Nimetembelea tovuti ya Wizara ya Fedha nikakutana na mgawanyo wa fedha za Majimbo yote. Fedha hizi zinafanya kazi gani majimboni?
Inawezekana kabisa fedha nyingi hapa nchini zinaishia kwenye siasa hizi.
Kwa hali hii kila mtu anaweza kuwa mbunge kwa sababu fedha za kutekeleza ahadi zako tayari zinakuwepo.
------ Tutor B anajibu----
YAFAHAMU MALENGO YA MFUKO WA JIMBO.
Mfuko wa jimbo ni mfuko ulianzishwa kisheria na ulipitishwa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na lengo kuu la kupitishwa kwa mfuko huo ni kuchochea na kuongeza kasi katika miradi mbali mbali iliyoanzishwa na wananchi katika majimbo yao (The Constituencies Development Catalyst Fund Act. Na. 16 ya mwaka 2009)
Kama ilivyoahinishwa hapo juu lengo la kuanzishwa kwa mfuko huu ni kuchochea maendeleo katika majimbo ya uchaguzi. Ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo ufanyika kwa juhudi za wananchi wakishirikiana na mbunge wao, pamoja na serikali kuu kama mchochezi mkuu anayetoa pesa husika.
Serikali kupitia bunge tukufu ilifanya hivi hili kurahisisha maendeleo kwa kasi katika majimbo husika; ikiamini kuwa kwa kuwa mbunge yupo karibu na wapiga kura wake itamuwia rahisi kutekeleza maendeleo hayo japo, maskini serikali haikujua kuwa asilimia kubwa ya wabunge wetu wanaishi mbali na sisi na huwa tunaonana nao kipindi cha kuomba tena ridhaa yetu.
Kama wengi wasemavyo kuwa "ukitaka kupima utu wa mtu mwangalie katika mambo mawili PESA na CHAKULA" mara nyingi pesa hizi zimekuwa hazifahamiki matumizi yake hasa baada ya serikali kuzitoa. Kunakuwa hakuna ufuatilia wa kina juu ya matumizi yake; jambo ambalo limekuwa faida kwa wabunge.
Utaratibu unasema kuwa pesa hizi za mfuko wa maendeleo ya jimbo (CDF) hupewa kwa kila mbunge wa jimbo na huwabagua wabunge wa viti maalumu na wale wabunge wa kuteuliwa na Rais.
Mfuko huu hudhibitiwa na kamati maalumu ya watu sita (6) kama sikosei ambao wote huteuliwa na mbunge husika ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa mfuko huo. Kamati hii hukoma pale mbunge husika anapokoma kuwa mbunge kwa kushindwa ubunge, kung'olewa na mahakama au kifo.
Mbunge na kamati yake ndiyo wenye kauli ya mwisho juu ya matumizi ya pesa za mfuko huu na si lazima matumizi hayo yaende sambamba au yawiane na vipaumbele vya halmashauri ya mji,wilaya au manispaa.
Wabunge wa viti maalumu wanataka pia kupewa pesa za CDF kwa madai kwamba wana majukumu sawa au hata kupita yale ya wabunge wa majimbo. Kabla ya kufikiria kuwajumuisha wabunge wa viti maalumu na wale wa kuteuliwa na Rais katika kupata fedha za mfuko wa jimbo ni vema ukaguzi na upembuzi ufanyike kwanza ili kubaini manufaa ambayo yameletwa na mfuko huu kama yapo.
Ushirikishwaji wa wananchi katika hili umekuwa haufahamiki, ajabu ukijaribu kuwahoji hata baadhi ya madiwani katika halmashauri zetu mbalimbali hawajui huwepo wa pesa hizi na kama wanajua hawafuatilii matumizi ya pesa hizi.
Miradi mingi ya wananchi inakwama kwasababu ya kukosa kichocheo muhimu kama hichi ambacho serikali iliona umuhimu wake ila ikasahau kufuatilia utekelezaji wake.
Suhala la shule kutokuwa na huduma bora zinazopaswa hupelekea wanafunzi wengi wa sekondari kukata tamaa na kuacha shule kabisa ama kupata matokeo mabaya mwishoni. Lakini ukiwasikiliza watu hawa wana moyo na hali yakujitoa ila support ya viongozi husika inakuwa ndogo! Mfuko wa jimbo na ubunifu wa viongozi wetu ukitumika tunaweza kutatua tatizo hili maana naamini inawezekana sana.
