Azoge Ze Blind Baga
JF-Expert Member
- Mar 8, 2019
- 366
- 1,376
Nchi hii ya Tanzania baada ya uchaguzi wa mwaka 2020 chini ya mwendazake majimbo yote yalikua chini ya CCM likiwemo hili la Nyamagana chini ya uongozi wa Stanslaus Mabula.
Huyu mbunge sijui kama yupo hapa Mwanza. Barabara nyingi za jimbo lake hasa maeneo ya pembeni ambayo kimsingi ndio yana watu wengi na wapiga kura wengi ni mbovu vibaya mno.
Barabara ya kutoka IGOMA kwenda KISHIRI inatia kichefuchefu kwa kweli.
Barabara ni mbovu, mashimo mwanzo mwisho. Utembee kwa daladala kero, bajaji kero, private car kero na kuna mbunge analipwa zaidi ya milioni 12 kwa mwezi na kuna mfuko wa jimbo.
Kishiri wamesahaulika na huyu Mabula na CCM yake. Na jinsi viongozi wa CCM walivyo wanafiki watajifanya wanachonga barabara na kuwajali wananchi miaka hii ya uchaguzi 2024/2025.
Mbunge na CCM yako mjitafakari barabara ya Kishiri mbovu mno ichongwe na kumwaga hata kifusi huku wanaishi wapiga kura wenu wengi tu na sisi wafanya biashara tunaitumia hii barabara ila imekua kero kwetu.
Mwananchi hapa wa Ilemela- Buswelu kwa Angelina Mabula.
Huyu mbunge sijui kama yupo hapa Mwanza. Barabara nyingi za jimbo lake hasa maeneo ya pembeni ambayo kimsingi ndio yana watu wengi na wapiga kura wengi ni mbovu vibaya mno.
Barabara ya kutoka IGOMA kwenda KISHIRI inatia kichefuchefu kwa kweli.
Barabara ni mbovu, mashimo mwanzo mwisho. Utembee kwa daladala kero, bajaji kero, private car kero na kuna mbunge analipwa zaidi ya milioni 12 kwa mwezi na kuna mfuko wa jimbo.
Kishiri wamesahaulika na huyu Mabula na CCM yake. Na jinsi viongozi wa CCM walivyo wanafiki watajifanya wanachonga barabara na kuwajali wananchi miaka hii ya uchaguzi 2024/2025.
Mbunge na CCM yako mjitafakari barabara ya Kishiri mbovu mno ichongwe na kumwaga hata kifusi huku wanaishi wapiga kura wenu wengi tu na sisi wafanya biashara tunaitumia hii barabara ila imekua kero kwetu.
Mwananchi hapa wa Ilemela- Buswelu kwa Angelina Mabula.