Elections 2010 Kikwete azomewa Bukombe!

Wadau, nimeona niwakumbushe , kuhusu huyu mgombea wa ubunge ,kupitia CCM EMAMANUEL LUHAHULA, huyu ni yule mbunge ambaye mwaka jana alivamiwa na majambazi na kupolwa bastola na majambazi, kwa kushindwa kuitumia.


Mbunge Luhahula acharangwa mapanga
• Avamiwa na majambazi, aporwa bastola

na Stella Ibengwe, Shinyanga







KUNDI la watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wamemvamia Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoa wa Shinyanga, Emmanuel Luhahula, pamoja na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya hiyo, Mberito Magova, na kuwajeruhi vibaya kwa mapanga na marungu.
Licha ya kuwajeruhi vibaya, majambazi hayo yalifanikiwa kupora bastola na vitu vingine walivyokuwa navyo mbunge huyo na katibu huyo.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana katika kijiji cha Nasikukulu wilayani Bukombe mkoani hapa, majira ya saa 4 za usiku wakati mbunge huyo akitoka Kahama kuelekea nyumbani kwake Bukombe.
Luhahula alikuwa akitumia gari yake aina ya Toyota Cresta yenye namba za usajili T 510 ANV. Akakumbana na tukio hilo akiwa amebakiza kilomita 20 kufika eneo la Ushirimbo ambako ni nyumbani kwake.
Alipofika katika kijiji hicho, alikuta mawe makubwa yamepangwa barabarani na ghafla alivamiwa na kundi la watu waliokuwa wamejificha vichakani na kuanza kuwashambulia.
Habari zaidi zinasema, mbunge huyo alifika Kahama usiku na kulazimika kutafuta dereva ili amsaidie kuendesha gari kuelekea jimboni kwake.
Habari zaidi zinasema, mbunge huyo aliokolewa na wananchi waliofika eneo la tukio hali iliyosababisha majambazi hayo kukimbia.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Sospiter Boyyoh, alisema Luhahula alijeruhiwa vibaya sehemu za kichwa; ameshonwa kwenye majeraha yake matatu.
Alisema mbali ya kuumia kichwani, pia alitokwa na damu nyingi hali iliyosababisha kuwekwa chumba maalumu cha uangalizi ili kuokoa maisha yake, tofauti na ilivyokuwa wakati anafikishwa hospitalini hapo.
Alisema mbunge huyo alijeruhiwa mkono wake wa kulia na kukatwa na panga kichwani na kuporwa simu yake ya mkononi na fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu, Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Magova, alisema katika tukio hilo, alifanikiwa kukimbia baada ya kuvamiwa ingawa tayari alikuwa amekwishajeruhiwa kichwani kwa kukatwa na panga.
Alisema hadi jana mbunge huyo alikuwa amelazwa katika hospitali ya wilaya na kwamba hali ya mbunge huyo haikuwa nzuri.
Kamanda wa polisi mkoani Shinyanga, Daudi Siasi, alithibitisha kutokea kwa tukio na kwamba hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa.
"Nimemwagiza mkuu wa polisi wa wilaya (OCD) kufuatilia suala hilo kwa makini ili kubaini wahusika ili sheria ichukue mkondo wake," alisema Kamanda Siasa.
 
Hapo, mida ya saa tano, nilipata ujumbe kutoka kwa rafiki yangu, ambaye ni mfanyakazi wa halmashauri ya bukombe,ambao unasomeka hivi.

DOGO LEO TUNAYE BABA WA MAFISADI ,KIKWETE, TUMELAZIMISHWA, WAFANYAKAZI WOTE WA HALMASHAURI, TWENDE TUKAMSIKILIZE.


baadaye, nikamuuliza vipi mmepewa fulana, za ccm, akaniambia ndiyo, ila yeye amekataa, na wenzake wamezivaa

na kwenye kupiga kura inakuwa hivi hivi. haya tusubiri!
 
Hebu nisaidieni. Hivi ni hapo Bukombe ndipo JK aliingia na helikopta saa 12 jioni na kuanza kuhutubia kwa dak 10 tu hivi akaondoka? Katika Channel 10 habari za saa moja usiku huu niliipata mwisho mwisho mtangazaji Charles Hilila akielezea jinsi wananchi walivyochoka kusubiri kumngojea JK, amoja na kutumbuizwa na TOT pamoja na wale wanaume wavaa sidiria.

Hivi kulikuwa hakuna polisi pale mkutanono wa kumteremsha JK kutoka jukwaani kwa sababu alipitiliza saa za kampeni.
 
Wengi wamekuwa wezi, utajiri kuwania
Mbinu zao ziko wazi, kwa hakika twazijua
Fedha za sera azizi, kwa hila hujichotea
Na hutumia ghawazi, kuhonga kila njia.

Wadau, imekaa vizuri sana, kwa niaba ya wapenda mabadiliko, nimeona nidedicate kwa JK, MRAMBA, LOWASA,CHENGE..............
 
na kwenye kupiga kura inakuwa hivi hivi. haya tusubiri!

