Kikwete bila Lowassa ndiyo maana amepwaya!?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Mambo mengi yamesemwa humu ndani kuhusu uhusiano wa Lowassa na Jakaya Kikwete na ile hoja kwamba wawili hawa hawakukutana barabarani inajulikana na kila mmoja wetu. Lakini Historia inaonyesha kwamba ni Lowassa ndiye aliyemtengeneza Kikwete kuwa "Presidential material" na wala si Kikwete aliyemtengeneza Lowassa. Kwa maana nyingine Kikwete ni zao la Lowassa.

Hata timu za ushindi na jinsi ya kukusanya fedha na kuteka nyara vyombo vya habari likuwa ni kazi ya Lowassa. Ukiangalia kwa undani bila ya makengeza ya ushabiki utagundua kwamba Kikwete "aliwekwa" na wanamtandao na wanamtandao ni kazi ya mikono ya Lowassa.

Walipoingia madarakani ni Lowassa ndiye aliyekuwa anaonyesha njia ni wapi wanaelekea, shule za kata na hata kuhimili serikali za mitaa ilikuwa ni kazi ya Lowassa. Lakini tangu Lowassa alipopata "ajali ya kisiasa" na "kuachia ngazi" serikali ya Kikwete imepata myumbo mkubwa sana na hakuna dalili kwamba itatoka huko iliko na badala yake siku hadi siku inapoteza uhalali wa kutuongoza watanzania.

Lakini swali langu linalohitaji kujadiliwa ni kama Kikwete amepoteza Mwelekeo kutokana na Lowassa kujiondoa kwenye serikali yake au tangu mwanzo wakiwa na Lowassa tayari walishapoteza mwelekeo?
 
hakuna presidential materail ndani ya ccm. JK alipata kuteuliwa kugombea kwa neema tu maana hata ripoti yake alikuwa nafasi karibu na ya 10. amshukuru ben otherwise angeliusikia uraisi bombani.
 
Inawezekana pakawa na ukweli katika hilo. Ninachokifurahia zaidi ni kwamba Hon. Edward Ngoyai Lowassa ndiye rais ajaye wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
hakuna presidential materail ndani ya ccm. JK alipata kuteuliwa kugombea kwa neema tu maana hata ripoti yake alikuwa nafasi karibu na ya 10. amshukuru ben otherwise angeliusikia uraisi bombani.

Hakuwa mbali kihivyo ila nakumbuka kwa usahihi kwamba alipata asilimia 33 ya kura zote za NEC kwa maana nyingie asilimia 67 ya wajumbe wa NEC walikuwa hawana imani na Kikwete. Na ndiyo maana utaona ni kwa jinsi gani aivyoingia tu kwenye uenyekiti wa CCM mwaka 2006 aliisambaratisha Sekretarieti ya Nec bila huruma kwa sababu Sekretarieti hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Mangula ilikuwa haina imani naye!!
 
Inawezekana pakawa na ukweli katika hilo. Ninachokifurahia zaidi ni kwamba Hon. Edward Ngoyai Lowassa ndiye rais ajaye wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
tupate rahisi mtuhumiwa wa Rushwa Zinza umepotea.
Mkumbuke nyerere alisema mke wa kaisari hatakiwi kutuhumiwa.
au mtu anayetumia hella kuingia ikulu niwa kuogopwa kama ukoma,kwa nini kama yeye ni bora atumie hela?kuingiza mtandao wake waliiba hela za EPA hadi leo mtuhumiwa mkuu wa epa kagoda yuko nje na yeye kama wairi mkuu hakufanya jitihada za kumkamata.
hana uchungu na masikini wa tanzania ndiyo maana anaitafuta ikulu kwa pesa na nyie msiojitambua poleni sana
 
mimi kama mimi peter kilawe
nachojua lowasa nimtu ambae atatuondoa ama kutukomboa hapa tulipo
namkubalisana
jiulize istoria ya nyuma dawasa mwekezaji alipewa masaa mangapi .?awe ashaondoka hapa nchini?
lowasa lowasa kurayangu nakupa namkubali mmno
 

