Tehe tehe teheeeeeeeeeeee mambo ni matamu, naona ndg zangu mna nena kwa lugha sasa. Sauti ya umma imeamua; tafadhali muwasiliane na ndg huko Bariadi Magharibi na Mashariki, inasemekana kuna mvutano usio wa kawaida; na wa ccm hawaafiki maamuzi wa umma.
Kwa taarifa nyepesi toka mwanza nyamagana- masha wa ccm yuko hoi bin taabani mbele ya mgombea wa chadema kwa mbali sana. Karibu sehemu zote za udiwani chadema washachukuwa ushindi tayari. Pia ilemela dialo yuko kwenye intesive care unit, chadema inaongoza kwa juu sana. Hivyo mwanza wamempeleka slaa ikulu.
Wilson Kabwe (msimamizi wa uchaguzi) tokea awali alishajionyesha ameegemea upande gani. Ila hili la kuzuia kutangazwa matokeo litamtokea puani. Asishindane na nguvu ya umma, jiji zima imeshafahamika Masha kaachwa mbali na ndio maana watu wanasherehekeaRichard Leo, anawasilisha masuala ya Mwanza, maelezo yake anadai wasimamizi wa jimbo la Nyamagana wametoa maelekezo kwa wasimamizi wasitoe matokeo ili isije ikaharibu hali ya usalama. Wadau, sijaelewa. Mwenye data tafadhali tumwagieni hapa.