Elections 2010 Mbowe Afanyiwa Fujo Kubwa Hai

Ilikuwa kama sinema za akina Rambo ama matukio ya Rwanda Genocide. Mgombewa ubunge jimbo la Hai kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akiwa katika mkutano wa hadhara huko Masama Kati ghafla kijana mmoja wa Green Guard alivamia mkutano kwa lengo la kuanzisha fujo. Kikosi cha ulinzi cha CHADEMA kilimdhibiti kijana huyo na kumhifadhi katika gari moja kwa lengo la kupisha mkutano uendelee.

Kumbe kijana huyo alikuwa ametangulizwa tu na kwamba pamoja naye walikuwepo vijana wa Green Guards wasiopungua 100. Vijana hawa wakiongozwa na Mgombea udiwani wa CCM katika kata hiyo walikwenda kufunga barabara ili msafara wa Freeman usipite eneo hilo. Kwa kawaida msafara wa Mbowe hutanguliwa na pick-up ambayo hubeba jukwaa na viti. Vijana hawa wa CCM waliliteka gari hilo lililokuwa linaendesha na Ndg. Lootore Lema na kumchukua kumpeleka katika nyumba ya mwanaCCM mmoja katika eneo hilo la Masama Mbweera.

Mbowe kusikia kuwa kamanda wake ametekwa alivunja mkutano na kuondoka kwenda kumwokoa. Walipofika kama 200m toka eneo la mkutano walikuta jeshi kubwa la vijana wa CCM wakiwa wameshikilia mapanga, mawe, majembe na vyuma. Hapo vita kamili ikaanza.

Katika vita hiyo magari ya msafara wa Mbowe yapatayo 6 yamevunjwa vunjwa vioo. Wanachama wa CHADEMA wameumizwa. Hata hivyo vijana wa CHADEMA walijitahidi kumlinda mwenyekiti wao wa taifa kwa kuongoza mapigano kama vita vya kawaida kabisa vya msituni. Ilimlazimu Mheshimiwa Mbowe kutoa bastola yake na kufyatua risasi kadhaa hewani ndipo Green Guards waliporudi nyuma na hivyo kuwezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara ambayo yangetokea kwa vita hiyo kuendelea uso kwa uso.

Ilikuwa patashika. Walinzi wa Mbowe walikuwa wakiwafuata Green Guards na kuwanyang'anya silaha zao na kuzitumia kuwapiga nazo. Kwa nasibu vijana kadhaa wa CCM wamekamatwa na kwa sasa wako katika kituo cha polisi cha wilaya ya Hai kwa ajili ya kuandika maelezo.

Taarifa zilizonifikia punde zinasema kuwa kijana mmoja ambaye amepigwa vizuri na CHADEMA ameomba asidhuriwe zaidi kwani atasema yote; namna walivyotumwa kuvamia na kuharibu mikutano ya Mbowe.

Waheshimiwa haya ni matunda ya mafunzo ya kijeshi ambayo CCM waliyafanya kwa vijana wao wapatao 5000 huko Iringa mwezi March mwaka huu na baadaye kule Moshi Vijijini ambako walitoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana 350.

Chonde Chonde CCM!!
Madaraka mnayataka, Sawa; Lakini Damu yetu mnaitakia nini?
TUACHIENI AMANI YETU!!!!!!!!!
Kamende, kwanza nakushukuru kwa taarifa hii, pili poleni kwa maswahibu hayo, huo ni mwanzo tuu au rasharasha, fainali ni October 31. Nimesema hiyo ni rasharasha tuu kwa sababu sikio la kufa, halisikii dawa, na mfa maji haachi kutapatapa, hii ni dalili ya maji ya shingo, hongereni.

Pia nina ushauri tuu kuwa inapotokea serious issue kama hii, wewe kama muhabarishaji, tuhabarishe facts tuu bila kuonyeshea wewe uko upande gani. Kwenye taarifa hii, wewe umejitanabaisha na Chadema. Hata kama ni kweli wewe ni Chadema, bado ungeweza kutuhabarisha kwa kutumia fairness, balance, objectivity na impartiality hivyo kuipa taarifa hii more credibility, otherwise itageuka sehemu ya campaign machinery.

