Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Hii Habari ya Lema kila mtu anajifanya ni analyst na mwandishi mzuri,
lakini aingii akilini kulinganisha ya Lusinde na ya Lema, na kama kuna mwandishi mzuri ama analyst anaelinganisha vitu basi angeweka hapa ni kipi alichokisema Lema (ambacho ni tusi) ukilinganisha na cha Lusinde
Lakini cha muhimu pia tujiulize na kuanalyze hicho alichokisema Lema (ambacho ni tusi) ndilo lililomvua Ubunge?
WanaJF,
Nimerudia kusikiliza rekodi ya hotuba ya Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera (CCM) wakati akimwaga MATUSI katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki, mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Ngarasero. Nimeandika zaidi ya sentensi 15, ambazo ni matusi au zina viashiria vya lugha ya matusi.
Karibuni, Katibu Mkuu wa CCM, Mh. Mkama amesikika akitetea kwamba Lusinde alikuwa anajibu hoja za wapinzani wake, CDM.
Aidha jana, tarehe 5/4/12, ubunge wa Mh. Godbless Lema (Arusha Mjini, CDM), umetenguliwa kwa kile kinasemwa kufanya kampeni bila kuzingatia maadili ya kampeni, ikiwepo matumizi ya lugha inayotafasiriwa kwamba ni matusi. Jambo zuri tu, kama kweli tunataka kulenga kampeni za kistaarabu!
Katika dk 16:06 zilizorekodi hotuba ya Lusinde kama ilivyo katika mtandao, nimetambua mambo haya kama matusi au lugha ya matusi, wastani wa karibu sentinsi/tusi moja katika kila dk moja aliyotumia kuongea Lusinde:-
- Kuda-dada-deki (amerudia karibu mara sita).
- Wewe umekuwa ukiwachanja chale mpaka matakoni (akimlaumu Prof. Majimarefu).
- Hata wao ni mashoga basi, (akihusisha kutoga masikio na suala la ushoga).
- Nani hafahamu kwamba mbunge wa Arusha mjini aliolewa kule mahabusu/amepata bwana, (akihusisha Lema kuwa mahabusu na kwamba aliolewa), (ikiwa ni sodomization kwa tafsiri yangu).
- Dk. Slaa alitimuliwa uPadri baada ya kuwatia mimba wanakwaya. (akimtukana Dk. Slaa moja kwa moja)
- ***** huyu - Vicent Nyerere, ana akili mbovu. (akimtukana Mh. Vicenti Nyerere)
- Ameliwa -------- siye hatusemi. (ikimaanisha kuwa sodomized, iwapo sikujua anamtukana Vicent Nyerere au Godbless Lema).
- Acheni ushamba nyie. (akiwatukana wananchi, ambao wanaonyesha kuwa wafuasi wa CDM)
- Washamba wakubwa nyie x 2. (akiwatukana wananchi)
- Washamba wakubwa ----, Dk. Slaa mshamba mkubwa, akivaa kombati, anakuwa kama kajinyea. (akimtukana Dk. Slaa)
- Viongozi wa CDM vichaa wa kulogwa. (akiwatukana viongozi wa CDM)
- Dk. Slaa anatishia kujamba wakati anaharisha. (akimtukana Dk. Slaa)
- Sera ya CDM ni sera ya jogoo, jogoo linamuahidi kuku gauni, huku lenyewe hata chupi halina. (akikitukana chama kwa ujumla wake).
- Mbowe anasema ana uchungu, kwani ana mimba? (akimtukana Mbowe)
- Mbowe pigwa mimba! Slaa pigwa mimba! Nasari pigwa mimba! (akiwatukana Mbowe, Slaa na Nasari).
Sasa, nimeambiwa kupitia vyombo vya habari kwamba watu 3 ndiyo waliomfungulia mashtaka Mh. Godbless Lema, kufanya illegal practices katika kampeni wala siyo aliyeshindana naye katika ubunge Batilda Burian, vema. NANI WATAMFUNGULIA MASHTAKA LUSINDE KWA KUFANYA ILLEGAL PRACTICES katika kampeni za Arumeru Mashariki kama kweli tunatendeana haki?
Sentensi na maneno ya viashiria vya matusi niliyotaja mnaweza kuyafanyia uchambuzi zaidi, na kurudia kuisikiliza hotuba ile ili kujenga hoja vizuri. Najua kuna mdau alikwisha uliza hoja kama hii humu mtandaoni, lakini sijui hatua gani zimeendelea kuchukuliwa.
Nasisitiza wanasiasa kujenga hoja za msingi wakati wa kampeni. Ushahidi unajionyesha wengi wamekuwa wanajikita zaidi katika kumshambulia mgombea kuliko kushambulia-kwa uchambuzi na mikakati mambo ambayo ni matatizo na changamoto katika maendeleo ya wananchi. Lusinde alitumia zaidi ya dk 15, kushambulia watu, sio kushambulia kwa uchambuzi na mikakati matatizo ya wanaArumeru Mashariki.
Kwa mzaha kabisa, Katibu Mkuu wake anaunga mkono kwamba huko ilikuwa kujibu hoja za wapinzani wake. Hapa unajua unashindwa kutafsiri hekima na busara ya kiongozi mkuu wa chama, katika kukiwezesha chama chake kupaa na kuaminiwa. Sijui bwana, SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA!
Perecy Ugula
MwanaJF Mchanga,
Email: ugulapp@yahoo.co.uk
Simu: +255 766 082388
Matusi ya lusinde kila mtu ameona.unaweza kutudhibitishia kuwa Lema ametukana?walalamikaji walidai hivyo lakini mimi sijaona uthibitisho wowote walioitoa kuithibitishia mahakama kuwa Lema alitukana?
Msitake kuishi kinafki kama kweli ni mfatilia siasa unajua kabisa mdee, lema, na sugu hawana kauli nzusisisi kwenye hili jukwaa tusingependa habari ndefu na hotuba ndefu! tunaomba utupe ushahidi wa matusi ya lema,sugu na mdee! usiweke habari ndefu isiyo na vielelezo! tunakushuru kwa kuandika ujumbe mzuri ila tusaidie ushaidi uliyo nao!. Amani kwako
Kamanda naona umeweka nyama za kutosha kwenye makala yako.Unaweza toa angalau clip moja ya ushahidi wa matusi ya Lema na Mdee kama ilivyofanyika kwa Lusinde?. Umenifunua kumbe Mdee na Lema nao ni watukanaji ! !Kuna tatizo kuu la msingi ambalo nisiposema dhamiri yangu itanihukumu na sitakaa kimya kwa sababu wengine wameamua kukaa kimya.
Jamii ya Tanzania iko kwenye ugonjwa mkubwa na tusipoudhibiti huu ugonjwa hakuna wa kutusaidia. Tunaiumiza jamii, tunaharibiu vizazi vijavyo kwa kisingizio cha mabadiliko!
Sera ya chadema si matusi!! Sera ya chadema ni mabadiliko, sijawahi kuona Slaa akitoa matusi ya nguoni, sijawahi kuona Mbowe akitoa matusi ya nguoni, wala sijawahi kuona Zito akitukana, these people they are still high in their positions na popular kwenye siasa na wanaaminika kwenye jamii kwa kuleta mabadiliko
Ila nimemsikia Mdee akitukana( personally nilimkataza) , nilimsikia Lema akitukana, tumeona Sugu akitukana mpaka kujirekodi!! Hawa ndio wabunge wetu, ndio tuliowapa dhamana ya kuongoza taifa letu kwa nafasi zao…ila wanatukana, wakitukana hawa ni sawa??
Nani kasema?
Kuna uwezekano mkubwa akina Mbowe, slaa hawawezi kuwadhibiti akina Lema, kwa sababu ya kuwaonea aibu!! Unapopagawa na siasa na kuona kila unachotukana kinashangiliwa, basi jamii nzima inakuwa imeoza! Msikilize Lusinde utaamini!
ILA; Ukiwa mpinzani lazima uangalie zile nafasi/chances/ opportunities ambazo adui yako anaweza kuzitumia kukuangamiza!
Kama CCM wametumia mahakama kumuondoa adui yao Lema, it is okay na wametumia karata yao vizuri sana.
Lakini kama si CCM na mahakama, je matusi yanakubaliwa katika jamii yetu??
Hivi Mdee, sugu, Lema na Lusinde tofauti yao ni nini??
Na sisi wataka mabadiliko , ukweli wa mioyo yetu na matusi uko wapi? Kuwa tutukane tu kwa sababu kwa kufanya hivyo ndio tunahimiza moto wa mabadiliko??
Matusi mangapi yanatukanwa humu ndani? Wanaotukana ni akina nani? Je wakipewa uongozi hawatatukana kwa sababu ni viongozi? Yaani uongozi una mechanism ya kuzuia matusi biologically? Matusi tumeyakubali, tunaishi nayo, tunalala nayo kila kona ya nchi yetu si kwa hao niliowataja, yako kila kona, kwenye madaladala, kwenye michezo name it!
Lema ameadhibiwa na mahakama, Lusinde ameadhibiwa na wananchi-ambao wengi wao wanatukana, mwisho wa siku wote ni watukanaji! Ikifika hatua tukaona Lema ni shujaa tunakuwa tumevua akili zetu na utu wetu na kuuweka kando na sisi……..tunaishi kinafiki , tuna post kinafiki kwani usafi na intergirty is not part of our life!!
In this case mahama iko clean..tena wanapongezana, hivi..juzi tu tumelia Lusinde anatukana-tukasema kila kona na kulaani, leo hii Lema anavuliwa ubunge kwa kutukana tunaona ubaya?? Kweli??
perecy,wewe ni zaidi ya great thinker!
Waberoya yu sahihi kimantiki,kwa maana
hakuna justification ya mtu yeyote kutukana!
Lakini,WANAO DAI LEMA katukana,wameshndwa kutoa ushahd timilifu usio na shaka kama ulivyo fanya!
U are Unique!
Waberoya umeongea vizuri sana.
Mdee, Sugu, Lema nao ni watukanaji na wenye kutumia lugha mbovu mbovu kwa wapinzani wao.
Na kwa sisi kuwashangilia na hata kuwatukuza wakati mwengine kunaonyesha tu sisi Watanzania ni watu wa aina gani. Hatuna integrity.
Mtu kama Mdee kumwita Wassira Sokwe-mtu ni aibu........kwa misingi yote iliyopo ya kibinaadamu