Mkuu wa Wilaya aliyecharaza Walimu huyu Hapa

Kenge (Eng)

JF-Expert Member
Dec 7, 2006
543
156
Mh. Mnali mwenye miwani na suti ya kijivu anavyoonekana katikati ya wachezaji wa timu ya Kagera Sugar.
i229_Picture070.jpg

Huyu bwana pamoja na kukosea kiuwajibikaji alikuwa na kila haki ya kuwacharaza walimu kwani sio tu labda ni kwa sababu ya kutolipwa masilahi yao kwani wanayo pesa nyingi kutokana na miradi yao inayowachukulia muda wao kiasi cha kutowahi au kutofika kazini kabisa.

Hawa walimu wa shule zilizotajwa "Katerero", "Kanazi" na "Kansenene" wapo katika center ya biashara ya abiria na mizigo hasa siku za meli Jumatatu, Jumatano na Ijumaa ambazo ni siku za kazi wao ufanya biashara ya kusafirisha abiria kutota bandarini Kemondo (ipo jirani na shule hizi kata ya KATERERO) kutumia pikipiki zao walizozipata kupitia SACCOS na Pesa za KIKWETE. Hii biashara ni maarufu sana mjini bukoba na vitongoji vyake, tuseme Mkoa wa Kagera kwa ujumla.

Huyu Mh. pamoja na hasira za wilaya yake kuwa ya mwisho kimkoa darasa la saba alijagundua chanzo ni hawa jamaa kutokuwa na moyo wa kazi hiyo tena, nani anapenda pesa ya mwisho wa mwezi wakati ipo ya papo kwa papo. amini usiamini kichwa (abiria) kikikatiza karibu na darasa hilo somo limekufa.

Helmet na majacket mazito ya kuzuia baridi yanakaa tayari darasani.
("Mwalimu Juma kuna kichwa kituoni") hizi shule zote zipo kando kando ya barabara kuu na zina vituo vya abiria.

Mh. Mkuu hakuvumilia pale alipoenda na kukuta kila mmoja anakuja kwa wakati wake ali hali wanafunzi wapo wanacheza.

Aliuliza "Kama mtoto anachelewa anapigwa viboko nipe tofauti yake na wewe ndani ya mazingira ya shule"

Wakacharazwa bwana wee!!! Lakini bila hii Reli ya Kati enzi za Mjerumani ingekuwa ndoto.

Pole Mkuu, ninakuombea JK akufikilie tena kwani umeteleza katika dhamira ya kuinua morali ya kazi sio lazima masilahi hata bakora.

Heko mh. pamoja na kuwa upo nje ya ajira.
Umepoteza kazi ila "MESSAGE SENT"
 

Attachments

  • Picture 070.jpg
    Picture 070.jpg
    353.2 KB · Views: 245
Huyu Mkuu DC atakuwa very marketable kwenye private sector.Apumzike kwanza kisha Auze CV yake.
I wouldnt mind engaging such a self motivated guy to supervise my biz! TZ tunahitaji a few of the likes of this DC!
 
Huyu Mkuu DC atakuwa very marketable kwenye private sector.Apumzike kwanza kisha Auze CV yake.
I wouldnt mind engaging such a self motivated guy to supervise my biz! TZ tunahitaji a few of the likes of this DC!

WoS kumbuka Albert Mnali ni ret Col wa Jeshi!!
 
WoS kumbuka Albert Mnali ni ret Col wa Jeshi!!
Hhahahhha!
Ofcourse I know..im just kidn..
ila on a serious note...kuna laxity ya ajabu sana katika utendaji serikalini..na inahitaji some very draconian measures kuwafanya watu wawe na discipline...
 
Huyu jamaa actually namtafuta tufanye biashara.

Sijui ana professiona gani!

Actually he is for presidential post in TZ, zile issue za akina Lowasa, Karamagi n.k kwenye RICHMOND, angezishughulikia mwenyewe achilia mbali kama asingewapiga shaba wezi wa EPA!

Hao walimu kuona wanastaili, wakakubali kulala chini kupigwa yaishe ala!
 
Vip? Mbona JK kashindwa kumvua na kumfukuza Naibu waziri wa mambo ya ndani Balozi Kaghasheki aliyemchapa na kumcharaza polisi (trafiki)vibao eneo la sayansi, barabara ya Ali hassan mwinyi,Cha kufuraisha Balozi kaghasheki ni mbunge wa Bukoba mjini wilaya inayoongozwa na kanalli mnali alyecharaza walimu
 
Ukweli ni kuwa tunahitaji watu kama hawa!

Sasa kama waalimu hawaji shuleni au wanachelewa...ni sheria tu za Kichana!

Yaani DC katumia sheria za Kichina hapa watu wanamlaumu kwa human rights!

Righjts gani ktkt ya rushwa na uzembe???

Hivi mwizi wa EPA ana rights gani?

JF naona double standards!

Sheria za China kwanza kuleta dicspline ktk kazi!

Tutofautishe kazi na siasa!
 
Mimi nashangaa hii serikali na maamuzi yake, yule mkurugenzi aliyesababishia serikali hasara ya 2 bil Tsh kule tabata alizawadiwa kuhamishwa kituo na kupelekwa shinyanga lakini huyu jamaa aliyewaashibu waalim kwa kuto kuhudhuria vipindi na hatimaye shule zao kuwa za mwisho kafukuzwa kazi.
Bongo kweli panashangaza.
 
Ok first I thought what DC did was messed, then Nikampigia mama mdogo aliye bongo ( by the way we are from Bukoba, kanazi area where these teacher taught). Mama mdogo kanieleza one of the teacher his her uncle. Kiufupi kasema huyo uncle kazi yake kupokea mshahara kulewa tu na shule haendagi kufundisha au akifika amelewa. Sasa jamani hawa ndiyo walimu wakuwatetea? sikubaliani na viboko lakini something needs to be done.
 
Tukipata watu kama hawa kila Wizara na mkoani,wilayani tanzania itafika mbali
 
Huyu Mkuu DC atakuwa very marketable kwenye private sector.Apumzike kwanza kisha Auze CV yake.
I wouldnt mind engaging such a self motivated guy to supervise my biz! TZ tunahitaji a few of the likes of this DC!

Nadhani hata yeye sio muwajibikaji. Inakuwaje mpaka matokeo mabaya ndio aseme walikuwa hawafiki kazini na wakifika wanafika kwa kuchelewa. Angekuwa makini angekuwa alishawawajibisha siku za nyuma sio baada ya matokeo ya wanafunzi. He deserves severe punishment
 
No, huyu jamaa acheni awe fired. Kwanza ameingilia majukumu ya Mkurugenzi wa Wilaya. Yeye ana maeneo yake ya kazi kama vile siasa na ulinzi katika wilaya yake.
 
Nadhani hata yeye sio muwajibikaji. Inakuwaje mpaka matokeo mabaya ndio aseme walikuwa hawafiki kazini na wakifika wanafika kwa kuchelewa. Angekuwa makini angekuwa alishawawajibisha siku za nyuma sio baada ya matokeo ya wanafunzi. He deserves severe punishment

sidhani kama hicho ni kipimo cha kutokuwajibika, as logical thinker lazima uwe na ground for whatever argument you are possing. huyu bwana katumia kigezo cha watu kuferi, hakuishia hapo pia ameenda mwenyewe kufuatilia ili kujua tatizo wakati anafuatilia ndio akakumbana na hayo.

tujaribu kuwa wakweri watendaji wengi wa taasisi za umma wako so relaxed, wanafanya kazi kwa kutaka na kwa utaratibu wanopanga wenyewe kufanyiwa hayo ni sahihi 100%

mtu akitoka serikali huwa ni vigumu sana kwake kufanya kazi na private sectors as they are irresponsible.
 
Ok first I thought what DC did was messed, then Nikampigia mama mdogo... Sasa jamani hawa ndiyo walimu wakuwatetea? sikubaliani na viboko lakini something needs to be done.

NAUMIA,

Kwani watu wanatetea walimu kwamba ni wazuri au wanatetea kwamba wasichapwe viboko period?

Kama hujui kinachoendelea hapa, wengi tunapinga walimu kupigwa, period, na kama wewe unasema hukubaliani na viboko basi na wewe uko pamoja na wanaotetea walimu!

Maana naona unachokitetea, unachozungumza, inawezekana hata hukijui!
 
Hata kama wale walimu walikuwa na makosa kiasi gani......VIBOKO? Hapana kabisa.......nyie mnao msupport yule DC, ivi assume wangekuwa ni mama zenu wazazi mnaowapenda, eti unarudi nyumbani unaambiwa eti DC kaja kawachapa viboko kwasabau ya uzembe kazini.......No jamani isiwe mkuki kwa KTM kwa binadamu uchungu.......!

Ok DC anawezakuwa na dhamira ya kweli ya maendeleo wilayani kwake, hata hivyo viboko si suruhisho kwa walimu kufundisha vizuri na wanafunzi kufaulu.....combination ya many factors inahitajika hapa kuanzia makao makuu ya wilaya mpaka kwa wanakijiji!

Nakubaliana na yeye kwamba kufeli kwa wanafunzi si jambo jema kabisa and that something should be done lakini sio VIBOKO kwa walimu .....No!No!
 
Watu wengi walibisha sana maamuzi ya huyu DC leo wengi wanaona alicho kifanya kilikuwa jambo la maana sana.Jamani asikwambie mtu ina udhi sana mtu mzima kuanza kumsukuma kama mtoto mdogo au una mbembeleza aende akafundishe wkt ni ajibu wake.
 
.......nyie mnao msupport yule DC, ivi assume wangekuwa ni mama zenu wazazi mnaowapenda, eti unarudi nyumbani unaambiwa eti DC kaja kawachapa viboko kwasabau ya uzembe kazini.......No jamani isiwe mkuki kwa KTM kwa binadamu uchungu.......!
Wachapwe tu.....uzembe kazini ndio dawa yake bakora tu........china wameendelea na wanazidi kusonga mbele kwa kuwa nidhamu kazini......
 
Huyu bwana ni shujaa na anastahili mapokezi makubwa sana atakapokuwa anarejea nyumbani kwao, mbona watu flani flani huwa pokea kwa mbwembwe mafisadi wanaporejea katika majimbo yao? si vyema zaidi tukashabikia mambo yaliyo bora kama haya ya mkuu huyu wa wilaya mwenye uchungu na watoto wa taifa hili? Na kwa ndugu zetu wanaotetea 'haki za binadamu' eleweni kuwa huo ulevi wenu mnaopewa na viji donation kutoka nje ili mpinge hata mambo ya msingi utatushinda wananchi. kuna uhalali gani kwa afisa wa Legal and human right ya dar es salaam kuandaa maandamano ya kupinga kitendo cha mkuu wa wilaya ya bukoba wakati wakazi wa wilaya hiyo walio wengi(ukiachilia wale waliochapwa) wanamtetea mkuu wa wilaya? Nilikwisha sema huyu bwana ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wote, nini bakora kwa wazembe hata risasi piga tu kwani uzembe wao pia unapoteza maisha ya watu wasio na hatia..nyambaffff
 
Back
Top Bottom