Kijana miaka 38 amempenda mwanamke wa miaka 44 leta maoni ya busara

Aisee wewe jamaa elewa mke si kwa ajili ya kumgalagaza tu, mke ni zaidi ya ngono, na kuna watu wanaowana na hawahitaji watoto. pamoja na sifa zote mke ni lazima muendane mnapokwenda sehemu na siyo yeye anaamkiwa na wewe unaambiwa mambo vipi!
Na wale wanaume wanaoa wanawake sawa na binti zao wa mwisho au mjukuu na mume wakipita wote anaamkiwa shikamoo babu inakuwaje? Na mke anaamkiwa mambo vipi na vijana wadogo. Masuala ya kuishi watu wawili kama mke na mume ni zaidi ya umri!!! Hvi kwa Tz hakuna mwanamke ameolewa na kijana say amempita miaka hata 10 na wanaishi vizuri? Nina mfano mmoja kuna mama amemzidi mke kwa miaka 8 na wanishi vizuri mno!!!! Inabidi wakati mwigine tubadilike na tusikilize kwanza feelings za watu. Ni kwa sababu hii sikutaka kumpa majibu ya haraka nikataka nipate mawazo hapa jamvini na nimeyapata ninashukuru mno kila mtu kwa mtizamo wake.
 
Umri una husu nini katika mapenzi? mijitu mingine sijui ikoje? Mradi kati yao hakuna mtoto mdogo sioni tatizo.
 
Tuache kudanganyana huyu unayemuona hapa haonekani mzee si kwa sababu ni Mmarekani bali kwa sababu ni Millionaire, pesa yake ndio inamfanya aendelee kuonekana wamo na alifanyiwa surgery ya hips.

45921-OprahWinfrey3.jpg


Wapo pia wanawake wa Kitanzania siku hizi ukiambiwa ana 50 unakataa. Maisha yamebadilika!!! Akina mama wanalingana kabisa na mabinti zao!!! Hujawaona!! Umri wa mtu unategemea na anavyojiweka kilishe na mambo mengine!!! Tuko nao maofisini na tunashangaa ukisikia bado say 3 years astaafu!!! Mwonekano wako unaelezea kiasi kikubwa maisha unayoishi.
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Umri una husu nini katika mapenzi? mijitu mingine sijui ikoje?

Sure Zomba, halafu huyu wamepishana tu 6 years!! Mwanamume 38, ni mtu ndogo huyo kweli? Kama ingekuwa 20s kwa 40s ingekuwa taabu sana na singeuliza hata ushauri wa kumpatia huyu ndugu yangu. Nafikiri kama ni chini ya 10 years si vibaya sana. Ninachoogopa tu ni kuoa au kuwa na afair na mwanamke sawa na umri wa mama yako, but kama ni umri wa dada yako tena under 10 years sioni tatizo. Ninaomba endeleeni kunipa mazuri ya kumpa kijana. Otherwise, thanks to u all for your comments and advice.
 
Umri una husu nini katika mapenzi? mijitu mingine sijui ikoje? Mradi kati yao hakuna mtoto mdogo sioni tatizo.
Something wrong in ur brain, kama hakuna tatizo asingeomba mtu ushauri, mbona wengine wanaoa bila kuomba ushauri? wewe huoni tatizo ila mimi naliona tena kubwa tu.
 
Something wrong in ur brain, kama hakuna tatizo asingeomba mtu ushauri, mbona wengine wanaoa bila kuomba ushauri? wewe huoni tatizo ila mimi naliona tena kubwa tu.

Nawasikitikia sana mnaoona tatizo wawili kupendana, hata msemo wa kiswahili "ukipenda tongo waona kengeza" hamuuelewi maana yake:
England, A 61 years old woman and her 29 years old husband, "normal love"!
His lover is 10 years older than his mother!

