Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

TAHADHARI KWA WANAONUNUA MAGARI: Kabla ya kununua gari ulilochagua, iwe show room au kwa mtu mwengine yeyote hakikisha kabla ya kufanya malipo chukua nambari ya chassis ya gari hilo na uwasiliane na ofisi ya Interpol iliyopo ghorofa ya saba Jengo la Makao Makuu ya Polisi mtaa wa Ghana mkabala na jengo la Posts ili waangalie kwenye system ya Interpol iwapo gari hilo halijawahi kusajiliwa kuwa ni la wizi miongoni mwa nchi zaidi wanachama wa Interpol duniani.

Bila kupata uhakika kutoka interpol kuna hatari ukanunua gari la wizi na ukajikuta unaliacha mikononi mwa polisi pindi ukikamatwa nalo wakati wa operesheni za interpol za kukamata magari ya wizi miongoni mwa nchi wanachama zinazofanyika kila Mwaka.
 
Iwapo umenunua gari kutoka nchi jirani na unataka kuliingiza nchini Tanzania hakikisha unapata " clearence" ya ama SARPCCO kama umenunua kusini mwa Afrika au ya EAPCCO kama umenunua nchi yeyote ya Afrika mashariki.

Clearance hiyo ni uthibitisho kwamba gari hilo halijawahi kusajiliwa kuibiwa katika nchi yeyote mwanachama wa interpol
 
.... KAMA OFISA WA POLISI ANAKUTUHUMU KWAMBA
UMEFANYA KOSA : Mara nyingi utapewa uchaguzi wa
kukubali kosa na kulipa faini ya sh. 20,000 siku hizi wanachukua 30,000/=
 
TAHADHARI KWA WANAONUNUA MAGARI: Kabla ya kununua gari ulilochagua, iwe show room au kwa mtu mwengine yeyote hakikisha kabla ya kufanya malipo chukua nambari ya chassis ya gari hilo na uwasiliane na ofisi ya Interpol iliyopo ghorofa ya saba Jengo la Makao Makuu ya Polisi mtaa wa Ghana mkabala na jengo la Posts ili waangalie kwenye system ya Interpol iwapo gari hilo halijawahi kusajiliwa kuwa ni la wizi miongoni mwa nchi zaidi wanachama wa Interpol duniani. Bila kupata uhakika kutoka interpol kuna hatari ukanunua gari la wizi na ukajikuta unaliacha mikononi mwa polisi pindi ukikamatwa nalo wakati wa operesheni za interpol za kukamata magari ya wizi miongoni mwa nchi wanachama zinazofanyika kila Mwaka.


...ofisi za Polisi ! .... kumueleza kuwa ofisi zao
zimejaa ukiritimba wa kutotoa ushirikiano na kuficha
taarifa.
 
Mkuu kuna mtu aliniuzia gari, kanikabidhi document zote kuhusiana na gari, ila wakati wa kuandikishana tuliandikiana makubaliano tu bila kwenda kwa mwanasheria na shahidi akiwepo.

Je kuna madhara yeyote naweza kupata
 
Airbag inahitaji service mara nyingi lifespan ya airbag ni miaka 10, baada ya hapo lazima ufanye service au saa nyingine ni wiring inahitajika kumuona mtaalam

Nilitaka kupita tu, lkn nilipoona kuna service ya Airbag nimelazimika kupiga breki ili kupata elimu ya service ya hiyo kitu. Mkuu Mshana, hebu tupe elimu sie wengine tusiojua Service ya Airbag, ipoje hii?
 
Nilitaka kupita tu, lkn nilipoona kuna service ya Airbag nimelazimika kupiga breki ili kupata elimu ya service ya hiyo kitu. Mkuu Mshana, hebu tupe elimu sie wengine tusiojua Service ya Airbag, ipoje hii?

