Kama kuna hoja hakuna tatizo. Watu wananmwuliza aonyeshe hayo mambo yanayohatarisha amani. Jibu lake ni kuwa waraka utawagawa watanzania. Kwa mtu wa namna hii kuna haja gani ya kumsikiliza? No resesearch no right to speak inafanya kazi hapa.Kingunge kama Mtanzania mwengine (bila kujali umri wake) ana haki ya kutoa maoni yake na kushawishi kwa hoja kile anachoamini (in this case yuko kinyume na Kanisa kuhusu waraka). Haki hiyo ya kutoa maoni yake haizeeki au kupungua kwa kadiri mtu anavyoingia uzee. Na kimsingi haipimiki kwa umri, usomi, n.k
Ni vizuri basi tukahukumu hoja zake na kuzionesha jinsi gani zilivyo dhaifu bila ulazima wa kuziunganisha hoja hizo na umri wake kwani kwa kufanya hivyo tunatengeneza ubaguzi wa kiumri - kuwa wazee hawatakiwi kutoa maoni yao! .
Unakataa uzee usitumike kujadili pumba zake ambazo wewe unaita maoni wakati huohuo wewe mwenyewe unasema uzee wao usitumike hapa uko upande upi? Kilichowazi lazima kutafuta chanzo cha mtu kutoa pumba kama za huyu mzee. Moja wapo ni kuishiwa uwezo wa ufikiri ukihusishwa na umri kumtupa mkono. Kubwa zaidi ni UFISADI ambao ndio umemsukuma kutamka hayaNa vile vile wale ambao ni wazee wasitumie uzee wao kufikiri ya kwamba ndio kunawapa haki zaidi ya kutoa maoni au kwa sababu ya umri basi maoni yao yana nguvu zaidi au yasikilizwe zaidi. Kila maoni au hoja ipimwe kwa ushahidi wake wa kimantiki na mvuto wake wa vithibitisho vyake.
mmh huyu mbunge sijui wa chama gani?maana sijamuelewa kabisa yuko upande ganiTUNACHOTAKIWA Watanzania wote kwa pamoja ni kuamua je, tunachotaka kuweka mbele ni UTANZANIA na UAFRIKA wetu au kabila, dini, rangi, jinsia, usomi, vyeo, kazi, mali au ukoo wetu ?
Kama tumeamua kumpa MUNGU kilicho cha Kaizari sawa!!!
Kama tumeamua kwamba mpanda fahali wawili hawezi kupasuka msamba basi tuendelee na kupanda fahali wawili!
Kama tumeamua kwamba kujenga ufa ni kwa kuongeza ufa mwingine tufanye hivyo!
Kama tumeamua kwamba gauni au suruali mpya hupatikana kwa kushona kiraka juu ya kraka tuendelee vivyo hivyo!
Kama tumeamua kwamba akumulikaye mchana usiku hatakuchoma bali atakumwagia maji ya baridi kwanini tuogope maji ya baridi?
Kama akili ni nywele na kila askofu na sheikh ana mvi na sio nywele nyeusi na tumezipenda mvi zisizo na hekima wala busara kwanini tusizipende!!!
Kama tunadhani fataki hawezi kuwepo kwenye majengo ya makanisa na misikiti tuendelee kuruhusu hata wenda nusu uchi kuja kuswali.
Kama hatujui asiyekutaka au anayekutakia baya hawezi kukwambia toka au hawezi bayana bin bayana kukulaani ngoja asubihi ipishe mchana na jioni ipishe usiku.
mmh huyu mbunge sijui wa chama gani?maana sijamuelewa kabisa yuko upande gani
Nimekuelewa vema, hata hivyo wale wanao lilia wembe wakiamini haukati si wapewe?TUNACHOTAKIWA Watanzania wote kwa pamoja ni kuamua je, tunachotaka kuweka mbele ni UTANZANIA na UAFRIKA wetu au kabila, dini, rangi, jinsia, usomi, vyeo, kazi, mali au ukoo wetu ?
Kama tumeamua kumpa MUNGU kilicho cha Kaizari sawa!!!
Kama tumeamua kwamba mpanda fahali wawili hawezi kupasuka msamba basi tuendelee na kupanda fahali wawili!
Kama tumeamua kwamba kujenga ufa ni kwa kuongeza ufa mwingine tufanye hivyo!
Kama tumeamua kwamba gauni au suruali mpya hupatikana kwa kushona kiraka juu ya kraka tuendelee vivyo hivyo!
Kama tumeamua kwamba akumulikaye mchana usiku hatakuchoma bali atakumwagia maji ya baridi kwanini tuogope maji ya baridi?
Kama akili ni nywele na kila askofu na sheikh ana mvi na sio nywele nyeusi na tumezipenda mvi zisizo na hekima wala busara kwanini tusizipende!!!
Kama tunadhani fataki hawezi kuwepo kwenye majengo ya makanisa na misikiti tuendelee kuruhusu hata wenda nusu uchi kuja kuswali.
Kama hatujui asiyekutaka au anayekutakia baya hawezi kukwambia toka au hawezi bayana bin bayana kukulaani ngoja asubihi ipishe mchana na jioni ipishe usiku.
badilisha rangi, kisha jifunze kuweka spacing
badilisha rangi, kisha jifunze kuweka spacing
Sioni mahali popote ambapo waraka huo wa Katholiki unashabikia kwa namna yoyote uwakilishi wa kidhehebu. Waraka huo haujasema kiongozi bora ni lazima awe mkristu, au ni lazima aamini lolote linaloaminiwa na wakristu, wala anaeshiriki katika mambo yanayoshirikisha ukristu.Hata kama kimantiki, Waraka wa Wakatoliki unazungumzia uraia mwema na jinsi wananchi watakavyoweza kupata viongozi bora, ukweli upo pale pale kwamba "muwamba ngozi huvutia kwake"; na kama kila dhehebu litatoa waraka kwa waumini wake mwishowe tutakuwa na wawakilishi wa kidhehebu.
Serikali inapaswa kutoa mwongozo kwamba siasa zisiwe jambo la mahubiri katika vikao vya dini ama katika nyaraka zao. Hilo halitakuwa jambo jipya. Hata Katiba ya Tanzania, Ibara 19 inatamka dini itakuwa sio shughuli za Serikali. Kwa hiyo dini zisiingilie katika uchaguzi wa viongozi wa Serikali.
Mkuu, sidhani kuwa hayo yamesemwa kwenye waraka huo. Labda utusaidie kujua ni kwenye kurasa zipi maneno hayo yaliandikwa.mimi nahsi mzee kingunge amesema kweli. kwani amesema ndani ya waraka huo uansema " kanisa litahakikisha linaweka watu wake na kuwadhibiti" sasa jee kanisa litapofanikiwa kuweka watu wake na kuwadhibiti . itakuwa kwa manufaa ya nani?
Jana Mzee wetu alitoa nafasi nzuri sana kwa Waandishi wetu kwa niaba ya Watanzania kumuuliza maswali mazuri na mazito ambayo pengine yangetusaidia kuelewa tamko lake lile kule Bungeni lilikuwa na maana gani. Nahisi nafasi ile haikutumika vizuri aidha kwa kuwa waandishi waliokwenda pale hawakujiandaa kwa lolote upande wao zaidi ya yale mazoea ya kwenda kuwasikiliza viongozi wetu na kesho yake kuwanukuu kwenye magazeti au Wahariri wetu waliudharau mkutano ule wakawatumaa waandishi-wanafunzi wengi.
Nasema hivyo kwa kuwa nimepitia magazeti kadhaa asubuhi hii sijaona swali zito na la maana aliloulizwa Kingunge kama vile:
1. Mahakama ya KADHI iliingiaje kwenye ILANI ya uchaguzi ya CCM 2005?
2. Waraka ule umeandaliwa na MAASKOFU au CPT?
3. Nini hasa kilichomo kwenye waraka ule ambacho ni cha KIDINI?
4. Waraka hu ni wa kwanza kutolewa na CPT?
5. Utajiri wa kupindukia walio nao baadhi ya wanasiasa unatokana na nini?
6. Utajiri wa mwanae Kinjekitile hauna uhusiano na yeye anayekataa kuwa sio FISADI
Na mengine mengi tu. Waandishi ambao sasa mnajiita MHIMILI wa NNE wa DOLA zitumieni vizuri nafasi hizi kwa niaba yetu.