Img249438072.jpg

Source: A 80 old wife and her 38 young husband (photos) - Chinese Forum
 
Na huyu aseme nini:


107-year-old wife pines for detained young husband

20091104.093516_oldwoman1.jpg
blank.gif


blank.gif
Wook Kundur, 107, believed to be the oldest woman in Terengganu, is feeling rather lonely and is appealing to the authorities to shorten her 38-year-old husband's detention at the Sungai Besi Narcotics Addiction Rehabilitation Centre in Kuala Lumpur.

Soma zaidi: 107-year-old wife pines for detained young husband


 
Nawasikitikia sana mnaoona tatizo wawili kupendana, hata msemo wa kiswahili "ukipenda tongo waona kengeza" hamuuelewi maana yake:
England, A 61 years old woman and her 29 years old husband, "normal love"!
His lover is 10 years older than his mother!

Img249438072.jpg

Source: A 80 old wife and her 38 young husband (photos) - Chinese Forum
zomba sitegemei mtu kama wewe uchukuwe reference za wazungu kuzitumia kwa Waafrika, huku ni kuishiwa maarifa, kwahiyo na Cameron anavyopigia upatu ndoa za jinsia moja unataka tuone ni sawa kwa sababu wao wazungu wanafanya?
 
Last edited by a moderator:
age ant nothing but a number.............
Mwambie asongeshe tu, tena ndoa yao itadumu mbaya.......
 
zomba sitegemei mtu kama wewe uchukuwe reference za wazungu kuzitumia kwa Waafrika, huku ni kuishiwa maarifa, kwahiyo na Cameron anavyopigia upatu ndoa za jinsia moja unataka tuone ni sawa kwa sababu wao wazungu wanafanya?

Sitegemei kama wewe ni mbaguzi kiasi hicho, wazungu na sisi tofauti ni rangi tu, hakuna kingine. Ngoja nikutafutie reference za Kiafrika ili uridhishe roho yako.
 
age ant nothing but a number.............
Mwambie asongeshe tu, tena ndoa yao itadumu mbaya.......
Hata wewe unakuja na kauli za rejareja namna hii? age aint nothing but a number Africa? kwa nini msimuige huyo mliyemcopy huo msemo R Kelly ambaye alikuwa ni mtu mzima lakini akawa anamtafuna Aliayah ambaye alikuwa bado kinda?
 
zomba sitegemei mtu kama wewe uchukuwe reference za wazungu kuzitumia kwa Waafrika, huku ni kuishiwa maarifa, kwahiyo na Cameron anavyopigia upatu ndoa za jinsia moja unataka tuone ni sawa kwa sababu wao wazungu wanafanya?

Haya, hii ya Waafrika, usije ukasema sasa nikuletee ya Wachagga:




I was completely stunned when i saw this Photo Online. At first, i thought it was a burial ceremony not knowing its was actually a Wedding of a 27 Year Old Man and 83 Years Old Woman.
Source:
http://revealzone.blogspot.com/2012/10/27-year-old-nigerian-marries-83-year.html
 
Haya, hii ya Waafrika, usije ukasema sasa nikuletee ya Wachagga:




I was completely stunned when i saw this Photo Online. At first, i thought it was a burial ceremony not knowing its was actually a Wedding of a 27 Year Old Man and 83 Years Old Woman.
Source:
http://revealzone.blogspot.com/2012/10/27-year-old-nigerian-marries-83-year.html
Kwahiyo wewe unadhani vichaa wapo Mirembe tu? huyo ukimpima akili hawezi kuwa na akili timamu ni mapenzi yepi hapo kama si ushirikina tu.
 
Kwahiyo wewe unadhani vichaa wapo Mirembe tu? huyo ukimpima akili hawezi kuwa na akili timamu ni mapenzi yepi hapo kama si ushirikina tu.

Nimekuletea ya Waingereza nikakuletea ya Waasia hukuridhika, nimekuletea ya Waafrika sasa unawaita vichaa, na hii hapa ya mchanganyiko:

image.aspx
 
Nimekuletea ya Waingereza nikakuletea ya Waasia hukuridhika, nimekuletea ya Waafrika sasa unawaita vichaa, na hii hapa ya mchanganyiko:

image.aspx
Hapo akili yote apate Makaratasi tu, ananyonya mpaka kinyesi, akili kichwani mwake hapa tunaweza kuumiza vichwa kumbe jamaa ni Mario Baroteli na kaona demu ana mkwanja sasa wewe hata umwambie tofauti ya miaka na age ambayo ameifikia Mwanamke hawezi kukuelewa.

Lakini mimi siku zote nitasimama kwenye kweli, hakuna mtu yeyote aliyeshangaa Bekham kumuoa Posh ambapo Bekham amezidiwa mwaka mmoja, lakini hii ya 38 na 44 kuna after something hapo tusidanganyane.
 
Kuna vitu vingine wala havitaji Degree kuelewa which is which, mwambie ndugu yako apate tuition ya bure hapa kwa Zuma.
Huyu ni mke wa ujana.

090514_newsmaker1.jpg


Lakini baadaye akaona kumbe Dunia ni pana zaidi na alikuwa kwenye nafasi sasa ya kuchaguwa kitu roho inapenda, akaibuwa chombo hiki.

Jacob-Zuma-arrives-at-Hea-001.jpg

ZUMA-ART_1589120c.jpg
 
EMT Mtambuzi FirstLady1 Smile Kongosho na mashostito wengine hebu mje kutoa ushauri, yaani kama kupenda ndio huku namuomba Mungu aniepushe mbali na upofu huu

Kwanza tukubali kuwa suala la umri siyo shida sana kwa wazungu. Lakini kwetu sisi kuna tamaduni (unaweza kusema ni nzuri au mbaya) za mwanaume kutomwoa mwanamke aliyemzidi umri. Hii tunayoita ni "kawaida" kwa mume kuwa mkubwa kuliko mke wake inatokana pia na mazoea, jambo ambalo limekuwa likifanyika tangu zamani za kale. Lakini naona kama vile watu wanaweza kutumia Adam kuumbwa kabla ya Hawa. Maana Hawa alitengenezwa baada ya Adamu kuwepo. Kwa hiyo "mume" kama "Adam" anatakiwa kuwa mkubwa kuliko "mke" kama Hawa.

Hata hivyo, mila na tamaduni zetu ndizo zinazotazama mambo kwa mazoea (maana Adam na Hawa tumewasikia juzi juzi tuu baada ya kutawaliwa na wazungu). Kama huyo mwanamke anafungwa na mitazamo ya tamaduni zetu the asiolewe mtu anayemzidi umri. Zipo sababu za kitamaduni kama watazijali sana. Mke kama ni mkubwa kwa mume ataanza kuzeeka kabla ya mume. Hii imewafanya wengi waamini kwamba siyo vyema kuoa mke ambaye ana umri mkubwa kukuzidi.

Yawezekana pia kukawa na sababu nzuri tu za kimwili ambazo zinatoa angalizo na tahadhari kwa mke kuwa mkubwa (sana) ki-umri kuliko mumewe, ambazo pengine tulishazisikia. Kwa hiyo kama zina manufaa mimi naona ni vizuri tu to take them into account kuliko kutofanya hivyo. Kuna mambo assuredly4 ameyaongelea hapo juu.

Hata hivyo, uzoefu wa kisayansi unaonesha kwamba wanaume hufariki mapema zaidi kuliko wanawake. Kuna mifano mingi tuu ya wanaume waliokufa wakiwa na umri wa miaka 60 wakawaacha wajane wakiwa na umri wa miaka 56. Wajane hao wameendelea kuishi hadi takribani miaka 20 tangu kufiwa na waume zao.

Hata hivyo, kibayolojia mwanamke akitimiza miaka 40 huenda akaacha kuona siku zake za hedhi ikiwa ni dalili kwamba hawezi kushika mimba tena maishani mwake. Wanawake wanashauriwa kuacha kuzaa kabisa wakiwa katika umri huo wa miaka 40. Wapo wanaoshauri kutooa mwanamke mwenye zaidi ya miaka 40 kama una mpango wa kuzaa watoto.

Wanasema kama huna mpango wa kuzaa nae watoto , mwanamke mwenye umri kama huo ni bomba sana. Anafaa sana sana, wanadai. Hamtakuwa na purukushani za watoto tena bali mtakuwa mnakula bata tuu bila kuzuiliwa na majukumu ya malezi kwa watoto. Ndiyo labda wako walioamua kuzaa mapema ili wawe wanakula bata wakifikisha miaka ya 40.

On the hand, kizazi cha sasa tumetawaliwa sana na tamaduni za kizungu kiasi kwamba tamaduni zetu whether mbaya or nzuri does not matter anymore. Kufunga ndoa na mke anayekuzidi umri hakuna tatizo lolote litakalokupata katika masuala yote ya ndoa na kibayolojia. Isipokuwa tu wanandoa wanaweza wasijisikie vizuri kisaikolojia kutokana na mitazamo ya jamii inayowazunguka kama akina Matola kuwa na mtazamo kwamba umri ni tatizo katika masuala ya mapenzi na ndoa.

Pia kama alivyosema Zion Daughter, inategemea pia na huyo mwanamke mwenyewe anavyojisikia kuolewa na mwanaume ambaye ni mdogo kiumri kwake. Niseme pia kwa huyo mwanaume. In fact ukiangalia wala hajamzidi sana kiumri. Kama alivyosema Sal "38 and 44 ni watu wazima waliokomaa kiakili na wanajua wanataka nini katika maisha yao" na suala la "mtoto hayo ni majaliwa ya mwenyezi mungu maana hata wadogo pia hukosa watoto" Kuna watu wameoana wakiwa wadogo lakini wanashindwa kupata mtoto.

Lakini bado hili suala siyo simple kama wengi wetu tunavyodhani. Maana watu wakishapendana ni ngumu sana kushaurika. Wengi watakuwa wameshafanya maamuzi wanatafuta approval tuu. Lakini kama kweli anatafuta ushauri na siyo approval ningeshauri kuwa kama kweli wanapendana sioni nafasi ya kigezo cha umri kuwatenganisha. Lakini kwa upande mwingine, perception za watu juu ya mwanamke kumzidi umri mumewe siyo nzuri kwenye jamii yetu kama alivyodhihirisha Matola na wengine. Inawa-affect sana mwanamke husika kisaikologia. Nafikiri hata mwanaume. Ndiyo maana huyo mwanamke anataka kujua kama halitakuwa tatizo kwa upande wa mwanaume na ndugu zake. That itself is a good step maana anaonyesha yuko aware na akina Matola.

Kama kweli wanapendana, wachukue msimamo wao kisha wasimame kuutetea milele wala wasikatishwe tamaa na jamii au watu watakaowaona wa tofauti. Naamini jambo kuu katika katika maisha ya ndoa ni upendo na siyo umri. Upendo hausitiri mabaya yote. Kama kweli wanapendana hawatanyapaana tuu kwa sababu ya umri wake mdogo au mkubwa kwake. Upendo ndicho kipimo kisichokoma na kitachowaunganisha kukaa pamoja miaka mingi.

Upendo na tabia ya mtu haijalishi umri. Kama mtu anatabia nzuri na anajua nini maana ya kupenda haijalishi umri mkubwa wala mdogo. Hao walioko kwenye ndoa tunaweza kusema kuwa ndoa zao ziko salama au zimetulia kwa sababu tuu mke hajamzidi umri mume? Mke ni mke awe mdogo au mkubwa muhimu umpate mwenye upendo na tabia njema. Wapo wanawake makini na ndoa zao na wamezidiwa umri na waume zao lakini wanalia katika ndoa zao kila siku. Aombe Mungu ampate mke mstaarabu na mwenye kujua nini maana ya ndoa.
 
Kinachotokea hapa ni mapz ya muda tu 44 akifika 50 bleed inafunga hasikii hata nyege na ndipo inabidi ahangeike kutafuta maradhi nje labda kwa hiyo age m'ke ana pesa ndo anachotafuta
 
Back
Top Bottom