Kingunge amechanganyikiwa?

Mkuu umesema vizuri sana kwamba wewe HUONI popote penye matatizo.. Mimi naona sehemu nyingi sana kwani siku zote ktk Uongozi wa nchi, taasisi za kidini zinapoingilia kati ndipo utata huanza.

Unajua nchi za kiarabu kuna mengi ya wahubiri wa dini huzitaka serikali zao kufanya mema kwa faida ya wananchi wote lakini utata huja pale sisi tunapotazama nafasi ya dini na uongozi wa nchi hizo pamoja na kwamba population ya nchi hiyo ni 99 waislaam. Kifupi kanisa wala Msikiti hautakiwi kabisa kuingiza hoja zake serikalini unless swala hilo linahusiana na waumini wake.

Ni makanaisa na misikiti ilotuchanganya akili wakati wa uchaguzi wa Mkapa na huyu JK..ni hao hao waliowatukuza na kuwaona viongozi bora, leo hii tunapewa somo jingine tena wakati wa uchaguzi ukikaribia.
Trust me mkuu wangu hakuna mtu hata mmoja asiyefahamu nani kiongozi mzuri hata iwe jangwani au kijijini ndani kabisa Umasai...wote hawa walikuwa na mila za kuchagua viongozi wao na walitoa sifa au kashfa kutokana na kiongozi aliyepo.
Tatizo ni kwamba, kiongozi mzuri hana alama usoni nahata siku moja huwezi kukisia ila kwa ahadi zake..Kinachomtangulia kiongozi ni mfumo bora wa utawala.. Maadili na miiko ya Uongozi ndio road signs za kiongozi yeyote yule..kisha wananchi nao wapate somo la haki za uraia wao na sii somo la kumchagua kiongozi mzuri ambaye hajawahi kuongoza. zaidi ya hapo Mbunge sii kiongozi hata siku moja ila ni mwakilishi wa wananchi..

Hivi kweli unaweza kunipa sifa za kumchagua mtu kati Mwakyembe na Mwakalinga kwa kutumia vigezo hivyo?.. Mwakyembe tunamjua na mapungufu yake, mtu kama Mwakalinga hatumjui hivyo.. somo linatuambia nini kuhusu watu kama hawa?.. Je, linazungumza nini kuhusu wagombea wa vyama vya upinzani..Tunatazama mtu au chama? maanake nashindwa kuelewa inaonyesha kama waraka huu unataka tuishague CCM lakini tuwachuje viongozi wake badala ya kutazama upana na sera za vyama..
Siku zote uchaguzi wa viongozi hutokana na sera za chama sasa tukianza kuweka macho yetu kwa watu na tabia zao sijui nani mbora kuliko mwingine...
Hivyo pamoja na makosa ya mzee Kingunge ktk mtazamo wa wengi bado mzee huyu ana haki sawa ya kuelezea yale anayoyaona yeye kuwa ndio safi na tumkosoe kwa alosema tukizingatia kwamba tupo radhi kupokea maagizo kama haya ya waraka toka dini tofauti..
Binafsi sipo radhi kabisa na itajenga uhasama zaidi inapofikia viongozi wa dini kuitumia serikali kujenga kitu chochote kile..
Waraka wenyewe huu hapa View attachment 5607
Tuonyeshe wapi una kasoro badala ya kuja na hoja za kidini dini tu.
 
mzee Kingunge kama na anataka ajue position yake ktk siasa za sasa, asikilize wimbo mpya wa MRISHO MPOTO, baada ya ule wa NIKIPATA NAULI...
 
Swali ninalojiuliza ni kwa nini JK amekuwa kimya sana juu ya swala hili?ni kwa nini Pinda aliposema kule bungeni hakutoa kauli nyooofu?bila shaka watanzania wenzangu kuna jambo hapa linalofichwa hapa na serikali yetu....Hii ni dalili tosha ya aina ya viongozi tulionao
1) Huficha ukweli
2) Kila anayejitahidi kuleta mabadiliko hupigwa vita
3) Njia rahisi kwao ya kutatua matatizo ni kuyakwepa

Mkuu, mwaka 1992 Maaskofu wa Kanisa Katoliki Malawi waliandika waraka kukosoa utawala wa Dk Kamuzu Banda kuhusu elimu, afya, ustawi wa jamii, vita dhidi ya umaskini, HIV/Aids, mgawanyo wa raslimali za taifa, haki ya mtu kutoa maoni bila kuingilia na vyombo vya dola nk.

Serikali ilipiga marufuku waraka huo kukutwa na mtu yeyote (kwani ilikuwa marufuku nchini humo kuikosoa Serikali isipokuwa kusifia tu mema yake) na hata printing press iliyouchapisha waraka huo ilichomwa moto na kuteketea kabisa.

Kwa vile yaliyokuwemo yalikuwa yanawagusa watu, vikundi mbalimbali viliweza kuunga mkono waraka huo wa Kanisa na kwa mara ya kwanza kulitokea referundum na kwenye uchaguzi Mkuu 1994 Dk Banda na chama chake MCP wakatupwa nje ya uringo na Bakili Mluzi kupitia United Democratic Front (UDF) akaibuka kidedea kwenye Uchaguzi Mkuu!

Haki na ukweli hujulikana baadaye hata kama itachukua muda! Malumbano ndani ya chama tawala ni mwanzo wa mfumo wake wa utawala kuingia nyufa na hatimaye CCM haitakuwa na nguvu tena kama zamani!

Watz wataendelea kudanganywa ndio na kura zitaendelea kuibiwa lakini siku moja kutatokea mabadiliko yatakayosimamia UKWELI n HAKI - maslahi ya wananchi. Kilio cha wanyonge kinasikika sana!

Wale wanaokumbatia au kutetea ufisadi wataona aibu baadaye! Hivi kweli watu wanapopinga kuchagua viongozi waadilifu na wenye sifa za uongozi, wanataka nini, tuendelee kutawaliwa na viongozi wenye uroho wa mali na uchu wa madaraka? Nashindwa kabisa kuwaelewa Watz wenzangu!

Ningefurahi sana kama wakosoaji wa waraka wangeainisha 'point' kwa 'point' au kipaumbele kimoja baada ya kingine yale wanayoona ni upungufu kwenye huo waraka kwa nia ya kuuboresha au wao wenyewe kutoa vipaumbele mbadala kuliko kutoa 'blanket statement' kuwa ni "waraka wa hatari" au "unaleta udini". Nami nashawishika kusema kuwa wote wanaopinga waraka huo ni mafisadi tena wa kutupwa!
 
.

Mimi nafikiri ungeweka bayana nini kingunge amesema badala ya kumuhukumu na kumwita kachanganyikiwa.

Hakika hata mimi nilipousoma niliona kuna athari kubwa sana katika jamii ya watanzania. Athari hizo ni :
1. Kwa kuwa umetolewa na madhehebu ya kidini, ulikuwa na lengo la kuelimisha waumini wake nini wafanye katika kuchagua viongozi wa kisiasa. Sasa nilijiuliza vipi wao viongozi wa kikatoliki, je walichaguliwa na nani kuwa viongozi, je waumini walishiriki katika kutoa mapendekezo au hata kuwachagua? au Pope aliwachagua ?

2. sasa nilijiuliza kama wao wliingia katika madaraka ya kuwa mapadr au hata maaskofu kwa kuchaguliwa na Pope , sasa vp waingile mambo ya kisiasa?

3. je kama Padre au Askofu anafundisha kuhusu Yesu vipi mtu huyu atasema achaguliwe mtu wa dhahebu lingine?

4. waraka ulikuwa na mengi yaliyojificha na yenye viashiria za ubaguzi ingawa yalipambwa na maneno mazuri sana.

Kijumla waraka ule ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa hususan kipindi hichi cha kupamba kwa UDINI huko Tanzania.

Namuunga mkono mzee Kingunge. maneno yake kuntu


Wewe inaelekea umechanganyikiwa zaidi kuliko hata huyo kikongwe KINGUNGE!
 
Ana vilaana vya ufisadifisadi na laana kubwa kubwa za kula rushwa na kutetea wala rushwa, kama ufisadi ndio hiyo hiyo rushwabasi jamaa ana JILAANA LA UFISADI
 
.

Mimi nafikiri ungeweka bayana nini kingunge amesema badala ya kumuhukumu na kumwita kachanganyikiwa.

Hakika hata mimi nilipousoma niliona kuna athari kubwa sana katika jamii ya watanzania. Athari hizo ni :
1. Kwa kuwa umetolewa na madhehebu ya kidini, ulikuwa na lengo la kuelimisha waumini wake nini wafanye katika kuchagua viongozi wa kisiasa. Sasa nilijiuliza vipi wao viongozi wa kikatoliki, je walichaguliwa na nani kuwa viongozi, je waumini walishiriki katika kutoa mapendekezo au hata kuwachagua? au Pope aliwachagua ?

