ni vijimambo vya hapa JF.

Back to our business, naomba mkuu uwe realistic, kweli upo tayari mamako achapwe eti kwa sababu ya watoto wasio na hatia wamefeli? Kuwa mkweli basi!.........! unauchungu zaidi na jirani yako kuliko familia yako? charity begins home mkuu!

Huko Msondo ngoma, ndiko na sisi tulikosomea lakini hatukuwahi kuona mateacher wetu wakichapwa, ingetokea kipindi kile tungewacheka sana na kuwadharau!

Mkuu inaokena pia hujui sana utendaji wa kazi kwenye maofisi ya serikali, kiasi cha kuona hilo kosa la walimu adhabu pekee ilikuwa kuwachapa bakora (kuchukua sheria mkononi)

Hebu nenda pale Uhamiaji, wizara ya Elimu, Baraza la mitihani, Ofisi za Elimu za Wilaya e.g Morogoro, Wizara ya Ardhi just to mention a few......! na kwambia kama utakuwa huna siraha mkononi kwa mtaji huu (kujichukulia sheria mkononi), utavua viatu vyako na kuwarushia wale watendaji jinsi walivyo na jeuri as if ofisi zile ni za baba zao!
 
Rais alifikia hatua hiyo kutokana na kitendo cha Mkuu huyo wa Wilaya kuamuru walimu wa shule tatu za msingi kucharazwa viboko kwa madai kuwa wana tabia ya kutoroka na kuchelewa kufika kazini, vitendo vilivyosababisha wanafunzi wa shule za wilaya hiyo kufanya vibaya katika mitihani ya taifa ya kuhitimu elimu ya msingi.

Mkuu huyo wa Wilaya alifanya kituko hicho Jumatano iliyopita alipoamua kufanya ziara ya ghafla katika baadhi ya shule zilizopo katika Wilaya ya Bukoba akiwa amefuatana na koplo wa Polisi kisha kumuamuru koplo huyo awachape walimu viboko viwili hadi vinne.

Mnali alipoulizwa kama adhabu hiyo haikuwa inawadhalilisha walimu, alijibu haiwadhalilishi kwa kuwa haikutolewa mbele ya wanafunzi na kwamba yeye si mtu wa kwanza kutoa adhabu ya aina hiyo anayoona kuwa ni ndogo.

Hata hivyo serikali imeamua kuchukua hatua za haraka kumfuta kazi Mkuu huyo wa Wilaya kutokana na ukweli kwamba amekwenda kinyume na taratibu za kazi na kamwe kitendo hicho hakiwezi kukubalika katika mfumo wa madaraka unaozingatia sheria, haki na utawala bora.

Ingawa Mnali ameshafukuzwa kazi, makosa aliyofanya ni changamoto kwa serikali kwa kuwa yanadhihirisha kuwa wapo viongozi ambao hawajui mipaka ya kazi zao wala Kanuni ya Sheria ya Utumishi wa Umma. Ukosefu wa elimu ya Kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma unasababisha baadhi ya viongozi kwenda kinyume cha sheria, kujichukulia madaraka mikononi na wengine kushindwa kutimiza majukumu yao kwa ukamilifu.

Pia wapo wanaotumia madaraka kwa maslahi binafsi kwa kuwa hakuna mfumo thabiti wa kufuatilia na kutathmini mara kwa mara utendaji katika utumishi wa umma na kama mfumo huo upo basi haufanyi kazi ipasavyo hususan kwa kufuatilia utendaji wa viongozi katika taasisi mbalimbali za serikali.

Ingawa serikali imefanya jambo la busara kuchukua hatua za haraka na kumfuta kazi Mkuu huyo wa Wilaya ili kutoa fundisho kwa viongozi wengine, ni vyema ikaangalia kiini cha tatizo. Kama itabaini kuwa chanzo ni ukosefu wa elimu juu ya Kanuni na Sheria za Utumishi wa Umma, basi elimu hiyo itolewe kwa watumishi wote wa umma ili kuzuia ukiukwaji wa sheria hiyo.

Pia walimu na watendaji wengine wasidhani kuwa serikali imemwadhibu Mnali kwa sababu inakubaliana na uzembe unaorudisha nyuma maendeleo ya taifa. Ni vyema ifahamike kuwa Mnali amefukuzwa kazi kwa kosa la kuamuru walimu wachapwe kwani alipaswa kutumia njia sahihi kuwawajibisha walimu hao.

Mnali alikuwa akitetea jambo la msingi na la muhimu katika maendeleo ya taifa lakini hakutumia njia sahihi kulitekeleza. Hivyo ni wajibu wa serikali kuendelea kutetea maendeleo ya elimu katika Wilaya ya Bukoba kwa kuwaondoa walimu na watendaji wote wazembe.


From:- HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | Mkuu wa Wilaya Bukoba ametoa changamoto
 
haaaaah ahaaaaah!:confused:.......! is the following post done by Burn's grade 3 daughter?

hiyo no babake ndi mwenye msimamo na wazembe mkulu

.......begins home mkuu!
Kwa hiyo mkulu na kina Liyumba kujigawia keki ya taifa na kuzinufaisha familia zao ni sawa? maana charity begins at home.

Huko Msondo ngoma, ndiko na sisi tulikosomea lakini hatukuwahi kuona mateacher wetu wakichapwa, ingetokea kipindi kile tungewacheka sana na kuwadharau!

Labda walimu wenu walikuwa wawajibikaji au hamkuwa na viongozi wawajibikaji ka afande Mnali

Mkuu inaokena pia hujui sana utendaji wa kazi kwenye maofisi ya serikali, kiasi cha kuona hilo kosa la walimu adhabu pekee ilikuwa kuwachapa bakora (kuchukua sheria mkononi)

Ni kweli mkulu lakini pia si angalii viboko tu kama adhabu, bali hiyo nia yake ya kusimamia maadili, hapa mzee watu wamependa huo ujasiri wa kusimamia haki na uwajibikaji

Hebu nenda pale Uhamiaji, wizara ya Elimu, Baraza la mitihani, Ofisi za Elimu za Wilaya e.g Morogoro, Wizara ya Ardhi just to mention a few......! na kwambia kama utakuwa huna siraha mkononi kwa mtaji huu (kujichukulia sheria mkononi), utavua viatu vyako na kuwarushia wale watendaji jinsi walivyo na jeuri as if ofisi zile ni za baba zao![/QUOTE]

At least you have shown some sense of concern, SOMETHING NEED/ HAS TO BE DONE. Na wakati wa vita unatumia siraha unayoweza kuipata kwa wakati huo halafu utajibu masuala ya haki za binadamu ukishinda au vp?
 
WoS kumbuka Albert Mnali ni ret Col wa Jeshi!!

Hapana. Katika gazeti la leo 18 Feb 'Majiri' page 5 Makao Makuu ya Jeshi yamekanusha taarifa kuwa mnali alikuwa mwanajeshi wala hawana jina kama hilo katika maofisa wake waliostaafu.

Hata mimi ningeshangaa. Jeshi lina discipline. Utachapaje watu viboko? Huko ni kukiuka haki za binadamu. Nawashangaa wale wote wanaoshabikia akina mama kuchapwa viboko mpaka wanapoteza siku zao.

Jamani tusifanye maskhara katika mambo haya. Huu ndio mwanzo wa nchi kuendeshwa kinyume cha sheria. Siku yakiwakuta na ninyi, dada zenu, wake zenu na shangazi zenu wakatandikwa viboko msije mkalalamika. Waulizeni wenzenu huko Uganda yaliyowakuta wakati wa Iddi Amin.
 
Sasa ni zamu ya Madakari na Manesi kucharazwa viboko. Maendeleo hayaji kwa kubembelezana bwana.
 
