affinitytz
JF-Expert Member
- Feb 10, 2020
- 206
- 983
Wasalam,
Kwa mkuu wa shule,
Awali ya yote nipongeze uongozi wa Capacity Building Trust kwa namna ambavyo unajitahidi kuboresha mazingira ya shule na kukuza maendeleo ya kitaaluma ya shule hii.
Kwa wasiofahamu Capacity Building Nursery and Primary School ni shule ya mtaala wa kiingereza iliyopo eneo la Kisiwani huko Kigamboni.
Ni shule nzuri na Ina matokeo mazuri kitaaluma.
Leo nataka kufikisha ujumbe kutoka kwa wazazi ambao wamechoshwa na baadhi ya tabia za Walimu ( ni baadhi ya Walimu, zingatia hilo) ambao wamekuwa na tabia ya kunyanyasa na kupiga watoto bila kufuata utaratibu wa adhabu.
Zingatia, wazazi hawana tatizo na adhabu ila zufuate utaratibu na kwa kiwango stahiki.
Baadhi ya Walimu wanapiga watoto mpaka wanavimba mikono, viwiko , wengine wanapiga watoto migongoni. Na wengine imekuwa ni kawaida kumchapa mtoto kila anapokosea kwenye homework.
Na wengine wanatumia mikono kufinya, kusukuma kupiga makofi na hata mateke kupiga wanafunzi
Wazazi wengi wamepokea malalamiko kwa Walimu wa darasa la tatu, nne na tano.
Mkuu wa shule ndugu Abraham Ntengwi , kaa na Walimu wako na uwaelekeza namna bora ya kutoa adhanbu na sio kuwaonea watoto.
Mnawapa tabu wazazi maana watoto mpaka wanagoma kuja shule kwa sababu ya baadhi ya Walimu kuwa wakali na kutoa adhabu zisizofa.
Zingatia: Hali ya Walimu wako ikiendelea hivi tutawataja majina ili kila mtu ajue.
Tunathamini kazi ya ualimu lakini sio kutesa watoto kwa bakora na kuwapiga tena bila kuzingatia muongozo wa kutoa adhabu.
Wazazi wana group la Whatsapp na wanajadili haya mambo, ni suala la muda tu kabla makubwa hajaibuka, huwezi kupiga mtoto wa miaka 9 mgongoni mpaka ukaacha alama za bakora. Wengine mnawapiga mpaka mikono inavimba.
Zungumza na Walimu wako wafanye kazi kwa weredi na kwa kuzingatia muongozo.
Ukicheka nao wataipa shule sifa mbovu na litakuwa jambo baya sana.
Wako katika ujenzi wa taifa.
Kwa mkuu wa shule,
Awali ya yote nipongeze uongozi wa Capacity Building Trust kwa namna ambavyo unajitahidi kuboresha mazingira ya shule na kukuza maendeleo ya kitaaluma ya shule hii.
Kwa wasiofahamu Capacity Building Nursery and Primary School ni shule ya mtaala wa kiingereza iliyopo eneo la Kisiwani huko Kigamboni.
Ni shule nzuri na Ina matokeo mazuri kitaaluma.
Leo nataka kufikisha ujumbe kutoka kwa wazazi ambao wamechoshwa na baadhi ya tabia za Walimu ( ni baadhi ya Walimu, zingatia hilo) ambao wamekuwa na tabia ya kunyanyasa na kupiga watoto bila kufuata utaratibu wa adhabu.
Zingatia, wazazi hawana tatizo na adhabu ila zufuate utaratibu na kwa kiwango stahiki.
Baadhi ya Walimu wanapiga watoto mpaka wanavimba mikono, viwiko , wengine wanapiga watoto migongoni. Na wengine imekuwa ni kawaida kumchapa mtoto kila anapokosea kwenye homework.
Na wengine wanatumia mikono kufinya, kusukuma kupiga makofi na hata mateke kupiga wanafunzi
Wazazi wengi wamepokea malalamiko kwa Walimu wa darasa la tatu, nne na tano.
Mkuu wa shule ndugu Abraham Ntengwi , kaa na Walimu wako na uwaelekeza namna bora ya kutoa adhanbu na sio kuwaonea watoto.
Mnawapa tabu wazazi maana watoto mpaka wanagoma kuja shule kwa sababu ya baadhi ya Walimu kuwa wakali na kutoa adhabu zisizofa.
Zingatia: Hali ya Walimu wako ikiendelea hivi tutawataja majina ili kila mtu ajue.
Tunathamini kazi ya ualimu lakini sio kutesa watoto kwa bakora na kuwapiga tena bila kuzingatia muongozo wa kutoa adhabu.
Wazazi wana group la Whatsapp na wanajadili haya mambo, ni suala la muda tu kabla makubwa hajaibuka, huwezi kupiga mtoto wa miaka 9 mgongoni mpaka ukaacha alama za bakora. Wengine mnawapiga mpaka mikono inavimba.
Zungumza na Walimu wako wafanye kazi kwa weredi na kwa kuzingatia muongozo.
Ukicheka nao wataipa shule sifa mbovu na litakuwa jambo baya sana.
Wako katika ujenzi wa taifa.