Wengine wamevaa fulana kwa kuogopa kupoteza vibarua vyao, lakini, wengi watachagua chadema, na hata mkutano wa DR SLAA, pale bukombe ulijaza watu,kuliko hata wa ccm .
 
Wengine wamevaa fulana kwa kuogopa kupoteza vibarua vyao, lakini, wengi watachagua chadema, na hata mkutano wa DR SLAA, pale bukombe ulijaza watu,kuliko hata wa ccm .

PayGod, kumbuka kura ni siri ya mtu............ so anything is possible
 
PayGod, kumbuka kura ni siri ya mtu............ so anything is possible

Kura ni siri, lakini hali halihalisi huko bukombe, ni mbaya sana kwa ccm, Lakini pia huwezi hukawa unazomewa kwenye mkutano wako halafu, utegemee wananchi hao hoa watakupigia kura, hebu pitia blog ya FRANCIS GODWIN, utaona pia hii habari.
 
Huu utakuwa mwaka wa maajabu baada ya kiongozi mmoja wa CCM ngazi ya wilaya kusini mwa nchi hii kunitonya kuwa kura yake atampatia Dr Slaa. Sikuyaamini masikio yangu.
 
Huu utakuwa mwaka wa maajabu baada ya kiongozi mmoja wa CCM ngazi ya wilaya kusini mwa nchi hii kunitonya kuwa kura yake atampatia Dr Slaa. Sikuyaamini masikio yangu.

hahaaaa i cant wait to vote for Dr.Slaa on 31st October....Kama hii ni kweli basi JK jumba bovu linamuangukia sasa hivi
 
The CCM Bukombe parliamentary candidate, Mr Emmanuel Luhahula, found the going rough and tough at a campaign rally here today when thousands of CCM supporters rejected him before the party's Union presidential candidate, Mr Jakaya Kikwete.

People booed and made catcalls as Mr Luhahula, who is seeking another term, took to the rostrum at the rally held at the Igulwa Primary School ground at Ushirombo in Bukombe District.

Things went sour for the candidate as he was discussing implementation of the ruling party's 2005/10 election manifesto. It did not help either even when Mr Kikwete introduced him to the people, who continued to voice their disapproval.

After reading the situation, Mr Kikwete, who is also the present Union president, asked the people if they accepted him as their president. The crowd voiced a resounding ‘YES'. But when the president asked the same about Mr Luhahula, who led in the party's preferential poll, the people shouted a big ‘NO'.

The runner-up in the polls held in August, Professor Kulikoyela Kaige, ultimately left CCM and joined CHADEMA who picked him as their candidate. As the people booed him, they also raised a two-finger salute, which is the opposition party's symbol.
 
Huu utakuwa mwaka wa maajabu baada ya kiongozi mmoja wa CCM ngazi ya wilaya kusini mwa nchi hii kunitonya kuwa kura yake atampatia Dr Slaa. Sikuyaamini masikio yangu.

hao wako wengi, tena sana, wengi wanaogopa kupoteza kazi zao, endapo watasema hadharani kuwa hawampigii jk, kura october, 31,
 
Unamwaga uongo halafu unashangiliwa. Hii hutokea kwenye baa ya walevi tu. :becky: :becky: :becky:
 
Hahahah Dr.Slaa ni jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni..Chadema na isonge mbele mpaka kieleweke.
Ushauri kwenu wapenda Chama Cha Mafisadi kuzomewa mtazomewa mmeshajipaka matope kwishney..Serikali ya JK wadanganyika (kama mnavyowaona ninyi) mkiwatekelezea lifuatalo..Mahakama iamuru 'Chenge,Karamagi,Rostam Aziz,Mkapa,Lowassa wanasubiriwa segerea kesho asubuhi mtawapata wadanganyika woooote!!!!!' lakini kwa mtindo huu mwisho wenu ni sasa tutapangana mahakamani kuwasubiria mkifunika nyuso zenu kwa mashati mkisubiri karandinga la kwenda segerea..kwani segerea ilijengwa kwa ajili ya walala hoi tu hata ninyi pale panaitwa MTAKUJA UJAMAA VILLAGE.
 
Unamwaga uongo halafu unashangiliwa. Hii hutokea kwenye baa ya walevi tu. :becky: :becky: :becky:
Basi kama unadhani mimi ndiye namwaga uongo nadhani wewe ndiye mwongo maana nina hakika kitu nasema na kwa akili timamu.

Cha ajabu ni kipi wakati mimi nilikuwa mwana sisi m zamani kama wewe? Wewe leo ni garasha tu. Sikiliza dogo wakati wa kura za maoni ndani ya lichama lenu, kuna mgombea alipata zero votes na huku alikuwa na mawakala kwenye vituo hivyo hivyo. Unadhani nini kilitokea?

Kaa na ujinga wako unadhani kila kitu masihala. Kudadadeki.
 
Back
Top Bottom