Imesha kataliwa na vyombo vya juu vya jeshi jamaa sio col mstaafu na wala hajawahi kuwa mwanajeshi.LABDA MNAFIKIRI HIVYO KWA KUWA ALIYE KUWA MKUU WA MKOA WA KAGERA LT GEN KIHWELU Mtaafu alikuwa anawachapa viboko watumishi wazembe hasa walimu.
KTK KUTEKELEZA MALENGO KUNA NJIA NYINGI IKIWEMO VIBOKO KUTUMIKA. Hongera DC na pole kwa kibarua kuota mbawa lakini wananchi wanajua ulichotaka na wako nyuma yako
 
pamoja na hizo pongezi anazopewa bwana mnali, mimi nafikiri ameongeza tatizo na wanafunzi wa wilaya yake watafeli zaidi. nasema hivyo kwa sababu, kwa waalim kuchapwa tena mbele ya wanafunzi, imewaondolea ujasiri na authority waliyokuwa nayo kwa wanafunzi wao. waalim wamedhalilishwa na hii kisaikolojia itaendelea kuwatafuna hasa wakihisi kudharauliwa na wanafunzi wao. Hivyo moyo wa kujiamini wanapofundisha umepokonywa labda wahamishiwe mikoa mingine wasikojulikana.
 
mimi nafikiri ameongeza tatizo na wanafunzi wa wilaya yake watafeli zaidi

Napingana na wewe, iwapo wanafunzi watafeli zaidi idadi ya bakora itaongezeka, nakumbuka Tosamaganga constant ilikuwa fimbo 6, ukipata constant 2 maanake bakora 12. Sidhani kama kuna mwalimu atakubali idadi ya bakora itaongezeka kwa kutofaulisha watoto
 
Last edited:
good! kama viongoz wangemwiga huyu tusingekua na mafisadi wala vihiyo! iwe changamoto kwa viongozi wa juu.hongera MNALI ujumbe wako umefika! GOD BLESS U WHEREVER U`RE!
 
Mtu ambaye hajafika Bukoba vijijini hawezi kuelewa kero ambazo walimu wanawapa wazazi. Wengi wa walimu hawafundishi wanafanya miradi yao ikiwemo tuition za nguvu.
DC alichofanya si sahihi ila msg imefika kwa walengwa. waziri wa elimu awawajibishe waratibu kata wa elimu na afisa elimu wilay kwa kutofuatilia
 
kusema kweli kabisa wanatakiwa akina mnali kama 200 hivi,kuanzia ikulu iwe bakora tu maana nidhamu ya kazi haipo kabisa,uzembe kila mahali mpaka muhimbili wakapasua kichwa badala ya mguu.hongera mnali 2010 gombea ubunge wa kinondoni uwachape mateja wote wanaosumbua vituoni
 
jamani... salam hazikumfikia mjomba wetu....
sasa tukipata nauli tutamfata huko huko....tusubiri korosho zitie tiki ili tupate hiyooo nauli
 
Last edited:
DC Mnali (aliyefukuzwa) alitokea ofisi ya bunge kabla ya kuwa DC. Ni DC mzoefu kwa takriban muongo mmoja na nusu! Kabla ya Bukoba huko kwingine alikopita kuna taarifa zozote kuwa alitumia madaraka yake vibaya? Bukoba wanamuunga mkono-wanaonaje wakimwita akagombea ubunge? Halafu maafisa uchaguzi wote ni waalimu!!! kazi hapo
 
Mpya toka eneo la tukio.
Shule zote tatu zipo KATA YA KATERERO ambapo ni ngome ya CHADEMA na katika uchaguzi mkuu uliopita Mgombea wa UDIWANI wa CHADEMA Nd. Paschal "Mwingereza" Bashange (Leonard kama alivyozooeleka) kama sio nguvu ya pesa ya KARAMAGI ya kununua kura siku ya uchaguzi hakuna ubishi kiti cha udiwani kilikuwa cha CHADEMA iliyokuwa inaungwa mkono kwa nguvu zote na hao waalimu ambao ndo walikuwa wasimamizi wa vituo na ndo waliotoa siri na mbinu za ushindi wa CCM baada ya kura (a difference of only 46 votes, out of 8,000 voters).
serikali ya CM ilikuwa imewaweka kiporo inawatafutia siku.
Huyu bwana wa CHADEMA tayari amerudi toka DAR ambayo ndo makazi yake na yupo pamoja na waalimu akiwafariji na kupanga ni njia zipi za kisheria zifuatwe.
Vikao mbali mbali nje ya maeneo ya shule vinaendelea kwani jambo lenyewe limehamishwa kimtazamo na sasa limechukuliwa kama ni kulipiza kisasi cha kuhasi CCM.
Wasifu wa Bwana Mwingereza:- Ni mzaliwa wa Kata Katerero, kijiji cha Kanazi. Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa KAGERA, pamoja na kuwa ni mfanyabihashara maarufu wa INSURANCE na Building Contractor (Reg. CRB) ni Experienced na Senior Accountant of Ndesamburo (MP) Business (Keys Interprise (T)). Sasa hivi moto umewaka kwani huyu jamaa yupo eneo la tukio.
Obtained from reliable sources.
 
Kwa taarifa tulizo nazo DC huyu alikuwa anashughulikia elimu ila alikatishwa tamaa. Amekuwa anazungukia shule nyingi zikiwamo Kahororo, Ihungo na Nyakato na kuingia darasani kuhakiki kama walimu wanahudhuria vipindi vyao sawa. Siku moja alimchukua mwanafunzi wa kidato cha pili pale Kahororo baada ya kukuta ana daftari la Jiographia, mwaka mzima ameandika notice kurasa mbili tu. Shuleni akakuta mwanafunzi anahudhuria kila siku lakini mwalimu haingii darasani. Mwalimu alijieleza kurasa kumi.
 
Jamani kuanzi tarehe moja mwezi ujao, mtu yeyote yule ambaye atataka kumlipa mwenzake kiasi cha fedha cha zaidi ya milioni kumi (10,000,000) kwa kutumia cheki ya benki moja ili mlipwaji a-depositi benki nyengine (benki yake), haitawezekana tena.

Mfano mwengine ni huu; Yani kama unamdai mtu hela kiasi cha zaidi ya milioni kumi (10,000,000) kisha huyo mtu akulipe kwa kutumia cheki basi wewe kataa maana ukiipeleka hiyo cheki katika benki yako itakataliwa. Lakini kama cheki ni chini ya milioni kumi haina tatizo.

Hii ina maana kuwa Clearing House ya Benki Kuu ya Tanzania haikubali malipo binasfi ya cheki zinazo zidi milioni kumi. Badala yake kama unataka kumlipa mtu hela zaidi ya milioni kumi basi njia ni hizi zifuatayo;

1. Mdumbukizie pesa kwenye akaunti yake kwa kuenda wewe binafsi au mwakilishi wako katika benki yake.
2. Nenda katika benki yako kisha uiagize benki yako itume hela kwa mfumo wa TISS (Tanzania Interbank Settlement System)
3. Mlipe taslimu (cash).

UFAFANUZI
1. Kama mtu amekupa cheki ya benki ambayo wewe pia una akaunti kwa jina hilo hilo lililoandikwa kwenye Cheki basi haina noma hataka kama imezidi milioni kumi italipwa tu ilimradi mlipaji awe na hela za kutosha kwenye akaunti husika.
2. Malipo yote ya Cheki ya chini ya milioni kumi hatakuwa kama kawaida.
3. Special Clearance ya zaidi ya milioni kumi itakuwa hakuna tena.
4. Malipo yote ya Cheki za Serikali yatakuwa kama kawaida.

Ikumbukwe kuwa ni malipo yale tu yanayohusisha benki mbili yani (bank to bank payments) ndio tunayoyaongelea.

Source: Pwani Raha
 
Back
Top Bottom