Nova Kambota
Member
- Nov 12, 2009
- 62
- 1
LULA AMEPOTOSHA HOJA ZINAZOMHUSU DK. SLAA
Novatus .S. kambota
Leo nimejitokeza kwenye gazeti hili la Raia Mwema ili kujibu makala ya mwandishi Lula wa Ndali Mwananzela kwenye toleo namba 149 la septemba 1 mwaka 2010.
Kuna sababu kuu nne zilzonisukuma kujibu makala ile iliyokuwa na kichwa cha habari kwanini hoja ya upadre wa Dk. Slaa haina msingi, sababu hizo ni kama ifuatavyo ; kwanza nimeamua kujibu kwa sababu na amini kuwa Raia Mwema ni gazeti huru lisilo na upendeleo kwa yeyote hivyo basi ni matumaini yangu kuwa makala hi itachapwa kama ilivyo bila kupindishwa hata kidogo, pili ni kumkosoa Lula ambaye kwenye makala yake ile alishindwa kuchambua hoja za msingi zinazomhusu Dk. Slaa na badala yake alifanya usanii wa kuzungukazunguka hoja za msingi bila kuzama ndani ya hoja hizo, tatu ni kuzichambua hoja hizo bila kifcho ili watu waweze kumwelewa kiundani Dk. Slaa na nne ni kutoa angalizo kwa waandishi wengine kuwa si vema kufanya usanii kwa kutumia taaluma yao bali wanapaswa wawe wakweli na wasiwe wapiga debe wa wanasiasa.
Sasa nizame kwenye hoja zenyewe ambazo watu wanapaswa kuzielewa kiundani, hoja kuu hapa ni safari ya kisiasa ya Dk. Slaa yenye kila aina ya utata na alama nyingi za kuuuliza, safari hiyo ni ile ya kutoka kwenye kuta za seminari, altare ya Bwana, upadre, katibu wa baraza la maaskofu , ubunge wa karatu mpaka sasa anapowania urais kwa tiketi ya CHADEMA.
Naomba nitoe mifano halisi ili nieleweke, kwanza mimi mwenyewe nimesoma seminari ndogo ya Mtakatifu Maria visiga ya jimbo kuu la Dar es salaam kwa miaka minne (2004-2007).
Nilipokuwa seminarini hapo kwa kawaida walezi wetu walikuwa kila mmoja wetu iwapo kweli ana wito wa upadre au la, na iwapo ilibainika kwa hukuwa au matendo hayaendani na wito huo mtakatifu hakukuwa na subira isipokuwa kuondolewa seminarini sio hivyo tu ulipofika mda wa kuhitimu kidato cha nne kwa kawaida kulikuwa fomu maalumu za kujaza iwapo kweli unawito wa upadre au hapana na ili swala hilo lifanyike kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kulikuwa na sala maalumu iliyoongozwa na baba wa kiroho (spiritual father) kwaajili ya kumwomba Mungu ili amjalie kila mmoja wetu kutambua wito wake na hivyo kujaza fomu hizo kwa umakini na muongozo wa Roho Mtakatifu na ni matumaini yangu kuwa hata wakati wa kuhitimu kidato cha sita utaratibu ni huohuo na hata baada ya kuwa frateri na shemasi kuelekea upadre fomula ni hiyohiyo ya kumwomba Roho Mtakatifu akusaidie (mseminari) kutambua wito wako.
Sasa kwa mazingira haya sijui Lula ana la kujibu kuhusu Dk. Slaa? Kwa maana Dk. Slaa alipitia hatua hizi na kote huko aliongozwa na Roho Mtakatifu kufanya uamuzi wake na mpaka akafikia kwenye sakramenti takatifu (isiyofutika) ya upadre. Sasa kinachotutatiza wengi ni swala la Dk. Slaa kutoka kwenye wito wake wa upadre na kuingia kwenye siasa, hapa kuna maswali kadhaa ya msingi ya kujiuliza ; kwanza kwa kuacha upadre Dk. Slaa anataka kutudhihirishia kuwa alipokuwa seminari alikuwa bendera fata upepo? Mpaka akajikuta ameangukia kwenye upadre pasipo kuwa na wito huo? Au labda Dk. Slaa alidanganywa na Roho Mtakatifu na kujikuta amekuwa padre bila kupenda? Au Dk. Slaa ni mtu wa namna gani basi?
Kama ni kweli Dk. Slaa ni bendera fata upepo basi ni mtu hatari kwa maana kwa uelewa wa kawaida tu raisi mfata upepo hafai kwa maana si ajabu akiwa rais
anaweza kufanya maamuzi kwa kufata upepo na bila shaka ameshaonyesha mwenendo wake huo wa kufata mkumbo, kwa maneno yake mwenyewe Dk. Slaa amesema kuwa hakuwa na lengo la kuwania urais na kwamba alishachukua fomu ya kuwania ubunge wa karatu na ghafla kabadili mawazo na kuingia kwenye kinyanganyiro cha urais kwa kushawishiwa tu na wanachama wa CHADEMA , hii kweli ni ajabu na bila shaka inadhihirisha tabia ya kufata mkumbo ya Dk. Slaa.
Na iwapo alidanganywa na Roho Mtakatifu basi ni mwongo au sio msikivu kwa maana Roho Mtakatifu kamwe hawezi kuwa mwongo, pengine wakati Roho Mtakatifu alimfunulia Dk. Slaa kuwa upadre haukuwa wito wake yeye hakuwa msikivu alikuwa mkadi na hivyo alingangania na baadae upadre ukamshinda na ule methali maarufu ya asiyesikia la mkuu ..huvunjika guu imemtokea Dk. Slaa.
Sasa Lula ilibidi ajibu hoja hizi na sio kujikanyaga kanyaga kwenye makala yake ile ambayo kimsingi haikulenga kuchambua kwa mantiki hoja hizi badala yake ilikuwa makala ya kisiasa iliyolenga kumpigia debe Dk. Slaa, kwa kweli sikutegemea na kamwe sitaki kuamini kuwa makala ile iliandikwa na mwandishi wa viwango vya Lula labda siye yeye, pengine labda Lula alikuwa hayupo kwenye hali yake ya kawaida alikuwa anaumwa ladda kwa maana nilitegemea makala ile iandikwe na mkurugenzi wa propaganda wa CHADEMA (kama yupo) na sio mwandishi wa ubora wa Lula.
Lula alipaswa ajibu hoja za msingi kama vile kwa nini Dk. Slaa hana msimamo? Na je tukimpa urais hatokuwa na maamuzi legelege ya kufata mkumbo? Au hataendeleza tabia yake ya kutokuwa msikivu au mkaidi? Lula anapaswa ajue kuwa kuhoji maswali haya sio kumpinga Dk. Slaa bali kiu ya kujiridhisha kwa maana uraisi sio lele mama . Tunahitaji mtu makini ambaye ana utashi mkubwa wa kisiasa na mwenye kufikiri kwa mantiki na kuamua kwa hoja nzito na zenye mashiko na sio maamuzi legelege ya kufata mkumbo.
Lula alipaswa aende mbali zaidi kwa kuhusanisha hulka ya Dk. Slaa kutokuwa na msimamo na swala la padre huyo kuvunja viapo vyake vya upadre iwe kwa ruhusa ya Vatican au la? Kwanini Dk. Slaa ameoa na ana watoto wawili kinyume na maadili ya wito wake ambao yeye mwenyewe aliukubali pasipo kulazimishwa? Je yeye ni mwasi? Na je iwapo atabahatika kuingia kwenye kuta za magogoni hataasi kwa maana ya kutofata katiba ipasavyo kama alivyoasi kwenye kanisa katoliki?
Haya ni maswali ambayo Lula alipaswa kuyajibu kwa hoja moja baada ya lingine.
Kwa faida ya wasomaji wake Lula alipaswa kulitazama kiundani swala la hivi karibuni la Dk. Slaa kuachana na mkewe na kuoa mke mwingine, je lina uhusano na hulka yake ya kufata mkumbo au kufanya maamuzi legelege, je mwanzoni alifata mkumbo kumwoa mke wa kwanza na sasa amebadili uamuzi?
Pengine hapa mtu anaweza kuja na hoja kuwa Dk. Slaa ni mtu makini ambaye anajirekebisha haraka na kuchukua hatua au kwanini hoja za udhaifu wa Dk. Slaa zinajitokeza sasa hivi? Kwanini hazikuwepo alipokuwa mbunge wa karatu?. Labda nitoe angalizo kuwa hata kama Dk. Slaa ana tabia ya kujirekebisha haraka bado hafai kwa maana kuwa rais wa nchi sio sawa na kuwa class-monitor kwa maana kama Dk. Slaa ni mtu wa namna hiyo basi tujiandae na rais mkoseaji kila siku na wapiga kura wa Tanzania wajue kwamba nchi inahitaji maamuzi makini na sio kukoseakosea kwa maana kuna mambo mengine ambayo yakikosewa hata mara moja tu basi ni angamizo la taifa zima (one mistake one goal).
Pili Lula inabidi atambue kuwa kuna kila sababu ya kuhoji uimara wa Dk. Slaa na vilevile ni haki kabisa hoja hizi kuibuka wakati huu kwa maana raisi ni kiongozi mkuu wa nchi tofauti na mbunge ambaye ni mwakilishi wa jimbo lake (na hapa naomba nisieleweke vibaya kuwa natetea wabunge legelege), raisi akiboronga athari zake ni kubwa (tramendous effects) na zina uzito mkubwa sana tofauti na mbunge
akiboronga ingawaje kuboronga ni kuboronga na dhambi ni dhambi tu.
Lula inapaswa atambue kuwa Dk. Slaa hivi sasa anawahusu watanzania wote na sio wana karatu pekee hivyo tuna kila sababu ya kujiridhisha naye na anapaswa atoe ufafanuzi wa kina ili aeleweke na umma wa watanzania na sio kutoa majibu mepesi mepesi kwa hoja nzito kama alivyofanya Lula kwenye makala yake.
Mwishowe Lula anapaswa atambue kuwa uimara wa Dk. Slaa kamwe hauletwi na mifano ya watu ambao waliwahi kuwa mapadre na mwishowe kuukwaa urais, hapa nakusudia kusema kuwa hoja hizi kumhusu Dk. Slaa hazikupaswa kujibiwa kwa orodha ya mifano ya mapadre waliowahi kuwania urais au kuupata urais mifano hiyo ni pamoja na padre Edd Panlilio wa Ufilipino au Askofu Ferdando Lugo wa San Pedro Paraguay. Orodha hii aliyoitoa Lula haina maana yoyote na wala haitoi ufumbuzi kwa hoja na maswali yenye utata yanayomuhusu Dk. Slaa bali Lula anapaswa azijibu hoja hizi nzito na kuzitolea ufafanuzi wa kina ambao utaeleweka kwa wapiga kura wote wa Tanzania.
Mwandishi wa makala hii anajulikana kama Novatus .S. Kambota (Mwanamapinduzi), yeye ni msomaji wa Raia Mwema pia ni mhitimu wa kidato cha sita wa sekondari ya Ilboru, kwa hivi sasa nimwanaharakati wa mazingira wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Jitume Environmental Society (JES) ya Kiwalani Dar es salaam na vilevile ni mwanachama wa mtandao wa kijamii unojihusisha na uchambuzi wa maswala mbalimbali ya kisiasa unaojulikana kama Taifa Huru Tanzania.
Anapatikana kwa namba 0717-709618 au 0783-610926 au waweza kumwandikia kwa anwani ya barua pepe ; novakambota@gmail.com
Novatus .S. kambota
Leo nimejitokeza kwenye gazeti hili la Raia Mwema ili kujibu makala ya mwandishi Lula wa Ndali Mwananzela kwenye toleo namba 149 la septemba 1 mwaka 2010.
Kuna sababu kuu nne zilzonisukuma kujibu makala ile iliyokuwa na kichwa cha habari kwanini hoja ya upadre wa Dk. Slaa haina msingi, sababu hizo ni kama ifuatavyo ; kwanza nimeamua kujibu kwa sababu na amini kuwa Raia Mwema ni gazeti huru lisilo na upendeleo kwa yeyote hivyo basi ni matumaini yangu kuwa makala hi itachapwa kama ilivyo bila kupindishwa hata kidogo, pili ni kumkosoa Lula ambaye kwenye makala yake ile alishindwa kuchambua hoja za msingi zinazomhusu Dk. Slaa na badala yake alifanya usanii wa kuzungukazunguka hoja za msingi bila kuzama ndani ya hoja hizo, tatu ni kuzichambua hoja hizo bila kifcho ili watu waweze kumwelewa kiundani Dk. Slaa na nne ni kutoa angalizo kwa waandishi wengine kuwa si vema kufanya usanii kwa kutumia taaluma yao bali wanapaswa wawe wakweli na wasiwe wapiga debe wa wanasiasa.
Sasa nizame kwenye hoja zenyewe ambazo watu wanapaswa kuzielewa kiundani, hoja kuu hapa ni safari ya kisiasa ya Dk. Slaa yenye kila aina ya utata na alama nyingi za kuuuliza, safari hiyo ni ile ya kutoka kwenye kuta za seminari, altare ya Bwana, upadre, katibu wa baraza la maaskofu , ubunge wa karatu mpaka sasa anapowania urais kwa tiketi ya CHADEMA.
Naomba nitoe mifano halisi ili nieleweke, kwanza mimi mwenyewe nimesoma seminari ndogo ya Mtakatifu Maria visiga ya jimbo kuu la Dar es salaam kwa miaka minne (2004-2007).
Nilipokuwa seminarini hapo kwa kawaida walezi wetu walikuwa kila mmoja wetu iwapo kweli ana wito wa upadre au la, na iwapo ilibainika kwa hukuwa au matendo hayaendani na wito huo mtakatifu hakukuwa na subira isipokuwa kuondolewa seminarini sio hivyo tu ulipofika mda wa kuhitimu kidato cha nne kwa kawaida kulikuwa fomu maalumu za kujaza iwapo kweli unawito wa upadre au hapana na ili swala hilo lifanyike kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kulikuwa na sala maalumu iliyoongozwa na baba wa kiroho (spiritual father) kwaajili ya kumwomba Mungu ili amjalie kila mmoja wetu kutambua wito wake na hivyo kujaza fomu hizo kwa umakini na muongozo wa Roho Mtakatifu na ni matumaini yangu kuwa hata wakati wa kuhitimu kidato cha sita utaratibu ni huohuo na hata baada ya kuwa frateri na shemasi kuelekea upadre fomula ni hiyohiyo ya kumwomba Roho Mtakatifu akusaidie (mseminari) kutambua wito wako.
Sasa kwa mazingira haya sijui Lula ana la kujibu kuhusu Dk. Slaa? Kwa maana Dk. Slaa alipitia hatua hizi na kote huko aliongozwa na Roho Mtakatifu kufanya uamuzi wake na mpaka akafikia kwenye sakramenti takatifu (isiyofutika) ya upadre. Sasa kinachotutatiza wengi ni swala la Dk. Slaa kutoka kwenye wito wake wa upadre na kuingia kwenye siasa, hapa kuna maswali kadhaa ya msingi ya kujiuliza ; kwanza kwa kuacha upadre Dk. Slaa anataka kutudhihirishia kuwa alipokuwa seminari alikuwa bendera fata upepo? Mpaka akajikuta ameangukia kwenye upadre pasipo kuwa na wito huo? Au labda Dk. Slaa alidanganywa na Roho Mtakatifu na kujikuta amekuwa padre bila kupenda? Au Dk. Slaa ni mtu wa namna gani basi?
Kama ni kweli Dk. Slaa ni bendera fata upepo basi ni mtu hatari kwa maana kwa uelewa wa kawaida tu raisi mfata upepo hafai kwa maana si ajabu akiwa rais
anaweza kufanya maamuzi kwa kufata upepo na bila shaka ameshaonyesha mwenendo wake huo wa kufata mkumbo, kwa maneno yake mwenyewe Dk. Slaa amesema kuwa hakuwa na lengo la kuwania urais na kwamba alishachukua fomu ya kuwania ubunge wa karatu na ghafla kabadili mawazo na kuingia kwenye kinyanganyiro cha urais kwa kushawishiwa tu na wanachama wa CHADEMA , hii kweli ni ajabu na bila shaka inadhihirisha tabia ya kufata mkumbo ya Dk. Slaa.
Na iwapo alidanganywa na Roho Mtakatifu basi ni mwongo au sio msikivu kwa maana Roho Mtakatifu kamwe hawezi kuwa mwongo, pengine wakati Roho Mtakatifu alimfunulia Dk. Slaa kuwa upadre haukuwa wito wake yeye hakuwa msikivu alikuwa mkadi na hivyo alingangania na baadae upadre ukamshinda na ule methali maarufu ya asiyesikia la mkuu ..huvunjika guu imemtokea Dk. Slaa.
Sasa Lula ilibidi ajibu hoja hizi na sio kujikanyaga kanyaga kwenye makala yake ile ambayo kimsingi haikulenga kuchambua kwa mantiki hoja hizi badala yake ilikuwa makala ya kisiasa iliyolenga kumpigia debe Dk. Slaa, kwa kweli sikutegemea na kamwe sitaki kuamini kuwa makala ile iliandikwa na mwandishi wa viwango vya Lula labda siye yeye, pengine labda Lula alikuwa hayupo kwenye hali yake ya kawaida alikuwa anaumwa ladda kwa maana nilitegemea makala ile iandikwe na mkurugenzi wa propaganda wa CHADEMA (kama yupo) na sio mwandishi wa ubora wa Lula.
Lula alipaswa ajibu hoja za msingi kama vile kwa nini Dk. Slaa hana msimamo? Na je tukimpa urais hatokuwa na maamuzi legelege ya kufata mkumbo? Au hataendeleza tabia yake ya kutokuwa msikivu au mkaidi? Lula anapaswa ajue kuwa kuhoji maswali haya sio kumpinga Dk. Slaa bali kiu ya kujiridhisha kwa maana uraisi sio lele mama . Tunahitaji mtu makini ambaye ana utashi mkubwa wa kisiasa na mwenye kufikiri kwa mantiki na kuamua kwa hoja nzito na zenye mashiko na sio maamuzi legelege ya kufata mkumbo.
Lula alipaswa aende mbali zaidi kwa kuhusanisha hulka ya Dk. Slaa kutokuwa na msimamo na swala la padre huyo kuvunja viapo vyake vya upadre iwe kwa ruhusa ya Vatican au la? Kwanini Dk. Slaa ameoa na ana watoto wawili kinyume na maadili ya wito wake ambao yeye mwenyewe aliukubali pasipo kulazimishwa? Je yeye ni mwasi? Na je iwapo atabahatika kuingia kwenye kuta za magogoni hataasi kwa maana ya kutofata katiba ipasavyo kama alivyoasi kwenye kanisa katoliki?
Haya ni maswali ambayo Lula alipaswa kuyajibu kwa hoja moja baada ya lingine.
Kwa faida ya wasomaji wake Lula alipaswa kulitazama kiundani swala la hivi karibuni la Dk. Slaa kuachana na mkewe na kuoa mke mwingine, je lina uhusano na hulka yake ya kufata mkumbo au kufanya maamuzi legelege, je mwanzoni alifata mkumbo kumwoa mke wa kwanza na sasa amebadili uamuzi?
Pengine hapa mtu anaweza kuja na hoja kuwa Dk. Slaa ni mtu makini ambaye anajirekebisha haraka na kuchukua hatua au kwanini hoja za udhaifu wa Dk. Slaa zinajitokeza sasa hivi? Kwanini hazikuwepo alipokuwa mbunge wa karatu?. Labda nitoe angalizo kuwa hata kama Dk. Slaa ana tabia ya kujirekebisha haraka bado hafai kwa maana kuwa rais wa nchi sio sawa na kuwa class-monitor kwa maana kama Dk. Slaa ni mtu wa namna hiyo basi tujiandae na rais mkoseaji kila siku na wapiga kura wa Tanzania wajue kwamba nchi inahitaji maamuzi makini na sio kukoseakosea kwa maana kuna mambo mengine ambayo yakikosewa hata mara moja tu basi ni angamizo la taifa zima (one mistake one goal).
Pili Lula inabidi atambue kuwa kuna kila sababu ya kuhoji uimara wa Dk. Slaa na vilevile ni haki kabisa hoja hizi kuibuka wakati huu kwa maana raisi ni kiongozi mkuu wa nchi tofauti na mbunge ambaye ni mwakilishi wa jimbo lake (na hapa naomba nisieleweke vibaya kuwa natetea wabunge legelege), raisi akiboronga athari zake ni kubwa (tramendous effects) na zina uzito mkubwa sana tofauti na mbunge
akiboronga ingawaje kuboronga ni kuboronga na dhambi ni dhambi tu.
Lula inapaswa atambue kuwa Dk. Slaa hivi sasa anawahusu watanzania wote na sio wana karatu pekee hivyo tuna kila sababu ya kujiridhisha naye na anapaswa atoe ufafanuzi wa kina ili aeleweke na umma wa watanzania na sio kutoa majibu mepesi mepesi kwa hoja nzito kama alivyofanya Lula kwenye makala yake.
Mwishowe Lula anapaswa atambue kuwa uimara wa Dk. Slaa kamwe hauletwi na mifano ya watu ambao waliwahi kuwa mapadre na mwishowe kuukwaa urais, hapa nakusudia kusema kuwa hoja hizi kumhusu Dk. Slaa hazikupaswa kujibiwa kwa orodha ya mifano ya mapadre waliowahi kuwania urais au kuupata urais mifano hiyo ni pamoja na padre Edd Panlilio wa Ufilipino au Askofu Ferdando Lugo wa San Pedro Paraguay. Orodha hii aliyoitoa Lula haina maana yoyote na wala haitoi ufumbuzi kwa hoja na maswali yenye utata yanayomuhusu Dk. Slaa bali Lula anapaswa azijibu hoja hizi nzito na kuzitolea ufafanuzi wa kina ambao utaeleweka kwa wapiga kura wote wa Tanzania.
Mwandishi wa makala hii anajulikana kama Novatus .S. Kambota (Mwanamapinduzi), yeye ni msomaji wa Raia Mwema pia ni mhitimu wa kidato cha sita wa sekondari ya Ilboru, kwa hivi sasa nimwanaharakati wa mazingira wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Jitume Environmental Society (JES) ya Kiwalani Dar es salaam na vilevile ni mwanachama wa mtandao wa kijamii unojihusisha na uchambuzi wa maswala mbalimbali ya kisiasa unaojulikana kama Taifa Huru Tanzania.
Anapatikana kwa namba 0717-709618 au 0783-610926 au waweza kumwandikia kwa anwani ya barua pepe ; novakambota@gmail.com