Jamaa yangu ndio kwanza ameoa, yeye na mkewe wote wanafanya kazi benki, sio ofisi moja.
Katika pitapita zake kwenye internet, kakutana na blog ya facebook, kasachiiiiiiiii, hadi kikaeleweka kampata binti mmoja aliyemvutia kimeseji na kusikia ni wale watokao moja ya makabila ya Arusha, akazidi kuchanganyikiwa, maana kabila hilo wasichana wake huwa wanamuacha hoi daima, hata mkewe anatoka kabila hilohilo.
Sijui ni shetani, sijui ni kutoridhika na mkewe, sijui ni tamaa, au labda sijui ni ukware tu... ila kilichofuata ni kuwa akawa na mapenzi mazito na huyo dada. Yeye jamaa yangu hakutaja jina lake halisi.
Jana jioni waliamua wakutane saa 12 jioni kwenye bar fulani maeneo ya kinondoni. Kwa vile kila mtu ana simu ya mwenzake hivyo walikubaliana, wakifika sehemu hiyo watapigiana. Huyu jamaa ananiambia kuwa walielezana pia kuwa kila mtu atavaaje, huyo dada alisema angevaa gauni la blue na jamaa akasema atavaa shati jeupe mikono mirefu... nilishasema huyu jamaa ni benka hivyo hapo ni kuvua tai tu na kuingia bar.
Jamaa saa 12 kasorobo akatia timu bila kuchelewa, kabla hajafika eneo la tukio akapiga simu na akaelekezwa na bibie eneo alipokaa kwani yeye bibie keshafika saa nyingi anamngoja. Jamaa akaingia bar kwa mikogo yote huku akipepesa macho na udenda ukimtoka, kwa vyovyote ville mkono wa kulia ukiwa mfukoni mwa suruali.
Kulia alimwona mrembo mmoja amekaa kavalia gauni la bluu, looooh alipoangalia vizuri kumbe ni MKEWE WA NDOA NDIE WANATAZAMANA NAE USO KWA USO.
Anasikitika sana kwa yaliyomkuta, anasema sasa ndoa yake inalegalega, ANAMPENDA SANA MKEWE. ANAJUTIA FACEBOOK.
UNASEMAJE MWANA JF? AFANYEJE KUWEKA MAMBO SAWA?
Katika pitapita zake kwenye internet, kakutana na blog ya facebook, kasachiiiiiiiii, hadi kikaeleweka kampata binti mmoja aliyemvutia kimeseji na kusikia ni wale watokao moja ya makabila ya Arusha, akazidi kuchanganyikiwa, maana kabila hilo wasichana wake huwa wanamuacha hoi daima, hata mkewe anatoka kabila hilohilo.
Sijui ni shetani, sijui ni kutoridhika na mkewe, sijui ni tamaa, au labda sijui ni ukware tu... ila kilichofuata ni kuwa akawa na mapenzi mazito na huyo dada. Yeye jamaa yangu hakutaja jina lake halisi.
Jana jioni waliamua wakutane saa 12 jioni kwenye bar fulani maeneo ya kinondoni. Kwa vile kila mtu ana simu ya mwenzake hivyo walikubaliana, wakifika sehemu hiyo watapigiana. Huyu jamaa ananiambia kuwa walielezana pia kuwa kila mtu atavaaje, huyo dada alisema angevaa gauni la blue na jamaa akasema atavaa shati jeupe mikono mirefu... nilishasema huyu jamaa ni benka hivyo hapo ni kuvua tai tu na kuingia bar.
Jamaa saa 12 kasorobo akatia timu bila kuchelewa, kabla hajafika eneo la tukio akapiga simu na akaelekezwa na bibie eneo alipokaa kwani yeye bibie keshafika saa nyingi anamngoja. Jamaa akaingia bar kwa mikogo yote huku akipepesa macho na udenda ukimtoka, kwa vyovyote ville mkono wa kulia ukiwa mfukoni mwa suruali.
Kulia alimwona mrembo mmoja amekaa kavalia gauni la bluu, looooh alipoangalia vizuri kumbe ni MKEWE WA NDOA NDIE WANATAZAMANA NAE USO KWA USO.
Anasikitika sana kwa yaliyomkuta, anasema sasa ndoa yake inalegalega, ANAMPENDA SANA MKEWE. ANAJUTIA FACEBOOK.
UNASEMAJE MWANA JF? AFANYEJE KUWEKA MAMBO SAWA?