Mchumba wangu ana karama ya unabii, ananitisha!

Msiwe vichwa maji.

Nikisema kesi sio vita namaanisha mapambano hayawezi kufikia hatua ya kufanyiana ubaya. That is what I mean. Anayefanya ubaya anakuwa ametafsiri vibaya maana ya kesi ni vita/mapambano.

Sisi huku tunashindana kwa Sheria na Mantiki, sio mtutu wa bunduki.

Na kama ulikuwa hujui, Wanasheria tunahimizwa sana kumaliza kesi nje ya Mahakama, kuendelea na kesi iwe ni last resort. Ndio maana walipotuita hatukusita kwenda kuwaona. Ingawa wao walikuwa na nia ovu.
nisaidie hili wakili japo liko nje kidogo ya mada.

unawezaje kumtetea mtu aliyefanya uhalifu [tena akakueleza wazi kabisa uhalifu wake alioutenda] let say murder! (sio manslaughter). Mimi kwangu naona kama nashindwa!
 
nisaidie hili wakili japo liko nje kidogo ya mada.

unawezaje kumtetea mtu aliyefanya uhalifu [tena akakueleza wazi kabisa uhalifu wake alioutenda] let say murder! (sio manslaughter). Mimi kwangu naona kama nashindwa!
Ndiyo kazi ya Uwakili hiyo.
Kama unashindwa huwezi kuwa wakili.
Wakili pia hupaswi kuendekeza Dini, au kuwa na hofu ya mambo ya Dini.
 
nisaidie hili wakili japo liko nje kidogo ya mada.

unawezaje kumtetea mtu aliyefanya uhalifu [tena akakueleza wazi kabisa uhalifu wake alioutenda] let say murder! (sio manslaughter). Mimi kwangu naona kama nashindwa!
Then hufai kuwa wakili tafuta kazi nyingine! Haijalishi mteja wako ametenda uhalifu kiasi gani kazi yako ni kumtetea na siyo kumjudge.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hebu tafakari kwa upya. Kumbuka ndoa ina mambo mengi, kuna kupitiwa , huyu anakuumbua kabisa
Umejuaje kawakewa kwenye Pombe?
Au tafsiri ya 'Kinywaji' sikuhizi ni Pombe tu?
Brilliant observation mkuu, na nimeshaelezea hiki ulichosema kwenye comment yangu hapo mwanzoni.

Kwamba ni mwenye akili finyu tu atakayehitimisha kwamba kinywaji ni pombe pekee. Mimi situmii kabisa kilevi, na niliposema kinywaji nilimaanisha maji.

Sasa mtu anatoka huko ameshiba kande zake anakuja na conclusion kwamba maji ni pombe! Very pathetic
 
nisaidie hili wakili japo liko nje kidogo ya mada.

unawezaje kumtetea mtu aliyefanya uhalifu [tena akakueleza wazi kabisa uhalifu wake alioutenda] let say murder! (sio manslaughter). Mimi kwangu naona kama nashindwa!
Usishindwe mkuu

Unaweza kumtetea vizuri tu. Katiba inasema kila mtu ana haki ya kupata utetezi, no matter amefanya Kwa kukusudia au bila kukusudia.

Sasa kuna mambo mawili kwenye swali lako. Kuna yule amefanya kwa kukusudia kweli (murder), na anataka afanye confession (akiri) Mahakamani, ili kwenye maombolezo, wewe Wakili umuombee apunguziwe adhabu kwasababu amekiri na anajuta alichofanya, kwa maana nyingine hajaisumbua Mahakama hivyo imuhurumie impe adhabu ndogo.

Jambo la pili ni la yule aliyefanya kwa kukusudia kweli na anataka ufanye linalowezekana umtetee aonekana hajafanya kwa kukusudia (manslaughter). Hapa pia unaweza kumchomoa kwa kuchagua zile "defences to criminal liability' ambayo itafiti kwenye circumstance ya kesi yake. Kwa mfano kuna 'provocation'; yaani aliua kweli, ila ni baada ya kumfumania mkewe akifanywa na mwanaume mwingine kwenye kitanda chao cha ndoa, hivyo akawa provoked akajikuta hasira imempanda, ameua (kumbe wala hakuwa provoked, kwasababu baada ya kumfumania mkewe alimketisha mgoni wake, akampiga sana, hasira zikapoa, na akamwambia kabisa nakuua leo , so alijipanga, haikuwa hasira tena).

Mkuu, Wanasheria tunafundishwa tusiipotoshe Mahakama, ila kinachofanyika kwenye scenario ya pili ni kuipotosha Mahakama, kwasababu waliofanya kwa kusudi ndio walipaji wazuri sana wa fee ya Wakili . Mfano mzuri ni kesi ya mke wa Bilionea Msuya. Hii kazi inabidi uwe na Mungu kweli ndio uifanye kwa weledi. Vinginevyo, manung'uniko ya watu unaodhulumu haki zao hayatakuacha salama.
 
Wakuu habarini za wakati huu...

Niliwahi kuleta Uzi humu kuhusu mchumba wangu ambaye ni Mcha Mungu, bikira, mpole, mkarimu, mzuri n.k.

Nimegundua kwamba huyu mwanamke ana karama ya unabii pia (muonaji). Zamani manabii waliitwa waonaji.

Kwanini nimefikia hii conclusion? Mjomba wangu alikuwa anaumwa, yaani kaka yake mama yangu. Siku Moja kabla ya kifo cha mjomba wangu, mchumba wangu akanipigia simu kunimbia anaona huzuni KUBWA Kwa mama yangu, kesho yake mjomba akafariki, kweli mama aliumia sana!

Mimi ni Wakili, nilikuwa na kesi Tanga Jana, kabla sijaondoka akanipigia simu kuniambia anaona vita KUBWA kwenye hiyo kesi, na ananiona Niko hospitalini! Baada ya kesi, ule upande wa pili wakaniomba tuonane nje ya Mahakama nikiwa na mteja wangu ili tufute kesi tuyazungumze, kweli tukaenda kuonana nao, nikawekewa sumu kwenye kinywaji changu, nikapelekwa hospitalini kweli na nikalazwa, Sasa hivi ndio wameni-discharge.

Hayo ni machache tu kati ya mengi. Ama kweli, ukimtanguliza MUNGU mbele HUWEZI kuikataa taasisi ya NDOA. NDOA ni baraka.

Huyu nikimuoa inabidi niwe makini sana

Muwe na jioni njema.
Kwa nn huchukui hatua ukiambiwa kuna vita kubwa inabid uombe Mungusana
 
Wakuu habarini za wakati huu...

Niliwahi kuleta Uzi humu kuhusu mchumba wangu ambaye ni Mcha Mungu, bikira, mpole, mkarimu, mzuri n.k.

Nimegundua kwamba huyu mwanamke ana karama ya unabii pia (muonaji). Zamani manabii waliitwa waonaji.

Kwanini nimefikia hii conclusion? Mjomba wangu alikuwa anaumwa, yaani kaka yake mama yangu. Siku Moja kabla ya kifo cha mjomba wangu, mchumba wangu akanipigia simu kunimbia anaona huzuni KUBWA Kwa mama yangu, kesho yake mjomba akafariki, kweli mama aliumia sana!

Mimi ni Wakili, nilikuwa na kesi Tanga Jana, kabla sijaondoka akanipigia simu kuniambia anaona vita KUBWA kwenye hiyo kesi, na ananiona Niko hospitalini! Baada ya kesi, ule upande wa pili wakaniomba tuonane nje ya Mahakama nikiwa na mteja wangu ili tufute kesi tuyazungumze, kweli tukaenda kuonana nao, nikawekewa sumu kwenye kinywaji changu, nikapelekwa hospitalini kweli na nikalazwa, Sasa hivi ndio wameni-discharge.

Hayo ni machache tu kati ya mengi. Ama kweli, ukimtanguliza MUNGU mbele HUWEZI kuikataa taasisi ya NDOA. NDOA ni baraka.

Huyu nikimuoa inabidi niwe makini sana

Muwe na jioni njema.
Duh,!...
 
Usishindwe mkuu

Unaweza kumtetea vizuri tu. Katiba inasema kila mtu ana haki ya kupata utetezi, no matter amefanya Kwa kukusudia au bila kukusudia.

Sasa kuna mambo mawili kwenye swali lako. Kuna yule amefanya kwa kukusudia kweli (murder), na anataka afanye confession (akiri) Mahakamani, ili kwenye maombolezo, wewe Wakili umuombee apunguziwe adhabu kwasababu amekiri na anajuta alichofanya, kwa maana nyingine hajaisumbua Mahakama hivyo imuhurumie impe adhabu ndogo.

Jambo la pili ni la yule aliyefanya kwa kukusudia kweli na anataka ufanye linalowezekana umtetee aonekana hajafanya kwa kukusudia (manslaughter). Hapa pia unaweza kumchomoa kwa kuchagua zile "defences to criminal liability' ambayo itafiti kwenye circumstance ya kesi yake. Kwa mfano kuna 'provocation'; yaani aliua kweli, ila ni baada ya kumfumania mkewe akifanywa na mwanaume mwingine kwenye kitanda chao cha ndoa, hivyo akawa provoked akajikuta hasira imempanda, ameua (kumbe wala hakuwa provoked, kwasababu baada ya kumfumania mkewe alimketisha mgoni wake, akampiga sana, hasira zikapoa, na akamwambia kabisa nakuua leo , so alijipanga, haikuwa hasira tena).

Mkuu, Wanasheria tunafundishwa tusiipotoshe Mahakama, ila kinachofanyika kwenye scenario ya pili ni kuipotosha Mahakama, kwasababu waliofanya kwa kusudi ndio walipaji wazuri sana wa fee ya Wakili . Mfano mzuri ni kesi ya mke wa Bilionea Msuya. Hii kazi inabidi uwe na Mungu kweli ndio uifanye kwa weledi. Vinginevyo, manung'uniko ya watu unaodhulumu haki zao hayatakuacha salama.

Mkuu Ila Mimi naona mpo sahihi kuwatete wauaji

Maana haijalishi MTU ameua watu wangapi Ila second chance ni muhimu Sana.
 
Wakuu habarini za wakati huu...

Niliwahi kuleta Uzi humu kuhusu mchumba wangu ambaye ni Mcha Mungu, bikira, mpole, mkarimu, mzuri n.k.

Nimegundua kwamba huyu mwanamke ana karama ya unabii pia (muonaji). Zamani manabii waliitwa waonaji.

Kwanini nimefikia hii conclusion? Mjomba wangu alikuwa anaumwa, yaani kaka yake mama yangu. Siku Moja kabla ya kifo cha mjomba wangu, mchumba wangu akanipigia simu kunimbia anaona huzuni KUBWA Kwa mama yangu, kesho yake mjomba akafariki, kweli mama aliumia sana!

Mimi ni Wakili, nilikuwa na kesi Tanga Jana, kabla sijaondoka akanipigia simu kuniambia anaona vita KUBWA kwenye hiyo kesi, na ananiona Niko hospitalini! Baada ya kesi, ule upande wa pili wakaniomba tuonane nje ya Mahakama nikiwa na mteja wangu ili tufute kesi tuyazungumze, kweli tukaenda kuonana nao, nikawekewa sumu kwenye kinywaji changu, nikapelekwa hospitalini kweli na nikalazwa, Sasa hivi ndio wameni-discharge.

Hayo ni machache tu kati ya mengi. Ama kweli, ukimtanguliza MUNGU mbele HUWEZI kuikataa taasisi ya NDOA. NDOA ni baraka.

Huyu nikimuoa inabidi niwe makini sana

Muwe na jioni njema.
Huyo ndio mzuri sasa
Asante kwa kunitia moyo mkuu.
 
Mkuu Ila Mimi naona mpo sahihi kuwatete wauaji

Maana haijalishi MTU ameua watu wangapi Ila second chance ni muhimu Sana.
Sawa mkuu

Ingawa kuna mawakili wameokoka. Wao ukienda kukiri kwao umeua kwa kukusudia, wanazuga ratiba zao zimebana wanakuelekeza uende kwa Wakili mwingine. Kwasababu ukisema hutamtetea kwasababu ameua kwa kusudia na wewe umeokoka, wewe Wakili unakuwa umekosea kwa kukinzana na takwa la Katiba kwamba kila mtu ana haki ya kupata utetezi kwenye chombo chochote cha kutoa maamuzi.

So maadili ya Kiwakili yamekaa kimtego mtego sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom