Kwangu mimi hawa ndio wachezaji bora wa muda wote kwa timu za Yanga na Simba na Taifa Stars miaka ya 90s, wewe je?

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,865
12,297
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, sasa ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu wana JF kabla ya kuandika list ya wachezaji bora wa muda wote wa timu za Yanga na Simba, ningependa kwanza nijitambulishe kuwa mimi ni mshabiki mkubwa sana wa timu ya Yanga. Nimeanza kuipenda Yanga toka nilipoanza kupata akili na mpaka leo sijawahi kubadilisha msimamo wangu huo, pamoja na changamoto zote tunazozipitia na tulizozipitia huko nyuma. Nakumbuka miaka ya 90s kila time ilikuwa na tawi lake mtaani. Kwahiyo ilikuwa ni kawaida timu ya Yanga inapoifunga Simba, basi wana Yanga wote tunatoka katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es salaam, na kukimbilia Jangwani kuwapokea wachezaji wetu, huku tukiimba nyimbo mbali mbali za kuwasifu wachezaji wetu na timu yetu. Hivyo hivyo kwa upande wa Simba, walipopata ushindi wao dhidi ya Yanga, wana Simba nao walitoka katika maeneo mbali mbali ya jiji na kuelekea Msimbazi kuilaki timu yao. Kwahiyo naweza kusema kwangu mimi hakuna kipindi kilichokuwa kitamu kwa furaha ya michezo kama kipindi hicho. Hapa chini naweka kikosi kazi cha wachezaji wa Yanga ambao walikuwa tishio sana miaka hiyo. 1) Goli kipa- Steven Nemes, huyu hakuna mtu wa miaka hiyo, asiejua kazi kubwa aliyoifanya kwa timu ya Yanga pamoja na timu yetu ya Taifa (jamaa utahisi alikuwa na simaku mikononi kwa jinsi alivyoivuta mipira mikononi mwake). 2) Difenda- Mwanamtwa Kihwelo, huyu kumpita ilikuwa ni kazi ngumu sana kwa vile alikuwa na akili ya kile anachokifanya uwanjani (kwake yeye ilikuwa ni bora mpira upite ila mchezaji abaki, au mchezaji akipita basi mpira utabaki) 3) Keneth Mkapa, mkongwe halisi na moto wa kuotea mbali ambae hajawahi kutoa boko au kuharibu mpira hata siku moja (mkapa hata timu za nje zilikuwa zinamhofia sana, kutokana na umahiri mkubwa wa uchezaji wake). 4) Midfielders- Sanifu Lazaro, ukipenda mwite Mwiba (sifa zake hazina shaka kiuchezaji). 5) Thomas Kipese, winga machachari ya kushoto (ilikuwa ukimpa pasi anatembea na mpira mdogo mdogo, maana wachezaji wa timu pinzani walikuwa wanaogopa kumfuata asiwadhalilishe kwa kanzu au tobo. 6) Salvatory Edward, mzee wa pasi to pasi. 7) Nico Bambaga, kichoteo (yani alikuwa akishika mpira anauchota tu mpaka kwa mfungaji, sasa hapo inabaki kazi ya mfungaji, afunge au atoe nje) 8) Forwards- Salumu Kabunda, tingatinga (jamaa alikuwa kajaa kama mzee wa "GYM" afu misuli iliyokakamaa kiasi kwamba ukipigana nae bambi lazima utoke nje ukapokee matibabu) 9) Shaban Nonda (Mkongo), huyu nae hakuwa nyuma katika kufanya kile kilichompeleka uwanjani. 10) Saidi Mwamba Kizote, mzee wa kunyakuwa (alikuwa na uwezo wa kunyakua mpira juu ya kichwa cha mtu kupitia miguu yake mirefu tena bila kumgusa aliechukuliwa mpira) kwa ufungaji pia alikuwa tishio, George Weah hatosahau siku aliyopigwa tobo na baadae kanzu na mzee huyu wa kiminyio. wengi tulimfananisha na Rivaldo wa Brazil. 11) Edibilly Jonas Lunyamila, huyu hata ukienda Rwanda, Congo, Burundi, Zambia, Kaburu na kwengineko wanamfahamu fika kwa umahiri wake wa kutambaa na mpira hasa pembezoni mwa chaki, (mabeki walikuwa wanasakiziana kumfuata) na yeye alitumia mwanya huo kufanya yake, kwa kufunga magoli mengi. Nikija upande wa Simba naweza kusema wachezaji wao wengi nimewasahau ila kuna baadhi nawakumbuka kama vile 1) Goli kipa- Mohammed Mwameja, Tanzania one (huyu aliisaidia sana Simba na Taifa Stars, mpaka kuna watu walihisi labda jamaa ana mikono mingine pemben ya akiba) 2) Difender- Alphonsi Modest. 3) Husein Marsha. 4) Forwards kuna- Dua Saidi. 5) Madaraka Selemani, "mzee wa kiminyio" , yani alikuwa anatisha kama anaenda mbele afu anauminya mpira, beki anajikuta kapitiliza mzima mzima afu yeye anamua atoe pasi au aendelee na mpira akafunge. Hao ni baadhi ya wachezaji hodari na mahiri wa timu hizo wa muda wote. Ila kama kuna mdau mungine aliekuwa anafatilia timu hizi, na michezo kwa ujumla anaweza akaongeza wengine tuliowasahau kutoka hata timu zingine kongwe za miaka hiyo. Karibuni. Mods ndugu zangu, tafadhalini naomba uzi huu muuache ujitegemee ili kuweka kumbukumbu nzuri.
 
Simba tu (3-4-3)
1.Juma kaseja
2.Shomary kapombe
3.Pawasa
4.Yondani
5.Wawa
6.Matola
7.Okwi
8.Boban
9.Ema Gabriel
10.Chama
11.Mogela.


Yanga 4-4-2

Mapunda
Nsajigwa
Maftah
Canavaro
Ken mkapa
Fredy Mbuna
Abdi kasimu
Ngasa
Tabwe
Makambo
Said maulid


Nb,sijasoma umeandika vibaya
 
Simba tu (3-4-3)
1.Juma kaseja
2.Shomary kapombe
3.Pawasa
4.Yondani
5.Wawa
6.Matola
7.Okwi
8.Boban
9.Ema Gabriel
10.Chama
11.Mogela.


Yanga 4-4-2

Mapunda
Nsajigwa
Maftah
Canavaro
Ken mkapa
Fredy Mbuna
Abdi kasimu
Ngasa
Tabwe
Makambo
Said maulid


Nb,sijasoma umeandika vibaya
Kwa upande wa Simba wengine ni- Daniel Kimti, Mathias Mulumba, Shabani Ramadhani list ni ndefu. Kwa yanga- Issa Athumani, Goldwin Aswile, Athumani China, Abeid Mziba na wengine wengi list inaendelea....
 
Simba tu (3-4-3)
1.Juma kaseja
2.Shomary kapombe
3.Pawasa
4.Yondani
5.Wawa
6.Matola
7.Okwi
8.Boban
9.Ema Gabriel
10.Chama
11.Mogela.


Yanga 4-4-2

Mapunda
Nsajigwa
Maftah
Canavaro
Ken mkapa
Fredy Mbuna
Abdi kasimu
Ngasa
Tabwe
Makambo
Said maulid


Nb,sijasoma umeandika vibaya
Kumbe Musa Hassan Mgosi alikua wa kawaida eee?

Alafu kumbe Makambo amefanya makubwa Jangwani kumshinda Jerryson Tegete?
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, sasa ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu wana JF kabla ya kuandika list ya wachezaji bora wa muda wote wa timu za Yanga na Simba, ningependa kwanza nijitambulishe kuwa mimi ni mshabiki mkubwa sana wa timu ya Yanga. Nimeanza kuipenda Yanga toka nilipoanza kupata akili na mpaka leo sijawahi kubadilisha msimamo wangu huo, pamoja na changamoto zote tunazozipitia na tulizozipitia huko nyuma. Nakumbuka miaka ya 90s kila time ilikuwa na tawi lake mtaani. Kwahiyo ilikuwa ni kawaida timu ya Yanga inapoifunga Simba, basi wana Yanga wote tunatoka katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es salaam, na kukimbilia Jangwani kuwapokea wachezaji wetu, huku tukiimba nyimbo mbali mbali za kuwasifu wachezaji wetu na timu yetu. Hivyo hivyo kwa upande wa Simba, walipopata ushindi wao dhidi ya Yanga, wana Simba nao walitoka katika maeneo mbali mbali ya jiji na kuelekea Msimbazi kuilaki timu yao. Kwahiyo naweza kusema kwangu mimi hakuna kipindi kilichokuwa kitamu kwa furaha ya michezo kama kipindi hicho. Hapa chini naweka kikosi kazi cha wachezaji wa Yanga ambao walikuwa tishio sana miaka hiyo. 1) Goli kipa- Steven Nemes, huyu hakuna mtu wa miaka hiyo, asiejua kazi kubwa aliyoifanya kwa timu ya Yanga pamoja na timu yetu ya Taifa (jamaa utahisi alikuwa na simaku mikononi kwa jinsi alivyoivuta mipira mikononi mwake). 2) Difenda- Mwanamtwa Kihwelo, huyu kumpita ilikuwa ni kazi ngumu sana kwa vile alikuwa na akili ya kile anachokifanya uwanjani (kwake yeye ilikuwa ni bora mpira upite ila mchezaji abaki, au mchezaji akipita basi mpira utabaki) 3) Keneth Mkapa, mkongwe halisi na moto wa kuotea mbali ambae hajawahi kutoa boko au kuharibu mpira hata siku moja (mkapa hata timu za nje zilikuwa zinamhofia sana, kutokana na umahiri mkubwa wa uchezaji wake). 4) Midfielders- Sanifu Lazaro, ukipenda mwite Mwiba (sifa zake hazina shaka kiuchezaji). 5) Thomas Kipese, winga machachari ya kushoto (ilikuwa ukimpa pasi anatembea na mpira mdogo mdogo, maana wachezaji wa timu pinzani walikuwa wanaogopa kumfuata asiwadhalilishe kwa kanzu au tobo. 6) Salvatory Edward, mzee wa pasi to pasi. 7) Nico Bambaga, kichoteo (yani alikuwa akishika mpira anauchota tu mpaka kwa mfungaji, sasa hapo inabaki kazi ya mfungaji, afunge au atoe nje) 8) Forwards- Salumu Kabunda, tingatinga (jamaa alikuwa kajaa kama mzee wa "GYM" afu misuli iliyokakamaa kiasi kwamba ukipigana nae bambi lazima utoke nje ukapokee matibabu) 9) Shaban Nonda (Mkongo), huyu nae hakuwa nyuma katika kufanya kile kilichompeleka uwanjani. 10) Saidi Mwamba Kizote, mzee wa kunyakuwa (alikuwa na uwezo wa kunyakua mpira juu ya kichwa cha mtu kupitia miguu yake mirefu tena bila kumgusa aliechukuliwa mpira) kwa ufungaji pia alikuwa tishio, George Weah hatosahau siku aliyopigwa tobo na baadae kanzu na mzee huyu wa kiminyio. wengi tulimfananisha na Rivaldo wa Brazil. 11) Edibilly Jonas Lunyamila, huyu hata ukienda Rwanda, Congo, Burundi, Zambia, Kaburu na kwengineko wanamfahamu fika kwa umahiri wake wa kutambaa na mpira hasa pembezoni mwa chaki, (mabeki walikuwa wanasakiziana kumfuata) na yeye alitumia mwanya huo kufanya yake, kwa kufunga magoli mengi. Nikija upande wa Simba naweza kusema wachezaji wao wengi nimewasahau ila kuna baadhi nawakumbuka kama vile 1) Goli kipa- Mohammed Mwameja, Tanzania one (huyu aliisaidia sana Simba na Taifa Stars, mpaka kuna watu walihisi labda jamaa ana mikono mingine pemben ya akiba) 2) Difender- Alphonsi Modest. 3) Husein Marsha. 4) Forwards kuna- Dua Saidi. 5) Madaraka Selemani, "mzee wa kiminyio" , yani alikuwa anatisha kama anaenda mbele afu anauminya mpira, beki anajikuta kapitiliza mzima mzima afu yeye anamua atoe pasi au aendelee na mpira akafunge. Hao ni baadhi ya wachezaji hodari na mahiri wa timu hizo wa muda wote. Ila kama kuna mdau mungine aliekuwa anafatilia timu hizi, na michezo kwa ujumla anaweza akaongeza wengine tuliowasahau kutoka hata timu zingine kongwe za miaka hiyo. Karibuni. Mods ndugu zangu, tafadhalini naomba uzi huu muuache ujitegemee ili kuweka kumbukumbu nzuri.
Mzee number 8. umetokota, Kabunda hakuwa forward. Kama uliiangalia Yanga ya akina Nonda ktk list yako Mohamed Husen asingekosa
 
Mzee number 8. umetokota, Kabunda hakuwa forward. Kama uliiangalia Yanga ya akina Nonda ktk list yako Mohamed Husen asingekosa
Ya ni kweli mkuu.. nashukuru sana kwa ukumbusho wako. Ila ni muda mrefu sana kwahiyo kuna wachezaji wengine ambao nimewasahau kama Mohammed Husein, na wengine nimesahau hata possession zao uwanjani kama vile Salum Kabunda nk. Shukran sana mkuu 🙏
 
Yanga
1. Hamis Kinye
2. Yusuph Ismail Bana
3 Ahmed Amasha
4. Shomari
5.Isihaka Hassan
6 Juma Mkambi
7. Omar
8. Mkwassa
9. Homa ya Jiji
10 Abeid
11 Hanzuruni " mchawi'

Simba
1 Mahadhi/ Mambo sasa
2. Kiwhelo Mussa
3 Mohamed Kajole
4.
5 Mohamed Bakar Tall
6 Nicodemus Njohole
7
8 Ngulungu
9 Malota
10. Zamoyoni
11 Thuwen Ally
 
Yanga
1. Hamis Kinye
2. Yusuph Ismail Bana
3 Ahmed Amasha
4. Shomari
5.Isihaka Hassan
6 Juma Mkambi
7. Omar
8. Mkwassa
9. Homa ya Jiji
10 Abeid
11 Hanzuruni " mchawi'

Simba
1 Mahadhi/ Mambo sasa
2. Kiwhelo Mussa
3 Mohamed Kajole
4.
5 Mohamed Bakar Tall
6 Nicodemus Njohole
7
8 Ngulungu
9 Malota
10. Zamoyoni
11 Thuwen Ally
Swadakta kabisa mkuu.
 
