Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,998
mtumwitu, hili la Ukraine ni kilele cha uzembe na kutokuwajibika! Unaweza kupanga vipi kuwasaidia watu milioni 38 wakati watu 29 umeshindwa? Utaweza vipi kujenga mazingira ya kuondoa umasikini wa familia milioni mbili wakati familia 29 umeshindwa? Mtumwitu, kuweza kubuni mbinu za kutatua matatizo makubwa ni lazima uweze kubuni mbinu za kuweza kutatua matatizo madogo. Asiyeweza kusiba ufa, ataweza kweli kujenga ukuta?
Ni jambo moja kusema maneno ya matumaini na ahadi za mbingu, ni jambo jingine kabisa kutenda! Binafsi ningekuwa impressed kweli kwamba kweli Rais ni mtu wa watu kama mara moja angeamua kuingilia kati au kuamuru utatuzi wa jambo hili bila ya kuliacha libishaniwe hadharani.
Asiyeweza kuaminiwa kwa kitu kidogo, anaweza kuaminiwa kwa kitu kikubwa?
Ni jambo moja kusema maneno ya matumaini na ahadi za mbingu, ni jambo jingine kabisa kutenda! Binafsi ningekuwa impressed kweli kwamba kweli Rais ni mtu wa watu kama mara moja angeamua kuingilia kati au kuamuru utatuzi wa jambo hili bila ya kuliacha libishaniwe hadharani.
Asiyeweza kuaminiwa kwa kitu kidogo, anaweza kuaminiwa kwa kitu kikubwa?