Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,812
- 59,392
Katika mahusiano zile nafasi watu wanazokua nazo (mchumba,mpenzi,mke,mume) hua zina kutambulika ama kutotambulika, kukubalika ama kutokubalika, kupendwa ama kutokupendwa n.k Hayo ndio hua yanapelekea wahusika aidha kuwa kwenye kurasa moja au mmoja kuonekana analazimisha ama kutotaka/furahia mahusiano yale. Baada ya kufikiria namna ambayo mahusiano ya baadhi yetu hua kutokana na hayo nimejikuta napenda kujua nyie mnaona kipi ni bora kati ya . . . .
I) KUJITAMBUA bila KUTAMBULIKA. . . uko kwenye mahusiano na mtu ambae unamchukulia kama mpenzi, mchumba au hata mume/mke mtarajiwa ilhali yeye anakuona kama mtu wa kupitishia muda tu.
Mtu ambae hata akiulizwa "hivi fulani ni mpenzi/mchumba wako ehhh?!" anajibu "Ahh yule niko nae tu. . AU sio mpenzi wangu yule bwana." hivyo watu wengine nao wanakuchukulia kwamba sio mpenzi/mchumba wa fulani.
II)KUTAMBULIKA KWA WOTE isipokua MHUSIKA MKUU. . . upo kwenye mahusiano/ndoa ambayo inafanya waliopo nje (jamii/ndugu/marafiki) wanakutambua kama mke/mume/mchumba/mpenzi wa fulani wakati muhusika anakuchukulia/anakufanyia tofauti kabisa. Anakunyanyasa, anakudharau, anakupiga, hamna heshima wala mapenzi, hakushirikishi mambo yake au hata 'YENU'. . . yani kiufupi ni kwamba HAKUKUBALI kama mpenzi/mchumba/mume/ mke hivyo HAKUJALI.
III)KUTAMBULIWA na MHUSIKA ila sio na WATU WOTE. . mwenzako anakutambua na kukubali kama mke/ mume/ mchumba/ mpenzi wake na vitendo vyake haviko mbali katika kuthibitisha hilo ila waliopo nje (yaweza kuwa ndugu zake au zako, marafiki au majirani) wanakataa/shindwa kukutambua kama anavyokutambua mhusika.
I) KUJITAMBUA bila KUTAMBULIKA. . . uko kwenye mahusiano na mtu ambae unamchukulia kama mpenzi, mchumba au hata mume/mke mtarajiwa ilhali yeye anakuona kama mtu wa kupitishia muda tu.
Mtu ambae hata akiulizwa "hivi fulani ni mpenzi/mchumba wako ehhh?!" anajibu "Ahh yule niko nae tu. . AU sio mpenzi wangu yule bwana." hivyo watu wengine nao wanakuchukulia kwamba sio mpenzi/mchumba wa fulani.
II)KUTAMBULIKA KWA WOTE isipokua MHUSIKA MKUU. . . upo kwenye mahusiano/ndoa ambayo inafanya waliopo nje (jamii/ndugu/marafiki) wanakutambua kama mke/mume/mchumba/mpenzi wa fulani wakati muhusika anakuchukulia/anakufanyia tofauti kabisa. Anakunyanyasa, anakudharau, anakupiga, hamna heshima wala mapenzi, hakushirikishi mambo yake au hata 'YENU'. . . yani kiufupi ni kwamba HAKUKUBALI kama mpenzi/mchumba/mume/ mke hivyo HAKUJALI.
III)KUTAMBULIWA na MHUSIKA ila sio na WATU WOTE. . mwenzako anakutambua na kukubali kama mke/ mume/ mchumba/ mpenzi wake na vitendo vyake haviko mbali katika kuthibitisha hilo ila waliopo nje (yaweza kuwa ndugu zake au zako, marafiki au majirani) wanakataa/shindwa kukutambua kama anavyokutambua mhusika.