2. sasa nilijiuliza kama wao wliingia katika madaraka ya kuwa mapadr au hata maaskofu kwa kuchaguliwa na Pope , sasa vp waingile mambo ya kisiasa?

3. je kama Padre au Askofu anafundisha kuhusu Yesu vipi mtu huyu atasema achaguliwe mtu wa dhahebu lingine?

4. waraka ulikuwa na mengi yaliyojificha na yenye viashiria za ubaguzi ingawa yalipambwa na maneno mazuri sana.

Kijumla waraka ule ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa hususan kipindi hichi cha kupamba kwa UDINI huko Tanzania.

Namuunga mkono mzee Kingunge. maneno yake kuntu

Nikusaidie:

1. Kuna vijitabu viwili: Kimoja kinaitwa Mpango wa Kiuchungaji... Kijitabu hiki kina 'cover' ya kijani. Hiki kijitabu, kinachoelezea vipaumbele 7, kinaonyesha jinsi Kanisa lenyewe lilivyojipanga kutoa hiyo elimu ya uraia na kuwapata viongozi waadilifu na wenye sifa za uongozi hata ndani ya Kanisa lenyewe (yaani, ngazi mbalimbali za Kanisa). Wakati Kanisa linatoa elimu hii ya uraia kwa waamini wake, linataka pia viongozi wa Kanisa wchaguliwe kwa kufuata njia hiyohiyo ya uadilifu na sifa za uongozi!

Wewe unadhani waamini wa kawaida hawashirikishwi kuwachagua viongozi wa Kanisa. Siyo kweli. Soma The Code of Canon Law, linatoa mwongozo wa jumla nani anapaswa kuchaguliwa kuwa deacon (shemasi), padre na askofu. Kwa kifupi waamini wanashirikishwa katika ngazi mbalimbali.

Hata padre wa sehemu anakuwa anapata assessment kulingana na jinsi anavyoishi na kufanya kazi yake. Kama hafai, waamini wanaweza kimkataa na akishurutisha kukaa pale wanasusia kazi zake! Kwani hujasikia katika baadhi ya maparokia, waamini wanenda kumwona askofu kwamba hawamtaki padre fulani? Hata askofu asipokubalika ni hivyo tu.

Kwa taarifa yako: kijana anayejisikia ana wito anaomba kwenye jumuiya yake, ikimkubali anajaza fomu zinapelekwa parokiani. Viongozi wa parokia wanazipitisha na kisha kijana huyo jina lake linapelekwa kwa mkuu wa seminari. Kisha anaitwa kufanya mitihani kwa masomo yale ya sekondari. Muda wote anapoenda likizo, anakuwa na fomu inayopelekwa kwenye jumuiya yake ili waweze kuandika juu ya tabia yake na maendeleo yake na kisha inasainiwa na paroko.

Akimaliza masomo ya sekondari, anatuma maombi kwenda seminari kuu. Hayo maombi anayapeleka jumuiya ndogondogo (kwa Wakristo anaosali nao) ili wathibitishe kuwa wanamfahamu na anashiriki shughuli za kanisa na pia ana tabia nzuri.

Kabla ya kumaliza masomo ya seminari kuu, anaomba kuwa deacon (shemasi). Jumuiya yake inakuwa 'contacted' kama kuna pingamizi lolote. Kama hakuna na kama wanaona hawana shaka yoyote juu ya imani, tabia na wito wake anaitwa kuwa padre.

Kila padre ana faili lake pia na ripoti yake inatumwa Vatican kila mwaka kutoka jimboni mwake. Kulingana na kazi ya yule padre na kukubalika kwake katika Kanisa, kama kuna haja ya kupata askofu, anapendekezwa padre (kutoka jimbo lake) ambaye ana sifa na 'experience' ya kutosha ya kazi yake (including, pamoja na masomo mengine, awe ameshasoma na kufaulu vizuri Moral Theology na Canon Law).

Huu ndio utaratibu wa kuwachagua viongozi kama mapadre na maaskofu na wanakuwa kwenye 'screening' kali sana. Hivyo usidhani, padre, askofu au kardinali wanachaguliwa na papa (in fact, papa anapitisha jina lililopendekezwa na wengi by merit). Huwa kuna mapendekezo ya candidates kadhaa. Hata papa anachaguliwa kwa kura!

2. Kijitabu kingine - ILANI - kinatoa vipaumbele 7. Hiki kimetolewa kwa kila mtu anayeoona anaweza kukitumia. Hiki hakina maelezo mengine kama kile cha kijani kwa vile watumiaji wake wanaweza pia kuandaa utaratibu wao wa kutoa elimu hiyo kulingana na jinsi inavyowafaa wenyewe na siyo lazima wafuate maelezo yaliyomo ndani ya kile cha kijani kinavyoeleza kwani inawezekana mazingira na 'structures' za dhehebu au dini nyingine zikawa tofauti.

Ila cha muhimu ni elimu ya uraia ili wananchi wachague kwa utashi - yaani, watumie haki yao ya kupiga kura vizuri na wasidanganywe na hela, vitenge au pombe - vitu vinavyotolewa na baadhi ya viongozi. Kama wote hatutashiriki kuhakikisha tunachagua viongozi waadilifu ni sisi wenyewe tutakaokubali kuendelea kuongozwa na viongozi wabovu. Kwa hiyo, tunapolipinga Kanisa katoliki tujue tunachotaka kufanya ni kujipumbaza ili tuendelee kutawaliwa na viongozi wabovu!
 
Mimi nadhani ambaye hajamuelewa ni mbumbumbu [snip]............................Hivi kweli Mwenye akili timamu anataka watanzania tuongozwe na Mashikh na Maaskofu nani wa kumchagua.Au hizi fedha chafu zinazotolewa kama njugu kama misaada zinatufanye tupoteze misimamo yetu

Eeee! nawe kweli unafikiri.
Jaribu kubadili uelekeo wako wa kufikiri ili kila institution iliyoko nchini uione ni ya manufaa ktk ustawi wa nchi. Huwezi ukaruhusu institution zooote halafu ukasema za kidini NO!

Naamini kwamba serenity inaleta taabu kwa Kingunge na ni bahati mbaya kwamba Bunge letu linambeba na tutajikuta likitumika kama Nursing home ya wazee. Wakiwa kimya sawa lakini wakipewa nafasi kama hii, taaabu!
 
Mchukia Ufisadi,
Mkuu wangu nimekwisha sema sipendi kujihusisha na ubishi wa kidini hata kidogo lakini wazidi kunivuta tu ili mradi niingie upate kufurahi.. Ebu wewe mwenyewe soma tena huo waraka kisha nambie kuna sehemu ngapi wamenukuu Biblia na mafundisho yake ktk hujenga hoja nzima ya waraka huu...Kwanza tazama kichwa cha habari kinasema Mpango wa kuhamasisha HUDUMA YA KIUCHUNGAJI.. sasa ukisha elewa kwa nini Mkandara hakuwa mkristu ndipo utaelewa kwamba Mkandara hakubaliani na huduma za Kiuchungaji pamoja na kwamba lengo lake ni kutufikisha peponi..
Siku zote ktk waraka huru aya na sura hutumika kama mifano na sii sisitizo la waraka mzima, unless waraka huo umelenga waumini wake..
Mbali na hili nachokipinga mimi sio substance ya waraka mzima, isipokuwa uwakilishi wa waraka kama navyoikubali Biblia bila kuukubali uwakilishi wa kanisa Katoliki. Ukinielewa hapo tutakuwa msitari mmoja
 
Jamani mbona tunatupiana vijembe kwa jambo lililo wazi sana - Kingunge Ngombale Mwiru hajachanganyikiwa na anatekeleza wajibu wake kama ambavyo amekuwa akifanya miaka yote ya uhai wake - kutetea sera za CCM. Kingunge Ngombale Mwiru ni fisadi na kwa kuwa hila za fisadi siku zote ni kulinda usalama wake - usalama ambao Kigunge Ngombale Mwiru anajua fika kwamba hautapatikani nje bali ndani ya CCM.

Wakati wa awamu ya kwanza Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa Mkuu wa Chuo cha CCM cha Kivukoni - chuo kilichopika viongoji wa serikali na chama. Aliweza kuaminiwa na Mwalimu kiasi cha kuwa kama balozi maalum wa siasa ya Ujamaa na kujitegemea na ndiye aliyeendesha semina kibao nchini juu ya azimio la Arusha na kujadili miiko ya maadili kwa viongozi. Wengi wao hadi sasa bado wana nyadhifa mbalimbali na wanahusishwa na ufisadi.

Wakati wa awamu ya pili Kingunge Ngombale Mwiru aliishangaza UMMA alipogeuka na kuwa msemaji rasmi na Kinara wa kutetea Azimio la Zanzibar lililoizika Azimio la Arusha. Kuna wengine tuliodhani labda kachanganyikiwa lakini siku zilivyokwenda ndivyo ilivyodhihirika kuwa kingunge Ngombale Mwiru ni kinyonga aliyeweza kubadili rangi kulingana na mfumo uliopo wa utawala. Cha kujiuliza ni kuwa nyakati hizo alisukumwa na nini.

Katika awamu ya tatu ndipo Kingunge Ngombaloe Mwiru aliweza kuonyesha makucha yake halisi kwa kusimama kidete kutetea sera ya uwekezaji ya kuwajali wageni kuliko wananchi. Mpaka hapo alikuwa mshauri wa chini chini katika mbinu za kuuza rasilimali za taifa na kuingia mikataba mibovu ambayo haikunufaisha wananchi bali genge dogo la watawala yeye akiwa moja wao. Eti aliitwa waziri asiye na wizara maalum !

Hii awamu ya nne imekuwa tofauti kidogo hasa baada ya wananchi kuamka na kutokuwa tayari kuzugwa kama zamani. Kingunge Ngombale Mwiru akajaribu mbinu zile zile za kizamani lakini akakuta watu wako macho. Ghafla ukweli wa wazi na mwanga halisi ukamtokea na akang'amua janja yao imeshtukiwa na hatari ya CCM kupigwa mweleka inamkodolea macho. Kingunge Ngomale Mwiru, mpiga ramli mkuu wa CCM hakuweza kupata usingizi.

"List of shame" Mwembeyanga ndiyo ilikuwa indiketa ya mwanzo lakini akapuuzia. Ikaja Richmond na wakati mambo bao moto ikaingia EPA na hajakaa vizuri UBUNGO ikapiga hodi. Ya rabi ! chombo kinakwenda mrama na kaburi tayari linachungulia - Kingunge Ngombale Mwiru akapiga mahesabu na kukumbuka ile sayansi aliyoipata huko chuoni Ulaya ya Kati - mbinu ya kivita, to divert attention from the real enemy !

Kingunge Ngombale Mwiru anajua wazi kabisa waraka hauna walakini lakini ni mwiba kwa mafisadi - yeye akiwa moja wao. Anajua kabisa kuwa kwa hili la kifisadi watanzania wengi wanaanza kuuona ukweli na kuwa na mshikamano dhidi yake. CCM inajua nguvu ya adui iko katika umoja wao na huu waraka una hatari ya kuchochea hiyo hali - hivyo lazima upigwe vita kisayansi - kuzua malumbano nje ya hoja na kusambaratisha mshikamano.

Mpaka sasa CCM kwa kumtumia Kingunge Ngombale Mwiru inaonyesha kufanikiwa - tayari tunalumbana wenyewe kwa wenyewe. Kuna wanaoangalia huu waraka kidini na malumbano ya kidini yanaaza kutugawa - tunamsahau adui wetu nambari wani, UFISADI. Hii yote ni katika kuiokoa CCM na hivyo kuwaokoa mafisadi kwa kuingiza Udini katika hoja - Kingunge Ngombale Mwiru, mtu asiye na dini, anatumwa kurusha chambo na wengi tunanasa.
Tuna safari ndefu watanzania.
 
Ma3,
Mkuu wangu kwa hili namtetea Kingune, mzee huyu hana dini hawezi kukubali mafundisho ya kanisa kujenga mwongozo..Umesoma wito, mada zilizozungumziwa vipaumbele vyake vinapangwa kwa mujibu wa mafundisho ya kanisa kuhusu jamii..Kisha mambo yaliyopendekezwa kufanywa ktk kufundisha na kuhamasisha utu ni pamoja na mafunzo ngazi ya Parokia na taasisi za kanisa. Mkuu huyu mzee hana dini unapoanza na habari kama hizi hawezi kabisa kukubaliana na wewe mbali na hata angekuwa Muislaam au kwa udogo naweza sema Protestant..
 
Kingunge is right in all rights!
Religion has overstepped its objectives in a secular country. They need to back down or the government should act NOW to keep religion within its boundaries. Otherwise this country will end in a mess.
 
Wakuu heshima mbele sana,

- Sometiems tujifunze kuwaelimisha hawa viongozi wetu kwa kuwapa elimu ya ishus, ukweli ni kwamba Tanzania sasa hivi tuna vacuum ya uongozi wa taifa hasa wa juu that is what Kingunge na wachangiaji wengi wa topic tunashindwa kukiona katika big picture ya hii ishu,

- Taifa likishakuwa na vacuum ya uongozi wa juu kama tulivyo, inatoa nafasi kwa wananchi binafsi, private sectors, matajiri, au vikundi vya dini as of this ishu ku-set the national agenda, au kuingiza pua zao kwenye process ya national policy making na ndio hasa wanachokifanya hawa viongozi wa dini, badala ya kuliachia bunge na viongozi wetu responsible kisheria ya jamhuri yetu.

- Under Mwalimu, ilikuwa ni very clear kwamba tunasimamia wapi as far as national policies na national priorities zetu, lakini that is not the case today hatueleweki tunasimamia wapi, tunakwenda wapi ingawa tunajua tulikotoka matokeo yake ndio haya tuliyonayo yaani kila mtu anajitokeza na kujaribu ku-set the agenda na sisi Great Thinkers bado tunalilia siasa za personalities, kumbe wakati mwingine ishus kama hizi hazina uhusiano wowote na personalities,

Isipokuwa ni vacuum tu ya uongozi wa juu wa taifa!

Respect.

FMEs!
 
Wakuu heshima mbele sana,

- Sometiems tujifunze kuwaelimisha hawa viongozi wetu kwa kuwapa elimu ya ishus, ukweli ni kwamba Tanzania sasa hivi tuna vacuum ya uongozi wa taifa hasa wa juu that is what Kingunge na wachangiaji wengi wa topic tunashindwa kukiona katika big picture ya hii ishu,

- Taifa likishakuwa na vacuum ya uongozi wa juu kama tulivyo, inatoa nafasi kwa wananchi binafsi, private sectors, matajiri, au vikundi vya dini as of this ishu ku-set the national agenda, au kuingiza pua zao kwenye process ya national policy making na ndio hasa wanachokifanya hawa viongozi wa dini, badala ya kuliachia bunge na viongozi wetu responsible kisheria ya jamhuri yetu.

- Under Mwalimu, ilikuwa ni very clear kwamba tunasimamia wapi as far as national policies na national priorities zetu, lakini that is not the case today hatueleweki tunasimamia wapi, tunakwenda wapi ingawa tunajua tulikotoka matokeo yake ndio haya tuliyonayo yaani kila mtu anajitokeza na kujaribu ku-set the agenda na sisi Great Thinkers bado tunalilia siasa za personalities, kumbe wakati mwingine ishus kama hizi hazina uhusiano wowote na personalities,

Isipokuwa ni vacuum tu ya uongozi wa juu wa taifa!

Respect.

FMEs!

Religion shouldn't take advantage of Vacuum kupenyeza pua zao.
Mahakama za kadhi, Waraka wa dini, etc. What non-sense?!

Mahakama za kadhi:
- Naitwa kwenye mahakama ya kadhi kwa sababu...etc etc
- Nawajibu, nilibadilisha dini. Mimi sasa sina dini.
- Ha ha ha ha....watanifanya nini?

Waraka wa kiongozi:
- Dini mmemaliza kufundisha sasa mnataka kufundisha siasa?

When will this vacuum be filled?!!
 
Kingunge is right in all rights!
Religion has overstepped its objectives in a secular country. They need to back down or the government should act NOW to keep religion within its boundaries. Otherwise this country will end in a mess.

You are very wrong my friend - in 2005 when some of the very same religious leaders came out openly and declared Kikwete ni chaguo la Mungu, where was Kigunge and those of his ilk. If I remember right they all felt very comfortable with this, you know why ? - they could sit back and relax because the status quo was in no way threatened.

There are times when the populace has thrown blame to our religious leaders for keeping quiet when things go wrong. Kigunge has thrown a bait and surely people like you, Insurgent, are taking it line, hook and sinker - this was expected as it takes the pressure off and gives them the much needed breathing space.

The so called waraka does not introduce anything new but only reminds the wananchi to cast their votes wisely without looking at ones religion, race, gender or creed but to be wary of corrupt individuals - to oppose this, one must have some hidden and suspect motive up one's sleeve and Kigunge Ngombale Mwiru has plenty.
 
You are very wrong my friend - in 2005 when some of the very same religious leaders came out openly and declared Kikwete ni chaguo la Mungu, where was Kigunge and those of his ilk. If I remember right they all felt very comfortable with this, you know why ? - they could sit back and relax because the status quo was in no way threatened.

There are times when the populace has thrown blame to our religious leaders for keeping quiet when things go wrong. Kigunge has thrown a bait and surely people like you, Insurgent, are taking it line, hook and sinker - this was expected as it takes the pressure off and gives them the much needed breathing space.

The so called waraka does not introduce anything new but only reminds the wananchi to cast their votes wisely without looking at ones religion, race, gender or creed but to be wary of corrupt individuals - to oppose this, one must have some hidden and suspect motive up one's sleeve and Kigunge Ngombale Mwiru has plenty.

- Sawa sawa!

Respect.

FMEs!
 
..hivi Kingunge alipotumbukiza hoja ya Mahakama ya Kadhi kwenye ilani ya uchaguzi wa CCM alikuwa hajui kwamba dini inapaswa kutenganishwa na siasa?
 
Religion shouldn't take advantage of Vacuum kupenyeza pua zao.
Mahakama za kadhi, Waraka wa dini, etc. What non-sense?!

Mahakama za kadhi:
- Naitwa kwenye mahakama ya kadhi kwa sababu...etc etc
- Nawajibu, nilibadilisha dini. Mimi sasa sina dini.
- Ha ha ha ha....watanifanya nini?

Waraka wa kiongozi:
- Dini mmemaliza kufundisha sasa mnataka kufundisha siasa?

When will this vacuum be filled?!!

Not true!
Avoid being static and trigger your memory.

Many times ‘religions’ have been invited by the same government to provide solutions for problems which in all senses do not need heavenly power.

From corruption, HIV/AIDS problem, blessing of various government events (plus the parliament) to even rainmaking! Both churches and mosques have been used to assure the public that the government cares for them on all calamities.

Do you think this time the church needed to be invited for views and strategies upon the immoralities. The church has been doing these even without ‘vacuum’
 
Huyu mzee ameshachanganyikiwa sijui anachokitafuta ni nini while ameshajizeekea, KINGUNGE UMESHACHUKUA PESA ZETU VYA KUTOSHA SASA TUKIAMUA KUKUGEUKIA YATAKUKUTA MENGINE BADO PARKING ZOTE UNAWAKAMUA WATANZANIA, BADO STAND YA MKOA UNAWAKAMUA WATANZANIA HEBU TULIA USIJARIBU KUAMSHA HASIRA ZA WANANCHI BWANA
 
"Dini, katika Nchi yenye Madhehebu mbalimbali, kamwe haiunganishi Watu bali hutenganisha Watu. Ndiyo maana Waasisi wa Taifa hili wametumia Siasa, na siyo Dini, kuunganisha Watu", Kingunge Ngombae-Mwiru, akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam Agosti 12, 2009.

"Dola lazima isimamie Sheria ili kulinda Haki na kuhifadhi Amani. Wajibu huu usipozingatiwa, wataibuka Manabii wenye kuihubiri Haki kwa kuwahukumu wengine. Hamtabaki Salama mkifikia hapo," Mwalimu J.K. Nyerere, Dodoma 1995.

Nukuu hizo ni muhimu kwa mjadala unaendelea sasa kuhusu "Ilani" ya Wakatoliki na Udini!
Hao waliotoa Ilani hiyo ni kina nani hao, watufundishe sisi wote namna ya kuwapata viongozi wazuri? Kwa nini wasiandike Waraka wa namna nzuri ya kumchagua "Pope", ambaye hachaguliwi na wananchi na uchaguzi wake, ukichukulia kama inavyosemwa kuwa Vatican ni nchi, hufanywa "in the most undemocratic way!"
Pili, hawa (wanaotetea Ilani ya Wakatoliki) wanaomwita Ngombale-Mwiru na watu wengine kuwa ni "Mafisadi" na kwamba viongozi wa sasa hawafai na wanataka wapatikane wengine bora pamoja na kuwa tubadili Katiba, ndio "Manabii" aliowazungumzia Mwalimu hawa! Tujiangalie, tunaeleka mahali ambapo hatutakuwa salama!

Bwassa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom