Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Ilikuwa kama sinema za akina Rambo ama matukio ya Rwanda Genocide. Mgombe wa ubunge jimbo la Hai kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akiwa katika mkutano wa hadhara huko Masama Kati ghafla kijana mmoja wa Green Guard alivamia mkutano kwa lengo la kuanzisha fujo. Kikosi cha ulinzi cha CHADEMA kilimdhibiti kijana huyo na kumhifadhi katika gari moja kwa lengo la kupisha mkutano uendelee.
Kumbe kijana huyo alikuwa ametangulizwa tu na kwamba pamoja naye walikuwepo vijana wa Green Guards wasiopungua 100. Vijana hawa wakiongozwa na Mgombea udiwani wa CCM katika kata hiyo walikwenda kufunga barabara ili msafara wa Freeman usipite eneo hilo. Kwa kawaida msafara wa Mbowe hutanguliwa na pick-up ambayo hubeba jukwaa na viti. Vijana hawa wa CCM waliliteka gari hilo lililokuwa linaendesha na Ndg. Lootore Lema na kumchukua kumpeleka katika nyumba ya mwanaCCM mmoja katika eneo hilo la Masama Mbweera.
Mbowe kusikia kuwa kamanda wake ametekwa alivunja mkutano na kuondoka kwenda kumwokoa. Walipofika kama 200m toka eneo la mkutano walikuta jeshi kubwa la vijana wa CCM wakiwa wameshikilia mapanga, mawe, majembe na vyuma. Hapo vita kamili ikaanza.
Katika vita hiyo magari ya msafara wa Mbowe yapatayo 6 yamevunjwa vunjwa vioo. Wanachama wa CHADEMA wameumizwa. Hata hivyo vijana wa CHADEMA walijitahidi kumlinda mwenyekiti wao wa taifa kwa kuongoza mapigano kama vita vya kawaida kabisa vya msituni. Ilimlazimu Mheshimiwa Mbowe kutoa bastola yake na kufyatua risasi kadhaa hewani ndipo Green Guards waliporudi nyuma na hivyo kuwezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara ambayo yangetokea kwa vita hiyo kuendelea uso kwa uso.
Ilikuwa patashika. Walinzi wa Mbowe walikuwa wakiwafuata Green Guards na kuwanyang'anya silaha zao na kuzitumia kuwapiga nazo. Kwa nasibu vijana kadhaa wa CCM wamekamatwa na kwa sasa wako katika kituo cha polisi cha wilaya ya Hai kwa ajili ya kuandika maelezo.
Taarifa zilizonifikia punde zinasema kuwa kijana mmoja ambaye amepigwa vizuri na CHADEMA ameomba asidhuriwe zaidi kwani atasema yote; namna walivyotumwa kuvamia na kuharibu mikutano ya Mbowe.
Waheshimiwa haya ni matunda ya mafunzo ya kijeshi ambayo CCM waliyafanya kwa vijana wao wapatao 5000 huko Iringa mwezi March mwaka huu na baadaye kule Moshi Vijijini ambako walitoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana 350.
Chonde Chonde CCM!!
Madaraka mnayataka, Sawa; Lakini Damu yetu mnaitakia nini?
TUACHIENI AMANI YETU!!!!!!!!!
Kumbe kijana huyo alikuwa ametangulizwa tu na kwamba pamoja naye walikuwepo vijana wa Green Guards wasiopungua 100. Vijana hawa wakiongozwa na Mgombea udiwani wa CCM katika kata hiyo walikwenda kufunga barabara ili msafara wa Freeman usipite eneo hilo. Kwa kawaida msafara wa Mbowe hutanguliwa na pick-up ambayo hubeba jukwaa na viti. Vijana hawa wa CCM waliliteka gari hilo lililokuwa linaendesha na Ndg. Lootore Lema na kumchukua kumpeleka katika nyumba ya mwanaCCM mmoja katika eneo hilo la Masama Mbweera.
Mbowe kusikia kuwa kamanda wake ametekwa alivunja mkutano na kuondoka kwenda kumwokoa. Walipofika kama 200m toka eneo la mkutano walikuta jeshi kubwa la vijana wa CCM wakiwa wameshikilia mapanga, mawe, majembe na vyuma. Hapo vita kamili ikaanza.
Katika vita hiyo magari ya msafara wa Mbowe yapatayo 6 yamevunjwa vunjwa vioo. Wanachama wa CHADEMA wameumizwa. Hata hivyo vijana wa CHADEMA walijitahidi kumlinda mwenyekiti wao wa taifa kwa kuongoza mapigano kama vita vya kawaida kabisa vya msituni. Ilimlazimu Mheshimiwa Mbowe kutoa bastola yake na kufyatua risasi kadhaa hewani ndipo Green Guards waliporudi nyuma na hivyo kuwezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara ambayo yangetokea kwa vita hiyo kuendelea uso kwa uso.
Ilikuwa patashika. Walinzi wa Mbowe walikuwa wakiwafuata Green Guards na kuwanyang'anya silaha zao na kuzitumia kuwapiga nazo. Kwa nasibu vijana kadhaa wa CCM wamekamatwa na kwa sasa wako katika kituo cha polisi cha wilaya ya Hai kwa ajili ya kuandika maelezo.
Taarifa zilizonifikia punde zinasema kuwa kijana mmoja ambaye amepigwa vizuri na CHADEMA ameomba asidhuriwe zaidi kwani atasema yote; namna walivyotumwa kuvamia na kuharibu mikutano ya Mbowe.
Waheshimiwa haya ni matunda ya mafunzo ya kijeshi ambayo CCM waliyafanya kwa vijana wao wapatao 5000 huko Iringa mwezi March mwaka huu na baadaye kule Moshi Vijijini ambako walitoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana 350.
Chonde Chonde CCM!!
Madaraka mnayataka, Sawa; Lakini Damu yetu mnaitakia nini?
TUACHIENI AMANI YETU!!!!!!!!!