Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,780
- 15,257
Kilichosainiwa na Magufuli ni ngumu sana kukipuuza, jamii itakuzomea mpaka ukome, muulize Makamba alipoleta tantarila kwenye bwawa.Walinyang'anywa Shule zao wakakaa kimya
Walinyang'anywa Hospitali zao wakakaa kimya.
Walinyang'anywa vyuo vyao wakakaa kimya.
Leo waliosoma kwenye shule walizonyang'anywa ndio hao hao wanaosema kuwa maaskofu wanachanganya dini na Siasa.
Wale wale wanaotumia Hospitali za Kanisa badala ya kujenga za umma ndio hao hao wanaosema Kanisa linapendelewa na Serikali kupewa ruzuku ya kuziendeshea Hospitali hizo.
Wanasiasa waliodhulumu mali za Kanisa ndiyo hao hao leo wanawaambia Maaskofu wasichanganye Dini na Siasa.
Anayesema hivyo ni Mwanasiasa Muislam akiwa kwenye madhabahu ya Kanisa.
Yeye kimempeleka nini kanisani wakati siyo mkristo? Siyo yeye ndiye anayepeleka Siasa kanisani?