TUMBIRI
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 1,933
- 1,199
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Emmanuel Nchimbi ameteua Kamati Maalumu ili kukamilisha mchakato wa kupendekeza vazi la Taifa ambalo litakuwa miongoni mwa vitambulisho mbalimbali vinavyotambulisha utaifa wa Tanzania.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam inasema kuwa kamati hiyo imeanza kazi mara baada ya uteuzi na itatakiwa kukabidhi taarifa yake Februari 28, 2012 kwa Dk. Nchimbi. Alisema hatua inayofuata sasa ni kuwashirikisha wananchi kuhusu mapendekezo yaliyopo na hatimaye kupendekeza vazi mahususi linalotambulisha utaifa wa Watanzania.
Wajumbe waliochaguliwa katika kamati hiyo ni pamoja na Joseph Kusaga ambaye atakuwa Mwenyekiti; Angela Ngowi Katibu; wajumbe ni Habibu Gunze, Joyce Mhaville, Mustafa Hassanali, Absalom Kibanda, Makwaia Kuhenga na Ndesambuka Merinyo.
"Mchakato wa kupata vazi la taifa umeshapiga hatua kubwa, wabunifu wazalendo wa mitindo ya mavazi wameshashirikikishwa na kutoa mapendekezo yao, alisema Waziri Nchimbi kwenye taarifa hiyo.
Source
HabariLeo | Kamati ya kupendekeza vazi la Taifa yatajwa