Attachments

  • Photo0003.jpg
    Photo0003.jpg
    27.6 KB · Views: 121
kwa nini mumfagilie mtuhumiwa mkuu wa ufisadi?hivi Tz imekosa watu makini kweli kwanza aje atuombe radhi kwa kutuingiza kwenye mkenge wa dowans na Richmond
 
Ole wenu mumkabidhi kichaa rungu,Yaani mie sielewi nitahamia nchi gani duniani.EL ni mtu wa visasi kupitiliza.Anamwondoa nani atamwaacha nani.Maana hata lile kabila lake la asili amelikana mbele ya uso wa dunia.Muogopeni mtu huyu kuliko kitu chochote kilicho hai juu ya uso wa nchi.:msela:
 
Nakubaliana na wewe kabisa...Kikwete bila Lowasa hakuna kitu ndio maana enzi zile wameingia madarakani kwa ARI MPYA watendaji wengi wa serikali walikuwa na dhana kuwa "BORA UKUMBANE USO KWA USO NA RAIS ILA SIYO WAZIRI MKUU"..
 
Inawezekana pakawa na ukweli katika hilo. Ninachokifurahia zaidi ni kwamba Hon. Edward Ngoyai Lowassa ndiye rais ajaye wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Umenena vema mkuu...japo akli yangu na iko CDM ila moyo wangu uko kwa LOWASSA.........
 
kwa nini mumfagilie mtuhumiwa mkuu wa ufisadi?hivi Tz imekosa watu makini kweli kwanza aje atuombe radhi kwa kutuingiza kwenye mkenge wa dowans na Richmond

Kutuhumiwa ni kutuhumiwa tu, hata Dr. Slaa anatuhumiwa kuchukua mke wa mtu na kumtelekeza mkewe wa zamani, lakini yote hiyo ni tuhuma tu bado hazijathibitishwa. Hapa hafagiliwi mtu tunachojaribu kuangalia nini mahusiano ya hawa watu wawili na taathira zake kwenye uongozi wa serikali ya Kikwete.

Sisi sote tusipojitia upofu tutaona kabisa kwamba Urais wa Kikwete ni kazi ya mikono ya Lowassa. Jee Kikwete yeye mwenyewe alikuwa keshajitayarisha kuwa Rais au Lowassa alimtumbukiza kwenye Urais ili yeye awe waziri mkuu mwenye nguvu kuliko Rais. haya ni sawa na yale ya Russia kati ya Vladimir Puttin na Dimitry Medvedev!!
 
Kuyumba kwa serikali sana kumejitokeza baada ya Lowasa kuachia ngazi, hakuna kiongozi anayeonekana kuwa na meno. Nakubaliana na dhana hii kwamba Lowasa ndiye aliyekuwa anafanya JK aonekane. Namkubali kwa urais Lowasa
 
Kutuhumiwa ni kutuhumiwa tu, hata Dr. Slaa anatuhumiwa kuchukua mke wa mtu na kumtelekeza mkewe wa zamani, lakini yote hiyo ni tuhuma tu bado hazijathibitishwa. Hapa hafagiliwi mtu tunachojaribu kuangalia nini mahusiano ya hawa watu wawili na taathira zake kwenye uongozi wa serikali ya Kikwete.

Sisi sote tusipojitia upofu tutaona kabisa kwamba Urais wa Kikwete ni kazi ya mikono ya Lowassa. Jee Kikwete yeye mwenyewe alikuwa keshajitayarisha kuwa Rais au Lowassa alimtumbukiza kwenye Urais ili yeye awe waziri mkuu mwenye nguvu kuliko Rais. haya ni sawa na yale ya Russia kati ya Vladimir Puttin na Dimitry Medvedev!!

Mbingu na nchi havifanani.Adui wetu ni umaskini uletwao na wafilisi wa inchi hii.swala sio wanahawa bali musa wa kututoa misri si kwa kutuibia bali kutuondolea utumwa huu wa umaskini toka misri ya wanyang'anyi,wa mali zetu.e.g JACOBO ZUMA. Hatuangali family affairs but brain values.
 
JK na lowassa ni Boys 2 Men! wametoka mbali mno tangu mwaka 1995 walipotaka kugombea urais! Nyerere aliwachinjia baharini kwa sababu hawakuwa na sifa za kuwa rais.
 
Ninaheshimu mawazo yenu wote lakini naomba tu kuwaza tofauti na ninyi kama hivi:
1. hawa jamaa walitumia njia nyingi za halali na haramu kwa zaidi ya Miaka 10 YAANI KABLA YA 1995 kujiandaa kuingia Ikulu,mara ya Kwanza Mwalimu Nyerere akawasambaratisha lakini kwa uzoefu wa kiaskari na suluba walijipa miaka 10 tangu hapo ya kujiandaa.
2.katika maandalizi yao haramu ama halali hawakuuhitaji ule mfumo rasmi uliopo wa kuweza kuingia Ikulu,yaani CCM na hata vyombo vingine.Walichofanya kama VIRUS wa UKIMWI, waliuzubaisha mfumo kias kwamba hawa jamaa walimshangaza hata Mzee wa Lushoto/Sea View/Nanyumbu akakuta hana njia ya kuwazima na mfumo wa kinga za mwili za serikali ukawa umeshaingiliwa kitaalamu wanasema immunity was compromised!
3.kwa kuwa kutawala kwa miaka hii ya sasa ni sayansi utaona kuwa EL alikuwa akifanya kazi ya kuzima moto labda kwa design au kwa kukosa uelewa,au kwa kuwa njia rahisi ya kufanya ufisadi usishtukiwe ni kuwa na majanga ya ajabu ajabu:mvua za kutengenezwa,richmond,madarasa fasta fasta,BARA BARA YA SHEKILANGO NA UPANUZI WA KI-UJIMA WA ALI HASSANI MWINYI ETI GARI MBILI KUELEKEA MJINI ASUBUHI NA MBILI KUELEKEA MWENGE JIONI,ni ishara tosha ya uongozi duni.Zingatieni kuwa mtu wetu EL anasema hata akirudishwa leo atafanya uamuzi richmond-shule za kata type!kura yangu ijapokuwa moja hawezi kupata!Ni kiongozi wa makabila ya ujima huko jirani na kilimanjaro lakini karne ya 21 ndiye siye!
3.Kutoka 2 hapo juu hawa jamaa hawakuwa na mfumo mpya waliotengeneza ama mkakati wa kututoa tulipoachwa na Mkapa.Hawakuwa na hata umoja kikazi kama serikali.Kama Rais anafika sehemu lilipovunjika daraja kabla ya waziri wa miundombinu tafsiri ni nini?japo daraja lile ni maeneo ya nyumbani kwa mtu.unaona ni wazi hakukuwepo na mpango wowote wa kukuza uchumi,kuongeza utoaji wa huduma muhimu wala kuongeza uwekezaji wenye manufaa kwa Watanzania.
4.Nione kwamba hata EL angekuwepo kwa Serikali ingeyumba tu maana msingi wake ni kama ile hadithi ya Biblia ya mtu aliyejenga nyumba yake mchangani ,mvua na mafuriko vilipokuja ilianguka!
 
Kikwete mtego wake ulikuwa na uwezo uwezo wa kumkamata Sungura lakini akawa anamuomba Mungu akute limenasa Tembo, Mungu nae hakufanya ajizi akasikia kilio chake akamleta Tembo kweli sasa ebu tujiulize usalama wa mtego.
 
JK na lowassa ni Boys 2 Men! wametoka mbali mno tangu mwaka 1995 walipotaka kugombea urais! Nyerere aliwachinjia baharini kwa sababu hawakuwa na sifa za kuwa rais.
unamaana ndo maana walimwekea sumu kwenye damu mpaka apate cancer ili watimize azma yao ya kuingiza genge ka mafia ikulu? Style waliyoitumia kwa wabaya wao wengine, mwakyembe na mwandosya.Ukiangalia utaona mbinu hizi zinaendelea kutumika (Ulimboka) japo Rostam Aziz na ED L hawapo serikalini .which leaves only one prime suspect in office.
 
Back
Top Bottom