Habari zenu wana JF wenzangu. Ama baada ya salam, sasa ningependa nijielekeze kwenye mada husika. Ndugu wana JF kabla ya kuandika list ya wachezaji bora wa muda wote wa timu za Yanga na Simba, ningependa kwanza nijitambulishe kuwa mimi ni mshabiki mkubwa sana wa timu ya Yanga. Nimeanza kuipenda Yanga toka nilipoanza kupata akili na mpaka leo sijawahi kubadilisha msimamo wangu huo, pamoja na changamoto zote tunazozipitia na tulizozipitia huko nyuma. Nakumbuka miaka ya 90s kila time ilikuwa na tawi lake mtaani. Kwahiyo ilikuwa ni kawaida timu ya Yanga inapoifunga Simba, basi wana Yanga wote tunatoka katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es salaam, na kukimbilia Jangwani kuwapokea wachezaji wetu, huku tukiimba nyimbo mbali mbali za kuwasifu wachezaji wetu na timu yetu. Hivyo hivyo kwa upande wa Simba, walipopata ushindi wao dhidi ya Yanga, wana Simba nao walitoka katika maeneo mbali mbali ya jiji na kuelekea Msimbazi kuilaki timu yao. Kwahiyo naweza kusema kwangu mimi hakuna kipindi kilichokuwa kitamu kwa furaha ya michezo kama kipindi hicho. Hapa chini naweka kikosi kazi cha wachezaji wa Yanga ambao walikuwa tishio sana miaka hiyo. 1) Goli kipa- Steven Nemes, huyu hakuna mtu wa miaka hiyo, asiejua kazi kubwa aliyoifanya kwa timu ya Yanga pamoja na timu yetu ya Taifa (jamaa utahisi alikuwa na simaku mikononi kwa jinsi alivyoivuta mipira mikononi mwake). 2) Difenda- Mwanamtwa Kihwelo, huyu kumpita ilikuwa ni kazi ngumu sana kwa vile alikuwa na akili ya kile anachokifanya uwanjani (kwake yeye ilikuwa ni bora mpira upite ila mchezaji abaki, au mchezaji akipita basi mpira utabaki) 3) Keneth Mkapa, mkongwe halisi na moto wa kuotea mbali ambae hajawahi kutoa boko au kuharibu mpira hata siku moja (mkapa hata timu za nje zilikuwa zinamhofia sana, kutokana na umahiri mkubwa wa uchezaji wake). 4) Midfielders- Sanifu Lazaro, ukipenda mwite Mwiba (sifa zake hazina shaka kiuchezaji). 5) Thomas Kipese, winga machachari ya kushoto (ilikuwa ukimpa pasi anatembea na mpira mdogo mdogo, maana wachezaji wa timu pinzani walikuwa wanaogopa kumfuata asiwadhalilishe kwa kanzu au tobo. 6) Salvatory Edward, mzee wa pasi to pasi. 7) Nico Bambaga, kichoteo (yani alikuwa akishika mpira anauchota tu mpaka kwa mfungaji, sasa hapo inabaki kazi ya mfungaji, afunge au atoe nje) 8) Forwards- Salumu Kabunda, tingatinga (jamaa alikuwa kajaa kama mzee wa "GYM" afu misuli iliyokakamaa kiasi kwamba ukipigana nae bambi lazima utoke nje ukapokee matibabu) 9) Shaban Nonda (Mkongo), huyu nae hakuwa nyuma katika kufanya kile kilichompeleka uwanjani. 10) Saidi Mwamba Kizote, mzee wa kunyakuwa (alikuwa na uwezo wa kunyakua mpira juu ya kichwa cha mtu kupitia miguu yake mirefu tena bila kumgusa aliechukuliwa mpira) kwa ufungaji pia alikuwa tishio, George Weah hatosahau siku aliyopigwa tobo na baadae kanzu na mzee huyu wa kiminyio. wengi tulimfananisha na Rivaldo wa Brazil. 11) Edibilly Jonas Lunyamila, huyu hata ukienda Rwanda, Congo, Burundi, Zambia, Kaburu na kwengineko wanamfahamu fika kwa umahiri wake wa kutambaa na mpira hasa pembezoni mwa chaki, (mabeki walikuwa wanasakiziana kumfuata) na yeye alitumia mwanya huo kufanya yake, kwa kufunga magoli mengi. Nikija upande wa Simba naweza kusema wachezaji wao wengi nimewasahau ila kuna baadhi nawakumbuka kama vile 1) Goli kipa- Mohammed Mwameja, Tanzania one (huyu aliisaidia sana Simba na Taifa Stars, mpaka kuna watu walihisi labda jamaa ana mikono mingine pemben ya akiba) 2) Difender- Alphonsi Modest. 3) Husein Marsha. 4) Forwards kuna- Dua Saidi. 5) Madaraka Selemani, "mzee wa kiminyio" , yani alikuwa anatisha kama anaenda mbele afu anauminya mpira, beki anajikuta kapitiliza mzima mzima afu yeye anamua atoe pasi au aendelee na mpira akafunge. Hao ni baadhi ya wachezaji hodari na mahiri wa timu hizo wa muda wote. Ila kama kuna mdau mungine aliekuwa anafatilia timu hizi, na michezo kwa ujumla anaweza akaongeza wengine tuliowasahau kutoka hata timu zingine kongwe za miaka hiyo. Karibuni. Mods ndugu zangu, tafadhalini naomba uzi huu muuache ujitegemee ili kuweka kumbukumbu nzuri.
Kama walikuwa ni moto wa kuotea mbali kwanini hawakuwahi kuchukua taji lolote kubwa ndani ya Africa? na kwanini hawakuweza kufanya vizuri kwenye timu ya Taifa zaidi ya kufuzu Afcon mara Moja na kuondolewa Kwenye hatua za mwanzo Mimi naona wahenga hao wachezaji mna wakuza Sana tofauti na uhalisia ninachoamini Mimi soka la Tanzania halijawahi kuwa na maajabu yoyote zaidi ya kukuzwa kwenye vyombo vya habari na mashabiki
 
Salum Kabunda Ninja alikuwa beki sio forward, list yako haitakamilika usipowataja Constantine Kimanda na marehemu Method Mogela
 
Hizi ni enzi nimeshakata shauri kufuatilua mpira, nilikua shabiki wa Yanga kupitiliza Hadi walipofungwa Kwa penalties Zanzibar usiku. David Mwakalebela alikosa penalty akaipa Simba ushindi.

Bila kujali timu walizichezea, Hawa jamaa walivuma enzi hizo.

Sanifu Lazaro ( Tingisha)
Said Swed hii ilijulikana kama scud
Makumbu Juma
Hamiss Thobias Gagarino
Said Mwamba Kizota
Thomas Kipese (Uncle Tom)
 
Back
Top Bottom