Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,865
- 12,297
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, sasa ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu wana JF kabla ya kuandika list ya wachezaji bora wa muda wote wa timu za Yanga na Simba, ningependa kwanza nijitambulishe kuwa mimi ni mshabiki mkubwa sana wa timu ya Yanga. Nimeanza kuipenda Yanga toka nilipoanza kupata akili na mpaka leo sijawahi kubadilisha msimamo wangu huo, pamoja na changamoto zote tunazozipitia na tulizozipitia huko nyuma. Nakumbuka miaka ya 90s kila time ilikuwa na tawi lake mtaani. Kwahiyo ilikuwa ni kawaida timu ya Yanga inapoifunga Simba, basi wana Yanga wote tunatoka katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es salaam, na kukimbilia Jangwani kuwapokea wachezaji wetu, huku tukiimba nyimbo mbali mbali za kuwasifu wachezaji wetu na timu yetu. Hivyo hivyo kwa upande wa Simba, walipopata ushindi wao dhidi ya Yanga, wana Simba nao walitoka katika maeneo mbali mbali ya jiji na kuelekea Msimbazi kuilaki timu yao. Kwahiyo naweza kusema kwangu mimi hakuna kipindi kilichokuwa kitamu kwa furaha ya michezo kama kipindi hicho. Hapa chini naweka kikosi kazi cha wachezaji wa Yanga ambao walikuwa tishio sana miaka hiyo. 1) Goli kipa- Steven Nemes, huyu hakuna mtu wa miaka hiyo, asiejua kazi kubwa aliyoifanya kwa timu ya Yanga pamoja na timu yetu ya Taifa (jamaa utahisi alikuwa na simaku mikononi kwa jinsi alivyoivuta mipira mikononi mwake). 2) Difenda- Mwanamtwa Kihwelo, huyu kumpita ilikuwa ni kazi ngumu sana kwa vile alikuwa na akili ya kile anachokifanya uwanjani (kwake yeye ilikuwa ni bora mpira upite ila mchezaji abaki, au mchezaji akipita basi mpira utabaki) 3) Keneth Mkapa, mkongwe halisi na moto wa kuotea mbali ambae hajawahi kutoa boko au kuharibu mpira hata siku moja (mkapa hata timu za nje zilikuwa zinamhofia sana, kutokana na umahiri mkubwa wa uchezaji wake). 4) Midfielders- Sanifu Lazaro, ukipenda mwite Mwiba (sifa zake hazina shaka kiuchezaji). 5) Thomas Kipese, winga machachari ya kushoto (ilikuwa ukimpa pasi anatembea na mpira mdogo mdogo, maana wachezaji wa timu pinzani walikuwa wanaogopa kumfuata asiwadhalilishe kwa kanzu au tobo. 6) Salvatory Edward, mzee wa pasi to pasi. 7) Nico Bambaga, kichoteo (yani alikuwa akishika mpira anauchota tu mpaka kwa mfungaji, sasa hapo inabaki kazi ya mfungaji, afunge au atoe nje) 8) Forwards- Salumu Kabunda, tingatinga (jamaa alikuwa kajaa kama mzee wa "GYM" afu misuli iliyokakamaa kiasi kwamba ukipigana nae bambi lazima utoke nje ukapokee matibabu) 9) Shaban Nonda (Mkongo), huyu nae hakuwa nyuma katika kufanya kile kilichompeleka uwanjani. 10) Saidi Mwamba Kizote, mzee wa kunyakuwa (alikuwa na uwezo wa kunyakua mpira juu ya kichwa cha mtu kupitia miguu yake mirefu tena bila kumgusa aliechukuliwa mpira) kwa ufungaji pia alikuwa tishio, George Weah hatosahau siku aliyopigwa tobo na baadae kanzu na mzee huyu wa kiminyio. wengi tulimfananisha na Rivaldo wa Brazil. 11) Edibilly Jonas Lunyamila, huyu hata ukienda Rwanda, Congo, Burundi, Zambia, Kaburu na kwengineko wanamfahamu fika kwa umahiri wake wa kutambaa na mpira hasa pembezoni mwa chaki, (mabeki walikuwa wanasakiziana kumfuata) na yeye alitumia mwanya huo kufanya yake, kwa kufunga magoli mengi. Nikija upande wa Simba naweza kusema wachezaji wao wengi nimewasahau ila kuna baadhi nawakumbuka kama vile 1) Goli kipa- Mohammed Mwameja, Tanzania one (huyu aliisaidia sana Simba na Taifa Stars, mpaka kuna watu walihisi labda jamaa ana mikono mingine pemben ya akiba) 2) Difender- Alphonsi Modest. 3) Husein Marsha. 4) Forwards kuna- Dua Saidi. 5) Madaraka Selemani, "mzee wa kiminyio" , yani alikuwa anatisha kama anaenda mbele afu anauminya mpira, beki anajikuta kapitiliza mzima mzima afu yeye anamua atoe pasi au aendelee na mpira akafunge. Hao ni baadhi ya wachezaji hodari na mahiri wa timu hizo wa muda wote. Ila kama kuna mdau mungine aliekuwa anafatilia timu hizi, na michezo kwa ujumla anaweza akaongeza wengine tuliowasahau kutoka hata timu zingine kongwe za miaka hiyo. Karibuni. Mods ndugu zangu, tafadhalini naomba uzi huu muuache ujitegemee ili kuweka kumbukumbu nzuri.