Kamende, kama ulivyonisaidia Busanda na Biharamulo, nitahitaji msaada wako siku ya Jumatano, nakuja kunyooshea miguu kidogo hapo Moshi na Arusha.
 
Hii sumu inayomwagwa sisi m inaanza kututafuna kwa kasi zaidi. Hivi baada ya 31/10 wataongea nini wakati wanaishi eneo moja au wanasahu kuwa visasi na chuki vikikomaa ni balaa
 
sasa Jk aeleze anayemwaga damu ni nani. Huu ni ufedhuli wa hali ya juu. Eti anajifanya vyama vinataka kumwaga damu huku anatuma green guards.
 
vijana wa green guard hawana akili na Fuya ameshashindwa, walicofanya hakina maana... kani mbowe ameonyesha upuuzi mkubwa kama mwenyekiti wa chama kushindwa kumalizia mkutano na kufuata utaratibu wa sheria (ambao yeye kwa wilaya ya hai ana priviledge hiyo kubwa tu na anaijua) kumtoa kijana wake

Kama tunalaani violence, basi tuifanye kwa vitendo... kwa kwenda kufanya mambo ya tambaza nimesikitika sana

siamini mtu mwenye staha anaweza kuvunja mkutano kwenda kuokoa kwa staili ya kibohehe, mringa au tambaza

angetuma vijana

Nimesikitishwa na green guards lakini nimesikitishwa zaidi na mbowe

ukifanya ya kipumbavu na mpumbavu, watu hawatajua tofauti yenu
Acid, sometimes tit for tat does work!. Kuna wakati wa kutumia ustaarabu kuepusha shari lakini pia kuna wakati wa kutumia shari kuzima shari, yaani you beat them on their own game.
 
CHADEMA waombe kibali cha kutrain green guard wao na wenyewe. Wauambie umma namna ambavyo wanaumizwa na waeleze nia yao ya kujilinda kwa njia ya kutrain walinzi wao. Kwa kuwa CCM imetrain 5000 CHADEMA wanaweza kutrain hata 10000, wiki mbili hizi zinatosha kabisa kutoa mafunzo kamili kujiandaa na vita ya tar 1/11 yatakapotangazwa matokeo. Vinginevyo CCM watatumaliza na hatutakuwa na namna ya kujitetea.
 
chadema wanailaumu ccm na ccm nao wanawalaumu chadema kuwa ndio wanaoanzisha fujo na kutumia silaha maana sio ccm wenye walinzi peke yao hata chadema nao wana walinzi wao hivyo hatuwezi kuwa upande mmoja na kulaumu upande mwingine bila uchunguzi wa kina kufanyika na ndipo atajulikana nani anaetaka kumwaga damu za wa tz ili aingie ikulu!!!

Ama kuhusu member wa jf hatuna budi kuacha uchochezi na kuweka maslahi ya nchi kwanza kinyume chake nchi yetu itaingia ktk machafuko na watakao athirika ni watoto wetu, mama zetu, baba zetu, mabibi na mababu zetu!!!
Hivi wewe magazeti yote yanayoripoti kila siku taarifa za wafuasi wa CCM kuwashambulia wafuasi wa CHADEMA hujayaona? Watu wengine bwana, wana macho lakini hawaoni, wana masikini lakini hawasikii, wana pua lakini hazinusi. Unataka hadi upigwe kibao ndiyo utaelewa kwamba CCM imeanzisha vita? Hebu jaribu kuwa mzalendo kwa nchi yako kuliko kushikilia ushabiki usio na kichwa wala miguu.
 
vijana wa green guard hawana akili na Fuya ameshashindwa, walicofanya hakina maana... kani mbowe ameonyesha upuuzi mkubwa kama mwenyekiti wa chama kushindwa kumalizia mkutano na kufuata utaratibu wa sheria (ambao yeye kwa wilaya ya hai ana priviledge hiyo kubwa tu na anaijua) kumtoa kijana wake

Kama tunalaani violence, basi tuifanye kwa vitendo... kwa kwenda kufanya mambo ya tambaza nimesikitika sana

siamini mtu mwenye staha anaweza kuvunja mkutano kwenda kuokoa kwa staili ya kibohehe, mringa au tambaza

angetuma vijana

Nimesikitishwa na green guards lakini nimesikitishwa zaidi na mbowe

ukifanya ya kipumbavu na mpumbavu, watu hawatajua tofauti yenu

wanaccm kwa spin bana, eti amesikitishwa na mbowe. Mbowe angekosea sana kumuacha mmoja wa wafanyakazi wa kampeni yake kwenye mikono ya green guards. These are trained killers.
 
Ilikuwa kama sinema za akina Rambo ama matukio ya Rwanda Genocide. Mgombe wa ubunge jimbo la Hai kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akiwa katika mkutano wa hadhara huko Masama Kati ghafla kijana mmoja wa Green Guard alivamia mkutano kwa lengo la kuanzisha fujo. Kikosi cha ulinzi cha CHADEMA kilimdhibiti kijana huyo na kumhifadhi katika gari moja kwa lengo la kupisha mkutano uendelee.

Kumbe kijana huyo alikuwa ametangulizwa tu na kwamba pamoja naye walikuwepo vijana wa Green Guards wasiopungua 100. Vijana hawa wakiongozwa na Mgombea udiwani wa CCM katika kata hiyo walikwenda kufunga barabara ili msafara wa Freeman usipite eneo hilo. Kwa kawaida msafara wa Mbowe hutanguliwa na pick-up ambayo hubeba jukwaa na viti. Vijana hawa wa CCM waliliteka gari hilo lililokuwa linaendesha na Ndg. Lootore Lema na kumchukua kumpeleka katika nyumba ya mwanaCCM mmoja katika eneo hilo la Masama Mbweera.

Mbowe kusikia kuwa kamanda wake ametekwa alivunja mkutano na kuondoka kwenda kumwokoa. Walipofika kama 200m toka eneo la mkutano walikuta jeshi kubwa la vijana wa CCM wakiwa wameshikilia mapanga, mawe, majembe na vyuma. Hapo vita kamili ikaanza.

Katika vita hiyo magari ya msafara wa Mbowe yapatayo 6 yamevunjwa vunjwa vioo. Wanachama wa CHADEMA wameumizwa. Hata hivyo vijana wa CHADEMA walijitahidi kumlinda mwenyekiti wao wa taifa kwa kuongoza mapigano kama vita vya kawaida kabisa vya msituni. Ilimlazimu Mheshimiwa Mbowe kutoa bastola yake na kufyatua risasi kadhaa hewani ndipo Green Guards waliporudi nyuma na hivyo kuwezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara ambayo yangetokea kwa vita hiyo kuendelea uso kwa uso.

Ilikuwa patashika. Walinzi wa Mbowe walikuwa wakiwafuata Green Guards na kuwanyang'anya silaha zao na kuzitumia kuwapiga nazo. Kwa nasibu vijana kadhaa wa CCM wamekamatwa na kwa sasa wako katika kituo cha polisi cha wilaya ya Hai kwa ajili ya kuandika maelezo.

Taarifa zilizonifikia punde zinasema kuwa kijana mmoja ambaye amepigwa vizuri na CHADEMA ameomba asidhuriwe zaidi kwani atasema yote; namna walivyotumwa kuvamia na kuharibu mikutano ya Mbowe.

Waheshimiwa haya ni matunda ya mafunzo ya kijeshi ambayo CCM waliyafanya kwa vijana wao wapatao 5000 huko Iringa mwezi March mwaka huu na baadaye kule Moshi Vijijini ambako walitoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana 350.