Kwakweli sidhani kama hapa kwetu tuna wataalam wa hiyo kitu ila najua Nairobi ipo, kinachoangaliwa ni pressure, sensor na wiring kama hakuna malfunctions, ndo maana huwa unakuta kuna baadhi ya magari ikitokea mizinga airbags hazifunguki

Makampuni makubwa kama Toyota Nissan nk nafikiri wanaweza kuwa na hiyo mitambo
 
Mkuu kuna mtu aliniuzia gari, kanikabidhi document zote kuhusiana na gari, ila wakati wa kuandikishana tuliandikiana makubaliano tu bila kwenda kwa mwanasheria na shahidi akiwepo. Je kuna madhara yeyote naweza kupata

Tatizo si kubwa Kama wote mna nia njema, tunawatumia wanasheria kwasababu siku hizi kuna watu na viatu, watu ni wengi lakini binadamu ni wachache

Cha muhimu sana sana kabla hujafanya manunuzi yoyote hasa hizi gari za mkononi ni vema ukapata copy ya kadi ya gari uende nayo TRA makao makuu gorofa ya nne ni kitengo cha investigation, hapo hakuna urasimu wowote, utaambiwa ukweli kuhusu usajili wa gari na kama hakuna shida yoyote

Kingine epuka kununua gari yenye kadi original lakini ni duplicate, wengi wameumizwa sana kwa kuuziwa magari ya wizi na utapeli
 
.... KAMA OFISA WA POLISI ANAKUTUHUMU KWAMBA
UMEFANYA KOSA : Mara nyingi utapewa uchaguzi wa
kukubali kosa na kulipa faini ya sh. 20,000 siku hizi wanachukua 30,000/=

Bunge ndio limepitisha sheria ya kosa moja kuwa elfu 30, badala ya 20 ili kuweza kuwabana zaidi wakosaji lakini badala yake imekuwa ni ulaji mwingine wa polisi wasio waadilifu
 
HAKI ZA DEREVA ANAPOKAMATWA NA TRAFFIC
- Trafiki hana idhini ya kukulazimisha kumkabidhi leseni yako

-Akikukuta na kosa na kukuandikia notification na ukalipa ni lazima akupe risiti ya serikali

-Hana haki ya kukuulizia kuhusu road licence hiyo ni kazi ya TRA kwakuwa siku utakapoenda kulipa utalipia na faini

-kama huna leseni una haki kisheria kuipeleka kituoni ndani ya Massa 72 ya kazi tangu ulipotakiwa kufanya hivyo

-Akikusimamisha una haki ya kusimama sehemu ile ambayo utaona ni salama na si lazima usimame anapotaka yeye

- Sio kila kosa ni la kuadhibiwa, mengine ya kuonywa au kuelimishwa
 
Nini usalama kiafya wa kile chombo cha kupimia kirevi? Wanapimiwa watu wangapi kwa siku? Kinasafishwaje? Dereva yyte anapimwa? Au ni daradara na gar za abiria tu?

Mimi sidhan kama ntakubali kupimwa bila kujiridhisha kuhusu hayo maswali
 
Nini usalama kiafya wa kile chombo cha kupimia kirevi? Wanapimiwa watu wangapi kwa siku? Kinasafishwaje? Dereva yyte anapimwa? Au ni daradara na gar za abiria tu? Mimi sidhan kama ntakubali kupimwa bila kujiridhisha kuhusu hayo maswali

Kenya walikikataa kwa hoja na wakashinda, kuna mengi hayakuzingatiwa kwenye kile kifaa hasa linapokuja suala la afya na magonjwa ya kuambukiza
 
Last edited by a moderator:
Hili wameligomea hata sijui kwa nini, tumeomba sana sana!!!!
Linaweza punguza hata ajali za barabarani pia sababu tutakutana huko na kupeana ushauri!!!

MANI, RRONDO, Kaizer! !!

mshana jr kazi nzuri sana kaka, Invisible japo sticky meanwhile

Taratibu wanaweza kufikiria au njia nyingine ni kuwa uzi kama huu amabapo uchangiaji unakuwa ni wa mara kwa mara.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom