Wachezaji wanaoachwa na Yanga wakikutana wanaikamia Yanga tofauti na wale wa Simba

bryan2

JF-Expert Member
Jun 8, 2016
3,323
4,667
Kumekucha tena ni siku nyingine nzuri, wengi wanapenda kutumia hii kauli Soka letu tunalifahamu wenyewe au soka letu kivyetu vyetu.

Nimetizama mechi kadhaa za Yanga nakugundua pindi Yanga inapokutana na wachezaji iliowaacha na kwenda timu nyingine timu hizo wakikutana na Yanga wale wachezaji mwanzo mwisho ni kukaza.

Rejea mchezo wa Mashujaa hiyo jana Golikipa Johora alikua yupo radhi kufia kiwanjani ila Yanga isipite goli tu, angalia gemu na Namungo golikipa Dida Munishi alimwaga mchozi kabisa baada ya kufungwa pamoja na Pius Buswita aliyecheza Jihad mwanzo mwisho na mwenzake Domayo.

Mifano ni Mingi swali la kujiuliza je wanataka kuwaonyesha Yanga walifanya makosa kuwaacha au yanakua ni maelekezo kutoka kwa makocha wao.

Njoo sasa upande mwingine pale Simba asilimia kubwa ya wachezaji wanaoachwa na Simba wakienda upande mwingine ni ka vile bado wanakua wanatumika na Simba kuhujumu hizo timu rejea penalti ya Kagere na Singida Utd Kombe la mapinduzi jamaa ni kama alimpa mpira kipa, pia kipindi cha nyuma mchezaji Ulimboka aliwahi kushutumiwa kutumika kuwapa wachezaji wa timu pinzani mlungula ili waachie ushindi kwa Simba.

Sio wachezaji tu hata makocha rejea kocha wa Tabora Utd mserbia Karpunovic naye alipita Simba ajabu anashangaa na kusema kuna matukio yalitokea ndani ya masaa 24 kuonyesha kwamba kulikua na viashiria vya rushwa kwa wachezaji wake na kubaki kulalamikia nyasi ndefu wakati uwanja ni wao kila siku.
 
Kumekucha tena ni siku nyingine nzuri, wengi wanapenda kutumia hii kauli Soka letu tunalifahamu wenyewe au soka letu kivyetu vyetu.
a Utd mserbia Karpunovic naye alipita Simba ajabu anashangaa na kusema kuna matukio yalitokea ndani ya masaa 24 kuonyesha kwamba kulikua na viashiria vya rushwa kwa wachezaji wake na kubaki kulalamikia nyasi ndefu wakati uwanja ni wao kila siku.
Johora yuko sahihi maana si mchezaji wa Yanga bali Mashujaa. Amesajiliwa ili Mashujaa isifungwe na timu yoyote.
 
Jamaa unatapatapa.Kwanza walikuwa TFF,mara ratiba sasa wachezaji waliohama Yanga.Ulitaka walegeze?Mpira wa kwenye vikao vya kahawa. Wacha ushamba.Vipi Songwe Airport imehama Mbeya?
 
Hapana mkuu, mapumziko ya AFCON, wachezaji wetu binafsi naona walijiachia sana inaonyesha....wanajitafuta sana ,viwango vimeshuka kidogo.Pia nahisi Kocha wetu bado hajajua kuwatumia baadhi ya wachezaji
Naheshimu sana wapenzi kama wewe.Hamna visingizio vya kitoto. Ndio ukomavu huo. Bravo.
 
Kumekucha tena ni siku nyingine nzuri, wengi wanapenda kutumia hii kauli Soka letu tunalifahamu wenyewe au soka letu uhujumu hizo timu rejea penalti ya Kagere na Singida Utd Kombe la mapinduzi jamaa ni kama alimpa mpira kipa, pia kipindi cha nyuma mchezaji Ulimboka aliwahi kushutumiwa kutumika kuwapa wachezaji wa timu pinzani mlungula ili
Akuna lolote hapo kinachoisumbua yanga kwa sasa ni kukosa match fitness baada ya mapumziko ya mda mrefu kwa wachezaji wake hasa hasa wale wa kikosi Cha kwanza kwa maana ni Kama wanaoanza upya wakati huo huo wametoka kwenye mazoezi mazito miili bado aijafunguka ndio maana Kuna mda wanashindwa kufanya maamuzi ya haraka kwenye matukio muhimu!

Wataendelea kufunguka kadri watakavyokuwa wanacheza mechi bahati nzuri wanakusanya alama licha ya shida iliyopo na nafasi wanatengeneza nyingi tu kwa maana iyo ni suala la muda tu watarudi kwenye ubora wao!

Sababu hizo za kiufundi ndio zinafanya Aya yaliyopo na sio habari za kukamiwa kwa sababu Kama wanakamia mbona nafasi zinatengenezwa nyingi za kufunga licha ya wapinzani kukaa nyuma ya mpira mda mwingi?

Wafungaji ndio bado tatizo presha ya kufunga na utayali wa miili yao kufanya maamuzi ya haraka kwenye 18 ya mpinzani ndio vinawatafuna akuna kingine!
 
Hapana mkuu, mapumziko ya AFCON, wachezaji wetu binafsi naona walijiachia sana inaonyesha.... wanajitafuta sana, viwango vimeshuka kidogo. Pia nahisi Kocha wetu bado hajajua kuwatumia baadhi ya wachezaji.

Hii ndo kweli hata ukiangalia simba wanacheza lakini kwa kusua sua saana ile ball itembee haipo ni butua butua
 
Hii ndo kweli hata ukiangalia simba wanacheza lakini kwa kusua sua saana ile ball itembee haipo ni butua butua
Kwa teams hizi zetu,kumuacha mchezaji huru wiki tu,hafanyi programs alizopewa.... wachezaji wetu ni semi- professional hawawezi kujisimamia, ndiyo maana kambi zinakuwa mara kwa mara cos hawawezi kujitunza,na umaarufu wao kila wanapopita offers za vilevi, wanawake kuwakimbilia ni changamoto
 
Kumekucha tena ni siku nyingine nzuri, wengi wanapenda kutumia hii kauli Soka letu tunalifahamu wenyewe au soka letu kivyetu vyetu.

Nimetizama mechi kadhaa za Yanga nakugundua pindi Yanga inapokutana na wachezaji iliowaacha na kwenda timu nyingine timu hizo wakikutana na Yanga wale wachezaji mwanzo mwisho ni kukaza.
Utaropoka sana leo kama umekunywa maji ya chooni na bado utavua nguo kabisa
 
Kwa teams hizi zetu,kumuacha mchezaji huru wiki tu,hafanyi programs alizopewa.... wachezaji wetu ni semi- professional hawawezi kujisimamia, ndiyo maana kambi zinakuwa mara kwa mara cos hawawezi kujitunza,na umaarufu wao kila wanapopita offers za vilevi, wanawake kuwakimbilia ni changamoto
Nimekuelewa sana mkali.
 
Hahahaa Mzee upaniki sana au bado zile tano zipo kwa Oblangata nini
Wewe ndiye umepaniki unaanzisha nyuzi za kiwendawazimu,hivi unavyosema kukamia una maana gani? Timu yoyote inapoingia uwanjani inakamia ili kupata ushindi.
 
Kwa Rage rejea kauli ya Rage mashabiki wa Simba ni.....malizia methali hiyo.
Luc Eymael alisema washabiki wa yanga ni nyani
FB_IMG_1707213280656~3.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom