Kikwete siyo safi! - yes I said it!

Kazi ipo kweli kweli.

Dr Slaa alipotaja majina ya Mafisadi hakumpa upendeleo Kikwete kwa kuweka hofu ni Rais, yeye alitaja list ya Mafisadi na sababu za kuwaita Mafisadi na kuacha wakachambuane wenyewe huko mbele ya safari nani Bosi nani tarishi.

Rais wa nchi siyo Mungu na wala hatakua Mungu hata siku moja.
pamoja na ukweli kwamba katiba ya nchi imejaribu kumjengea throne ya kuonekana Mungu.

Rais akiiba anaitwa mwizi kama mtu mwingine yeyote yule.

Amini alikuwa rais wa Uganda akaua watu kibao na aliitwa Muuaji.

Endapo ushahidi wote unaonyesha Kikwete ni Fisadi

Tamko kwamba Tanzania ilifanya makosa makubwa sana kumchagua MH Kikwete kuwa Rais kwa sababu ni Fisadi pia anakumbatia Maharamia wa ndani na nje ya nchi kama mzungu Sinclair linakuwa na mantiki makubwa kwa Watanzania.

Najua Watanzania wengi list ya Mafisadi imetuduwaza hata tumefikia hatua ya kuto jua cha kufanya kwa vile Rais naye yumo kwenye List ya Mafisadi.
Hiki ni kilio chetu wananchi wenyewe jambo limo mikononi mwetu, sisi ndio mahakimu na wasemaji wa mwisho. Tukimaliza mjadala hapo 2010 utakuwa ni wakati mwafaka wa kutoa hukumu kwa wahusika wote na wengine watakao tajwa, kwa haki.

Kukataa ukweli kwa vile tu anayesemwa ni Rais ni kurudi nyuma katika mapambano haya makali na ya kihistoria na kuepuka kutoa hukumu ya haki na inayostahili.

Bado hatujafikia hatua ya kumshika Pembe fahari wetu na kumgaragaza.

Hapa tunatekenya Kende za fahari wetu kwa unyoya mrefu wa jogoo kimaudhi maudhi. Hatari kubwa hapa si kupigwa pembe, ni kupigwa mateke ndiyo maana tunachomeka unyoya wetu kwenye fimbo ndefu na kuzitekenya kwa mbali Hii! Hii! Hii!

Maudhi yakizidi atasema yote na ulimi wake mwenyewe ndo utamponza.
 
Urais ni kazi nzito sana, inayohitaji kutumia busara kabla ya kufanya maamuzi muhimu ya taifa, ikiwa ni pamoja na kuwasikiliza kwa makini washauri wake wa kuitawala na kisiasa, pamoja na kisheria, mambo ya kukurupuka yalituponza taifa tukawalipa mamillioni lukuki watu fulani wa benki kuu, enzi zile za Mkapa, tumewalipa mamillioni lukuki ndugu wa Kombe, kutokana na kurupu kurupu!
Hapa kuna ukweli lakini yeye ameshakuwa kwenye hiyo nafasi kama amiri jeshi mkuu kwa takribani miaka miwili,Hivyo kama ni uchunguzi na kuweza kujiridhisha ktk ishu mbali mbali amepata muda wakutosha na imefikia wakati wa kuyatolea maamuzi na kuyasimamia maamuzi yake kwa manufaa ya taifa na si kwa manufaa ya kundi lake au wanaojiita wafadhili au wawekezaji.
Binafsi bado niko radhi kusubiri, na sijafikia hatua ya kuamini kuwa Muungwana ni mchafu, just because hasikilizi mob justice, hapana urais una maadili yake na miiko yake, na busara zake tofauti kabisa na busara za kuwa upinzani kwenye siasa za taifa, au hii forum,
Ni kweli Urais una maadili yake Lakini yeye ameonyesha mengi kutoyafuata,Kuna mambo yanahitaji maelezo ya haraka kutoka kwa watendaji wako ili waonyeshe uwajibikaji na wanaposhindwa kuyatolea maelezo na wananchi wakarithika huna budi kuwawajibisha hata kwa kuwaambia waachie ngazi Lakini kuendelea kuwakingia kifua kunamfanya na yeye kuingia moja kwa moja kwenye kundi hilo kwa kutoonyesha uwajibikaji pia kama amiri jeshi mkuu na kutofanya maamuzi sahihi.
 
Mh! Nchi ilianza kuliwa zamani. Lowassa na Karamagi walikutana Hotelini kwa bahati mbaya? Hii haiwezi kuwa hoja, waeleze kwa kina ilikuwaje hadi wakagongana, ni dhahiri ilipangwa.
 
Wanduguzanguni! Mmesahau kuwa kuna kiongozi mmoja aliwahi kusema kuwa RADA NA NDEGE YA RAIS LAZIMA VINUNULIWE HATA KAMA WATANZANIA WATAKULA NYASI? Je, huyu alikuwa ni Kikwete? Kama hakuwa yeye, do you think kwa kuwa WAZIRI WA MABO YA NJE, au whatever, yeye angeweza kuzuia, ikiwa ni pamoja na kum-counter attack Rais Mkapa? Mkataba wa IPTL unafall kwenye similar analogue. Mzee mwanakijiji wkt mwingine unaleta threads zenye biases 100%!
 
kikwete licha ya kuwa alifanya ufisadi kwa kutotetea mikataba mibovu, na kuendelea kutia saini mikataba hiyo bila ya kujali masilahi ya wananchi, yeye anaingia kwenye ufisadi kwa kuwa anawakumbatia mafisadi hawa. lazima tuukubali ukweli wa kuwa unapowakumbbatia mafisadi na wewe unakuwa mmoja wao
 
Binafsi naamini kumuingiza JK kwenye list ya Mafisadi lilikuwa ni kosa kubwa. Kwanza ushahidi wa ufisadi wake ni wa kimazingira zaidi kuliko data za uhakika. Pili kwa kumwingiza na yeye kwenye hilo kundi tayari inakuwa ngumu kwake kuwawajibisha wale wengine kwa kutumia kigezo cha ufisadi maana kama wale ni mafisadi na yeye ni mmoja wapo.

Mimi bado naamini ingelikuwa vizuri sana kumtenganisha JK na mtu kama Lowassa, lakini kwasasa tumewaunganisha kwa kuwafunga pamoja kama mafisadi.

Kuhusu hotuba zake kuwa tofauti anapokuwa nje na nchi na zile anazotoa TZ. Hilo nafikiri linaeleweka, akiwa ndani anataka kuwahakikishia wana CCM kwamba bado wanashika UTAMU, maana kwa makada wasingetaka compromise ya aina yoyote. Anapokuwa nje anafurahisha wanaompa misaada.

Utendaji wa JK umekuwa mbovu mno kuliko watu wengi tulivyotegemea, ila tu ana muda, kama atajirekebisha mapema basi anaweza kuokoa jahazi. Kumbukeni rais Clinton alivyovurunda wakati wa kipindi cha kwanza cha urais wake lakini akaweza kubadili mwelekeo muda mfupi kabla ya uchaguzi uliofuata.

Je JK ni fisadi? Mimi kwasasa nitakuwa NEUTRAL juu ya dai hili, sijawa convinced na vigezo vinavyotumika kumhukumu lakini pia sijafurahishwa na ukimya wake.
 
Wakuu naona twende mbele na nyuma pia tuangalie, kazi za rais ni nini na ni zipi? Na the good president kwa standard zetu hapa forum, since so far wengi tunaamini kuwa ameshindwa in 23 months, alitakiwa awe amefanya nini so far? na awe hakufanya nini

I am just curious?
 
Je JK ni fisadi? Mimi kwasasa nitakuwa NEUTRAL juu ya dai hili, sijawa convinced na vigezo vinavyotumika kumhukumu lakini pia sijafurahishwa na ukimya wake.

Mtanzania inategemea kwako definition ya ufisadi ni nini. Kama una maana kupokea na kutoa rushwa (moja ya ahadi 10 za mwana TANU) Basi huenda ntakubaliana na wewe kuwa neutral, Lakini kama ufisadi ni more that receiving bribes, naweza kupingana na wewe? Kwa lay man kama mimi naweza kujiuliza kwanini JK anatetea Richmond, Kwanini anamlinda Mkapa, kwanini anamlinda yule mhindi aliyetuingiza mkenge kwa rada, kwanini anamchekea Karamagi, kwanini anakumbatia ufisadi??????
Unajua wakati mwingine inaweza kuwa ni vigumu ukianza kuwaambia watu wa-prove the obvious, outsiders tunaona kuwa haya mambo yanaonesha kuwa many things are wrong there (na sio something is wrong somewhere)
Ukisikia sasa hivi watu wanasema kuwa JK ni safi wanaogopa kwa sababu yeye ni Rais, lakini hii haina maana kuwa ni kweli yeye ni safi. Kama angekuwa safi Rugemalila sasa hivi angekuwa ndani, Buzwagi asingeikalia kimya, na Mkapa asingemkalia Kimya.
 
Kikwete ni fisadi tu..

richmonduli, buzwagi, nk vyote vimefanyika chini yake na anahusika moja kwa moja kama rais. Mikataba mingine ya madini yote "inayorekebishwa" Kikwete anahusika na sofar guys mnaona mikataba "iliyorekebishwa" ilivyo...

Kashfa zake akiwa madini zilimhusu yeye moja kwa moja. Miezi sita ya kwanza ya Kikwete ikulu, taarifa ya mkaguzi wa hesabu iligundua matumizi ya karibu billion moja yasiyothibitishwa kwa receipts au authorizations( kwa lugha rahisi - bilioni ziliibwa).

Huu usafi wa Kikwete uko wapi?

Documentation za mambo yake ni nyingi ila mengine yanatunzwa tu hapa yasiweke hadharani na lawyers wake wakajiandaa na utetezi. Huyu Kikwete lazima atasimama mahakamani siku moja kujibu!
 
Kikwete ni fisadi tu..

richmonduli, buzwagi, nk vyote vimefanyika chini yake na anahusika moja kwa moja kama rais. Mikataba mingine ya madini yote "inayorekebishwa" Kikwete anahusika na sofar guys mnaona mikataba "iliyorekebishwa" ilivyo...

Kashfa zake akiwa madini zilimhusu yeye moja kwa moja. Miezi sita ya kwanza ya Kikwete ikulu, taarifa ya mkaguzi wa hesabu iligundua matumizi ya karibu billion moja yasiyothibitishwa kwa receipts au authorizations( kwa lugha rahisi - bilioni ziliibwa).

Huu usafi wa Kikwete uko wapi?

Documentation za mambo yake ni nyingi ila mengine yanatunzwa tu hapa yasiweke hadharani na lawyers wake wakajiandaa na utetezi. Huyu Kikwete lazima atasimama mahakamani siku moja kujibu!

Sasa mtu mchafu inakuwakuwaje akachaguliwa kuwa raisi kwa asilimia zote hizo? Si mambo kama haya (uchafu) ndio yalitakiwa yazungumzwe kwenye kampeni. Na kama yalizungumzwa na watu bado wakamchagua, hiyo inasema nini kuhusu watu hao?
 
Sasa mtu mchafu inakuwakuwaje akachaguliwa kuwa raisi kwa asilimia zote hizo? Si mambo kama haya (uchafu) ndio yalitakiwa yazungumzwe kwenye kampeni. Na kama yalizungumzwa na watu bado wakamchagua, hiyo inasema nini kuhusu watu hao?

Hii inasema kuwa hao watu wanahitaji kufanyiwa mental evaluation kama kweli walimchagua huyu Kikwete. Au sivyo inawezekana hawa watu hawakuelezwa ukweli halisi kuhusu huyu guy ukichukulia media kampeni ya Rostam Aziz.

Kama viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe, I am afraid soon nitaanza kukubaliana na arguments zako kuwa kuna tatizo na sisi watanzania na waafrika kwa ujumla!
 
Sasa mtu mchafu inakuwakuwaje akachaguliwa kuwa raisi kwa asilimia zote hizo? Si mambo kama haya (uchafu) ndio yalitakiwa yazungumzwe kwenye kampeni. Na kama yalizungumzwa na watu bado wakamchagua, hiyo inasema nini kuhusu watu hao?

Kazi ya spinning hiyo mazee na wanawanchi wakavaa mkenge kama wamesimama :(
 
Hii inasema kuwa hao watu wanahitaji kufanyiwa mental evaluation kama kweli walimchagua huyu Kikwete. Au sivyo inawezekana hawa watu hawakuelezwa ukweli halisi kuhusu huyu guy ukichukulia media kampeni ya Rostam Aziz.

Kama viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe, I am afraid soon nitaanza kukubaliana na arguments zako kuwa kuna tatizo na sisi watanzania na waafrika kwa ujumla!

Kama huamini kwamba viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe subiri ifikapo 2010. Mtanikumbuka! Ila kwangu mimi binafsi sioni haja ya kusubiri hadi 2010. Nilishaliona hilo toka zamaaaaani na ndio maana sikuona chochote alichokuwa nacho huyo Kikwete zaidi ya personality. Kwa kweli ningefurahi kama Salim Ahmed Salim angekuwa raisi. But oh well....we deserve the people we elect.
 
Hadi leo watu mna-amini jk alipata kura 80 percent? believe this? you will believe everything!!!
Listen in 2002 Sadam hussein got 99.9 percent of all votes
Mugabe got almost 80 Percent in last election!

Tuliambiwa ati Mkapa ni Mr. Clean; sasa tunamwitaje? Tungojee baada ya miaka 10!!!
 
Kama huamini kwamba viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe subiri ifikapo 2010. Mtanikumbuka! Ila kwangu mimi binafsi sioni haja ya kusubiri hadi 2010. Nilishaliona hilo toka zamaaaaani na ndio maana sikuona chochote alichokuwa nacho huyo Kikwete zaidi ya personality. Kwa kweli ningefurahi kama Salim Ahmed Salim angekuwa raisi. But oh well....we deserve the people we elect.

Nyani,

nakumbuka arguments zako against Kikwete kipindi kile cha kampeni. Inasikitisha jinsi supporters wa Kikwete walivyokuwa na zero answer wakiulizwa sifa za kiutendaji za Kikwete.

Mama yangu mzazi mwenyewe alimpigia Kikwete kampeni big time. Kila tukimuuliza nyumbani kwa nini anataka Kikwete awe prezida yeye anasema vitu kama handsome boy, JK kuhudhuria mashindano ya mamiss, ni mpole kwa hiyo hataleta fujo nchini, and so on.

Well, Labda nikubaliane na wengine kuwa ndio imetoka hivyo. The guy akipenda ataiba kura 2010 na ataendelea kuwa rais na kuvumbua dunia upya (as if Vasco da gama na Columbus hawajafanya hivyo tayari).

Kila siku mikataba hii ikivuja hapa, ninamtumia my mom copy ili asikilize muziki mpya wa handsome boy!.... poor mom, utakuwa kiziwi mwaka huu!
 
Kuna hii theory pia kwamba watz tunapenda kusifia watu wanaopaa kimaisha kiajabujabu, mtu anaporomosha majumba harakaharaka, tunamchekea, mshikaji anafanya TRA anapiga deal za kukwepesha kodi, tunamshangilia, mtu akifake receipt ofisini anasifika. Mtu akirudisha imprest ambayo hakutumia tunamshangaa na kumcheka. Na huu ndio ufisadi wenyewe tunaongelea, je ndio tuseme watz tunapenda ufisadi au namna gani?
 
Nadhani hapa mnaibua mambo muhimku sana "Kwanini Kikwete alichaguliwa?" ni swali muhimu sana katika mjadala huu.
 
kikwete siyo msafi-hata mwalimu alijua!
mie naumia sana hasa nikisoma mikataba inayoingiwa na hawa wanojifanya mbumbuu,
ipo siku..
ipo siku watang'oka tu!
 
Back
Top Bottom