Jicho la tatu Arusha na Lema linavyoona


jitekenyeni alafu chekeni wenyewe, ila CCM hapa arusha mtapasahau milele.
Kwa taarifa za jikoni Lema hakati rufaa na ndiyo mgombea wa CDM tena.
Tunamuaibisha shetani kwenye ballot kwa mara ya pili.
Keshashikishwa adabu tayari...this time hata kama atagombea tena(though atashindwa vibaya) lakini tayari ameshafunzwa adabu!!
 
Lema najua anakubalika lakini kichama lazima kutakua na mchakato ndio maana hasa ya demokrasia ..Ikiwa kama bado wanachama wapiga kura wana imani naye hilo ndilo la muhimu ..lakini pia kama kuna mtu mwingine mwenye mawazo mapya ndani ya chama akaonekana kua na sera nzuri na vision zaidi yake ..pia tumpe ..Lema ni kamanda wa ukweli lakini makamanda ndani ya chama wako wengi sana ,,ndio maana ya mabadiliko sio kwa CCM tu hata kwa CDM ..

CDM haina sababu ya kugoma kumsimamisha Lema.
Lema ni mbunge wa maisha hapa arusha mjini.
Tunawaabisha tena kwa mara nyingine.
 
Ndugu Kitalolo. Hoja zako ni dhaifu sana na sijui kama unaishi Arusha. Lema anaweza akawa na udhaifu wa hapa na pale lakini ni mwanasiasa mwenye nguvu na mvuto ktk mji wa Arusha. Napenda kukuhakikishia kwamba CCM itaambulia kipigo kingine cha aibu hata wamlete nani kama mgombea wao!
 
Mkuu usikonde,
Nasubili nakala ya mahakama juu ya hukumu Lema,pengine kesho jioni mwanasheria wangu akaipata nakala hiyo,kisha j,3 ntafunguka kwa waandishi wa habari pale GOLDEN ROSE HOTEL!

Siyo nasubili ni nasubiri!!!!!!!
 
Kwenye kesi zote zinazohusu uchaguzi wa 2010 CCM wameanza kuchangisha pesa kwa ajili ya chaguzi ndogo, inawezekana wanajua kile kinachoendelea kwenye hukumu za kesi hizo.
Unapojaribu kutoa mawazo ya kufanyia kazi au utaonekana zumbukuku, ila ni vema kuzingatia kinachoongelewa kwenye jukwaa.
Wengine wanageuza eneo hili kama sehemu ya kuwaona wenzao hawana akili, jamani tubadilike ushabiki wetu ni mzuri lakini pia tuangalia yale yaliyo mbele yetu.
 
Hizi ndizo mbinu za kimafia ambazo ccm watazitumia ili waweze kulipata jimbo la arusha mjini

1.kuingiza mamluki chadema kwenye kura za maoni ya kupitishwa ubunge arusha mjini au kuleta ushabiki wa kisiasa ndani ya chadema utakaoweza kuleta makundi ndani ya chama...!

2.kutumia jeshi la polisi kutisha watu, ili kupunguza idadi ya wapiga kura na wakati wa kulinda kura

3.kutumia makada wao akiwemo mkuu wa mkoa magessa mulongo,ocd wa wilaya sambamba na wafanyakazi wengine serikalini ili waweze kuchakachua kura

4.kumwekea pingamizi lolote mgombea wa jimbo la arusha mjini

5.kufanya kampeni za matutsi dhidi ya g.lema

6.kukaa chini na wafanyabiashara kuhakikisha wanaichangia ccm

7.kufanya jambo lolote la kimafia ikiwemo kuua kama walivyotaka kufanya kule ilemela dhidi ya mb.higness kiwia
 
Kweli roho za watawala huwa ni ngumu kama jiwe; Anyway, hata enzi za Mussa kuwakomboa wana wa Israel, Mungu aliifanya roho ya mtawala Herode kuwa ngumu ili Mungu adhihilishe uwezo wake! katika hili Roho ya CCM imefanywa kuwa ngumu ili Mola azidi kudhihilisha uwezo wa CHADEMA kujenga hoja huku CCM ikiendelea kudhihilisha udhaifu wake wa sera!
 
Hawa ni mashujaa na wanastahili hadhi ya kitaifa,
Lema ni mbaguzi/mdini na anachochea ukanda na ukabila, LEMA amesababisha watu waichukie Chadema Hafai wala hafai hata kidogo.
Hongera Majaji na mahakimu kwa kutenda haki.
Hongera mliomfungulia mashtaka, Mungu awalipe.
Ameeeeeeeeeeeen

SASA NDO TUTAJUA NANI ATASHINDA MUNGU WA MAFISADI AU MUNGU WETU...ALIYETUONGOZA TOKA ARUMERU.......AMBAYE TULIANZAN NAYE TUKAMALIZA NAYE
MWISHO NASEMA HAWA WALIOMFUNGULIA KESI LEMA WATAAIBIKA KWA LAANA ITAANZA KUWAPATA VERY SOON HAWA (Waliomshtaki lema (Musa Mkanga, Happy Kivuyo na wenzako.!). ). PIA ALIYEWEKA MKONO WAKE KATIKA HILI HATABAKI SALAMA!!! DAMU ILIYOMWAGIKA WAKATI WA UMEA NDIYO ITAKAYOCHOCHEA NGUVU YA UMA
MUNGU IBARIKI CDM MUNGU IBARIKI A TOWN
PEOPLESSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS...........................POWERRRRRRRRRRRRRRRRRRRRRRRR!
 
kama wapi walifanya ivyo???
hapa hakuna cha maoni wala vitisho vya polisi,
Lema ni mbunge wa Arusha mjini na safari hii tunawatandika CCM kipigo cha mbwa mwizi.
 
Napenda kuwaeleza kwamba, haya yote yanayomkuta Lema ni kutokana na nyie kutumiwa na mafisadi kuweza kukandamiza haki ya mnyonge.
Tazameni sasa damu yetu wana Arusha inaenda kumwagika wakati wote wa kampeni mpaka uchaguzi ujao hapo Arusha.
Mmekubali kutumika ili kuweza kumkomoa lema lakini kumbukeni kwamba nguvu ya umma kamwe haiwezi kuzimwa na nyie. Kitu gani kiliwawasha mpaka mkafanya hivyo?
Anyway mumjgu yupo one day atakuja kudhihirisha ukweli juu ya jambo hili.
Kweli yupo... Kudaadeki!
 
Back
Top Bottom