Mheshimiwa Mbowe usije kufungua Ofisi ya CHADEMA Arusha

Nakumbuka wiki iliyopita uongozi mzima wa Chadema ulikuwa uje kufungua ofisi ya kata ya Olorien- Chadema lakini kutokana na kikao cha dharula ilibidi uongozi mzima uwepo Dar es Salaam hivyo uzinduzi huo ukahairishwa mpaka wiki hii

Kwa mtazamo wangu ofisi kama hizi za kata zinatakiwa kufunguliwa na wenyeviti wa mikoa hivyo mheshimiwa tunaomba upumzike kwa hilo na kuwaachia viongozi wa mkoa
Binafsi ningependa kukuona ukizindua ofisi za mikoa na wilaya badala ya hizi za kata. Kifupi ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawajui hata ofisi za chadema za mikoa zilipo na pia ofisi zenye bado hazikidhi mahitaji ya chadema kikubwa kama chadema. Tunawaomba uongozi mfanye mikakati ili chama kiweze kuwa na ofisi zinazoeleweka ambapo ndo tutapenda mheshimiwa Mwenyekiti uje kufungua badala ya hizi za kata

Nashukuru na natumaini utakuwa umenielewa

Katika mada yako umepungukiwa na mawazo yakinifu mara usije kufungua ofisi za kata, mara fungua za mikoa, mara ofisi zenu azieleweki zilipo. je uonii kuwa ni chama kinachostawi na machungu ya umaskini, haki na usawa? mbona hicho kinachojulikana ofisi zake hawalipi kodi? na hua wanatumia majengo rasilimali za wananchi bure? sasa kipi bora hapo weee mtoa mada. Jambo lolote linaweza kufanyika ila inategemea mipango ya chama au unaogopa kuja kupata wafuasi wengi zaidi uko nini?

Tumekutuhumu wewe kachori
 
Namvua ipo stand kuu ya mabasi zamani ilikuwa inaitwa stadium store,
Mantisa mie sikuelewi mbali ya kuwa diwani mimi ni mwenyekiti wa vijana mkoa,na katika maandalizi ya kufungua hiyo ofisi ya olorien hatukumwalika mwenyekiti taifa kwa kuwa tunatambua majukumu aliyokuwa nayo kitaifa,sasa sijui kwa nini ulazimishe kuwa alikuwa aje.Kimsingi kama akiwa na muda sio vibaya yeye kufungua ofisi ya kata maana chadema tujijenga kuanzia ngazi ya shina,tawi,kata,wilaya,mkoa,kanda,na taifa,
Hiyo ofisi ya mkoa imezinduliwa kitambo,swala la kuwa ni wachache wanaifahamu ni sawa,na sisi tunajitahidi kuwajulisha wananchi nakuomba na wewe uendelee kuwajulisha ofisi ya mkoa ilipo,

Nanyaro Ephata, Nimefurahia unyenyekevu wako katika majibu hayo. You are a leader.
 
Hilo ghorofa la Namvua lipo mahali gani hapo Arusha? Naombeni mnisaidie kupafahamu.


liko pale stand kubwa ya mabasi linatazamana kwa upande mmoja na uwanja wa michezo wa sheikh amri abeid na kwa upande mwingine linatazamana na na kile choo cha kulipia ambacho ndani yake kuna ofisi kibao (ushaona ofisi ndani ya choo weye au umezoea kuona choo ndani ya ofisi tu) zamani jengo hilo likiitwa stadium store kama sikosei kabla ya kujengwa horofa niko tayari kurekebishwa kama nimekosea au ulizia standi ya kwenda loliondo ukishaiona hapo utakuwa umefikia karibu kabisa na hilo jengo karibu muzeiya uje kujitwalia kadi
 
Mantisa pamoja na hoja yako umepotosha umma maana si kweli kuwa Mwenyekiti taifa alikuwa aje kufungua hiyo ofisi,ni uongozi wa mkoa,na wilaya ndio walikuwa wafungue ila kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo tukaahirisha.Lakini pia hata Mwenyekiti taifa akifungua ofisi ya kata tatizo ni nini?
Ofisi ya mkoa ipo jengo la Namvua ghorofa ya nne

Ila hata mkifungua OLOLOO hatuwataki ng'o, sie na GAINO na akimaliza atagombea ubunge na pia CCM tuna vijana wetu wanakua tartibu so you bettr come up with a different strategy
 
Chadema wasimamishe kwanza ofisi ya mkoa na wilaya.. Hizi za kata na kijiji siyo lazima sana kwa sasa...
 
Kuna sababu gani za msingi kwa Mbowe kuja kufungua ofisi ya kata wakati hata Ofisi ya wilaya kama Arusha or Monduli watu hawaijui?
Ni mara ngapi tunamlaumu ****** kwende kufungua shule za msingi, zahanati, chekechea then why Mbowe au unataka kuniambia a spear is for a pig?

tunamlaumu kilaza kufungua shule za primary si ofsi za siasa,take care. Ok ok nimegundua,ulivoweka stori,unarelate kutojulikana kwa ofsi ya mkoa,ok. Kumbe unataka ofisi zenye adhi ya kifisadi ok. Ila sisi tuko tayari kukutana chini ya mwembe,mpapai au mchungwa kuikomboa nchi. Hatutaki ofisi za kifisadi. Au una lako jambo mkuu?
 
Kwetu sisi matawi ya huko waliko wananchi kwenye kata haswaa ndiko kuliko na umuhimu zaidi kwa CHADEMA na kila Mtanzania mmoja anayeongezeka kujiunga na chama kwetu sisi mtu huyo ni wa muhimu sana na ataendelea kuwa wa umuhimu huo huo kwa kipindi chote cha uanachama wake sawasawa na jinsi tunavyowaona umuhimu wa viongozi wa kitaifa.

Kwa maelezo haya, chonde mkaribisheni mwenyekiti wetu kufungua ofisi huko kwenye Jiji la Machalii na Mashujaa / Vinara wa Wabadiliko ya kweli kote Tanzania

Nakumbuka wiki iliyopita uongozi mzima wa Chadema ulikuwa uje kufungua ofisi ya kata ya Olorien- Chadema lakini kutokana na kikao cha dharula ilibidi uongozi mzima uwepo Dar es Salaam hivyo uzinduzi huo ukahairishwa mpaka wiki hii

Kwa mtazamo wangu ofisi kama hizi za kata zinatakiwa kufunguliwa na wenyeviti wa mikoa hivyo mheshimiwa tunaomba upumzike kwa hilo na kuwaachia viongozi wa mkoa
Binafsi ningependa kukuona ukizindua ofisi za mikoa na wilaya badala ya hizi za kata. Kifupi ni kwamba asilimia kubwa ya wananchi hawajui hata ofisi za chadema za mikoa zilipo na pia ofisi zenye bado hazikidhi mahitaji ya chadema kikubwa kama chadema. Tunawaomba uongozi mfanye mikakati ili chama kiweze kuwa na ofisi zinazoeleweka ambapo ndo tutapenda mheshimiwa Mwenyekiti uje kufungua badala ya hizi za kata

Nashukuru na natumaini utakuwa umenielewa
 
liko pale stand kubwa ya mabasi linatazamana kwa upande mmoja na uwanja wa michezo wa sheikh amri abeid na kwa upande mwingine linatazamana na na kile choo cha kulipia ambacho ndani yake kuna ofisi kibao (ushaona ofisi ndani ya choo weye au umezoea kuona choo ndani ya ofisi tu) zamani jengo hilo likiitwa stadium store kama sikosei kabla ya kujengwa horofa niko tayari kurekebishwa kama nimekosea au ulizia standi ya kwenda loliondo ukishaiona hapo utakuwa umefikia karibu kabisa na hilo jengo karibu muzeiya uje kujitwalia kadi

Asante sana. Nimepafahamu vizuri ila kadi ninayo tangu 1995, wakati Edwin Mtei alipokuwa anagombea ubunge wa Arusha mjini!
 
Katika mada yako umepungukiwa na mawazo yakinifu mara usije kufungua ofisi za kata, mara fungua za mikoa, mara ofisi zenu azieleweki zilipo. je uonii kuwa ni chama kinachostawi na machungu ya umaskini, haki na usawa? mbona hicho kinachojulikana ofisi zake hawalipi kodi? na hua wanatumia majengo rasilimali za wananchi bure? sasa kipi bora hapo weee mtoa mada. Jambo lolote linaweza kufanyika ila inategemea mipango ya chama au unaogopa kuja kupata wafuasi wengi zaidi uko nini?

Tumekutuhumu wewe kachori

Mimi nafikiri kuna vingi watu huwa hatufahamu bali tunakurukpuka na kushabikia tu. in short chadema ni chama ambacho kinakubalika na kimekuwa kikipendwa sana na watu wengi kutokana na kuwa na viongozi wenye uwezo wa kufichua mambo ambayo kimsingi wengi tusingeweza kuyajua, Hili limewapa umaarufu sana na kukifanya kuwa kweli chama cha kwanza kwa upinzani Tanzania. Ukiangalia hata uchaguzi ulipita watu wengi sana walikuwa wakikuunga mkono hata kuelekea kushinda uchaguzi kwa mujibu wao. Lakini kama kweli wao wanajipanga kuchukua nchi hii wangepigania yafuatayo kabla ya uchaguzi ujao:
1. Kuanzisha ofisi za kueleweka hasa za wilaya na mikoa ili waweze kujizolea wanachama lukuki ambao wengi wao ni washabaki. Mtu anayetoka wilayani anawezaje kuwa mwanachama wakati chama hakina Ofisi. Nikiuliza swali rahisi tu ofisi ya chadema ya Wilaya iko wapi hapa Arusha ni shida kujibiwa. Itakuwaje huko huko Lindi?
2. Baada ya hapo ndo kitaingia kwenye kata na ndo maana nikamuomba Mbowe asije kufungua ofisi hii ambayo ni kata ili apeleke hizo nguvu kufungua ofisi za wilaya na mkoa
 
Chadema wasimamishe kwanza ofisi ya mkoa na wilaya.. Hizi za kata na kijiji siyo lazima sana kwa sasa...

top-down or botton-up. Nadhani wana CDM na wapenzi wengi wako vijijini; hivyo wananchi wanapohamasika kuwa na ofisi vijijini/katani ni bora zaidi kuliko hata mkoani/wilayani (ingawa ni lazima tuwe na ofisi wilaya/mikoa haraka iwezekanavyo)
 
Back
Top Bottom