Kikwete bila Lowassa ndiyo maana amepwaya!?

JK na lowassa ni Boys 2 Men! wametoka mbali mno tangu mwaka 1995 walipotaka kugombea urais! Nyerere aliwachinjia baharini kwa sababu hawakuwa na sifa za kuwa rais.
unamaana ndo maana walimwekea sumu kwenye damu mpaka akapata cancer na kufa ili watimize azma yao ya kuingiza genge la mafia ikulu? Style waliyoitumia kwa wabaya wao wengine, mwakyembe na mwandosya.Ukiangalia utaona mbinu hizi zinaendelea kutumika (Ulimboka) japo Rostam Aziz na ED L hawapo serikalini .which leaves only one prime suspect stll in office.
 
Kwa hakika EL alikuwa ndiyo "google" ya JK.
Nakumbuka (tena bila unafiki) kwamba, walau kwa kipindi kile kifupi ambacho Edo alikuwa PM, tuliona kucha za serikali.
Tuliwaona Wakurugenzi wa Halmashauri wakifanya kazi.
 
kwa nini mumfagilie mtuhumiwa mkuu wa ufisadi?hivi Tz imekosa watu makini kweli kwanza aje atuombe radhi kwa kutuingiza kwenye mkenge wa dowans na Richmond

Mtu makini kwako ni nani, zaidi ya Lowasa? Una ushahidi wa hayo unayoongea? Uko tayari kuuwakilisha?
 
Kikwete mtego wake ulikuwa na uwezo uwezo wa kumkamata Sungura lakini akawa anamuomba Mungu akute limenasa Tembo, Mungu nae hakufanya ajizi akasikia kilio chake akamleta Tembo kweli sasa ebu tujiulize usalama wa mtego.

Lakini mtegaji ni Lowassa kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mtego, Nyara ni ya Lowassa Jakaya alipewa kazi ya kuchinja mnyama aliyenaswa, Kaja na kisu cha kuchinjia Sungura kumbe kanasa Tembo.
 
tatizo la lowassa ni moja tu japokua huyu jamaa namfagilia sana lakini akichukua madaraka ataanza kuingiza serikalini wakwe zake kama akina siyoi na mwishowe serikali itakua ya kifamilia kama ambavyo mwenzake anafanya sasa hivi...
 
tatizo la lowassa ni moja tu japokua huyu jamaa namfagilia sana lakini akichukua madaraka ataanza kuingiza serikalini wakwe zake kama akina siyoi na mwishowe serikali itakua ya kifamilia kama ambavyo mwenzake anafanya sasa hivi...

mtoto wa mjini hilo siliafiki hata kidogo kwani wako wapi watoto wake? umewah kumsikia hata mmoja akiwa siasani? mkewe je?
 
Serikali ya J.K haijapwaya hata kidogo,tuliopwaya ni sisi maskini wa kutupwa tunaotegemea kila kitu tufanyiwe na serikali (tulio wengi tunafikili kuwa serikali ndio baba/mama).Dhana hii imekuwa si sawa kwamba mimi siwezi bila fulani,na ndio inaharibu kila kitu kiasi kwamba mfumo wetu inaendelea kuwa tegemezi kifikra,kiutamaduni,kiuchumi,kisiasa na kimaamuzi.Suala la EL na JK hapo awali kuwa katika teamwork moja hilo siwezi kulisemea.
 
mimi kama mimi peter kilawe
nachojua lowasa nimtu ambae atatuondoa ama kutukomboa hapa tulipo
namkubalisana
jiulize istoria ya nyuma dawasa mwekezaji alipewa masaa mangapi .?awe ashaondoka hapa nchini?
lowasa lowasa kurayangu nakupa namkubali mmno

sasa hii picha ya jengo ni ya nini mkuu?
 
Serikali ya J.K haijapwaya hata kidogo,tuliopwaya ni sisi maskini wa kutupwa tunaotegemea kila kitu tufanyiwe na serikali (tulio wengi tunafikili kuwa serikali ndio baba/mama).Dhana hii imekuwa si sawa kwamba mimi siwezi bila fulani,na ndio inaharibu kila kitu kiasi kwamba mfumo wetu inaendelea kuwa tegemezi kifikra,kiutamaduni,kiuchumi,kisiasa na kimaamuzi.Suala la EL na JK hapo awali kuwa katika teamwork moja hilo siwezi kulisemea.
Sasa kama hivyo ulivyovieleza si kazi ya serikali sasa kazi ya serikali ni ipi?
 
Jama hata mkipinga ila Lowasa jembe tena sana tuu, huu si ushabiki ila ni kutokana na utendaji wake wa kuto ogofya, tujaribu kumtizama kwa jicho la pili huyu jamaa.

Nadhani ni bora kuliko aliowaacha serikalini sema tuu walimbebesha zigo, ila akipata nafasi anaweza akadhihirisha uwezo wake. Swali ss kama si yy je ni yupi mngine ndani ya CCM ambaye si mamluki wa waliotangulia bila kufanya mageuzi yeyote?

naona huyu aliyetelekezwa anaweza akaja na ufahamu mwingine japo tunaomba asije na visasi kwani ikiwa hivyo patakuwa hapakaliki jamaa, tena nawalivyojizolea awamu hii wapi utapagusa usisikie hapo no pa one ooohh noumar!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mleta Uzi naunga mkono hoja yako kwa asilimia 100! Hata baba wa Taifa (R.I.P) alipomwambia Kikwete wewe subiri muda wakuutaka Uraisi bado wakati ule wa uchaguzi!Watanzania hawakumuelewa Baba wa Taifa vizuri, lakini kwa tafsiri ya Baba wa Taifa kwa Kikwete ilikua ni kwamba HAFAI kuwa Raisi wa nchi hii milele! na ndio maana baada ya kucheza mchezo mchafu na kuingia Ikulu ile awamu ya kwanza aliyekua anaendesha hii nchi ni Lowasa na wenzake kwaama hiyo Lowasa tunajua ni Fisadi lakini ni ni Mwanaume wa ukweli!Oneni baada ya Lowasa kuachia uwaziri mkuu nchi kila kukicha ni matukio ya kutisha na JK anakaa kimya na hajui lakufanya sanasana kwaaibu ndio maana anaishia nchi za nnje! Narudia tena usemi huu - BORA FISADI ANAYEIBA NA MALI ZAKE TUNAZIONA KULIKO MAFISADI WALIOTUIBIA NA HATUJUI MALI ZAO ZIKO WAPI!!!
 
We miss him in Zanzibar, alikuwa anakuja kukagua miradi ya maendeleo kila wiki, JK anakuja tu kama akiandaliwa dodo la ki Arabu. Pinda hakanyagi anaogopa
 
mtoto wa mjini hilo siliafiki hata kidogo kwani wako wapi watoto wake? umewah kumsikia hata mmoja akiwa siasani? mkewe je?

...Kwani Huyu wa Sasa Mlikuwa Mnawasikia watoto na mama watoto wake kabla Yeye hajaukwaa Ukulu?? Kilichofuata Baada ya yeye Kuukwaa Ukulu? Hata Mtoto wake wa Miaka Sijui 10 ni MWENYEKITI wa Chipukizi! Unahakikishaje kwamba Huyu naye Hatakuwa Hivyo?? Punguzeni Mahaba kwa Mtu kiasi cha Hata Kushindwa Kujiuliza Maswali ya Kawaida kabisa....!
 
Inawezekana pakawa na ukweli katika hilo. Ninachokifurahia zaidi ni kwamba Hon. Edward Ngoyai Lowassa ndiye rais ajaye wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kujiuzulu kwa Lowassa ilikua siyo pigo kwake binafsi bali na chama chake cha CCM. Licha ya matatizo yake yote, Lowasa ni mchapakazi,mbunifu na mhamasishaji wa maendeleo,sifa hadimu kwa wanaoitwa viongozi ndani ya CCM. Kuondoka kwake serikalini,kumeacha ombwe la uongozi/utawala ambalo hatujapata shuhudia tangu tumejitawala. Kwa wale wanaodhani kwamba akiteuliwa na chama chake,na pengine akafanikiwa kuwa rais ataisogeza mbele Tanzania,nasema hapana. Wakati wake umepita,afya yake haimwezeshi tena kuchukua majukumu mazito na pili ni aina ya watu wanaomwunga mkono ndani ya chama chake,ni watu wezi,matepeli na wahuni. Watu wa aina hii hawawezi saidia taifa,bali watajali maslahi yao.
 
Kuna watu hapa jamvini wanatoka mapovu tuu wakisikia jina la Lowasa, nadhani hawamjui vizuri. Hata mimi simpendi, lakini najua jambo moja tuu, Lowasa atakuwa Rais wa Tanzania from 2015-2025. Endeleeni tuu kupambana na ukweli.

Ni vyema tukawaza mengine,
 
Huyu mzee namkubali kwa philosophy yake ya "kuthubutu kufanya maamuzi magumu",tuache ushabiki mzee EL akimua ameamua jambo..Call a spade,spade! and for the same understanding he was the think tank wa JK,hilo la kupwaya liko wazi baada ya yeye kuondoka serikalini hata halihitaji uwe mchambuzi saana wa siasa za bongo kuliona!:smiling::becky:
 
Mambo mengi yamesemwa humu ndani kuhusu uhusiano wa Lowassa na Jakaya Kikwete na ile hoja kwamba wawili hawa hawakukutana barabarani inajulikana na kila mmoja wetu. Lakini Historia inaonyesha kwamba ni Lowassa ndiye aliyemtengeneza Kikwete kuwa "Presidential material" na wala si Kikwete aliyemtengeneza Lowassa. Kwa maana nyingine Kikwete ni zao la Lowassa.

Hata timu za ushindi na jinsi ya kukusanya fedha na kuteka nyara vyombo vya habari likuwa ni kazi ya Lowassa. Ukiangalia kwa undani bila ya makengeza ya ushabiki utagundua kwamba Kikwete "aliwekwa" na wanamtandao na wanamtandao ni kazi ya mikono ya Lowassa.

Walipoingia madarakani ni Lowassa ndiye aliyekuwa anaonyesha njia ni wapi wanaelekea, shule za kata na hata kuhimili serikali za mitaa ilikuwa ni kazi ya Lowassa. Lakini tangu Lowassa alipopata "ajali ya kisiasa" na "kuachia ngazi" serikali ya Kikwete imepata myumbo mkubwa sana na hakuna dalili kwamba itatoka huko iliko na badala yake siku hadi siku inapoteza uhalali wa kutuongoza watanzania.

Lakini swali langu linalohitaji kujadiliwa ni kama Kikwete amepoteza Mwelekeo kutokana na Lowassa kujiondoa kwenye serikali yake au tangu mwanzo wakiwa na Lowassa tayari walishapoteza mwelekeo?
umepewa Shilingi ngapi hadi unapost uzushi huu?, wewe hujui kikwete angekuwa rais wako hata kabla ya mkapa? na kipindi hicho lowasa alikuwa nani? kwani tayari kikwete alikuwa nakubalika toka enzi za mwalimu na alishapita kwenye kura za maoni ila kwa sababu busara ya mwalimu nyerere ilitaka mkapa apewe zawadi kwa sababu alikuwa mtu wake wa karibu basi ndo ikawa hivyo lkn Jk alikuwa na mvuto hata kabla ya mkapa, sasa nakushangaa unavosema eti lowasa alimbeba JK, huna unalojua ila inayoongea hapo ni nguvu ya tumbo.
 
Back
Top Bottom