Lula wa Ndali ushabiki pekee hautoshi tujadili kwa hoja

FROM PENPALS WEBSITE:

Posted: 16/08/2009, 12:21
Iam a boy aged 20 years living in Arusha Tanzania East Africa iam looking for a girl of any age the one who will love the one to care me. For more about me visit www.novadream.blog.com and my phone number is +255766730256 talk to me and welcome to mt kilimanjaro the highest peak in Africa.
Posted By: nova kambota
Location: United Republic of Tanzania
Email: novakambota@gmail.com


he is sooo gay!!!
 
Wana JF tuendelee kujadili au mmeshindwa? Someni pia kwenye menu kuu article yenye kichwa cha habari what is it?

Kwa uwezo wangu wa kujenga na kubomoa hoja nitakavyo wanajamii wenzangu mna kibarua kigumu sasa kwa maana hapa ni mwendo wa hoja tu hakuna jazba, fujo wala matusi ni hoja tu kwenda mbele.

dogo nakuonea huruma kwani aliyekutuma know exactly how stupid and degraded you are.... I am not homophobic but surely you are you have something phobic in you

may God lead you to understand things in abigger and experienced picture sooner rather than later
 
Wanajamii... for one to float discussions like nova did, clear understanding of the context is a must... unfortunately Nova ameshindwa hata kujua nini maana ya upinzani na pia nani ni mpinzani na kibaya zaidi hajui role ya upinzani

Kwa mtu kama huyu ku-stage choreographed scene yake kwenye jukwaa hili ni kitu cha kusikitisha zaidi ya kuudhi.. the boy is literally empty


too bad he tries to "educate us" about bible na roles za watu fulani wakati yeye mwenyewe hajaondoa najisi aliyonayo
 
FROM PENPALS WEBSITE:

Posted: 16/08/2009, 12:21
Iam a boy aged 20 years living in Arusha Tanzania East Africa iam looking for a girl of any age the one who will love the one to care me. For more about me visit www.novadream.blog.com and my phone number is +255766730256 talk to me and welcome to mt kilimanjaro the highest peak in Africa.
Posted By: nova kambota
Location: United Republic of Tanzania
Email: novakambota@gmail.com

Duh! mkuu wangu hii ya Girl of ANY AGE inatisha...
 
LULA AMEPOTOSHA HOJA ZINAZOMHUSU DK. SLAA

Novatus .S. kambota

Leo nimejitokeza kwenye gazeti hili la Raia Mwema ili kujibu makala ya mwandishi Lula wa Ndali Mwananzela kwenye toleo namba 149 la septemba 1 mwaka 2010.

Lula alipaswa ajibu hoja za msingi kama vile kwa nini Dk. Slaa hana msimamo? Na je tukimpa urais hatokuwa na maamuzi legelege ya kufata mkumbo? Au hataendeleza tabia yake ya kutokuwa msikivu au mkaidi? Lula anapaswa ajue kuwa kuhoji maswali haya sio kumpinga Dk. Slaa bali kiu ya kujiridhisha kwa maana uraisi sio lele mama . Tunahitaji mtu makini ambaye ana utashi mkubwa wa kisiasa na mwenye kufikiri kwa mantiki na kuamua kwa hoja nzito na zenye mashiko na sio maamuzi legelege ya kufata mkumbo......


SWALI: JE ni nai unaye fikiri ni bora ya SLAA kwa mtazamo wako?....naomba jibu
 
LULA AMEPOTOSHA HOJA ZINAZOMHUSU DK. SLAA
Sasa kwa mazingira haya sijui Lula ana la kujibu kuhusu Dk. Slaa? Kwa maana Dk. Slaa alipitia hatua hizi na kote huko aliongozwa na Roho Mtakatifu kufanya uamuzi wake na mpaka akafikia kwenye sakramenti takatifu (isiyofutika) ya upadre. Sasa kinachotutatiza wengi ni swala la Dk. Slaa kutoka kwenye wito wake wa upadre na kuingia kwenye siasa, hapa kuna maswali kadhaa ya msingi ya kujiuliza ; kwanza kwa kuacha upadre Dk. Slaa anataka kutudhihirishia kuwa alipokuwa seminari alikuwa bendera fata upepo? Mpaka akajikuta ameangukia kwenye upadre pasipo kuwa na wito huo? Au labda Dk. Slaa alidanganywa na Roho Mtakatifu na kujikuta amekuwa padre bila kupenda? Au Dk. Slaa ni mtu wa namna gani basi?
Kwanza, elimu yako ya kidato cha nne ktk upadre ni ndogo sana[introduction to..]. Kwa wana Theologia wanajua mipaka na miiko ya kazi zao.
Kama kuacha upadre ni bendera fuate upepo, vipi wale ma-protestant! nao walifuata upepo gani kujitoa vatcan

Kama ni kweli Dk. Slaa ni bendera fata upepo basi ni mtu hatari kwa maana kwa uelewa wa kawaida tu raisi mfata upepo hafai kwa maana si ajabu akiwa rais
anaweza kufanya maamuzi kwa kufata upepo na bila shaka ameshaonyesha mwenendo wake huo wa kufata mkumbo, kwa maneno yake mwenyewe Dk. Slaa amesema kuwa hakuwa na lengo la kuwania urais na kwamba alishachukua fomu ya kuwania ubunge wa karatu na ghafla kabadili mawazo na kuingia kwenye kinyang’anyiro cha urais kwa kushawishiwa tu na wanachama wa CHADEMA , hii kweli ni ajabu na bila shaka inadhihirisha tabia ya kufata mkumbo ya Dk. Slaa.
Kiongozi bora anatambuliwa na jamii, hajitambui. Wale wanaoutaka uongozi kwa nia na nguvu zao wana ajenda ya siri. Angalia NEC ya CCM ilivyosheheni wanaoutaka uongozi na adha wanayoipata watanzania
Na iwapo alidanganywa na Roho Mtakatifu basi ni mwongo au sio msikivu kwa maana Roho Mtakatifu kamwe hawezi kuwa mwongo, pengine wakati Roho Mtakatifu alimfunulia Dk. Slaa kuwa upadre haukuwa wito wake yeye hakuwa msikivu alikuwa mkadi na hivyo aling’ang’ania na baadae upadre ukamshinda na ule methali maarufu ya asiyesikia la mkuu……..huvunjika guu imemtokea Dk. Slaa.
Masuala ya roho mtakatifu ni baina ya DR Slaa na roho wake. Sisi tunamjua kama Dr Slaa na si wajibu wetu kumjua kwa roho mtakatifu wake. Tunataka kuchagua Rais wa nchi ambayo haina dini bali raia wana dini, unapotushawishi kuhusu roho mtakatifu si jamii yote inaamini kuhusu utakatifu huo, kuna imani tofauti. Hiki ni kipimo kizuri kuhusu mtazamo wako kwa jamii na uelewa mdogo wa kuwasiliana na jamii. Wapagani, Hindu, Budhist, Waislam hawakuelewi unaongelea nini, muongelee Slaa kama mgombea na uadilifu wake kijamii si kwa imani.
Sasa Lula ilibidi ajibu hoja hizi na sio kujikanyaga kanyaga kwenye makala yake ile ambayo kimsingi haikulenga kuchambua kwa mantiki hoja hizi badala yake ilikuwa makala ya kisiasa iliyolenga kumpigia debe Dk. Slaa, kwa kweli sikutegemea na kamwe sitaki kuamini kuwa makala ile iliandikwa na mwandishi wa viwango vya Lula labda siye yeye, pengine labda Lula alikuwa hayupo kwenye hali yake ya kawaida alikuwa anaumwa ladda kwa maana nilitegemea makala ile iandikwe na mkurugenzi wa propaganda wa CHADEMA (kama yupo) na sio mwandishi wa ubora wa Lula.
Tuliyoisoma tunajua Lula alikuwa fit ila tunawasi wasi na afya yako hasa katika uchambuzi ambao hutegemmea sana utimilifu wa kufikiri.
Lula alipaswa ajibu hoja za msingi kama vile kwa nini Dk. Slaa hana msimamo? Na je tukimpa urais hatokuwa na maamuzi legelege ya kufata mkumbo? Au hataendeleza tabia yake ya kutokuwa msikivu au mkaidi? Tueleze ukaidi upi Slaa aliowahi kulifanyia taifa.Lula anapaswa ajue kuwa kuhoji maswali haya sio kumpinga Dk. Slaa bali kiu ya kujiridhisha kwa maana uraisi sio lele mama . Tunahitaji mtu makini ambaye ana utashi mkubwa wa kisiasa na mwenye kufikiri kwa mantiki na kuamua kwa hoja nzito na zenye mashiko na sio maamuzi legelege ya kufata mkumbo. Tutajie huyo kiongozi makini na utueleze umakini wake, maana tunawajua wapo wanne, Nyerere, Mwinyi, Mkapa na JK. Kati ya hawa ni yupi dhaifu sana, anayesema bila kufikiri? Dr slaa ndiye kiongozi mwenye msismamo Tanzania, fuatilia matukio yake hata pale alipotishiwa kupelekwa mahakani aliendelea kuwa na msimamo ule ule. Alwahi kusema bungeni yeye ndiye anampa kubenea Nyeti bila kumung'unya maneno. Humjui Slaa kwasababu hukumfuatilia kuanzia mwanzo bali umemjua pengine wiki mbili baada ya kusoma uzushi wa ndoa yake
Lula alipaswa aende mbali zaidi kwa kuhusanisha hulka ya Dk. Slaa kutokuwa na msimamo na swala la padre huyo kuvunja viapo vyake vya upadre iwe kwa ruhusa ya Vatican au la? Kwanini Dk. Slaa ameoa na ana watoto wawili kinyume na maadili ya wito wake ambao yeye mwenyewe aliukubali pasipo kulazimishwa? Je yeye ni mwasi? Na je iwapo atabahatika kuingia kwenye kuta za magogoni hataasi kwa maana ya kutofata katiba ipasavyo kama alivyoasi kwenye kanisa katoliki?
Hivi kuacha upadre na kuoa si ukomavu huo, vipi ulitaka Dr Slaa awe kama Padre Sixtus Kimaro, akiwa ndani ya ngozi ya kondoo unayemwita roho mtakatifu. Kwa faida ya wasomaji wake Lula alipaswa kulitazama kiundani swala la hivi karibuni la Dk. Slaa kuachana na mkewe na kuoa mke mwingine, je lina uhusano na hulka yake ya kufata mkumbo au kufanya maamuzi legelege, je mwanzoni alifata mkumbo kumwoa mke wa kwanza na sasa amebadili uamuzi? Hatuchagui mtu na mkewe au hawara, tunamchagua Rais wa nchi. Kama ni muhimu kufuatilia mambo yao binafsi, mbona hatujaelezwa mzee anaumwa nini.
Pengine hapa mtu anaweza kuja na hoja kuwa Dk. Slaa ni mtu makini ambaye anajirekebisha haraka na kuchukua hatua au kwanini hoja za udhaifu wa Dk. Slaa zinajitokeza sasa hivi? Kwanini hazikuwepo alipokuwa mbunge wa karatu?. Labda nitoe angalizo kuwa hata kama Dk. Slaa ana tabia ya kujirekebisha haraka bado hafai kwa maana kuwa rais wa nchi sio sawa na kuwa class-monitor kwa maana kama Dk. Slaa ni mtu wa namna hiyo basi tujiandae na rais mkoseaji kila siku na wapiga kura wa Tanzania wajue kwamba nchi inahitaji maamuzi makini na sio kukoseakosea kwa maana kuna mambo mengine ambayo yakikosewa hata mara moja tu basi ni angamizo la taifa zima (one mistake one goal). Rais aliyepo madarkani aliwahi sema, miaka 2 ya mwanzo ilikuwa ya kujifunza, mbona hilo hujaliona na kulizungumzia kama mfano wa kukosea kosea. Kumbuka Urais si ndoa bali ni taasisi inayoongozwa na katiba ya nchi.
Pili Lula inabidi atambue kuwa kuna kila sababu ya kuhoji uimara wa Dk. Slaa na vilevile ni haki kabisa hoja hizi kuibuka wakati huu kwa maana raisi ni kiongozi mkuu wa nchi tofauti na mbunge ambaye ni mwakilishi wa jimbo lake (na hapa naomba nisieleweke vibaya kuwa natetea wabunge legelege), raisi akiboronga athari zake ni kubwa (tramendous effects) na zina uzito mkubwa sana tofauti na mbunge
akiboronga ingawaje kuboronga ni kuboronga na dhambi ni dhambi tu. Kwahiyo unataka kutuaminisha kuwa huyu aliyepo ni safi na hajaboronga. Kuboronga kupi unakoongelea maana tunaweza kuwa na maana tofauti ya kuboronga
Lula inapaswa atambue kuwa Dk. Slaa hivi sasa anawahusu watanzania wote na sio wana karatu pekee hivyo tuna kila sababu ya kujiridhisha naye na anapaswa atoe ufafanuzi wa kina ili aeleweke na umma wa watanzania na sio kutoa majibu mepesi mepesi kwa hoja nzito kama alivyofanya Lula kwenye makala yake. Kama ambavyo Rais JK anatuhusu watanzania wote na tunasababu ya kujirisha kuhusu afya yake kama ilivyo ndoa ya Slaa.!!!
Mwishowe Lula anapaswa atambue kuwa uimara wa Dk. Slaa kamwe hauletwi na mifano ya watu ambao waliwahi kuwa mapadre na mwishowe kuukwaa urais, hapa nakusudia kusema kuwa hoja hizi kumhusu Dk. Slaa hazikupaswa kujibiwa kwa orodha ya mifano ya mapadre waliowahi kuwania urais au kuupata urais mifano hiyo ni pamoja na padre Edd Panlilio wa Ufilipino au Askofu Ferdando Lugo wa San Pedro Paraguay. Orodha hii aliyoitoa Lula haina maana yoyote na wala haitoi ufumbuzi kwa hoja na maswali yenye utata yanayomuhusu Dk. Slaa bali Lula anapaswa azijibu hoja hizi nzito na kuzitolea ufafanuzi wa kina ambao utaeleweka kwa wapiga kura wote wa Tanzania. Ufafanuzi upi ambao wewe umeutoa kama si kumtuhumu Lula kwa hoja nyepesi zisizo na mantiki wala mashiko.
 
Nova, nakubaliana kabisa na wachangiaji wengine waliosema kwamba hoja zako za kuhusu Dr Slaa hazina nguvu. Haingii akilini kwa mtu mweledi kuyahukumu maisha yote ya Slaa eti kwa sababu "alishindwa" (hata kama alishindwa kweli) upadre! Hiyo ni hoja ya kitoto sana. kwani ukishindwa area moja ya maisha ndo maisha yote yameshindikana? Wewe ulisoma seminari, uliposhindwa kuendelea na upadre ndo ukawa umeshindwa maisha yako yote?? Sisi sote huwa tunajaribu means mbalimbali ili kujiendeleza, huwezi kusema kuwa kwa kuwa nimeshindwa kilimo ndo basi maisha yote yamenishinda. Hiyo ni hoja isiyoendana na uhalisi wa maisha ya watu.
 
lula wa ndali ni mmoja kati ya watu ninaowaheshimu sana. anauwezo mzuri wa kujenga na kutetea hoja zake. ndugu yetu novatus hoja zako kwa mtazamo wangu naona kama umezitengeneza huku ukiwa na mtazamo chanya juu ya Dr.slaa. pia hoja zako ni ndefu na hazina mashiko. lakini endelea mwisho wa siku unaweza pata cheo ccm.
maana ni heri mtu akasoma hoja zako kuliko za makamba .kinanna .kikwete. kwa hivyo ndugu nova endelea kuweka hoja jamvini lakini jaribu kuzifupisha. habari za wewe kuwa mwana mazingira n.k hazituzaidii sana hapa jamvini
 
mail
Swala la kumheshimu lula lipo palepale kama nilivyosema kwenye makala yangu lakini naomba ieleweke kuwa nachojaribu kuchambua ni jinsi lula alivyoshindwa kujadili hoja ile.........sasa huku si kutomheshimu kwa kuwa hata kusoma na kukosoa makala yake ni kumheshimu pia.....zaidi kutokana na mjadala huu nimejifunza kuwa kuna wengi wanaoshiriki mijadala lakini kuna wachache sana wanaofahamu msingi wa kuendesha mijadala..............wengine wanadhani hii ni sehemu ya matusi, kashfa na ugomvi.............just imagine watu wanaibua shutuma na matusi kuhusu mimi ambayo si sehemu ya mjadala huu.........hili ni tatizo wengine wanasema mimi ni mwanaume jina na wengine wanadai mimi nilifukuzwa seminari..............huu ni upuuzi, ujinga, upumbavu ,kukosa maono na kukosa weledi ni dalili za kuishiwa hoja. Najaribu kutafakari haya yanafanywa kwa lengo gani? ........nagundua ni kwa lengo la kunitisha niache kuongea.........hili ni tatizo lingine lakini nachoshukuru katika kashfa hakuna ambayo hata moja iliyojikita katika kujibu hoja zangu.Haitoshi mimi ni mtu nileyelelewa na kuwa mtu msikivu, kujali utu, kusema ukweli,kudadisi, kutafiti na kuheshimu watu hizi ndio tuzo za mwanadamu. Sitaki kuamini kuwa walionikashifu wameishiwa hoja lakini nalazimika kuamini kwa dalili ya kwanza ya kuishiwa hoja ni ugomvi, matusi na fujo hizo ndizo tunu za ushetani. Hivyo natoa wito kwa wanajamii wenzangu kujikita zaidi katika kuchambua yale niliyoyaandika kwenye makala yangu inapaswa kupangua hoja vinginevyo ni ubatili mtupu.
 
nova hebu soma, makala ya hii ya ayubu riyoba, mwananchi 18-09-2010
Kiongozi anahitaji mwenza wa aina gani kwa maisha ya umma? -


KATIKA kampeni za mwaka huu suala la mke wa kiongozi limevuta hisia za wengi wanaofuatilia mambo ya siasa. Lakini hatuna budi kuangaza kwingineko kuona mifano ambayo tunaweza kuitumia kujifunza kifikra badala ya kujadili mambo kwa hisia.

Wiki iliyopita nilidadisi hoja inayohusu umuhimu wa kiongozi kuwa na familia (mke au mume na watoto). Nikasema hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaotetea hoja kwamba ili mtu awe kiongozi bora ni lazima awe na familia.

Lakini tukiitanua hoja hii zaidi tunaweza kubaini kwamba familia inao umuhimu wake. Na wataalamu wanaeleza jinsi familia inavyoweza kujenga mazingira mazuri ya kifikra, kimaadili na upendo kwa wanafamilia. Familia nzuri yenye misingi mizuri, mara nyingi hutoa watu wazuri wenye misingi mizuri. Familia hutoa kimbilio kwa mwanafamilia aliyegubikwa au kusongwa na matatizo, hofu na hata msongo wa mawazo. Lakini, hata hivyo, hali yaweza pia kuwa kinyume.

Hapa ndipo linapokuja suali kwamba je, kiongozi awe na mwenza wa aina gani. Je mke (au mume) wa kiongozi anakuwa na nafasi gani katika suala la uongozi wa familia yake? Hili ni suala linalohitaji ufafanuzi wa kitaalamu. Lakini madhali sasa hivi linajadiliwa na karibu kila anayejisikia kufanya hivyo, nitajaribu kudadisi tu mifano ya viongozi mbalimbali na wenza wao ili kuongeza changamoto katika ufahamu na mwelekeo wa mjadala wenyewe.

Kwa bahati mbaya, suala hili limegubikwa na mijadala ya hasira, chuki na hata matusi. Na kwa hakika kujadili kwa hasira na chuki jambo muhimu kama hili hakutatusaidia kama taifa linalotambua kuwa linao watoto wanaopaswa kujifunza kutoka kwa watu wazima na viongozi wao.

Ninakubaliana na hoja kuwa suala la mwenza wa kiongozi ni la binafsi linalomhusu yeye na familia yake. Lakini pia ninatambua kuwa suala la mwenza wa kiongozi lina nafasi muhimu katika maisha ya umma ya kiongozi husika.

Ndiyo maana katika utamaduni tuliourithi kutoka kwa Waingereza, mke wa rais huitwa: First Lady (hatuna Kiswahili chake fasaha). Huenda siku tukiwa na Rais mwanamke, basi mumewe (kama atakuwa naye) ataitwa First Gentleman.

Katika historia, wake wa viongozi (kuna mifano michache ya waume wa viongozi) wametekeleza majukumu tofauti na kuonyesha tabia tofauti ambavyo viliwafanya wawe tofauti kwa wananchi wao. Wapo waliopendwa zaidi kuliko hata viongozi wenyewe. Wapo ambao tabia zao ziliwachukiza wananchi. Wapo walioanzisha na kutekeleza mambo makubwa yenye manufaa kwa nchi zao.
Wapo walioamua kutoonekana hadharani na kubaki wakitunza familia wakati waume zao wakizunguka huku na kule katika mambo ya siasa. Wapo waliojiandaa na kushika madaraka baada ya waume zao kumaliza vipindi vyao vya kutawala. Wapo waliowaingiza waume zao majaribuni (kuhusu wizi wa mali za umma), wapo waliohakikisha waume zao (viongozi) wanapata liwazo na mapenzi ya hali ya juu baada ya mikiki mikiki ya kuongoza nchi. Lakini wapo pia waliowaua waume zao kwa shinikizo la damu kutokana na tabia zao za kuwanyanyasa kisaikolojia na hata kimatendo.

Ndiyo maana suala la mke au mume wa kiongozi si suala la kujadili kwa mzaha, hasira au chuki kama tunavyoelekea katika mjadala wa sasa. Ni suala la kutafakari na kujadili kwa kujenga kwani kesho, tukimaliza kampeni za uchaguzi, bado tutahitaji kuangaliana usoni kama Watanzania, watu wazima tunaojiheshimu mbele ya watoto wetu na tunaojali hisia za watu wengine.

Katika baadhi ya mifano ambayo nimeitembelea nimeweka wake wa viongozi katika makundi kadhaa. Wapo waliojulikana zaidi kwa urembo wao kama alivyokuwa Jackie Kennedy. Jackie alikuwa mke wa Rais wa Marekani, John F. Kennedy, aliyeuwawa miaka ya 1960.

Kundi jengine ni lile la mke wa rais ambaye pia anaamua kuwa mwanasiasa. Mke wa Rais wa Arjentina, Cristine Fernandez de Kirchner alimrithi mumewe Nestor Kirchner katika kiti cha urais mwaka 2007. Hapa jirani (Uganda) Mama Janeth Museveni ameingia katika siasa na sasa ni waziri katika serikali ya mumewe, Yoweri Museveni. Hillary Clinton, mke wa Rais Bill Clinton wa Marekani pia yupo katika kundi hili. Winnie Mandela wa Afrika kusini naye yupo katika kundi hili.

Kundi jengine ni la mke wa rais ambaye ni mtunza familia. Wapo wake wa viongozi ambao huchagua kutulia nyumbani kuiangalia familia wakati kiongozi anapokuwa katika harakati zake za kisiasa. Mfano mzuri kwetu sisi ni Mama Maria Nyerere ambaye hakujihusisha sana au kuwa na majukumu rasmi ya umma kipindi ambacho Baba wa Taifa alikuwa kiongozi.
Kundi jengine ni la mke wa rais mjasiriamali. Wapo wake wa marais ambao huamua kuwa wafanyabiashara wakubwa, wakinyang’anyana fursa na wananchi wao na kuwazidi kete kutokana na nafasi zao. Yupo mke wa rais mmoja wa Afrika Magharibi aliyeamuru umeme ukatwe nchini kwake ili yeye auze kwanza jenereta zake alizokuwa ameingiza kutoka Asia.

Lipo pia kundi la mke wa rais ajulikanaye kwa ukorofi. Yeye anaweza kuwazaba makofi maafisa wa serikali mbele ya mumewe pale anapohisi wamemkosea adabu. Na pale waandishi wa habari wanapomkorofisha yeye huenda moja kwa moja chumba cha habari na kuwazaba vibao. Mama Lucy Kibaki yupo katika kundi hili.

Kuna kundi pia la mke wa rais mwanaharakati wa masuala ya jamii. Hapa kwetu Mama Salma Kikwete, kupitia taasisi ya WAMA, amekuwa akiendesha harakati za kuhakikisha kuwa watoto, hasa wa kike, wanalindwa ili waweze kukua na kutimiza ndoto zao. Mama Anna Mkapa alijihusisha pia na harakati za kusaidia akina mama kiuchumi kupitia mfuko wake wa Fursa Sawa kwa Wote.

Ipo haja ya sisi kujifunza katika mifano kama hii ili tutafakari aina ya majukumu au mwenendo ambao tungependa mwenza wa rais awe navyo katika maisha yake ya umma. Ninaamini kuwa si jambo jema na wala si hekima kuwajadili watu na maisha yao binafsi hasa pale ambapo maisha yao hayaathiri maslahi ya umma kwa ujumla. Tuache siasa za majitaka zitiririke kuelekea zinakostahili – katika bwawa la majitaka na si vinginevyo.


ayubrioba@hotmail.com
 
mail
Narudia tena kuitwa mtoto mdogo mimi hakunikatishi tamaa kwangu hakuna vikwazo nayapokea haya kama changamoto kamwe sitaacha kusema ukweli wala kutoa hoja kwa maana huu ndio msingi wa uanaharakati.............tujadili kwa hoja sio vitisho wala jazba...........swala si kuachana na mimi point ni mkuchambua hoja zilizoko kwenye article yangu .......swala si udogo wangu point ni nini kilichomo ndani ya article yangu .........swala si mimi ni nani point ni nini nimeandika kwenye article yangu.
 
Dogo tunashukuru kwa mchango wako,hakuna haja ya kukushutumu kwa mchango wako ulioutoa, kwani huo ni mtazamo wako.Nakushauri ujiendeleze kielimu zaidi kwa kuwa kwa sasa bado una elimu ndogo sana!
 
mail
......so do not be afraid of people.Whatever is now covered up will be uncovered, and every secret will be made known.........(Luke12;26) haya ni maneno yanayonifariji kwa hakika kwa maana sihofii mtu hapa ukweli utasemwa tu hata kama unauma potelea mbali. Hata baba wa taifa Mwl Nyerere alipata kusema kuwa ukichukua maji ya kwenye dimbwi ukayaweka kwenye glass bado yatafanana na yale ya kwenye dimbwi. Vivyo mtu mwenye maadili mema anaweza kuwa kiongozi bora and the vice versa is the fact.........kama mtu hana maadili mema kwenye ndoa yake atawezaje kuwa na maadili kwenye kazi yake? haya ni maswali ya msingi............angalia baba vwa taifa alikuwa na maadili mema kuanzia kwenye ndoa yake mpaka kwenye uongozi wake(ikulu).
 
mail
......so do not be afraid of people.Whatever is now covered up will be uncovered, and every secret will be made known.........(Luke12;26) haya ni maneno yanayonifariji kwa hakika kwa maana sihofii mtu hapa ukweli utasemwa tu hata kama unauma potelea mbali. Hata baba wa taifa Mwl Nyerere alipata kusema kuwa ukichukua maji ya kwenye dimbwi ukayaweka kwenye glass bado yatafanana na yale ya kwenye dimbwi. Vivyo mtu mwenye maadili mema anaweza kuwa kiongozi bora and the vice versa is the fact.........kama mtu hana maadili mema kwenye ndoa yake atawezaje kuwa na maadili kwenye kazi yake? haya ni maswali ya msingi............angalia baba vwa taifa alikuwa na maadili mema kuanzia kwenye ndoa yake mpaka kwenye uongozi wake(ikulu).

Nova hoja zinajibiwa kwa hoja wewe mwenyewe badala ya kujibu hoja za msingi unakimbilia kujibu hoja ambazo unaona hazijibu hoja yako. Kuna watu wengi wamejaribu kukujibu lakini hujatoa majibu. wewe unakimbilia kuwajibu wale ambao hawakujibu.

Uzi wa 91 nimeandika hivi
Hivi

  • ukishindwa kukubaliana na mzazi wako kwa jambo fulani ni kukosa adabu au kukosa msimamo?
  • kuendelea kuishi na mke au mume hata msiyekubalina kwa mambo ya msingi ni ujasir?
  • Kuhama chama kutokana na kutokubaliana na maamuzi ya chama fulani ni kitendo kizuri au kibaya?

To befair hoja alizosema mkuu zina pande mbili na sio pande moja kama anayooshesha . Alitwakiwa aangalie na upande mwingine wa shilingi na kama mchambuzi alitakiwa waonyeshe watu pande mbili ili wasomaji waamue na sio moja?

Yes inawezekana dr slaa hana msimamo lakini upande mwingine inawezekana dr slaa ni jasiri. kama umesoma semianry ulitakiwa kujua kitendo cha kutoka kwenye upadri sio umamuzi mwepesi. Ulitakiwa kujua kuwa kitenda cha Mkristu kuamua kuachana na ndoa ya kutenganishwa na kifo ni ujasiri vilevle. haya sio maamuzi mepesi.

Ukweli from your angle of view and analysis uko sahihi lakini waambie wasomaji hujaangalia upande mwingine wa shilingi kwa sababu unazozijua

Unayemlaumu na wewe ni wale wewe tu. Huyu kaona kwenye shilingi kuna mwenge wewe umona kwenye shilingi kuna kichwa. Who is right? Who is wrong?

Sasa nakushauri ebu na wewe jaribu kujibu hoja
 
Back
Top Bottom