Wabunge wengi wa majimbo ukitaka kugombana nao wahulize kuhusu pesa za mfuko wa jimbo. Kijana mmoja aliwahi kumhoji mbunge wake lakini alichojibiwa hakikuwa kizuri kwa ustawi wa uwajibikaji kwa wananchi waliomchagua.
Mara nyingi wabunge wetu wakitumia pesa za jimbo katika shughuli ndogo za kijamii ujinasibu kuwa hizo ni pesa zao wenyewe toka mfukoni mwao, wanatumia mihanya hiyo ya wananchi kutojua ukweli wa jambo hili.
Hivyo uzitumia pesa husika kujihimarisha kisiasa, ndiyo maana wanaharakati wengi wamekuwa wakiishauri serikali kufuta sheria hiyo na kuondosha hii mifuko ya jimbo kwani imeonekana ilianzishwa kwa lengo zuri ila usimamizi na utekelezaji wake hauleti hali chanya kwa walengwa.
Ukiangalia kwa mfano Mgawanyo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo 2010/2011 majimbo kama kielelezo kwenye picha kinavyoonesha yalipata pesa nyingi tu lakini nani anaweza kujua zilitumikaje katika majimbo yetu?
WITO WANGU KWA WANANCHI, baada ya kutambua matumizi na malengo ya pesa za jimbo tuanzishe miradi mbalimbali na tuwashirikishe wabunge wetu na wakigoma kutusupport tuwahoji hizi pesa zilitumika kwa matumizi gani?
Yamkini viongozi wetu (wabunge) wamejisahau sasa tuwakumbushe kwa kuanzisha miradi mbalimbali na kutaka mchango wao toka mfuko wa jimbo.
ANDIKO HILI LINALENGA KUEMILIKISHA JAMII JUU YA SHERIA YA MFUKO WA JIMBO NA MALENGO YAKE.
-----
Pia soma
>Mfuko wa Jimbo kupingwa mahakamani - JamiiForums
>Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo: CDCF - JamiiForums
Inawezekana kabisa fedha nyingi hapa nchini zinaishia kwenye siasa hizi.
Kwa hali hii kila mtu anaweza kuwa mbunge kwa sababu fedha za kutekeleza ahadi zako tayari zinakuwepo.
------ Tutor B anajibu----
YAFAHAMU MALENGO YA MFUKO WA JIMBO.
Mfuko wa jimbo ni mfuko ulianzishwa kisheria na ulipitishwa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na lengo kuu la kupitishwa kwa mfuko huo ni kuchochea na kuongeza kasi katika miradi mbali mbali iliyoanzishwa na wananchi katika majimbo yao (The Constituencies Development Catalyst Fund Act. Na. 16 ya mwaka 2009)
Kama ilivyoahinishwa hapo juu lengo la kuanzishwa kwa mfuko huu ni kuchochea maendeleo katika majimbo ya uchaguzi. Ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo ufanyika kwa juhudi za wananchi wakishirikiana na mbunge wao, pamoja na serikali kuu kama mchochezi mkuu anayetoa pesa husika.
Serikali kupitia bunge tukufu ilifanya hivi hili kurahisisha maendeleo kwa kasi katika majimbo husika; ikiamini kuwa kwa kuwa mbunge yupo karibu na wapiga kura wake itamuwia rahisi kutekeleza maendeleo hayo japo, maskini serikali haikujua kuwa asilimia kubwa ya wabunge wetu wanaishi mbali na sisi na huwa tunaonana nao kipindi cha kuomba tena ridhaa yetu.
Kama wengi wasemavyo kuwa "ukitaka kupima utu wa mtu mwangalie katika mambo mawili PESA na CHAKULA" mara nyingi pesa hizi zimekuwa hazifahamiki matumizi yake hasa baada ya serikali kuzitoa. Kunakuwa hakuna ufuatilia wa kina juu ya matumizi yake; jambo ambalo limekuwa faida kwa wabunge.
Utaratibu unasema kuwa pesa hizi za mfuko wa maendeleo ya jimbo (CDF) hupewa kwa kila mbunge wa jimbo na huwabagua wabunge wa viti maalumu na wale wabunge wa kuteuliwa na Rais.
Mfuko huu hudhibitiwa na kamati maalumu ya watu sita (6) kama sikosei ambao wote huteuliwa na mbunge husika ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa mfuko huo. Kamati hii hukoma pale mbunge husika anapokoma kuwa mbunge kwa kushindwa ubunge, kung'olewa na mahakama au kifo.
Mbunge na kamati yake ndiyo wenye kauli ya mwisho juu ya matumizi ya pesa za mfuko huu na si lazima matumizi hayo yaende sambamba au yawiane na vipaumbele vya halmashauri ya mji,wilaya au manispaa.
Wabunge wa viti maalumu wanataka pia kupewa pesa za CDF kwa madai kwamba wana majukumu sawa au hata kupita yale ya wabunge wa majimbo. Kabla ya kufikiria kuwajumuisha wabunge wa viti maalumu na wale wa kuteuliwa na Rais katika kupata fedha za mfuko wa jimbo ni vema ukaguzi na upembuzi ufanyike kwanza ili kubaini manufaa ambayo yameletwa na mfuko huu kama yapo.
Ushirikishwaji wa wananchi katika hili umekuwa haufahamiki, ajabu ukijaribu kuwahoji hata baadhi ya madiwani katika halmashauri zetu mbalimbali hawajui huwepo wa pesa hizi na kama wanajua hawafuatilii matumizi ya pesa hizi.
Miradi mingi ya wananchi inakwama kwasababu ya kukosa kichocheo muhimu kama hichi ambacho serikali iliona umuhimu wake ila ikasahau kufuatilia utekelezaji wake.
Suhala la shule kutokuwa na huduma bora zinazopaswa hupelekea wanafunzi wengi wa sekondari kukata tamaa na kuacha shule kabisa ama kupata matokeo mabaya mwishoni. Lakini ukiwasikiliza watu hawa wana moyo na hali yakujitoa ila support ya viongozi husika inakuwa ndogo! Mfuko wa jimbo na ubunifu wa viongozi wetu ukitumika tunaweza kutatua tatizo hili maana naamini inawezekana sana.
Wabunge wengi wa majimbo ukitaka kugombana nao wahulize kuhusu pesa za mfuko wa jimbo. Kijana mmoja aliwahi kumhoji mbunge wake lakini alichojibiwa hakikuwa kizuri kwa ustawi wa uwajibikaji kwa wananchi waliomchagua.
Mara nyingi wabunge wetu wakitumia pesa za jimbo katika shughuli ndogo za kijamii ujinasibu kuwa hizo ni pesa zao wenyewe toka mfukoni mwao, wanatumia mihanya hiyo ya wananchi kutojua ukweli wa jambo hili.
Hivyo uzitumia pesa husika kujihimarisha kisiasa, ndiyo maana wanaharakati wengi wamekuwa wakiishauri serikali kufuta sheria hiyo na kuondosha hii mifuko ya jimbo kwani imeonekana ilianzishwa kwa lengo zuri ila usimamizi na utekelezaji wake hauleti hali chanya kwa walengwa.
Ukiangalia kwa mfano Mgawanyo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo 2010/2011 majimbo kama kielelezo kwenye picha kinavyoonesha yalipata pesa nyingi tu lakini nani anaweza kujua zilitumikaje katika majimbo yetu?
WITO WANGU KWA WANANCHI, baada ya kutambua matumizi na malengo ya pesa za jimbo tuanzishe miradi mbalimbali na tuwashirikishe wabunge wetu na wakigoma kutusupport tuwahoji hizi pesa zilitumika kwa matumizi gani?
Yamkini viongozi wetu (wabunge) wamejisahau sasa tuwakumbushe kwa kuanzisha miradi mbalimbali na kutaka mchango wao toka mfuko wa jimbo.
ANDIKO HILI LINALENGA KUEMILIKISHA JAMII JUU YA SHERIA YA MFUKO WA JIMBO NA MALENGO YAKE.
-----
Pia soma
>Mfuko wa Jimbo kupingwa mahakamani - JamiiForums
>Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo: CDCF - JamiiForums