Mkuu Molemo, kama umenisoma vizuri nimeeleza mazingira ya ushirikiano na kusisitiza kuwa Chadema itake isitake, ni LAZIMA ishirikieane na wengine!.
Katiba mpya itatamka wazi kuwa ili chama kitawale Tanzania, lazima kipate kura za sehemu zote za Muungano!. CCM tayari inazo kura zake Zanzibar, na CUF inazo kura zake Zanzibar, to be honest, I don't see kura za Chadema Zanzibar, hivyo hata Chadema washinde kwa 98% ya kura za bara, wataishia kuwa disqualified kwa kwa technical knock out kwa kukosa kura za Zanzibar!. Mark my words!.
No, wait a minute Pasco, Ina maana mpo mnaojua au mliokwisha iona draft ya Katiba mpya?
Suppose wabara wakadai nchi yao? Watu tusipokuwa makini hapa hili litasababisha pata shika. Hivi Pasco, unavyosema hivyo una maanisha kuwa kwako wewe uwiano uliopo wa idadi ya wananchi Tanzania bara na Zanzibar ni haki kwa watu wa bara kuwa wanaamuliwa uongozi wa nchi na wachache Zanzibar milele bila ukomo?. Sasa nimeamini 100% kuwa jinsi muungano ulivyoundwa upo kwa ajili ya kudhoofisha na kuua upinzani kutoka pande zote na kwamba hapatatokea upinzani kuchukua uongozi wa nchi. Na hapa ndiyo inathibitika wazi sababu zinazopelekea CCM kutamka kila mara kuwa watatawala milele. Na bila shaka sasa ni wakati kabisa wa kuuweka huu muungano uwe wa sayari hii, au serikali moja nchi nzima au serikali tatu. Hakuna kitakachokuwa sahihi nje ya hapo.