Kuna uhusiano gani kati ya Lowassa na TBC?

Hop it woz
rekoded SHOW!
Lowasa kuongea TBC wala si tatizo. Kilichonishangaza mi labda na wengineo ni kasi aliyotumia kutoka uwanjani mpaka TBC! Kwani dakika tu alikuwa stadium na nguo zake zilezile!. Na mtangazaji aliyemuhoji ameonekana kama kampokelea getini ndipo wakaelekea wote ndani studio(alikuwa anamsubiria getini!?). Tutaona mengi kabla ya 2015!
 
Kwa mahesabu ya haraka haraka,EL lazima agombee urais kwa tiketi ya ccm, sioni wa kumsimamisha kwenye harakati zake hizo.

Keshajipanga, kina Nape kweli hamnazo...Hawatomweza hao labda wahame chama.
 
Weusi ni rangi halisi ya kaniki... Hata ukiifua kwa mashine za kisasa haiwezi kubadilika na kuwa nyeupe abadan.
 
Hata wewe umetumwa nae kwani baba wa taifa alipomkataa alikosea? Si tumekuja kumwona mwenyewe ****** alipompa uwaziri mkuu hata hajakaa fresh kapiga bingo la hatari. Kwahiyo kijana kubali kataa tetea kwa kulipwa jamaa hatufai kwasababu ni fisadi na sio mwadilifu

Umesomeka vizuri saaaana.
 
EL ana mbinu kabambe, kashawateka UVSISIEM na sasa anawaingia waandishi wa habari. Kwakweli bado tuna safari ndefu.
 
Hata uwizi au ufisadi nao ni sifa. Kama sifa hizo ndizo watanzania wanazihitaji kutumia kumpata Rais, basi Lowasa atakuwa...

Wewe raia wa nchi gani? Rais wa TAnzania huchaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM. EL akishapitishwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM basi tayari atakuwa Rais watanzania hawawezi badilisha matakwa ya CCM.
 
Achana na habari zote za ovyoovyo, Lowassa leo amefunguka kuhusu namna ambavyo serikali inaweza kutengeneza ajira kwa vijana akitolea mfano wa Misri walivyokuwa wanafanya kipindi akiwa Waziri wa Maji. Amesema serikali inaweza kukopa na kuanzisha viwanda ambavyo vitatoa ajira kwa vijana wengi au vijana wakakopeshwa zana za kilimo na pesa kwa ajili ya kujiajiri ki ukweli amenivutia sana kwa sehemu hiyo.

Alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 2, kwanini hakufanya hivyo kipindi hicho? Walikuja na "Mabilioni ya JK" na mpaka leo haijulikani yaliishia wapi. Hizo fedha ambazo anasema wangekopeshwa vijana ili wajiajiri kwenye sekta ya kilimo zingeishia mikononi mwa wajanja.

Sera ya serikali kuanzisha viwanda inapingana na sera ya serikali kujitoa kwenye shughuli za uzalishaji. Serikali ikianzisha hivyo viwanda ajira zake zitaenda kwa kujuana na baada ya muda mfupi serikali inakufa.

Hivi hamjiulizi "Mabilioni ya JK" yaliishia wapi? Yalifika vijijini au kwa wamachinga wa Manzese? Bank zilizopewa jukumu la kutoa mikopo hiyo hazina matawi kwenye wilaya, matawi yake yako makao makuu ya mikoa, je, vijana wako mijini tu? Wilayani hakuna vijana?

Nchi hii mpaka tutakapoacha nepotism kwenye ajira na kutoa tender ndipo tutaweza kujikwamua. Viongozi wetu wametawaliwa na ubinafsi na hakuna means za kuwabana, na hata kama sheria zipo bado wale wanaotakiwa kuwashughulikia wanaangalia ni nani wa kumbana. Lowassa na JK wanajadili kwamba ni nani awasaidie kutatua tatizo la Umeme, wao wenyewe wanakwenda kumwomba Rostam Aziz, halafu unategemea tatizo liishe? Maana tender yenyewe imetolewa kishikaji na utekelezaji ni wa kishikaji tu na hata ikishindikana poa tu. Kuna watu wengi sana wamepewa tender na hawakumaliza kazi hizo na wakalipwa fedha yote na bado wanaendelea kupewa tender mpya.

Lowassa anasema serikali ijenge viwanda, kwa umeme upi? Mgao kila kona.
 
Anasisitiza kuwa ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiri muda wake kulipuka!!!

Mtu aliyekosa sera utamuona tu. Lowasa alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, kilimshinda nini kutatua tatizo la ajira kwa vijana hata leo alione ktk mtizamo huu? Kila akipewa jukwaa kuzungumza, basi hana kitu kipya zaidi ya ajira kwa vijana. Kwanini asije na ufumbuzi wa tatizo hilo badala ya kuja na lawama kila siku? Suala la ajira ni tatizo kubwa, sio kwa Tanzania tu, bali dunia nzima, lakini mbona sijawahi kumsikia akitoa mipango mbali mbali ya ufumbuzi wa tatizo hili? Mzee TUMEKUCHOKA, TAFUTA HOJA NYINGINE TUKUSIKILIZE.
 
Kwa mahesabu ya haraka haraka, EL lazima agombee urais kwa tiketi ya ccm, sioni wa kumsimamisha kwenye harakati zake hizo.

Keshajipanga, kina Nape kweli hamnazo...Hawatomweza hao labda wahame chama.

Mimi ninaangalia tu ... maana naona kuna watu wanapigana vita ambayo mpaka sasa kuna dalili zote za kushindwa.

Kwanza, Mwenyekiti wao amepoteza mwelekeo au amewaingiza mjini kwani walihisi wako nae lakini sasa ni dhahiri kwamba yuko upande mwingine au hajulikani yuko upande gani.

Vita ya ufisadi ambayo ndo ilikuwa silaha yao, inaelekea kupoteza kasi. Sasa hivi Nape haongelei tena operation vua gamba na hana ujasiri wa kwenda kwenye mikutano ya hadhara na kuanza kutamba kwamba sasa CCM inapigana vita kikweli kweli maana hatujaona lolote mpaka sasa.

Fisadi anayepigwa vita anapewa coverage kubwa na vyombo vya habari, sasa hivi kila siku atakuwa kwenye TV maana ana nguvu za kutosha na ameishajua ameshinda vita. Yule jamaa ana ujasiri wa kifisadi na amerudi kwa kasi kubwa sana ... Nape ili kuonyesha msimamo wake wa dhati aendelee na CCJ yake au aende CCK.

Ile picha ya Mkutano wa NEC, Lowassa akisalimiana na Nape ilikuwa na tafsiri nyingi sana maana kuna alikuwa yuko poa na mwingine alikuwa amenyong'onyea, na siyo yule aliyekuwa anatamba kwenye majukwaa ya Operation Vua Gamba.
 
Lowassa alistahafu? Ask Membe.....he was sucked.

Mimi nakushauri uwe unatumia kiswahili kama maneno ya kingereza yanakusumbua.Lazima ujifunze kutofautisha kati ya neno 'sucked' na 'sacked'
was sucked =alinyonywa/alifyonzwa
was sacked =alifukuzwa kazi

Kwa hiyo EL was not sucked.NI hayo tuu..be careful Kabembe
 
guys labda nina mtzamo tofauti kwangu mimi EL ndo rais safi 2015 kama 2nataka maendeleo na tamati la ufisadi. Nasema kwa kuwa EL hana aibu na anaweza kuwashkisha adabu mafisadi na watendaji wabovu vile vile kwa kuwa anakashfa ya ufisadi na kama mnavyojua EL anapenda sifa so atataka kuwaonyesha watanzania kuwa alipakaziwa kama anavyodai daily, pia kijana ana uwezo wa kufanya maamuzi magumu ambayo JK hawezi
 
Back
Top Bottom