Ndugu wajumbe, nimekuwa nikifuatalia kwa karibu mwenendo wa siasa za nchi yetu kwa ukaribu sana. Mambo yanayotokea sasa yananishangaza na sikutarajia kama yangeweza kuja kutokea katika nchi yetu nzuri ya Tanzania. Kutokana na mambo hayo ningependa mnijulishe hasa wale waliosoma historia na sayansi ya siasa, je? yawezekana haya yanayotokea ni dalili za chama tawala kupoteza madaraka na ni mambo gani mengine tuyatarajie katika mlolongo huu wa mambo ya ovyo yanayotokea nchini?