Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,057
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema. Kama Lowassa aliona CCM wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?

Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Zitto amesema Lowasa alishinda 2015.😂😂😂
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Sasa, kama Lowassa alimwambia Kikwete anataka kujiuzulu, Kikwete akakataa, lakini Lowassa akalazimisha kujiuzulu, huoni Lowassa kajitakia mwenyewe kupigwa chini kwa kulazimisha kujiuzulu?

Ulitegemea vipi Kikwete aendelee ku support mbio za Urais za Lowassa baada ya Lowassa mwenyewe kulazimisha kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond?

Yani ulitaka Kikwete ampigie kampeni ya urais Lowassa aliyeshindwa Uwaziri Mkuu kwa kashfa?

Huoni kwamba Lowassa ndiye aliyemsaliti Kikwete hapo kwa kulazimisha kujiuzulu na kumuachia manyanga Kikwete, wakati labda alihitajika kupambana akiwa upande wa serikali?

Mtu aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu kutokana na msukosuko wa kashfa, unajuaje akipata urais na kupata msukosuko wa kashfa hatajiuzulu tena?

Lowassa alipewa mtihani wa uongozi, akashindwa. Kikwete akaona huyu kashindwa, twende na wengine.

Hata mimi ningemshangaa sana Kikwete kama angempigia kampeni Lowassa kwa sababu ni rafiki yake tu.
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa

Hoja ni kwaajili ya wenye akili timamu, siyo wewe.

Hakuna mahali iliposemwa kuwa Urais ilikuwa ni haki yake Lowasa bali kama umechaguliwa na wananchi, ni haki ya wananchi kuongozwa na mtu waliyemchagua.

Juzi umemsikia Prof. Tibaijuka akisema kwamba alimwambia Lowasa kuwa akigombea kuoitia chama kingine tofauti na CCM kwa mifumo ya nchi ilivyo, hatatangazwa kuwa Rais. Na ndicho alichokifanya Kikwete.
 
Nimeona huko X jamaa wanamuwakia moto huyu mzee, yaani walikuwa wanamsubiri aongee tu waluke naye.

Kuna picha nimeiona kwa karibu mzee anazeeka kwa hatua za haraka sana, mara nyingi dhuruma huwa haipiti hivi hivi, inakutafuna ukiwa hujijui, muangalie yule dokta pale JKIC anavyoliwa!.
 
Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.
It's not necessarily lazima ni JK!, sometimes wahafidhina wana nguvu kuliko rais!, ila mkubwa ni jalala!.
Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.
Ni kweli kwasababu by that JK alikuwa bado ni mjamaa, na EL alikuwa tayari ni bepari!, sasa wote ni mabepari!.
Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.
Sina uhakaki kama makubaliano haya yalikuwepo!, ila kunafanyika vitu vingi ambavyo sio, mfano kutoa fomu moja, kugombea kwa msesereko, kupokezana Mkristo na Muislam.
Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.
Sii kweli, jina la Lowassa lilichinjiwa baharini hata kwenye CC halikujadiliwa, ila akina sisi tuliisha muandaa kisaikolojia Elections 2015 - Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!
Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.
Sii kweli, jina la EL halikutoka hata CC, hivyo halikuingia hata NEC, ule wimbo wa "Tunaimani..." ni uliimbwa NEC! Elections 2015 - Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...
Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.
Sii kweli!, wanaoamua nani awe ngombea wa CCM, sio wana CCM, ni kitu kinachoitwa "the inner circle" angalia tarehe ya bandiko hili Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli
Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.
Sii kweli!, kura zote mpaka za urais zimehesabiwa vituoni na kila msimamizi alipewa copy ya matokeo!, TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia! ila kwa upande wa Zanzibar, kule ndio kweli EL alimbwaga JPM Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda
Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.
Hii sii kweli, Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake! makarateka yalifanywa uchaguzi wa 2020!.
Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.
Sii kweli, ni wahafidhina!, kwa siasa za Zanzibar, ni lazima CCM ishinde for the sake of Muungano!, ukisikia Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote, ushindi wa lazima wa CCM Zanzibar ni moja ya gharama hizo. Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?
Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.
ukitenda wema mwingi kuliko ubaya karma inarekebisha "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!
Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?
Baada ya ushauri huu, Ushauri wa bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya October 25!
Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Amen
 
Sasa, kama Lowassa alimwambia Kikwete anataka kujiuzulu, Kikwete akakataa, lakini Lowassa akalazimisha kujiuzulu, huoni Lowassa kajitakia mwenyewe kupigwa chinibkwa kulazinisha kujiuzulu?

Ulitegemea vipi Kikwete aendelee ku support mbio za Urais za Lowassa baada ya Lowasssa mwenyewe kulazimisha kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond?

Yani ulitaka Kikwete ampigue kamoeni ya uraus Lowassa aliyeshindwa Uwaziri Mkuu kwa kashfa?

Hata mimi ningemshangaa sana Kikwete.
Kashfa ile haikuwa ya Lowasa, ilikuwa kashfa ya Serikali nzima. Lakini Lowasa aliamua kuyabeba makosa ya Serikali nzima ili kuilinda Serikali ya rafiki yake.

Halafu kinavhoongelewa hapa siyo Kikwete kumsaidia Lowasa bali hata baada ya kuacha kumsaidia, bado aliamua kumdhulumu kwa kutumia madaraka ambayo rafiki yake huyo huyo alimsaidia kuyapata.
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
With RESPECT kwako, inaonekana wewe unaishi kule LALA LAND, kama hujui why Lowassa (MHSRIP)alirudi ccm, nikuache tu,kweli mkuu hujui kuwa alilazimishwa kwa kunyimwa haki yake kwa serikali ya ccm kutumia vyombo vya dola,basi wewe ni kenges
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Wote waliohusika na vifo mbalimbali ili kupalilia safari ya ikulu 2005 hawatobaki salama ni suala la muda tuu... Lowassa kalipa kwa sehemu yake na akina Kikwete watalipia pia.....

Kila nikikumbuka kifo cha Nyerere na Omari Ali Juma nasema hiiiii!
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Alaaniwe Jakaya Mrisho Kikwete na uzao wake wote Amen !
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Nakunukuu

"""Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?""""


Vita alivyo pigana JPM ndio vita vilivyo kua vya wana mabadiliko na for sure JOHN POMBE MAGUFULI alimuheshimu sana tena sana EDWARD LOWASSA na hakuwai toa shombo Wala shit zozote Kwa EL

Kama una clip tuwekee hapa

Na ndio maana LOWASSA alipo rudi CCM alisema maneno mawili NIMERUDI NYUMBANI

CCM YA JPM haikua na matatizo na EDWARD LOWASSA

MAGUFULI akiwa raisi aliwai kumkimbilia kumsalimia kaka yake EDWARD LOWASSA na hata kumpa mialiko ya ikulu....
 
Hatari sana, kwahiyo mlitaka JK amsaidie EL kushinda Urais? Eti kwakuwa walikuwa marafiki? Kwahiyo tunaunga mkono Urais kugawiwa kwa minajili ya urafiki?.

EL alikuwa CCM na tabia hizi tunazomsema nazo JK ndio hizi hizi wana CCM wote wanazo, EL aliondoka CCM baada ya kukatwa pale Dodoma, kama alikuwa mwema alipaswa kuikacha CCM toka 1995 na sio kusubiri maslahi yalipokoma.

EL na JK wanajuana kuliko Mimi na wewe tunavyowajua, unapokwenda kumlaumu JK huku humjui EL kiundani nawewe itabidi tukuite mnafiki au mmbeya.

Mwenyezi Mungu ndiye anapanga kifo cha kila mtu na namna gani kitokee.
 
Kashfa ile haikuwa ya Lowasa, ilikuwa kashfa ya Serikali nzima. Lakini Lowasa aliamua kuyabeba makosa ya Serikali nzima ili kuilinda Serikali ya rafiki yake.

Halafu kinavhoongelewa hapa siyo Kikwete kumsaidia Lowasa bali hata baada ya kuacha kumsaidia, bado aliamua kumdhulumu kwa kutumia madaraka ambayo rafiki yake huyo huyo alimsaidia kuyapata.
Sasa kama kashfa haikuwa ya Lowassa, ilikuwa ya serikali nzima, Lowassa kutaka kujiuzulu yeye ni kimbelembele.

Na mtu kimbelembele anaweza kuleta matatizo katika uongozi.

Ni hivi, ingekuwa Kikwete kamtuma Lowassa ajiuzulu, kamwambia "Edward, haya maji ni marefu, inabidi tumtoe mtu hapa ili kuinusuru serikali, tena mtu mzito, nakuomba kama rafiki yangu ujiuzulu ili kuinusuru serikali, halafu hapo baadaye mambo yakipoa, tutakurudisha ugombee urais nikimaliza mimi".

Halafu Lowassa akasema "Kweli? Serikali inaweza kuanguka? Na mimi kujiuzulu kwangu ndiko kutainusuru? Mnanitaka nijiuzulu halafu nitakuwa rais baada yako? Hapo hakuna shida, najiuzulu"

Halafu Lowassa akajiuzulu.

Halafu baadaye, alipotaka kuwa rais, Kikwete akamruka. Akamkata.

Hapo sawa, ungeweza kusema Kikwete mtu jahili na laghai, kamuhadaa mwenzake ajiuzulu, kwa ahadi kuwa atamfanya awe rais, mwenzake akajiuzulu, na urais akamkata.

Lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa maelezo yako, Kikwete hakutaka Lowassa ajiuzulu. Hata Lowassa alivyotaka kujiuzulu, Kikwete alikataa, Lowassa akalazimisha kujiuzulu.

Sasa hapo mpango wa Kikwete wa Lowassa kuendelea kuwa Waziri Mkuu umekataliwa na Lowassa.

Aliyemsaliti mwenzake kati ya Kikwete na Lowassa ni nani hapo?

Na kama Lowassa alikataa mpango wa Kikwete kuendelea kuwa Waziri Mkuu, kwa nini unafikiri ni sawa Kikwete kukubali mpango wa Lowassa kuja kuwa rais?
 
Back
Top Bottom