Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Mara nyingi sana huwa nawaza sana kuwa CHADEMA huwa inaokota wapi viongozi wake aina ya Godbless Lema ambao bado hawajakomaa na kupevuka kiakili katika masuala ya siasa na kuwapatia uongozi wa juu kama vile kuwa wajumbe wa kamati kuu? Mara nyingi nimesema na kuandika sana kuwa viongozi kama Lema ni watu wanaofanya mambo kihuni sana na kukosa sifa za uongozi.
Leo Lema anasema eti anataka kuwashawishi viongozi wake wakuu waache kusalimiana na Mheshimiwa Makonda na kwamba wawe wanamnunia. Hivi ndugu zangu Watanzania mnaona kweli ni akili hii au matope? Hamuoni Lema kuwa mgonjwa? Hamuoni kuwa bado ana akili ya kitoto? Hamuoni kuwa hajakomaa na kupevuka kiakili? Hamuoni kuwa bado ana ule utoto na uhuni wa kijiweni na uchochoroni? Hamuoni kuwa hastahili kuwa kiongozi ndani ya chama achilia mbali kuwa muwakilishi wa wananchi?
Tangia lini katika siasa ukajenga uhasama wa kijinga jinga usio na mashiko wa aina hiyo? Mara ngapi Lema na CHADEMA yake walimtukana matusi ya kumdhalilisha mzee Lowassa tangia mwaka 2008? Je 2015 hakuwa mgombea wao? Hakuwapa wabunge wengi na Ruzuku juu? Mara ngapi Lema na CHADEMA wamekuwa wakiwatukana viongozi wa serikali na CCM matusi pasipo sababu za msingi?
Tangia lini Lema amekuwa mtakatifu na mteule wa Mungu? Hivi Lema anajitambua kweli? Hafahamu kuwa katika siasa hakuna uadui wa kudumu wala rafiki wa kudumu na ndio maana Lowassa waliomdhalilisha kwa miaka mingi alikuja akaungana nao kama mgombea wao wa kiti cha Urais? Kwanini Lema hakui na kukomaa kiakili?
Lema hafai kuwa kiongozi wa aina yoyote ile katika ngazi ya aina yoyote ile, ni kwa bahati mbaya tu kwa kuwa ndani ya CHADEMA hakuna watu wenye uwezo wa uongozi ndio maana Lema pamoja na uhuni wake anapewa nafasi ya uongozi na kuonekana anafaa, lakini kama angekuwa ndani ya CCM Hawezi kupewa nafasi ya uongozi wa aina yoyote ile katika ngazi ya aina yoyote ile.
Hapa ndipo napoona kweli ni sahihi kwa Mheshimiwa Mbowe kuendelea kusalia katika nafasi yake ya uenyekiti kwa miaka yote, kwa kuwa watu waliopo ndani ya chama chake bado ni wachanga sana kiakili na hawawezi kukiongoza chama hata kwa mwezi mmoja tu kabla hawajakipasua na kukisambaratisha kama barafu.
Maana ni watu wa mihemuko, kukurupuka, kuropoka, kukosa hekima, busara, utulivu, subira, uvumilivu na unyenyekevu. Ni watu wasio na midomo na vifua vya kiuongozi. Mbowe pekee ndiye kiongozi ndani ya CHADEMA lakini hao wengine ni wahuni wahuni tu.
Lema na CHADEMA yake inaonyesha wakipewa madaraka ya kuongoza nchi wanaweza poteza watu wengi sana wale wote wanaowakosoa ama kuwapinga ama kutofautiana nao mitizamo au kuwa na mitizamo tofauti. Maana hii inaonyesha ni watu wanaojiona ni wakamilifu, malaika, watakatifu na miungu watu wanaostahili kuabudiwa na kusifiwa. Ndio maana chama hakikui wala kusonga mbele zaidi ya kurudi nyuma kila siku, kwa kuwa wameatamia mawazo ya kijima na kutaka kuendesha chama kidikteta kwa kutokutaka kukosolewa zaidi ya kusifiwa kwa kila kitu. Ndio maana ukiwa na mawazo tofauti ndani ya CHADEMA lazima ufurushwe kama mhamiaji haramu kwa kuonekana ni adui na kirusi ndani ya chama.
Mara nyingi sana huwa nawaza sana kuwa CHADEMA huwa inaokota wapi viongozi wake aina ya Godbless Lema ambao bado hawajakomaa na kupevuka kiakili katika masuala ya siasa na kuwapatia uongozi wa juu kama vile kuwa wajumbe wa kamati kuu? Mara nyingi nimesema na kuandika sana kuwa viongozi kama Lema ni watu wanaofanya mambo kihuni sana na kukosa sifa za uongozi.
Leo Lema anasema eti anataka kuwashawishi viongozi wake wakuu waache kusalimiana na Mheshimiwa Makonda na kwamba wawe wanamnunia. Hivi ndugu zangu Watanzania mnaona kweli ni akili hii au matope? Hamuoni Lema kuwa mgonjwa? Hamuoni kuwa bado ana akili ya kitoto? Hamuoni kuwa hajakomaa na kupevuka kiakili? Hamuoni kuwa bado ana ule utoto na uhuni wa kijiweni na uchochoroni? Hamuoni kuwa hastahili kuwa kiongozi ndani ya chama achilia mbali kuwa muwakilishi wa wananchi?
Tangia lini katika siasa ukajenga uhasama wa kijinga jinga usio na mashiko wa aina hiyo? Mara ngapi Lema na CHADEMA yake walimtukana matusi ya kumdhalilisha mzee Lowassa tangia mwaka 2008? Je 2015 hakuwa mgombea wao? Hakuwapa wabunge wengi na Ruzuku juu? Mara ngapi Lema na CHADEMA wamekuwa wakiwatukana viongozi wa serikali na CCM matusi pasipo sababu za msingi?
Tangia lini Lema amekuwa mtakatifu na mteule wa Mungu? Hivi Lema anajitambua kweli? Hafahamu kuwa katika siasa hakuna uadui wa kudumu wala rafiki wa kudumu na ndio maana Lowassa waliomdhalilisha kwa miaka mingi alikuja akaungana nao kama mgombea wao wa kiti cha Urais? Kwanini Lema hakui na kukomaa kiakili?
Lema hafai kuwa kiongozi wa aina yoyote ile katika ngazi ya aina yoyote ile, ni kwa bahati mbaya tu kwa kuwa ndani ya CHADEMA hakuna watu wenye uwezo wa uongozi ndio maana Lema pamoja na uhuni wake anapewa nafasi ya uongozi na kuonekana anafaa, lakini kama angekuwa ndani ya CCM Hawezi kupewa nafasi ya uongozi wa aina yoyote ile katika ngazi ya aina yoyote ile.
Hapa ndipo napoona kweli ni sahihi kwa Mheshimiwa Mbowe kuendelea kusalia katika nafasi yake ya uenyekiti kwa miaka yote, kwa kuwa watu waliopo ndani ya chama chake bado ni wachanga sana kiakili na hawawezi kukiongoza chama hata kwa mwezi mmoja tu kabla hawajakipasua na kukisambaratisha kama barafu.
Maana ni watu wa mihemuko, kukurupuka, kuropoka, kukosa hekima, busara, utulivu, subira, uvumilivu na unyenyekevu. Ni watu wasio na midomo na vifua vya kiuongozi. Mbowe pekee ndiye kiongozi ndani ya CHADEMA lakini hao wengine ni wahuni wahuni tu.
Lema na CHADEMA yake inaonyesha wakipewa madaraka ya kuongoza nchi wanaweza poteza watu wengi sana wale wote wanaowakosoa ama kuwapinga ama kutofautiana nao mitizamo au kuwa na mitizamo tofauti. Maana hii inaonyesha ni watu wanaojiona ni wakamilifu, malaika, watakatifu na miungu watu wanaostahili kuabudiwa na kusifiwa. Ndio maana chama hakikui wala kusonga mbele zaidi ya kurudi nyuma kila siku, kwa kuwa wameatamia mawazo ya kijima na kutaka kuendesha chama kidikteta kwa kutokutaka kukosolewa zaidi ya kusifiwa kwa kila kitu. Ndio maana ukiwa na mawazo tofauti ndani ya CHADEMA lazima ufurushwe kama mhamiaji haramu kwa kuonekana ni adui na kirusi ndani ya chama.