Chonde Chonde CCM!!
Madaraka mnayataka, Sawa; Lakini Damu yetu mnaitakia nini?
TUACHIENI AMANI YETU!!!!!!!!!

hi ndo tz bwana ya ccm
 
wanataka power kwa gharama yoyote ile
watanzania wajiandae sana tarehe 31, ccm wamepanga kufanya chinja chinja kama ya somalia
 
vijana wa green guard hawana akili na Fuya ameshashindwa, walicofanya hakina maana... kani mbowe ameonyesha upuuzi mkubwa kama mwenyekiti wa chama kushindwa kumalizia mkutano na kufuata utaratibu wa sheria (ambao yeye kwa wilaya ya hai ana priviledge hiyo kubwa tu na anaijua) kumtoa kijana wake

Kama tunalaani violence, basi tuifanye kwa vitendo... kwa kwenda kufanya mambo ya tambaza nimesikitika sana

siamini mtu mwenye staha anaweza kuvunja mkutano kwenda kuokoa kwa staili ya kibohehe, mringa au tambaza

angetuma vijana

Nimesikitishwa na green guards lakini nimesikitishwa zaidi na mbowe

ukifanya ya kipumbavu na mpumbavu, watu hawatajua tofauti yenu
Umeweka post makini sana.
Ni kweli Green Guards wamefanya uhalifu lakini MBOWE naye kama alifight back basi imetia doa sana demokrasia nchini.
Sasa hapo nani atamlaumu mwenzake? Ina maana kama siasa za CCM ni kuteka nyara wapinzani wao basi tuwaachie vyombo vya dola wawanyooshe na siyo jukumu letu kuchukua sheria mkononi.
Mungu ibariki Tanzania
Kura zetu kwa CHADEMA
Slaa for president
 
Acid, sometimes tit for tat does work!. Kuna wakati wa kutumia ustaarabu kuepusha shari lakini pia kuna wakati wa kutumia shari kuzima shari, yaani you beat them on their own game.

Asante umenikumbusha ule wimbo wa Kenny Rogers, 'sometimes you have to fight to be a man' - unaitwa nini, Coward of ?
 
Acid, sometimes tit for tat does work!. Kuna wakati wa kutumia ustaarabu kuepusha shari lakini pia kuna wakati wa kutumia shari kuzima shari, yaani you beat them on their own game.
I agree, lakini angalia Mbowe, mwenyekiti wa chadema, na kibaka anayejiita grin gad!!! Rationale....??? Hakuna

Angetuma vijana mia abaki na amelfu wanamsikiliza
 
Asante umenikumbusha ule wimbo wa Kenny Rogers, 'sometimes you have to fight to be a man' - unaitwa nini, Coward of ?
pole sana... dont compare apples and oranges

namlinganisha mbowe, lipumba na kikwete... national leaders... not street bangers!!
 
Ilikuwa kama sinema za akina Rambo ama matukio ya Rwanda Genocide. Mgombe wa ubunge jimbo la Hai kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akiwa katika mkutano wa hadhara huko Masama Kati ghafla kijana mmoja wa Green Guard alivamia mkutano kwa lengo la kuanzisha fujo. Kikosi cha ulinzi cha CHADEMA kilimdhibiti kijana huyo na kumhifadhi katika gari moja kwa lengo la kupisha mkutano uendelee.
Kamende, kitendo tuu cha Kikosi cha ulinzi cha CHADEMA kilimdhibiti huyo kijana na kumhifadhi katika gari moja kwa lengo la kupisha mkutano uendelee hii abduction na illegal deteintion, hicho kikosi cha ulinzi cha Chadema kilipata wapi uwezo huo?.

Kumdhibiti mfanya fujo its a right move hatua iliyotakiwa kufuata ni kumkabidhi kwenye vyombo husika na sio kumhifadhi katika gari, suppose anything fatal ingemtokea huyo kijana, Chadema ingeweka wapi sura yake?.

Kumbukeni mnagombea kisu chenye makali kuwili huku wenzenu wameshika kwenye mpini!.
 
wanaccm kwa spin bana, eti amesikitishwa na mbowe. Mbowe angekosea sana kumuacha mmoja wa wafanyakazi wa kampeni yake kwenye mikono ya green guards. These are trained killers.
usiwe haambiliki... na naomba uchukue sekunde kusoma post zangu, au muandikie MS atakuambia... he went even offiline kupambana na mimi

Lakini hatuwezi kuwa na blind love na kushangilia hata mtu akijisaidia sebuleni eti mtemi... hayo mambo ni ya kitoto

Mbowe made a huge mistake, he is carrying Dr Slaa kama partner kwenye siasa... unadhani image gani inakuja??

tuwe wakweli, anapokosea mtu aambiwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom