Elections 2015 Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Mkuu Barbaru, Mtambaza mwenzangu, wewe nione tuu kama unavtoniona kuwa mimi ni Mchadema na huu ndio muona wa Ki ccm zaidi kwa sababu baadhi ya dose zangu zinaichapa bakora CCM, na Chadema nao wananiona mimi ni Msisiem kufuatia kuwaambia ukweli.

Kiukweli from the botom of my heart mimi sina chama, naguzswa na uzalendo, na kiukweli kila Mtanzania mwenye uzalendo wa kweli kwa nchi hii, anawish CCM ipumzishwe, hata wana CCM wazalendo wa ukweli, wanajua chama chao kimechoka, kimelewa madaraka, kimejisahau na kinahitaji mapumziko!.

Kukitarget CCM kama ndie adai is a wrong move, CCM imewekwa na wananchi, tukiwatarget wananchi walioiweka CCM madarakani as our focal point, CCM itapigwa chini jumla!.
Kwa namna ambavyo tumekuwa tukiendesha chaguzi zetu kuu huwezi kusema WANANCHI wamekuwa wakiiweka madarakani CCM. Pasco utakubaliana nami kwamba kwa mfano ulio wazi kabisa CCM haijawahi kushinda uchaguzi wowote kule Zanzibar tangu mfumo wa vyama vingi uanze.
Uchaguzi wa mwaka 1995 Mh Mrema alipata kura nyingi sana. Ni baada ya uchaguzi huu ndipo ile sheria ya kumtangaza mgombea wa Urais kuwa ni mshindi hata kwa "simple majority" ilipopitishwa. Tulishuhudia pia Dr Slaa alivyomhenyesha Kikwete mwaka 2010 hadi JK kudhani ni DINI yake imechangia pia!
ADUI wa kweli kabisa anaweza asiwe CCM peke yake bali hata vyombo vya DOLA ambavyo hadi kesho vinaamini nje ya CCM hatuwezi kumpata RAIS anayetufaa WATANZANIA. Sielewi kama KATIBA MPYA itatusaidiaje katika hili. Kwamba JWTZ, UwT,NEC na vyombo vingine vituache waTanzania tuchaguane kwa haki, uhuru na amani.
 
Mkuu Pasco
Pamoja na changamoto nyingi unazozipata hapa jamvini bado umo tu..well done! nakupa kudos pia kwa hili maana bila mabadiliko ya mawazo na mitindo yetu ya maisha ya bora 'zimwi likujualo' ni ukweli CCM itaendelea kutawala.Wannanchi tumekuwa mstari wa mbele kufanya maamuzi ambayo baadaye tunayajutia simply because tunaogopa mabadiliko ya kiutawala...Naamini pamoja na challenge za hapa bado CDM wataliweka hili katika mikakati yao ya kuchukua nchi come 2015..
 
Kwa namna ambavyo tumekuwa tukiendesha chaguzi zetu kuu huwezi kusema WANANCHI wamekuwa wakiiweka madarakani CCM. Pasco utakubaliana nami kwamba kwa mfano ulio wazi kabisa CCM haijawahi kushinda uchaguzi wowote kule Zanzibar tangu mfumo wa vyama vingi uanze.
Uchaguzi wa mwaka 1995 Mh Mrema alipata kura nyingi sana. Ni baada ya uchaguzi huu ndipo ile sheria ya kumtangaza mgombea wa Urais kuwa ni mshindi hata kwa "simple majority" ilipopitishwa. Tulishuhudia pia Dr Slaa alivyomhenyesha Kikwete mwaka 2010 hadi JK kudhani ni DINI yake imechangia pia!
ADUI wa kweli kabisa anaweza asiwe CCM peke yake bali hata vyombo vya DOLA ambavyo hadi kesho vinaamini nje ya CCM hatuwezi kumpata RAIS anayetufaa WATANZANIA. Sielewi kama KATIBA MPYA itatusaidiaje katika hili. Kwamba JWTZ, UwT,NEC na vyombo vingine vituache waTanzania tuchaguane kwa haki, uhuru na amani.

Mkuu WildCard, mimi naamini katika msemo wa Kilatini usemao "Vox Populi is Vox Dei" ukimaanisha sauti ya watu ni sauti ya Mungu. Ule uchaguzi wa 2010 CCM imeshinda kwa kura milioni 5 tuu hapo ndio kujumlisha na uchakachuaji wote wa NEC, na michango ya ma RC, ma DC maofisa wote wa serikali, vyombo vyote vya dola, na ile mechanisim yao kubwa ya kugawa t-shirt na kofia, na kile kidogo dogo cha kugawa mlo wa shibe ya siku moja, lakini bado kura ndio zilikuwa hizo milioni 5 kati ya milioni 20, waliojiandikisha kupiga kura. Iwapo upinzania wangelijua hili na kuelekeza efforts kwenye zile milioni 15 wazipate wao, CCM hata ingeiba vipi, bado ingepigwa mweleka!. Ndio maana nimetoa angalizo, CCM sio adui yetu mkubwa, adui yetu mkubwa ni wananchi ambao wanaichagua CCM, na wale wengi zaidi ambao hawakupiga kura!.

Baada ya kauli ya Pinda kuhusu ma RC na ma DC kuhakikisha CCM inashinda na kutawala milele, inner concious yangu inanieleza maelekezo kama hayo hayakuishia kwa ma RC na ma DC pekee, bali ni kwa maofisa wote wa serikali na vyombo vyote vya dola!, that being the case, lets just leave CCM na serikali yake alone and concentrate on reaching out the great potential ya "vox populi" na mtaona matokeo yake!.
 


Mkuu WildCard, mimi naamini katika msemo wa Kilatini usemao "Vox Populi is Vox Dei" ukimaanisha sauti ya watu ni sauti ya Mungu. Ule uchaguzi wa 2010 CCM imeshinda kwa kura milioni 5 tuu hapo ndio kujumlisha na uchakachuaji wote wa NEC, na michango ya ma RC, ma DC maofisa wote wa serikali, vyombo vyote vya dola, na ile mechanisim yao kubwa ya kugawa t-shirt na kofia, na kile kidogo dogo cha kugawa mlo wa shibe ya siku moja, lakini bado kura ndio zilikuwa hizo milioni 5 kati ya milioni 20, waliojiandikisha kupiga kura. Iwapo upinzania wangelijua hili na kuelekeza efforts kwenye zile milioni 15 wazipate wao, CCM hata ingeiba vipi, bado ingepigwa mweleka!. Ndio maana nimetoa angalizo, CCM sio adui yetu mkubwa, adui yetu mkubwa ni wananchi ambao wanaichagua CCM, na wale wengi zaidi ambao hawakupiga kura!.

Baada ya kauli ya Pinda kuhusu ma RC na ma DC kuhakikisha CCM inashinda na kutawala milele, inner concious yangu inanieleza maelekezo kama hayo hayakuishia kwa ma RC na ma DC pekee, bali ni kwa maofisa wote wa serikali na vyombo vyote vya dola!, that being the case, lets just leave CCM na serikali yake alone and concentrate on reaching out the great potential ya "vox populi" na mtaona matokeo yake!.
Sanduku la kura kuiondoa CCM madarakani sio rahisi. Tulikofikishwa na CCM kama NCHI tunahitaji "vox populi" kama ile ya nchi za Kiarabu sio kupitia sanduku la kura kwa vyombo hivi vya DOLA tulivyonavyo. Vinginevyo tungoje CCM ipasuke mwaka 2015 watakaposhindwa kuafikiana nani agombee.
 
Sanduku la kura kuiondoa CCM madarakani sio rahisi. Tulikofikishwa na CCM kama NCHI tunahitaji "vox populi" kama ile ya nchi za Kiarabu sio kupitia sanduku la kura kwa vyombo hivi vya DOLA tulivyonavyo. Vinginevyo tungoje CCM ipasuke mwaka 2015 watakaposhindwa kuafikiana nani agombee.
Mimi bado nina imani kubwa na sanduku la kura, kama watu wakihamasishwa ipasavyo na wakajiandikisha kwa wingi na siku ya kupiga kura wakajitokeza kwa wingi, CCM inangoka tuu japo ni ngumu kama kisiki cha mpingo!.

Matokeo ya uchaguzi, yanachakachulika only if margin kati ya mshindi na mshindwa ni slim, ikiwa ni landslide, hata wachakachue vipi, matokeo hayachakachuliki. Matokeo ya Arumeru was a litmus paper ya CCM itabaki au inang'ooka, sasa ni zamu ya Igunga, CCM kwaheri!.

Hiyo "vox populi" kama ya waarabu kule Tunisia, Misri, Libya na sasa Syria, sisi Watanzania hatuiwezi, Watandania ni watu wa amani, utii, uvumilivu na ustahimilivu wa hali ya juu sana na ndio maana tumekuwa tukiichagua CCM,, mwaka hadi mwaka licha ya kututenda vilivyo!.
 
Pasco,

Kwa nini unaamini ili CCM ianguke lazima CDM iungane na vyama vingine (kuepuka huo "u-mimi")?

Pili kwa sasa CDM wanaendelea na M4C, umeshapima matokeo ya vuguvugu hilo kwa siasa za Tanzania kwa sasa?

Tatu, umezingatia "political dynamics" na factors nyingine ambazo hujazitaja, e.g. michapano ndani ya CCM, role ya mahakama katika baadhi ya kesi "hot" mf. Arusha Mjini & Igunga katika kubadili upepo wa kisiasa?

Nne, kwa nini uwalaumu CDM peke yao katika harakati za kuiangusha CCM?

Tano, kwa nini nawe umetaja (ama kwa makusudi au kwa malengo uyajuayo) "tuhuma" za udini, ukanda & ukabila? Je chaguo lako la maneno hayo lina msingi upi? Na kwa tawkimu zipi (ingawa umekwepa kuongelea)?
 
Kama umeshang'amua wananchi ndio wamerubiniwa na CCM ili kuichagua, then ili kuiondoa hiyo CCM iliyowarubuni ni kuwafikia hao wananchi na kuwaelkimisha ili wasiendelee kurubuniwa!. Wewe jiulize anayepiga kura kuchagua ni nani?, CCM si ni inachaguliwa?!, unatakiwa kumfuata mchaguaji na sio mchaguliwa!, ukiendelea kumtarget mchaguliwa tuu, mchaguaji ataendelea kumchagua huyo huyo mchaguliwa aliyemzoea, ukimtarget mchaguaji na kumuelimisha asiendelee kuchagua kwa mazoea bali kwa sababu, then, mchaguliwaji wa mazoea, hata chaguliwa tena na atajifia natural death!.

Sikio la kufa halisikii dawa
 
Wataalam wa demographia naomba mnisaidie, hivi hapa hapakuwa na usanii? Labda jibu nitalipata baada ya sensa inayokuja, ila kwa sasa ninayomashaka makubwa sana. Katika nchi zinazoendelea au maskini kama ya kwetu population pyramid zetu ni pana kwa chini na kupungua sana unavyopanda juu. Ila kwa Uandikishaji wa wapiga kura wa mwaka 2010 population pyramid yetu inaelekea kuwa kama ya nchi kama Sweden. Kwanini nayasema yote hayo?
Kakika mwaka 2010 ilikuwa inakadiriwa kuwa Tanzania ilikuwa na watu karibu milioni 40 sasa tunaposema kuwa watu zidi ya milioni 20 inamaana zaidi ya 50% ya watanzania ni watu walio na miaka 18 na kendelea. Na hawa ni wale waliojiandikisha, kwa kuwa kuna watu ambao hawakujiandikisha waliokuwa na sifa za kujiandikisha, kulikuwa na wazee wasiokuwa na uwezo wa kenda kijiandikisha tukiongezea wote hao tunaenda kwenye milioni 24. Hivi kunaukweli hapo au ni uchakachuaji kwa lengo maalum? Hebu wachambuzi angalia hili na wataalam wa demographia watusaidie.
 
Pasco,

Kwa nini unaamini ili CCM ianguke lazima CDM iungane na vyama vingine (kuepuka huo "u-mimi")?

Mkuu Ibambasi, "Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu"!.

Pili kwa sasa CDM wanaendelea na M4C, umeshapima matokeo ya vuguvugu hilo kwa siasa za Tanzania kwa sasa?
nimeipongeza hii move, target isiwe CCM, target iwe watu!,

Tatu, umezingatia "political dynamics" na factors nyingine ambazo hujazitaja, e.g. michapano ndani ya CCM, role ya mahakama katika baadhi ya kesi "hot" mf. Arusha Mjini & Igunga katika kubadili upepo wa kisiasa?
what for?, nazungumzia mpangaji wa ile nyumba nyeupe pale Magogoni mwaka 2015!.

Nne, kwa nini uwalaumu CDM peke yao katika harakati za kuiangusha CCM?
ndio one and only promising party besides CCM, mti wenye matunda!.

Tano, kwa nini nawe umetaja (ama kwa makusudi au kwa malengo uyajuayo) "tuhuma" za udini, ukanda & ukabila? Je chaguo lako la maneno hayo lina msingi upi? Na kwa tawkimu zipi (ingawa umekwepa kuongelea)?
I reserve my comments but the guilt are always afraid, hizi kauli za (ama kwa makusudi au kwa malengo uyajuayo) ni signs za a haunted house!.

Pasco.
 
Kuchangia sred ya Pasco.. Mimi huyu.. Aa.. !! Ila nadhani tatizo mwenzangu huyu ni mwiko kuangia football.. Meko, football Ina sehemu mbili, mchezo wenyewe ambao ndio utamu wa mtazamaji, lakini sehemu ya pili ni mfumo Yaani ukamisaa wa sheria za mcheZo wenyewe.. Kama mfumo wa mchezo umetungwa Na Yanga, unategemea Simba wataambulia Nini.. Mbona AKILI ndogo tu inaweza kutumika kuwaza Hilo ..

Mie hata keshokutwa bado ntasita kuamini hata hii Tume ya Katiba.. On hand inawajibika Kwa Rais na Urais(CCM )

Kwanini kuwa na uoga uliopindukia, mbona CAG ana over-sovereign power sasa kwanini tume isiwe hivyo?

Hatutaki Katiba ya CCM wala CUF wala CDM, Tume iwekwe kwa mamlaka ya wananchi Kwa Katiba ya wananchi.

Kama wawakilishi wetu, wabunge, wangelijua Hilo, pasingekuwa Na msuguano wowote Kwenye kugombea fito Kwa Ujenzi wa Nyumba moja

Siongelei habari Za Tume ila nataka kiduchu tu kuonyesha kwamba

TATIZO NI CCM.. Sasa chama chetu hiki ukikisema hakifurahi.. No .. Kama CCM watabadilika Na kutenda haki, Na Haki ikaonekana ikitendeka, kila Mtu ataiunga Mkono ..
 
PASCO umesema mambo mengi lakini bado naamini wewe kuna mahali unatumika.Na shawishika kuamini kuwa unatafuta ENTRY POINT ya kuingia kwenye upinzani ili hatimae uwadhoofishe kwa dhana kwamba CDM peke yao hawaiwezi CCM.uliona IGUNGA? ARUMERU MASHARIKI? hizi ni dalili tosha kwamba CDM wanaweza!!!! kama ccm walitumia bil 7 IGUNGA bado wakahitaji kuchakachua na kulazimisha ushindi,yafaa uone kwamba YOU ARE COMPLETELY WRONG.
 
Sikonge,....Ni kweli kabisa CCM inajiweka madarakani yenyewe!.. Na ndiyo maana kila uchaguzi mkuu unapofanyika wapo viongozi wanaoranda randa majimboni kuchakachua...........Wakati unapambana kuwaamsha wananchi na kuwaandaa kwa ajili ya mapinduzi, ni muhimu kupambana na hila za kila namna zinazofanywa na watu hawa!..... Maana hawaoni haya kumtangaza aliyeshinda kuwa ameshindwa, na aliyeshindwa kuwa ameshinda... reference, Shinyanga mjini 2010, Mbeya vijijini 2010, Sumbawanga mjini 2010! n.k.
 
Pasko wacha kutugeuza akili adui yetu mkubwa ni ccm . Angalia tume ya uchaguzi inavyo teuliwa na mwenyekiti wa ccm na inavyo wajibika kulinda maslahi yake. Alafu 2010 uliona jinsi vyombo vya dola vilivyo shiriki kuibeba ccm na mwisho nikukumbushe kwamba ccm haikushinda urais 2010 kwa kura za wananchi ,alafu swala la udini na ukanda hilo ni lako wewe na ccm mnalitumia kama silaha yenu ya mwisho.
 
Pasco,
Mimi nadhani ni vyema ukasahihisha kidogo kauli kwamba adui yetu siyo CCM ni wananchi wanaoichagua CCM.
Mimi ningesema adui yetu mkubwa ni wananchi wengi kukosa elimu na ufahamu sahihi wa demokrasia.
Ukiangalia kwa undani sana utaona kuwa wapo wananchi wengi kabisa haswa vijijini ambao hawaamini kabisaa kwamba kunaweza kuwepo na ubora au maana yoyote kupata chama kingine kuiongoza nchi hii.
Pili hata CCM yenyewe inao wasomi na tena viongozi ambao wamekuwa brain-washed kiasi hicho kwamba hawana uwezo wa kutafakari maana ya uwepo wa vyama vya upinzani. Mfano mdogo wa mawazo aina hiyo ni pale mtu anaposema yeye atakiunga chama hata kama hakituletei manedeleo yoyote, Nyerere aliyekianzisha aliwahi kuwasahihisha wenye mawazo kiwingu kwa kuwaambia "chama siyo mama yangu, kikiwa hakitendi mema nitajitoa".

Kuna wanaosema eti somo la Uzalendo lifundishwe mashuleni. Nadhani hawa ni wale ambao hawakuwahi kupitia jeshini (JKT) wakati huo. Nataka niwakumbushe tu kuwa hawa wanaolitafuna Taifa sasa hivi bila huruma na wakishirikiana na wageni kuuza nchi, ndiyo wale wale ambao walifundishwa sana somo hilo. Tena wengi wao wamepitia Kivukoni college. Waulize walikuwa wanafundishwa nini kule! Ndiyo walifundishwa u-CCM lakini uzalendo ulifundishwa sana. Sina sababu ya kuamini kuwa walifundishwa watoroshe mabilioni nje ya nchi yao na kuyaficha mabenki ya nje.

Mfumo huu wa CCM wa uongozi wa Taifa letu umepitwa na wakati na chakavu kiasi kwamba wale walio wazalendo wa kweli wa Taifa hili hawapewi nafasi bali wanapewa ama wale wanaowaabudu viongozi au wale wajanja sana-aka Mafisadi. Wale wanaoonyesha uzalendo ama watauwawa au kufanyiwa mizengwe ya kibabe, ama Uwt kutumwa kuwafilisi na kwadhoofisha hata kiafya ili tu wasalimu amri. Na kibaya zaidi mfumo umepelekea kutishia hata wasomi na wataalamu kwa sababu utaalamu hauthaminiwi kabisa katika mfumo huu. Mwanasiasa ndiye anayethaminiwa. Bahati mbaya zaidi wanasiasa wenyewe tulio nao wengi hawajaelimika hata kama wamesoma.

Mimi pia si mwanachama wa CDM, lakini nashindwa kukubali kuwa Chadema wanatakiwa wakawapigie magoti CUF. Kwanza CUF walishaonyeshwa uzalendo mzuri tu na Chadema wakati waliwaachia majimbo kule walikoonekana wanamvuto zaidi ili kuimarisha upinzani. CUF walishindwa ku-reciprocate! Nataka nikukumbushe tu kuwa CUF wameonekana kujikomba sana kwa CCM, wakitafuta wawe "endorsed" kama wapinzani wazuri na hiyo hiyo CCM. Mfano mzuri ni pale walipohudhuria ile sherehe ya kuapishwa Raisi halafu Prof. Lipumba akamkabidhi Kiwete nakala ya Itikadi ya CUF. Ukiweza kupata ile video clip ya lile tukio uiangalie vizuri halafu uangalie sura na reaction ya Mr. Clean na Kikwete mwenyewe hapo ndiyo utafahamu, and you will conclude something regarding CUF. Nataka nieleweke vizuri sana kuwa siichukii CUF lakini nitoe tu ushauri wajipambanue zaidi kuonyesha kuwa wapinzani wa kweli na kwa vitendo vya kuaminika. Watupe imani kuwa nia yao siyo tu kushika uongozi Zanzaibar bali wa Tanzania kwa ujumla.

Nikuulize swali, kwanini unadhani ni CDM tu wanaotakiwa kuwafuata CUF kutaka ushirikiano nao, je CUF nao hawatakiwi kulijua hilo kuwa wakiungana ndiyo watafikia malengo yao?? na kwa haraka zaidi?? Kama watakuwa mpaka leo hawajakubali kuwa Chadema ndiyo wameshika uongozi wa upinzani na kwamba kwa ajili ya kuboresha upinzani ili mafanikio yanayotafutwa sasa na wazalendo wa kweli yapatikane haraka iwezekanavyo, wanatakiwa kuwaunga mkono Chadema basi watatuacha tunajiuliza maswali mengi sana.

Usemi wako wa "if you can't beat them join them" should have as well applied in joining hands with Chadema to eject CCM from power. Na huo ndiyo ungekuwa Uzalendo wa kweli!
 
Adui Namba mmoja wa waTZ ni CCM, namba mbili ni wasomi wote ambao wamegeuka kuwa mchwa mchi hii ambao wanashindwa kusema na kukiri ukweli daima wamekuwa wakifanya propaganda kwa sababu ya maslahi binafsi tu.

Pasco kwa level yako kama huwezi kuji Identify na kuonekana kuwa huna chama, maana yake ni wewe unakuwa wa vuguvugu kitu ambacho hakitakiwi na ndiyo watanzania wengi tulionao na ndiyo wanaozamisha nchi hii kweye lindi hili la umasikini.

mini nimeipigia kura CDM tangu 1995 hadi leo, kwa maelezo yako ni kwamba inawezekana kabisa 2010 wewe hata kura hujapiga na kama ulipiga uliwapigia nani?????, maana kwa mahali tulipofikia watu wengi hawakubaliani na mambo yanayofanywa na CCM ndiyo maana wanaona ni adui yao namba moja, je wewe ni kwamba bado hujatambua madhara ya CCM???

Je kama akikufuata kijana wako anayetimiza 18yrs 2015 wewe utamshauri aipigie kura CCM au CDM??? au asipige kura kabisa???
 
Mhe. Pasco,

Umejitahidi sana kujaribu kueleza hali halisi. Ila kuna mambo ambayo napenda nikusahihishe.
  1. Si kweli kwamba adui wa Watanzania siyo CCM baali ni Watanzania wenyewe. Hii siyo kweli mheshimiwa. Kwa mtu makini na anayefuatilia chaguzi za Tanzania kuwa na ndogo atakubaliana na mimi kuwa CCM ndiyo wamekuwa adui mkubwa wa Watanzania kwasababu hata pale Watanzania walipochagua chama mbadala ya CCM, hawa CCM walifanya kila mbinu kubadilisha matokeo in their favour. Wizi wa kura,hongo na rushwa siyo jambo geni masikioni mwako. CCM ni wezi wa kura. Mifano halisi ni chaguzi ndogo za Igunga na Arumeru East.
  2. Pili ni kuhusu idadi ya wapiga kura 2010. Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha mwaka 2010 kuwa zaidi ya milioni 20 ni yenye kutia shaka. Kwa kifupi ni hesabu ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia wenyewe. Yawezekana kabisa NEC walichakachua idadi hii kwa makusudi ili kuweza kutumia idadi hiyo kuiba kura! Haiwezekani watu milioni 20 wajiandikishe halafu watu milioni 12 wasijitokeze kupiga kura. Huu ni uongo. Hiyo hesabu ilikuwa ni kupika kwa ajili ya kuwanufaisha CCM katika kuchakachua.
  3. Kama kweli mwaka 2015 kutakuwa na idadi ya Watanzania milioni 50 sidhani kama watakaojiandikisha watafikia milioni 35 uliyosema. Kwa predictions zangu inawezekana labda ndiyo ikafikia hiyo milioni 20 out of 50 milioni. Na turn over siku ya Uchaguzi ikafikia kwenye 15-18 milioni probably.
  4. Kama Uchaguzi utakuwa HURU na HAKI bila ya kuingiliwa na TISS,PCCB na POLICCM basi uhakika wa Watanzania kuipigia CHADEMA KURA ZA NDIYO na kuiweka madarakani ni kwa 80%. Hilo nina uhakika kabisa. Kama Mungu atatujalia uzima kufikia hiyo 2015 basi tutegemee uongozi mpya tofauti na CCM.

Wasalaam.
 
PASCO umesema mambo mengi lakini bado naamini wewe kuna mahali unatumika.Na shawishika kuamini kuwa unatafuta ENTRY POINT ya kuingia kwenye upinzani ili hatimae uwadhoofishe kwa dhana kwamba CDM peke yao hawaiwezi CCM.uliona IGUNGA? ARUMERU MASHARIKI? hizi ni dalili tosha kwamba CDM wanaweza!!!! kama ccm walitumia bil 7 IGUNGA bado wakahitaji kuchakachua na kulazimisha ushindi,yafaa uone kwamba YOU ARE COMPLETELY WRONG.
Mkuu malua, Watanzania wazalendo wa type yangu tupo wengi tuu ambao hatuna any political ambitions bali tunaumizwa na uchungu wa hali ya taifa letu ilivyo sasa na tunasupport juhudi zozote za ukombozi wa pili wa kweli wa taifa letu kutoka vyama vyovyote ikiwemo CCM!.

Kama unaamini, mimi natumiwa na kwa sasa ndio natafuta entry point kuingia upinzani ili niudhoofishe, you are very wrong!, mimi sio mwanachama wa chama chochote, sio mshabiki, mfuasi au mkereketwa wa chama chochote zaidi ya maslahi ya taifa!.

Sina sababu ya kujigamba humu offer ngapi za kujiunga na vyama vipi ili kupewa ulaji, nimezikataa!. Wengi wa wanasiasa wetu, wanaingia siasa kama ajira ili waweze kuishi maisha mazuri, sisi wengine kama mimi, ni masikini jeuri, tumeishauzoea umasikini wetu tena wa kujitakia!, na ikitokea nikaingia siasa, lengo litakuwa ni kuwatumikia wananchi, na sio kuchuma au kujineemesha!.

Wanasiasa wengi zaidi ni wachumia tumbo kuliko watumishi wa watu!. Mimi ni mtumishi zaidi wa watu na mara kibao hulala njaa huku nikismile, na hata zile siku ninapokuwa sina hata senti tano,mwili wangu huingia ganzi ya mfungo wa lazima na hata nikikaribishwa chakula au kinwaji bure, huwa sili!.
 
Mkuu malua, Watanzania wazalendo wa type yangu tupo wengi tuu ambao hatuna any political ambitions bali tunaumizwa na uchungu wa hali ya taifa letu ilivyo sasa na tunasupport juhudi zozote za ukombozi wa pili wa kweli wa taifa letu kutoka vyama vyovyote ikiwemo CCM!.

Kama unaamini, mimi natumiwa na kwa sasa ndio natafuta entry point kuingia upinzani ili niudhoofishe, you are very wrong!, mimi sio mwanachama wa chama chochote, sio mshabiki, mfuasi au mkereketwa wa chama chochote zaidi ya maslahi ya taifa!.

Sina sababu ya kujigamba humu offer ngapi za kujiunga na vyama vipi ili kupewa ulaji, nimezikataa!. Wengi wa wanasiasa wetu, wanaingia siasa kama ajira ili waweze kuishi maisha mazuri, sisi wengine kama mimi, ni masikini jeuri, tumeishauzoea umasikini wetu tena wa kujitakia!, na ikitokea nikaingia siasa, lengo litakuwa ni kuwatumikia wananchi, na sio kuchuma au kujineemesha!.

Wanasiasa wengi zaidi ni wachumia tumbo kuliko watumishi wa watu!. Mimi ni mtumishi zaidi wa watu na mara kibao hulala njaa huku nikismile, na hata zile siku ninapokuwa sina hata senti tano,mwili wangu huingia ganzi ya mfungo wa lazima na hata nikikaribishwa chakula au kinwaji bure, huwa sili!.

Hujajibu hoja kuhusu mtiti wa CDM Igunga na Arumeru Mashariki.
Naomba nikuthibitishie hapa kwamba katu asilani CDM haitaungana na vyama vibaraka katika harakati zake za kukomboa wanyonge.Tulijaribu mbinu hiyo kwa miaka 15 ikashindikana.
CDM kwa sasa itatumia vuguvugu la M4C kuwaunganisha watanzania popote pale walipo bila kuangalia rangi,dini,kabila wala jinsia na bahati nzuri wananchi wametuelewa.Lakini kama kuna watu wanadhani wataimaliza CDM kwa kuwashawishi kushirikiana na viongozi mamluki na vibaraka wa upinzani wamekosea sana.
CDM imetumia miaka 20 ya uhai wake kujifunza mengi.Kina Mbatia,Mtikila,Cheyo,Mrema na Lipumba waendelee na harakati zao na tunawatakia kila la kheri...
 
Hujajibu hoja kuhusu mtiti wa CDM Igunga na Arumeru Mashariki.
Naomba nikuthibitishie hapa kwamba katu asilani CDM haitaungana na vyama vibaraka katika harakati zake za kukomboa wanyonge.Tulijaribu mbinu hiyo kwa miaka 15 ikashindikana.
CDM kwa sasa itatumia vuguvugu la M4C kuwaunganisha watanzania popote pale walipo bila kuangalia rangi,dini,kabila wala jinsia na bahati nzuri wananchi wametuelewa.Lakini kama kuna watu wanadhani wataimaliza CDM kwa kuwashawishi kushirikiana na viongozi mamluki na vibaraka wa upinzani wamekosea sana.
CDM imetumia miaka 20 ya uhai wake kujifunza mengi.Kina Mbatia,Mtikila,Cheyo,Mrema na Lipumba waendelee na harakati zao na tunawatakia kila la kheri...
Mkuu Molemo, kama umenisoma vizuri nimeeleza mazingira ya ushirikiano na kusisitiza kuwa Chadema itake isitake, ni LAZIMA ishirikieane na wengine!.

Katiba mpya itatamka wazi kuwa ili chama kitawale Tanzania, lazima kipate kura za sehemu zote za Muungano!. CCM tayari inazo kura zake Zanzibar, na CUF inazo kura zake Zanzibar, to be honest, I don't see kura za Chadema Zanzibar, hivyo hata Chadema washinde kwa 98% ya kura za bara, wataishia kuwa disqualified kwa kwa technical knock out kwa kukosa kura za Zanzibar!. Mark my words!.
 
Mkuu Molemo, kama umenisoma vizuri nimeeleza mazingira ya ushirikiano na kusisitiza kuwa Chadema itake isitake, ni LAZIMA ishirikieane na wengine!.

Katiba mpya itatamka wazi kuwa ili chama kitawale Tanzania, lazima kipate kura za sehemu zote za Muungano!. CCM tayari inazo kura zake Zanzibar, na CUF inazo kura zake Zanzibar, to be honest, I don't see kura za Chadema Zanzibar, hivyo hata Chadema washinde kwa 98% ya kura za bara, wataishia kuwa disqualified kwa kwa technical knock out kwa kukosa kura za Zanzibar!. Mark my words!.

You are dreaming!
Kwa hiyo CDM haipatagi hata kura moja Zanzibar? Mbona husemi uchaguzi Jimbo la Uzini CDM ilishika nafasi ya pili? Kwa hiyo CDM ikipata kura 70% za urais itashindwa kutawazwa waipe CCM itakayokuwa imepata 25% kwa vile imepata kura nyingi Zanzibar? You are dreaming.Mark my words!
 
Back
Top Bottom