JokaKuu
Platinum Member
- Jul 31, 2006
- 30,441
- 55,018
..kwa kweli inachanganya mwenyekiti wa chama kinachofuata itikadi ya UJAMAA na KuJITEGEMEA anapotoa kauli kama hizi.
..hivi inawezekana tukawa na chama tawala cha kijamaa lakini serikali yake ikawa ya kibepari?
..hivi inawezekana tukawa na chama tawala cha kijamaa lakini serikali yake ikawa ya kibepari?
Naye Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alisema si rahisi kuwarudisha mawaziri darasani ila wanachopaswa kufanya ni kubadili fikra, ili kwenda na wakati na kuachana na tabia za urasimu.
Rais Kikwete alisema ujamaa ndio umesababisha watumishi wengi wa serikali kuona ubepari kama uadui hivyo hata mtu anayetaka kuja kuwekeza anasumbuliwa hadi anaamua kuondoka.
" Kweli ujamaa ndio umetufanya tuone ubepari ni dhambi hivyo mwekezaji akija anaangaliwa kama vile mwizi, na hilo linafanya wawekezaji wengine kuamua kwenda kutafuta sehemu zingine za kuwekeza, sisi serikalini tumeligundua hilo na ndo maana tumeanza mkakati wa kuajiri vijana wengi zaidi wenye fikra mpya katika nafasi mbalimbali," alisema Rais Kikwete.
"Bado kuna tatizo la watumishi kubadili fikra ili watekeleze maono yetu, hilo tunapambana nalo kweli kweli ili twende na dunia ya sasa, ila kuwarudisha darasani hapana," alisema Rais Kikwete na kusababisha kicheko.